Tatizo ni ubabe wa watendaji serikalini kutotaka kulipa madeni sio tu ya nje bali hata ya ndani. Mfano Katibu Mkuu Kiongozi alimuandikia barua Katibu Mkuu Wizara Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano tarehe 22/01/2019 akimuamuru alipe madai ya wastaafu ATCL ya PSSSF ( PPF) lakini hadi hi Novemba, 2019 hakuna alicholipa. Hii inadhihirisha umwamba wa viongozi serikalini wa kutotii mamlaka na kufanya yao au kwa kufuata maelekezo ya mkuu wa kaya.
Kama wastaafu ATCL wangekuwa wanaishi nje ya nchi naona nao wangepeleka suala hili mahakama za huko nje ili ndege zikamatwe kwani kuhusu suala hili shirika la PPF waliipeleka ATCL mahakamani hapa nchini na kuamriwa kukamata mali za ATCL na kuzinadi hali iliyopelekea Katibu mkuu Uchuku, Ujenzi na mawasiliano kuingilia kati na kuahidi kulipa kitu ambacho haja tekeleza hadi leo. Huu ndio ubabe wa wenye dhamana serikalini na ndio unaleta haya matatizo.
Kama wastaafu ATCL wangekuwa wanaishi nje ya nchi naona nao wangepeleka suala hili mahakama za huko nje ili ndege zikamatwe kwani kuhusu suala hili shirika la PPF waliipeleka ATCL mahakamani hapa nchini na kuamriwa kukamata mali za ATCL na kuzinadi hali iliyopelekea Katibu mkuu Uchuku, Ujenzi na mawasiliano kuingilia kati na kuahidi kulipa kitu ambacho haja tekeleza hadi leo. Huu ndio ubabe wa wenye dhamana serikalini na ndio unaleta haya matatizo.