TTCL fiber na Voda Supakasi ipi yafaa kwa matumizi ya home intaneti?

Chief nataka niunge T-Office Standard ya TTCL, ina 8Mbps kwa 1Mbps. Hii itafaa kweli? Waya upo wanauita FTTH, hapa nanunua modem kwa 55,000 na kufurushi 50,000

Nilitaka ni opt kwa fiber ila iko umbali wa kama mita 250 kutoka home hapa,

Niende na hiyo hiyo t-office, speed yake ikoje?
Hio ya 8mbps kwa 1mbps ni Adsl, kama huna option nyengine si mbaya, itafanya mambo ya kawaida vizuri.

Ila kama Fiber ipo na Gharama ya kuunga si kubwa chukua Fiber, utapata 20mbps download na 10mbps upload kwa hio 50,000.
 
Hio ya 8mbps kwa 1mbps ni Adsl, kama huna option nyengine si mbaya, itafanya mambo ya kawaida vizuri.

Ila kama Fiber ipo na Gharama ya kuunga si kubwa chukua Fiber, utapata 20mbps download na 10mbps upload kwa hio 50,000.
Asante chief, nimewaza pia hiyo 1Mbps ya upload ndi ndogo mno. Nasubiri wanitumie gharama ya fiber. Ipo umbali wa kama 250m sijajja itakua kiasi gani

Ila in the long run nadhan fiber itakua investment bora,
 
Asante chief, nimewaza pia hiyo 1Mbps ya upload ndi ndogo mno. Nasubiri wanitumie gharama ya fiber. Ipo umbali wa kama 250m sijajja itakua kiasi gani

Ila in the long run nadhan fiber itakua investment bora,
Kweli kabisa mkuu.

1mbps upload kwa matumizi ya kawaida kuangalia youtube, Netflix, kuperuzi, download za hapa na pale haina neno.

Ila kama unafanya Video calling, youtuber and developer unaye upload mara kwa mara, mambo ya p2p kama Torrent etc itazingua.
 
Kweli kabisa mkuu.

1mbps upload kwa matumizi ya kawaida kuangalia youtube, Netflix, kuperuzi, download za hapa na pale haina neno.

Ila kama unafanya Video calling, youtuber and developer unaye upload mara kwa mara, mambo ya p2p kama Torrent etc itazingua.
Nimekupata chief
 
me nlijiunga kifurushi cha 50k cha ttcl speed ilikuwa nzuri tu kilivyoisha nmejiunga tena cha50k speed imepungua na saingine haifanyi kazi kabisa shida inaweza kuwa nini
 
me nlijiunga kifurushi cha 50k cha ttcl speed ilikuwa nzuri tu kilivyoisha nmejiunga tena cha50k speed imepungua na saingine haifanyi kazi kabisa shida inaweza kuwa nini
Unatakiwa ku restart router, wasiliana na aliekuja kukufungia kama kasave configuration ili usije kupoteza data zako.

Unaingia menu ya router, most of time ni 192.168.1.1 unaandika hio adress kwenye browser na hakikisha upo connected na TTCL yako.

Ukishaingia itakuja sehemu ya Login, user ni admin na pass ni admin, login ingia ndani.

Juu utakuta menu mbalimbali angalia juu kulia kumeandikwa maintenace click hapo.

Chini kushoto utaona neno Reboot, click hapo then click tena reboot itakupa sekunde 64 za kujizima na kuwasha, itawaka ikiwa full speed.

Ni kawaida ya adsl kuzimwa na kuwashwa kila baada ya siku kadhaa, Ni analog hio.

Sema hakikisha unamuuliza jamaa aliekufungia router kama alisave config.
 
Unatakiwa ku restart router, wasiliana na aliekuja kukufungia kama kasave configuration ili usije kupoteza data zako.

Unaingia menu ya router, most of time ni 192.168.1.1 unaandika hio adress kwenye browser na hakikisha upo connected na TTCL yako.

Ukishaingia itakuja sehemu ya Login, user ni admin na pass ni admin, login ingia ndani.

Juu utakuta menu mbalimbali angalia juu kulia kumeandikwa maintenace click hapo.

Chini kushoto utaona neno Reboot, click hapo then click tena reboot itakupa sekunde 64 za kujizima na kuwasha, itawaka ikiwa full speed.

Ni kawaida ya adsl kuzimwa na kuwashwa kila baada ya siku kadhaa, Ni analog hio.

Sema hakikisha unamuuliza jamaa aliekufungia router kama alisave config.
shukran sana mkuu
 
Kuna wadau hapa wa Ateb Technologies wanaounganisha internet. Je kuna aliyeunga atupe mrejesho?
Nimeona tangazo lao
JamiiForums444183742.jpg


Sent from my SM-G935T using JamiiForums mobile app
 
Coverage?
Habari ndugu..!!

Karibu Katika kampuni pendwa ambayo imekuwa ikitoa huduma ya internet majumbani pamoja na offisini kwa bei Nafuu kabisa.

Ateb technology tunatoa internet yenye spend na kasi ya Hali ya juu ambayo itakuwezesha ku browse na kutumia electronic device Kama kompyuta simu na camera ..!!

Tuna Toa 5mps kwa nyumbani ambayo utaweza ku browse YouTube, video games online, na mambo mengine mengi we we pamoja na familia yako na ndugu zako mkubwa nyumbani

5mbs =100,000/- amabayo utalipa kwa mwezi

Installation cost ni 200,000/- amabyo Italipwa Mara moja.
Larkin pia tunatoa Huduma za internet ua maofisini mpaka MBPS 100 na ni dedicated
Na hii Huduma tunatoa kwa dar na dodoma

Tunapatikana pssf tower
Opposite na Mlimani city
0657451090
0766231496
Karibuni sana
Maelezo haya hapa mkuu kwa niaba ya member Elieza Msuya
 
Kwa aliyetumia kasi internet ya Vodacom, 37GB za high speed zikikata, speed inashuka mpaka ngapi kwa package ya 50000 unlimited?
 
Hii kitu inaukweli wowote wadau
 

Attachments

  • Screenshot_2022-06-12-13-42-58-66.png
    Screenshot_2022-06-12-13-42-58-66.png
    448.8 KB · Views: 72
Back
Top Bottom