Trust katika Mahusiano


Hata ukimkuta Juma/Amina njiani bora useme kama mlikutana na kuzungumza zaidi ya salam tu

Bora ajue unamwambia ukweli japo hampendi hiyo rafiki, kuliko kuonekana unaficha ficha
 

FP katika mahusiano kuna masuala really serious... Ila mwisho wa siku unaweza ishia kucheka. Lol!

BTW kuna watu ni waongo hadi baas! Hata watoto wenyewe ndani; unaweza kuta mtoto wako ambaye constantly yeye majibu yake muongo kwa vitu vidogo dogo hata hastahili kuongopa - sasa huyu katika mahusiano kimbembe...

Asante kwa mada yako relevant.
 
Hahahaaaaaa!!! Leo sijui FP umeamkia wapi dada yangu?
Vipi dada unaenda kwa shangazi au kwa kaka?

Back to topic.
Uaminifu umekuwa ni kitu hadimu sana katika maisha yetu ya kila siku. Ni watu wachache sana ambao katika maneno yatokayo mdomoni mwao kila neno huwa la kweli. Watu tumekua na udanganyifu katika maisha yetu ya kila siku, hii inatokana na jinsi tulivyojichagulia kuishi.

Binafsi nimekua mdanganyifu pale ninapoona mambo yanakuwa magumu, ila naamini sio mimi tu, tupo wengi wenye tabia hii ya udanganyifu.

Mfano:Mmeahidiana na Boss wako mkutane mahali fulani kwaajili ya kitu fulani, ila muda unakwenda halafu unakuta Boss amefika kabla yako na anapokupigia simu kukuuliza uko wapi? Unamjinu upo maeneo ya karibu na pale mlipoahidiana mkutane, wakati unawezakuta hiyo simu aliyokupigia Boss wao ndo imekukumbusha kwamba mlikua na appointment.

Hapo tunaona udanganyifu unaweza kukusaidia kufanikisha dhumuni mlilokuwa mnataka mlikamilishe au inaweza kukufanya upoteze uhusiano mzuri na wenzako pale utakapomdanyanya na akakusubiri kwa kipindi kirefu nila wewe kutokea.

Tumuomba Mungu atuomdolee tabia ya udanganyifu akilini mwetu huku nasi tukihjitahidi kujifunza kusema kweli ambayo itatuweka huru.
 
Last edited by a moderator:
na wewe kila siku nakuambiaga sisi wengine sayansi ilitutupa mkono tangu tunazaliwa sasa hapo kwenye RED umeandika nini? najua huwezi kunitusi, lol! mwenzio ukiona naandika mada kama hizi ujue kuna kitu kinanikula akili yangu.... si unajua mimi mama ushauri? sasa nikipataga kesi ambazo ninanikosesha usingizi ndo matokeo yake yanakuwa hivi.
kiukweli hakuna kitu kinachoniuma sana kama kuhisi nimedanganywa........ you know me, ni mwelewa sana, inapotokea hata mwanangu tu anidanganye huwa naumia sana, najiuliza maswali mengi, hivi kanionaje?
 
nilikuelewa rafiki, nikakukatia kiu tu, hakuna la zaidi
 
hapo ndo point yangu dada mdogo, na ndo kitu kinachouma zaidi. mtu anajua kabisa kuwa nikimwambia hivi atanielewa, kwa nini useme uongo? kuna ajenda gani hapo mpaka useme uongo? hapa sasa ndo inakuja ile dhana ya Baba_Enock kuwa inawezekana unadanganya sababu una mpango mwingine, tofauti kabisa na haya unayoyasema
 
Last edited by a moderator:
Kwa ujumla uongo sio kitu kizuri na hakuna anaependa kudanganywa au kudanganya . Naona AshaDii amejaribu kuzungumzia uhalisia au mazingira yanayopelekea mtu kusema uongo. Tunapoishi pamoja tunajuana mapungufu yetu na wakati mwingine nini hapendi/anapenda mwenzangu. Au una avoid hofu na kumvunja moyo mwenzio . kiukweli kudanganya/kudanganywa hakupendezi na ikumbukwe kuwa si kila wakati unapaswa kusema ukweli yapasa uzingatie mazingira na hisia za mwenzio.
 
Simpendi mtu mwongo kabisa hasa katika mahusiano.
Na kwa bahati mbaya ni rahisi kujua "huyu amenidanganya". Usipokuwa mwaminifu kwa mambo madogo makubwa je?
I can stand mpenzi wangu anitukane akiwa na hasira lakini siyo kunidanganya.
ha haaaa, nimekuelewa sana mtani. mimi pia sipendi uongo. nyumbani kwangu tunaambiana nataka kufanya hili, kama mwenzio hataki anakuambia usifanye na anakupa sababu kwa nini usifanye, mkielewana yanaishia hapo (itategemea nani atashinda katika maongezi yenu).
Mtu akinidanganya naona ananiona mimi mjinga, I can't think/ I don't understand...... yaani hawezi niambia kitu nikaelewa, ndo maana anaona dawa yake ni kunidanganya tu. I can stand mtu akinidanganya jambo lenye tija..... for God's sake husband hawezi niambia ukweli kuwa ana mpango wa kando, lazima adanganye.... nikimbamba kwa hilo nitaelewa kuwa hakupaswa kusema ukweli, alipaswa kunidanganya. hapo atasema kilichomsibu na kuomba msamaha.
cc. Kaizer, Dark City, Asprin, BAK, The Boss, KakaKiiza, Arushaone, Baba V
 
Last edited by a moderator:
Nadhan ukiwa na mtu mwenye mawivu ivi vtu vinakuwepo kupunguza maugomvi .hata mimi huwa nadanganya coz my bf anamaswali ya kero yanayopelekea tugombane.et"kila cku kwa aunt yako mnaendaga kuongea nini"mtu wa ivi lazma udanganywe cjui hamjiamini yan mnakera ndo sababu.
 
mimi mdada wangu ananayenisaidia home!uuuuuuuwih!anadanganya kila kitu!anaweza akaulizwa uko chumbani hachelewi kusema alitaka kwenda maliwato!eheehehhehhehe nishamzoea lakini hii tabia inanikera sana kwa kweli!zitu vingine yuko poa hadi raha!ila mwongo jamani! uuuuuuwih!sijui nafanyaje!
 
Halafu hii ya kuaga unaenda kwa shangazi kumbe unaenda kwa dada sio nzuri kabisa kiufupi uongo si kitu chema na ukisha kosa uaminifu ni vigumu sana mtu kukuamini tena hata kama siku nyingine utasema ukweli. Hasa kwenye mahusiano ndio mbaya kabisa
 
Unapoamua kusema uongo, mara nyingi unajaribu kutokumuudhi mwenzako kwa suala ambalo unajua hapendezwi nalo. Unakuwa unajua kwamba ukimwambia ukweli .. kwa kitu ambacho hapendi ataudhika, hivyo unadanganya. lakini madhara ya uongo ni makubwa zaidi kuliko kama ungemweleza ukweli, ingawaje pia angechukia.
 

@FP,

Hakuna mtu anayesema uongo bila ya kuwa na sababu...No, NEVER...!

Halafu pia, ni vigumu sana "kusoma ubongo" wa mtu mwingine, so, swali la "kufikiri" kuwa "x" nikimwambia hivi "atanielewa" siyo kweli hata kidogo. Na ndiyo maana unachoita "mambo ya kawaida", si sawa, hakuna "mambo ya kawaida".

Uongo mwingine unatengenezwa na mazoea katika mahusiano, na ni vizuri uwepo ili "kupitisha siku"...!

"Chakula tayari"? haiwezi kujibiwa na kauli ya "bado"....!
"Upo wapi"? haiwezi kujibiwa na kauli ya "nipo gesti hausi"...!
"Unafanya nini"? haiwezi kujibiwa na kauli ya "nina-do"...!
"Watoto wameshakula"? haiwezi kujibiwa na kauli ya "bado"...!

Kuna swali ambalo unaulizwa, na unajibu bila hata kufikiria, kwa maana unafahamu yule aliyekuuliza anataka jibu gani...!
 
ha haaa, nimekupata saaana mdogo wangu, hapo sasa.....
hebu fikiria sasa hapo shostito kama huyo utamweka katika kundi gani? anafaa au ndo wa kumwaga tu!
hivi cacico bado ananyonyesha? kawa adimu sana siku hizi mitaa hii
 
Last edited by a moderator:
Umenikumbusha mbali nilikua na mdada wa kazi bwana alikua muongo hata umbambe na kitu mkononi atakudanganya tu. Uzuri alikua mchapa kazi sana n aliwapenda sana wanangu .
 
Hata ukimkuta Juma/Amina njiani bora useme kama mlikutana na kuzungumza zaidi ya salam tu

Bora ajue unamwambia ukweli japo hampendi hiyo rafiki, kuliko kuonekana unaficha ficha
ha haaa, hiyo kali.....
kuna mkaka alipigwa kwara na mkewe asionane na mimi. mimi nikamwambia kwa kweli naheshimu sana ndoa za watu, mimi nawe hatuna chochote kitakachoharibika kama hatutakutana, nikamwambia tusionane tangu hiyo siku. Kuna siku tulionana barabarani na tukasalimiana, sasa sijui alienda mwambia mkewe kuwa tulionana? lol!
 
Reactions: BAK
ha haaa, hapo kwenye watoto ndo usiseme my dear, yaani ni majanga........
mimi huwa nasema tu mmmmmmmmhhhhhhhhhhh na jicho nimemkazia, utasikia Nimedanganya, lol!
 
ha haaa, nimekupata saaana mdogo wangu, hapo sasa.....
hebu fikiria sasa hapo shostito kama huyo utamweka katika kundi gani? anafaa au ndo wa kumwaga tu!
hivi cacico bado ananyonyesha? kawa adimu sana siku hizi mitaa hii

AH!kunyonyesha huko ananyonyesha kituo!
atupishe kule!hebu aje hapa!
ish kwani hapa mbn kama nna hasira sana!
we mke mwenza hebu kuja huku!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…