Tuache Wivu kwa Nehemia Mchechu

Tuache Wivu kwa Nehemia Mchechu

Status
Not open for further replies.
Angaliwe upya! Hana haja ya mshahara wote huo, maana anachokifanya sio faida kwa Watanzania walio wengi!

Mtu kama Mkurugenzi wa Muhimbili Hosp alistahili kulipwa zaidi ya Mchechu, maana anaokoa

kazi kwako kufuatilia.....!
Sioni sababu yakufanya namna hiyo kwavile naamini analipwa kutokana na Makubaliano yake na waliompa hiyo kz na uwezo wake wakufanyakazi
 
Nimekuwa nafuatilia mjadala hasa wa Rais Mtukufu bwana Magufuli kuhusu mishahara ya watumishi kuwa mikubwa.

KIMSINGI Nadhani rais ana nia njema ya kujenga moyo wa uzalendo kwa watu ili watangulize maslahi ya Taifa kwanza na yao binafsi yaje baadae.

Tatizo langu nikwamba watu wengi tumejikita zaidi kumshambulia Nehemia Mchechu CEO wa NHC. Eti tu kwa kiwango tunachokiita kikubwa cha mshahara wa M35. Wengi wetu hatuzungumzii Mchechu alikutoka alikuwa analipwa 26M.

Na alianza project ya kujenga nyumba akiwa kwenye taasisi yake ya zamani. So serikali iliona atafunika NHC zaidi kwasababu ni wazi shirika lilishakuwa kinapumulia mipira.

NHC kifupi ikishakaribia kufa Bwana Mchechu hakuomba kazi NHC serikali ilimfuata. Mchechu amefanya kazi kubwa sana NHC ukilinganisha na ilivyokuwa mwanzo. Mchechu anastahili kulipwa zaid ya hapoo.

NHC ni shirika la 3 now kwa Ubora wa mashirika ya Nyumba africa lakwanza NHS ya SA yapili Ethiopia na Tatu Tanzania. Sasa mnataka huyu kijana wa watu afanye nini? Watu wanaongea hoja ya nyumba za NHC kuwa za bei kali sio za watu wa hali ya Chini.

Thats true but we have to know kwamba Sera ya NHC haijawahi kuwa na sera hiyo ya nyumba za bei nafuu kwa watu wa Hali ya Chini. Hakuna mahala popote NHC iliwekwaa kwaajili ya kujenga makazi ya Wanyonge.

So kama kuna watu tunahitaji NHC iwe ya wanyonge ni kuwakumbusha watunga Sera wetu wakabadili sera ya NHC kuacha kujiendesha kibiashara. Mchechu hata kwa hako ka M30 anatuhurumia tuu.

Wenye vyeo kama chake huko kwenye taasisi aliyotoka sasa hivi wanakula mpaka M75. Ifike mahali tusisukumwe kwa wivu pekee juu ya Mchechu tuache wivu tumuache afanye kazi.


Kweli tukiendesha NCHI hii kwa wivu wa Vitu vidogo Kama kuonea wivu mishahara hii ya Dola 20'000 tutarudi kule NCHI kuwa NA mashirika ya ovyo ...tuziachie bodi ZA mashirika zipange mishahara ya wakuu wake ILI mradi wanna faida ...
Dunia Nzima CEO are highly paid kwa kuwa kazi zao ni Kama ZA ukocha Shirika likifanya vibaya ...wanatimuliwa ...the higher the risk the higher the salary ..
Badala ya kujadili mishahara ya mabosi wa NBC,CRDB ..NHC ,nssf etc tuzipe bodi imara ZA wakurugenzi ILI zisimamie mashirika vizuri ....
Nitashangaaa sana Kama watu wanataka CEO alipwe milioni 2 Kama DC
 
Kuna kazi huoni kwa macho kwa maana ya majengo lakini zipo documented sasa utasemaje. wapo walimu wazuri sana lakini utasifia wanafunzi kuwa wanaakili husifii mwalimu aliye mfundisha, kunaadministrators wazuri sana huwezi kuona utasikia wanasifiwa. Kuona majengo kunakufanya usifie mtu je umejua yanaleta faida gani katika uchumi wa nchi? Nini lengo la uanzishwaji NHC kujengea kina nani ? umefanya uchunguzi ni kina nani wanunuzi wa hizo nyumba? Baada ya miaka kadhaa nini itakua hali ya Mabenki ambayo yamefacilitate ujenzi wa majumba hayo? kuna mkakati gani wa kuzuia kilichotokea Dubai kiuchumi kisitokee huku? ukisha nijibu hayo maswali Mlipe Mchechu 35M will be very happy. naomba tuangalie kwa misingi hiyo sio kutaja majina ya watu
Amesema taja hao vijana na kazi zao. Hata hivyo mkuu utapimwaje kwa kazi zisizoonekana?
 
Acha bange wewe kijana... Kama mnamdanganya huyo Msukuma wenu hivyo basi mtoeni mueke kada wa chama hapo alafu muone atakapowafikisha...

Unashangaa Mchechu kulipwa zaidi ya Katibu Mkuu na Waziri lakini unajua DG wa Tanesco analipwa zaidi ya Katibu wake mkuu na waziri pia... Unajua DG wa Tanapa analipwa zaidi ya Katibu Mkuu wa Utalii na Waziri wake?? Na wa Ewura je?? Sasa povu haliwatoki kote huko ila linawatoka kwa Mchechu tu... Alafu unasema kabisa kajipangia mshahara, sijui uzoefu kazini, we pimbi kweli, Bade alikuwa na uzoefu gani mpaka akapewa TRA na kuachwa makamishna kibao pale bila kupandishwa?? Kama mnamtafutia kada hiyo nafasi hapo mpeni haraka sana, wapo akina Rage, Masaburi na wengine waliokosa ubunge muwape hiyo nafasi alafu muone matokeo...


Hii NCHI tutaenda kuuwa UCHUMI kwa kuwa kuna watu wanapiga watu vita ILI wachukue kazi zao .........hizi kazi ZA kuendesha mashirika yapate faida dunia Hii SIO rahisi .....NI Kama kufundisha timu iwe bingwa .....watu hawashangai kumlipa kocha wa TAIFA stars milioni 60 kwa MWEZI LAKINI wanaingikia mashirika ambayo yanatakiwa yapate faida .........NA tatizo mkuu wa Shirika AKIWA Tanzania mwenzao wanaona anapata pesa nyingi ....hawaulizi mishahara wa DG wa barrick...LAKINI watahoji mishahara wa Rweyemamu ..DG wa Stamico gold ..huo Mfano tu wa Kiwango chetu
Tuelewe kuwa SIO rahisi kupata MTU competent labda Kama tunataka mashirika yetu Yaongozwe NA watu wakupewa NA RAIS .......LAKINI ukitaka CEO mzuri ...aombe kazi NA afanyiwe interview kitaalamu NA RAIS apewe majina Matatu ...SIO MTU anapewa tu ..
 
mchechu hakutaka kuafanya kazi serikalini kwa sababu mbalimbali na mojawapo mishahara midogo. serikali ikamfuata na kutaka huduma yake, ni wazi jamaa ameweka dau analolitaka. sio kila mtu anaenjoy mishahara midogo na ukiritimba, na sio kila mtu yuko tayari kuwahudumia watanzania kwa kufanya kazi serikalini. kama magufuli na watanzania wengine wanafikiri mchechu anachofanya ni kibaya then wakatishe mkataba wake. aliamua kwenda private sector kwa sababu zake, msifamfanye awe sehemu ya kutoa nyongo zenu za chuki bila sababu za msingi

Naona haitapita mwaka mmoja cream nzuri ya watendaji waliotoka sekta binafsi kuwa serikalini katika reform ya uboreshaji wa sekta ya umma aliyoanzishaga Mkapa ...wataacha kazi serikalini. ........., hakuna atakayekubali kupokea mishahara wa masimango ....wakati akienda Exim analipwa milioni HADI 100 kwa MWEZI ...Tena mishahara wa Siri yake .....
 
Hii NCHI tutaenda kuuwa UCHUMI kwa kuwa kuna watu wanapiga watu vita ILI wachukue kazi zao .........hizi kazi ZA kuendesha mashirika yapate faida dunia Hii SIO rahisi .....NI Kama kufundisha timu iwe bingwa .....watu hawashangai kumlipa kocha wa TAIFA stars milioni 60 kwa MWEZI LAKINI wanaingikia mashirika ambayo yanatakiwa yapate faida .........NA tatizo mkuu wa Shirika AKIWA Tanzania mwenzao wanaona anapata pesa nyingi ....hawaulizi mishahara wa DG wa barrick...LAKINI watahoji mishahara wa Rweyemamu ..DG wa Stamico gold ..huo Mfano tu wa Kiwango chetu
Tuelewe kuwa SIO rahisi kupata MTU competent labda Kama tunataka mashirika yetu Yaongozwe NA watu wakupewa NA RAIS .......LAKINI ukitaka CEO mzuri ...aombe kazi NA afanyiwe interview kitaalamu NA RAIS apewe majina Matatu ...SIO MTU anapewa tu ..
Mkuu na kwa hii mentality ya huyu Rais wetu mimi nasubiri kitu kimoja tu... Alisema atafukuza wote pale ATCL alafu aajiri upya, then alete Airbus 6 mpya... Sasa na hapo waajiri DG wa ajabu watakayemlipa million 3 alafu wauone moto wake... Nchi hii kwasababu kule juu watu wanakurupuka basi huku chini full kupandikiziana majungu watu waporwe kazi zao...

Mh. Rais najua unapita humu na watu wako wanapita pia... Weka kada hapa ATCL alafu uumpe hizo ndege 6 uone baada ya mwaka atakotufikisha....
 
Mkuu na kwa hii mentality ya huyu Rais wetu mimi nasubiri kitu kimoja tu... Alisema atafukuza wote pale ATCL alafu aajiri upya, then alete Airbus 6 mpya... Sasa na hapo waajiri DG wa ajabu watakayemlipa million 3 alafu wauone moto wake... Nchi hii kwasababu kule juu watu wanakurupuka basi huku chini full kupandikiziana majungu watu waporwe kazi zao...

Mh. Rais najua unapita humu na watu wako wanapita pia... Weka kada hapa ATCL alafu uumpe hizo ndege 6 uone baada ya mwaka atakotufikisha....
unachotaka awabembeleze sindio mchukue pesa unasema password ilipotea muambiwe pole kwa vile mnaakili. kama mnaona nyinyi ni bora kuliko hata makatibu wakuu basi kazi sana. Cha maana cha kufanya ni kutuambia kwanini ATCL wasifukuzwe au huyo mchechu anaingiza ngapi ili alipwe 35M? basi hilo tuu
 
unachotaka awabembeleze sindio mchukue pesa unasema password ilipotea muambiwe pole kwa vile mnaakili. kama mnaona nyinyi ni bora kuliko hata makatibu wakuu basi kazi sana. Cha maana cha kufanya ni kutuambia kwanini ATCL wasifukuzwe au huyo mchechu anaingiza ngapi ili alipwe 35M? basi hilo tuu


CEO's ndio highly paid people everywhere .......unashangaa kumzidi mshahara Katibu Mkuu ....au waziri mwanasiasa ..???.

Basi utashangaa CEO wengi dunia Wana mshahara mkubwa kuliko Marais wengi .....akiwemo rais wa marekani ....
 
CEO's ndio highly paid people everywhere .......unashangaa kumzidi mshahara Katibu Mkuu ....au waziri mwanasiasa ..???.

Basi utashangaa CEO wengi dunia Wana mshahara mkubwa kuliko Marais wengi .....akiwemo rais wa marekani ....
siwezi kushangaa privet sector but katibu mkuu is not a ceremonial post ni mtendaji kuu wa wizara sasa unaposema umzidi kwa scheme ipi hii ya Tz. unatafuta matatizo tuu
 
Hawa ma DG wengine wa umma wanalamba hizo hizo 35M and above!!na bado wana other benefits kwa mwez znafikia hadi 10M....nenda private orgs kama TBL..VTL.. Alaf angalia ma Managers au head of departments wanalipwa ngapi?hadi 60 per month.. Kwaio kama mnataka NHC iendelee na mumuajiri DG ambae atalipwa kutokana na utendaj wake wa kazi Msechu is the person..ila kama mnataka mtu ambae mumlipe million 5 akubali huku anawaibia mil100 kwa mwezi go for another options na shirika litakufa in one year

Malengo ya Shirika la Nyumba la Taifa ni nini? Ni kuzalisha mapato kwa serikali? Ni kuhudumia matajiri ambao wangemudu kununua nyumba zinazojengwa na makampuni binafsi? Na kuwezesha matajiri ku-grab prime areas ambazo wasingeweza kuzipata kama business model ya NHC ingelenga wanyonge? Ni kuhudumia wanyonge kwa kuboresha makazi na kuhakikisha kuwa Watanzania wengi wanapata makazi yaliyo bora ama kwa kulipa ada ya pango kila mwezi au kununua nyumba kwa wale wanaomudu? Unadhani lengo la NHC ni kushindana na sekta binafsi katika kuzalisha mapato? Kama ni hivyo, kwa nini serikali imejiingiza kwenye biashara hiyo badala ya kuachia sekta binafsi na serikali ikabaki kama regulator? Mchechu anachofanya ni kuhamisha mali za umma kwenda kwa watu binafsi.
 
CEO's ndio highly paid people everywhere .......unashangaa kumzidi mshahara Katibu Mkuu ....au waziri mwanasiasa ..???.

Basi utashangaa CEO wengi dunia Wana mshahara mkubwa kuliko Marais wengi .....akiwemo rais wa marekani ....

Kwa kuwa "CEOs are highly paid people everywhere" basi yeyote mwenye hiyo title anapaswa kuwa 'highly paid" bila kujali anachofanya? Hoja iliyoko mezani ni kwamba huyu bosi wa NHC analipwa mshahara mkubwa kuliko anavyostahili au kinyume na scales za serikali etc. Majibu ya hoja hiyo hayawezi kuwa Mchechu ni kama CEO kama maCEO wengine eg. kama CEO wa Google. Mbona bosi wa Google analipwa pesa nyingi kuliko Obama? Hiyo haiwezi kuwa justification ya mshahara wa Ndugu Mchechu. Eleza, kwa nini Mchechu anastahili mshahara wa Tsh. 35 million kwa mwezi? Tuambie kwamba yeye ni alien, anatokea sayari nyingine ndio maana tunamlipa hivyo. Tutaelewa. Usimfananishe na CEO wa Google etc., for NHC si Google. Au unafikiri NHC=Google kwa kuwa Sundar Pichai na Nehemia Mchechu wote ni ma-CEO?
 
siwezi kushangaa privet sector but katibu mkuu is not a ceremonial post ni mtendaji kuu wa wizara sasa unaposema umzidi kwa scheme ipi hii ya Tz. unatafuta matatizo tuu

Unafahamu lolote juu ya public sector reform ya Mkapa ?? Ambapo aliruhusu ...mashirika ya umma yanayoendeshwa kwa faida au ambayo Serikali Ina hisa kupanga scheme ZA mishahara zinazoendana NA uzalishaji/ faida NA soko la Ajira ....ilionekana kuwa kwa wakati huo kulijitokeza tatizo la watumishi wengi wasomi serikalini .....wakishakuwa na uzoefu walikuwa wanakimbilia mashirika ya binafsi ...,
Gavana wa bank kuu Kabla ya hapo alikuwa analipwa kwa scheme ya Serikali ....LAKINI kwa utaratibu mpya analipwa kutokana NA mkataba wake NA makubaliano ...NA mshahara wake utakuwa mkubwa kuliko wa waziri au Katibu Mkuu ....vile vile MTU Kama mkurugenzi wa TRA etc
 
Kwa kuwa "CEOs are highly paid people everywhere" basi yeyote mwenye hiyo title anapaswa kuwa 'highly paid" bila kujali anachofanya? Hoja iliyoko mezani ni kwamba huyu bosi wa NHC analipwa mshahara mkubwa kuliko anavyostahili au kinyume na scales za serikali etc. Majibu ya hoja hiyo hayawezi kuwa Mchechu ni kama CEO kama maCEO wengine eg. kama CEO wa Google. Mbona bosi wa Google analipwa pesa nyingi kuliko Obama? Hiyo haiwezi kuwa justification ya mshahara wa Ndugu Mchechu. Eleza, kwa nini Mchechu anastahili mshahara wa Tsh. 35 million kwa mwezi? Tuambie kwamba yeye ni alien, anatokea sayari nyingine ndio maana tunamlipa hivyo. Tutaelewa. Usimfananishe na CEO wa Google etc., for NHC si Google. Au unafikiri NHC=Google kwa kuwa Sundar Pichai na Nehemia Mchechu wote ni ma-CEO?
Anapokea mshahara mkubwa kutokana NA makubaliano NA mkataba aliofikia wakati anaajiriwa ??? Simple ....Kama alikuwa poached toka private sector alikokuwa analipwa 25 million ....unategemea ahamie NHC akalipwe milioni 2 Kama kina DC Makonda ??
Kama unaona wanaendelea kuwa naye kwa mshahara huo ujue .....bodi ya wakurugenzi wanaridhika NA huduma yake !!

Mwaka Jana kulikuwa NA Sakala la mkurugenzi wa TIC ambaye NI mtanzania aliyekuwa akifanya kazi nje ....amekaa miaka miwili hajapokea mshahara kwa kuwa walikubaliana alipwe mshahara Kama alikokuwa akifanya kazi ....walipotaka kumlipa kwa scale zao ...akagoma kuchukua salary ...HADI muafaka Ufikiwe ...sijui imefikia wapi..

Ukiwa msomi NA una uwezo wa kazi NI lazima ujiamini ....don't settle for less .....!!!!!

MTU kasoma Harvard au vyuo Classic Mfano Ada usd 50'000 kwa mwaka ...kwa miaka 3 au 4 ...Bodo masters miaka miwili ....almost Dola 600,000 higher learning hapo hujaweka primary NA secondary ........akipokea mshahara wa milioni 2 ...unafikiri Kama alichukua mkopo wa elim atalipaje....,
Unapoajiri mtu huangalii degree tu Bali PIA unaangalia exposure ....
 
Anapokea mshahara mkubwa kutokana NA makubaliano NA mkataba aliofikia wakati anaajiriwa ??? Simple ....Kama alikuwa poached toka private sector alikokuwa analipwa 25 million ....unategemea ahamie NHC akalipwe milioni 2 Kama kina DC Makonda ??
Kama unaona wanaendelea kuwa naye kwa mshahara huo ujue .....bodi ya wakurugenzi wanaridhika NA huduma yake !!

Mwaka Jana kulikuwa NA Sakala la mkurugenzi wa TIC ambaye NI mtanzania aliyekuwa akifanya kazi nje ....amekaa miaka miwili hajapokea mshahara kwa kuwa walikubaliana alipwe mshahara Kama alikokuwa akifanya kazi ....walipotaka kumlipa kwa scale zao ...akagoma kuchukua salary ...HADI muafaka Ufikiwe ...sijui imefikia wapi..

Ukiwa msomi NA una uwezo wa kazi NI lazima ujiamini ....don't settle for less .....!!!!!

MTU kasoma Harvard au vyuo Classic Mfano Ada usd 50'000 kwa mwaka ...kwa miaka 3 au 4 ...Bodo masters miaka miwili ....almost Dola 600,000 higher learning hapo hujaweka primary NA secondary ........akipokea mshahara wa milioni 2 ...unafikiri Kama alichukua mkopo wa elim atalipaje....,
Unapoajiri mtu huangalii degree tu Bali PIA unaangalia exposure ....

Bado hujasema ni kwanini Mchechu analipwa mshahara wa Tsh. 35 million na zaidi. Kama analipwa hivyo kwa kuwa kasoma Harvard au kwamba masomo yake yaligharimu pesa nyingi, just say so.

Na ni kama vile unasema Watanzania hatuna haki ya kuhoji mishahara hii, provided Bodi ya Wakurugenzi imeridhia. Au kama mkataba wake unasema alipwe hivyo. Kwani huo mkataba umeshuka kutoka mbinguni? Mimi nafikiri watu wana haki ya kuhoji mishahara ya watumishi wa umma, bila kujali watumishi hao wametokea wapi, walikuwa wanalipwa nini kabla ya kujiunga na mashirika ya umma, au wamesoma wapi. Haki ya kuhoji ni ya msingi. Na watu wanapohoji, wanatarajia majibu ya kuridhisha. Hawatarajii dharau au kubezwa: kulipwa pesa nyingi kabla ya kujiunga na shirika la umma hakufanyi mshahara wako usihojiwe. Kusoma Harvard hakumaanishi kwamba haturuhusiwi kuhoji utendaji na mshahara wako, provided umechagua kuwa mtumishi wa umma.

And we are not saying Mchechu should settle for less. We just want to know the justifications for his pay. There must be justifications behind his compensation package. Just tell us on what basis did the government decide to award him over Tsh. 35 million monthly package? Simple. The rest are just speculations.
 
bora sisi wa kwetu TRC anakula 5m lkn anaonekana ana marupurupu balaaa mpk mwez unaisha kesha kula 50m hahaha
 
wa tri anakula 5m sijui kwa nini hakuna salary scale elekez kwa maMD wote ama inategemea na unachozalisha
 
Nimekuwa nafuatilia mjadala hasa wa Rais Mtukufu bwana Magufuli kuhusu mishahara ya watumishi kuwa mikubwa.

KIMSINGI Nadhani rais ana nia njema ya kujenga moyo wa uzalendo kwa watu ili watangulize maslahi ya Taifa kwanza na yao binafsi yaje baadae.

Tatizo langu nikwamba watu wengi tumejikita zaidi kumshambulia Nehemia Mchechu CEO wa NHC. Eti tu kwa kiwango tunachokiita kikubwa cha mshahara wa M35. Wengi wetu hatuzungumzii Mchechu alikutoka alikuwa analipwa 26M.

Na alianza project ya kujenga nyumba akiwa kwenye taasisi yake ya zamani. So serikali iliona atafunika NHC zaidi kwasababu ni wazi shirika lilishakuwa kinapumulia mipira.

NHC kifupi ikishakaribia kufa Bwana Mchechu hakuomba kazi NHC serikali ilimfuata. Mchechu amefanya kazi kubwa sana NHC ukilinganisha na ilivyokuwa mwanzo. Mchechu anastahili kulipwa zaid ya hapoo.

NHC ni shirika la 3 now kwa Ubora wa mashirika ya Nyumba africa lakwanza NHS ya SA yapili Ethiopia na Tatu Tanzania. Sasa mnataka huyu kijana wa watu afanye nini? Watu wanaongea hoja ya nyumba za NHC kuwa za bei kali sio za watu wa hali ya Chini.

Thats true but we have to know kwamba Sera ya NHC haijawahi kuwa na sera hiyo ya nyumba za bei nafuu kwa watu wa Hali ya Chini. Hakuna mahala popote NHC iliwekwaa kwaajili ya kujenga makazi ya Wanyonge.

So kama kuna watu tunahitaji NHC iwe ya wanyonge ni kuwakumbusha watunga Sera wetu wakabadili sera ya NHC kuacha kujiendesha kibiashara. Mchechu hata kwa hako ka M30 anatuhurumia tuu.

Wenye vyeo kama chake huko kwenye taasisi aliyotoka sasa hivi wanakula mpaka M75. Ifike mahali tusisukumwe kwa wivu pekee juu ya Mchechu tuache wivu tumuache afanye kazi.
 
unachotaka awabembeleze sindio mchukue pesa unasema password ilipotea muambiwe pole kwa vile mnaakili. kama mnaona nyinyi ni bora kuliko hata makatibu wakuu basi kazi sana. Cha maana cha kufanya ni kutuambia kwanini ATCL wasifukuzwe au huyo mchechu anaingiza ngapi ili alipwe 35M? basi hilo tuu
Hapo ATCL pameoza na hakuna anayestahili kulipwa chochote... Sasa wewe kwa akili yako anafananisha ATCL na NHC??

Alafu nimeshauri, Mh. Rais amesema kwenye mchakato wa kufufua ATCL atafukuza wafanyakazi wote, hilo naunga mkono... Lakini akitaka hilo Shirika lisifike kokote aajiri huyo DG atakayekubali kulipwa mshahara wa Million 2 kama Makonda alafu umpe dhamana ya kuongoza Shirika lenye thamani ya Mamilioni ya Dolla....
 
Wa TZ tuachekuwa narrow-minded-people kujadili watu badala ya ideas. Kama huyu bwana ana mawazo mazuri kwa taifa kwa nini asitunzwe vizuri! Ninachofahamu mimi nhc ilianza na nyumba zilizonyanganywa kwa watu fulani na baadae kujenga nyumba zake ambazo hazikuwa na mvuto sana na sasa tunaona miji ya kisasa ya nhc. Je haya mawazo yana thamani gani? Kuna watu wengi kwenye vituo vya mabasi wanalipwa kwa kusema basi linakwenda wapi ilhali mabasi hayo yameandikwa. Mbona hamlalamikii hiyo nguvu kazi inayopotea bureeeee
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom