Gift mzalendo
JF-Expert Member
- Dec 13, 2019
- 1,006
- 1,170
Kuna "misconceptions" nyingi kuhusu chanjo ya Covid19. Baadhi za kitabibu na nyingine za elimu ya tabia. Zile za kitabibu nawaachia madaktari na wataalamu wa afya wazijibie. Mimi najibu hizi ambazo ni Socio-Cultural infuenced.
1. Chanjo ya Corona ni mpango wa wazungu kutuua?
JIBU: Wazungu wangetaka kutuua wana njia nyingi za kutumia. 90% ya madawa na vifaa tiba tunavyotumia vimetoka nje. Kuanzia MRI na CT scan ya Muhimbili, hadi dawa ya panadol pale zahanati ya Nanjilinji vimetoka kwa mabeberu. Kwanini wasitumie njia hizo ambazo ni rahisi zaidi kutumaliza badala ya chanjo ya Corona?
Hata hivyo kuna chanjo nyingi sana tunazitumia kutoka kwa hao tunaowaita mabeberu. Mtoto akizaliwa hadi anapofikisha umri wa miaka mitano anachomwa jumla ya chanjo 13 za aina tofauti. Na hakuna hata moja tunayotengeneza sisi. Zote tunapewa msaada na mabeberu. Je wangekua na nia ya kutumaliza si wangesubiri chanjo ya Corona?
2. Kwanini chanjo ya Corona inatolewa bure?
JIBU: Ni chanjo ipi inatolewa hapa nchini kwa kulipiwa? Mbona hujahoji kwanini chanjo ya pepopunda, polio, tetekuwanga, homa ya ini zinatolewa bure, badala yake unahoji chanjo ya Corona tu? Halafu pia kwanini hauulizi mbona ARVs zinatolewa bure?
Je ungetakiwa kulipia ungeweza? Au serikali yako ingeweza kukununulia? Kwa mfano dozi ya mwezi ya ARVs ni kati ya $170 hadi $220 yani kati ya shilingi laki 4 hadi laki 5. Kwahiyo kama umeathirika na VVU kila unapoenda CTC kuchukua dawa kuna "mabeberu" wamekulipia laki 4 kila mwezi. Je serikali ya Tanzania ingeambiwa ikulipie ingeweza? Same applies to Corona vaccine.
3. Kwanini tusitengeneze chanjo yetu?
JIBU: Hata mimi natamani hivyo, lakini hatuwezi kwa sababu zilezile za History ya Form 2B. Poor technology, lack of capital, poor government support etc. Kama toothpick na toilet papers tunaagiza China, je tunaweza kutengeneza chanjo ya Corona?
Serikali haijawa na nia ya dhati ya kufanya uwekezaji wa wataalamu, teknolojia, na fedha. Tukiamua tunaweza. Lakini kabla ya kufikiria kutengeneza chanjo ya Corona tujiulize nini kimetushinda kutengeneza chanjo zingine kama ya polio, tetekuwanga, homa ya ini etc? Jibu utakalolipata lihamishie kwenye Corona.
4. Chanjo ya Corona imetumia muda mfupi kupatikana kwa hiyo ni feki.
JIBU: Muda wa chanjo kupatikana sio kigezo pekee cha ubora wa chanjo. Zipo chanjo nyingi zilizopatikana kwa muda mfupi na zikaonesha ufanisi mkubwa. Chanjo ya Corona imetumia miaka miwili, lakini chanjo ya matumbwitumbwi (mumps) ilitumia miezi 11 na mpaka leo inatumika.
5. Chanjo zinazotumika Ulaya sio hizi tunazoletewa Afrika.
JIBU: Sio chanjo ya Corona tu, hata ARVs tunazotumia Afrika sio zinazotumika Ulaya. Hata Toyota unayoendesha Afrika sio Toyota inayouzwa Ulaya. Kwahiyo kama unadoubt chanjo basi doubt na ARVs unazomeza. Hata malaria kuna wanaotibiwa kwa Mseto na wengine Decotexin. Muhimu ni kuzingatia ubora na usalama wa hizo chanjo na si kulinganisha za Ulaya na hapa.
6. Kwanini tunalazimishwa tuchanje?
JIBU: Hakuna aliyelazimishwa. Chanjo ni hiyari. Wewe kama hutaki basi usimuandame aliyeamua kuchanjwa, kama ambavyo yeye hakuandami wewe uliyegoma. Muhimu tafuta taarifa za kutosha kabla hujafanya maamuzi ya kuchanjwa au kutochanjwa.
7. Chanjo zina madhara.
JIBU: Hakina dawa isiyo na madhara. Hata tangawizi na malimao ya mwendazake vina madhara. Lakini mara nyingi madhara ya dawa ni madogo kulinganisha na faida itokanayo na dawa yenyewe (unless for the very rare cases kunaweza kutokea madhara makubwa).
8. Kwanini serikali haiheshimu hisia zetu sisi tuliokataa chanjo?
JIBU: Imeheshimu ndio maana hamjalazimishwa kuchanjwa. Lakini na nyie heshimuni hisia za wale waliokubali kuchanjwa. Uhuru wako usiingilie uhuru wa mwenzako.
9. Kwanini chanjo ya Corona imekua ya kwanza kupingwa, nyingine hazikupingwa?
JIBU: Si kweli kwamba chanjo ya Corona ndio ya kwanza kupingwa. Hakuna chanjo yoyote imewahi kubuniwa ikaacha kupata upinzani. Anti Vaxxers wamekuwepo tangu enzi na enzi na hawataisha hadi Yesu arudi.
Ugonjwa wa ndui (smallpox) ulipokua tishio Edward Jenner alitengeneza chanjo mwaka 1721 wakati ambapo maelfu ya watu walikufa kwa ndui. Lakini jamii ilimpinga sana. Mchungaji Cotton Mather aliikubali chanjo hiyo na kuwashauri waumini wake waitumie. Akapata upinzani mkali na kupoteza robo tatu ya waumini wake, wakimhusisha na dhana ya Mpinga Kristo.
Lakini miaka mingi baadae dunia nzima ilikubali chanjo hiyo, na kila mtu alichomwa chanjo ya ndui. Kwahiyo hakuna jipya kwa hawa Anti Vaxxers wa Corona.
1. Chanjo ya Corona ni mpango wa wazungu kutuua?
JIBU: Wazungu wangetaka kutuua wana njia nyingi za kutumia. 90% ya madawa na vifaa tiba tunavyotumia vimetoka nje. Kuanzia MRI na CT scan ya Muhimbili, hadi dawa ya panadol pale zahanati ya Nanjilinji vimetoka kwa mabeberu. Kwanini wasitumie njia hizo ambazo ni rahisi zaidi kutumaliza badala ya chanjo ya Corona?
Hata hivyo kuna chanjo nyingi sana tunazitumia kutoka kwa hao tunaowaita mabeberu. Mtoto akizaliwa hadi anapofikisha umri wa miaka mitano anachomwa jumla ya chanjo 13 za aina tofauti. Na hakuna hata moja tunayotengeneza sisi. Zote tunapewa msaada na mabeberu. Je wangekua na nia ya kutumaliza si wangesubiri chanjo ya Corona?
2. Kwanini chanjo ya Corona inatolewa bure?
JIBU: Ni chanjo ipi inatolewa hapa nchini kwa kulipiwa? Mbona hujahoji kwanini chanjo ya pepopunda, polio, tetekuwanga, homa ya ini zinatolewa bure, badala yake unahoji chanjo ya Corona tu? Halafu pia kwanini hauulizi mbona ARVs zinatolewa bure?
Je ungetakiwa kulipia ungeweza? Au serikali yako ingeweza kukununulia? Kwa mfano dozi ya mwezi ya ARVs ni kati ya $170 hadi $220 yani kati ya shilingi laki 4 hadi laki 5. Kwahiyo kama umeathirika na VVU kila unapoenda CTC kuchukua dawa kuna "mabeberu" wamekulipia laki 4 kila mwezi. Je serikali ya Tanzania ingeambiwa ikulipie ingeweza? Same applies to Corona vaccine.
3. Kwanini tusitengeneze chanjo yetu?
JIBU: Hata mimi natamani hivyo, lakini hatuwezi kwa sababu zilezile za History ya Form 2B. Poor technology, lack of capital, poor government support etc. Kama toothpick na toilet papers tunaagiza China, je tunaweza kutengeneza chanjo ya Corona?
Serikali haijawa na nia ya dhati ya kufanya uwekezaji wa wataalamu, teknolojia, na fedha. Tukiamua tunaweza. Lakini kabla ya kufikiria kutengeneza chanjo ya Corona tujiulize nini kimetushinda kutengeneza chanjo zingine kama ya polio, tetekuwanga, homa ya ini etc? Jibu utakalolipata lihamishie kwenye Corona.
4. Chanjo ya Corona imetumia muda mfupi kupatikana kwa hiyo ni feki.
JIBU: Muda wa chanjo kupatikana sio kigezo pekee cha ubora wa chanjo. Zipo chanjo nyingi zilizopatikana kwa muda mfupi na zikaonesha ufanisi mkubwa. Chanjo ya Corona imetumia miaka miwili, lakini chanjo ya matumbwitumbwi (mumps) ilitumia miezi 11 na mpaka leo inatumika.
5. Chanjo zinazotumika Ulaya sio hizi tunazoletewa Afrika.
JIBU: Sio chanjo ya Corona tu, hata ARVs tunazotumia Afrika sio zinazotumika Ulaya. Hata Toyota unayoendesha Afrika sio Toyota inayouzwa Ulaya. Kwahiyo kama unadoubt chanjo basi doubt na ARVs unazomeza. Hata malaria kuna wanaotibiwa kwa Mseto na wengine Decotexin. Muhimu ni kuzingatia ubora na usalama wa hizo chanjo na si kulinganisha za Ulaya na hapa.
6. Kwanini tunalazimishwa tuchanje?
JIBU: Hakuna aliyelazimishwa. Chanjo ni hiyari. Wewe kama hutaki basi usimuandame aliyeamua kuchanjwa, kama ambavyo yeye hakuandami wewe uliyegoma. Muhimu tafuta taarifa za kutosha kabla hujafanya maamuzi ya kuchanjwa au kutochanjwa.
7. Chanjo zina madhara.
JIBU: Hakina dawa isiyo na madhara. Hata tangawizi na malimao ya mwendazake vina madhara. Lakini mara nyingi madhara ya dawa ni madogo kulinganisha na faida itokanayo na dawa yenyewe (unless for the very rare cases kunaweza kutokea madhara makubwa).
8. Kwanini serikali haiheshimu hisia zetu sisi tuliokataa chanjo?
JIBU: Imeheshimu ndio maana hamjalazimishwa kuchanjwa. Lakini na nyie heshimuni hisia za wale waliokubali kuchanjwa. Uhuru wako usiingilie uhuru wa mwenzako.
9. Kwanini chanjo ya Corona imekua ya kwanza kupingwa, nyingine hazikupingwa?
JIBU: Si kweli kwamba chanjo ya Corona ndio ya kwanza kupingwa. Hakuna chanjo yoyote imewahi kubuniwa ikaacha kupata upinzani. Anti Vaxxers wamekuwepo tangu enzi na enzi na hawataisha hadi Yesu arudi.
Ugonjwa wa ndui (smallpox) ulipokua tishio Edward Jenner alitengeneza chanjo mwaka 1721 wakati ambapo maelfu ya watu walikufa kwa ndui. Lakini jamii ilimpinga sana. Mchungaji Cotton Mather aliikubali chanjo hiyo na kuwashauri waumini wake waitumie. Akapata upinzani mkali na kupoteza robo tatu ya waumini wake, wakimhusisha na dhana ya Mpinga Kristo.
Lakini miaka mingi baadae dunia nzima ilikubali chanjo hiyo, na kila mtu alichomwa chanjo ya ndui. Kwahiyo hakuna jipya kwa hawa Anti Vaxxers wa Corona.