Trust katika Mahusiano

Trust katika Mahusiano

Fixed Point

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2009
Posts
11,304
Reaction score
12,753
Poleni na majukumu wanaMMU...

Leo hili jambo la trust kwenye mahusiano limekuwa likijirudiarudia sana katika kichwa changu. Mahusiano mengi sana yanavunjika sababu ya kukosa uaminifu. Kuna vitu vingi nimekuwa nikijiuliza na kujijibu na vingine kukosa kabisa majibu. Kwa mtazamo wangu UAMINIFU ni jambo muhimu sana katika mahusiano. Mara nyingi napenda sana niwe katika hali ambayo namuamini mpenzi wangu, pia napenda sana kwa gharama yoyote ile kumfanya mpenzi wangu aniamini. Kama nikigundua ana wasiwasi na kitu ninachomwambia huwa najitahidi kumwuliza aniambie nifanye nini ili aniamini sababu sipendi akae akiwa na wasiwasi, na ukweli nitafanya hicho kitu ili tu aridhike.

Inawezekana mimi nipo complicated kidogo, huwa napenda sana mtu aniambie ukweli hata kama ni mbaya kiasi gani. Kwa kuujua ukweli nakuwa na uhuru wa nini la kufanya baada ya hapo.... kukusamehe na kuendelea na mahusiano au kukusamehe na kusitisha mahusiano (kusamehe kwangu huwa siyo option, lazima nisamehe ili niweze kuendelea na mambo yangu mengine).

Katika huu uzi nitazungumzia sana uaminifu wa mambo ya kawaida tu, siyo kutoka nje ya mahusiano (cheating). Utakuta sometimes mtu anaamua tu kudanganya kwa sababu yoyote anayoijua. Kwa mfano mtu anamwambia mpenzi wake naenda sokoni wakati anaenda salon, au naenda kwa dada wakati anaenda kwa shangazi.

Hivi ikatokea ndo upo kwa shangazi halafu dada akaja nyumbani kukuulizia wakati wewe uliaga kwenda kwa dada itakuwaje? hata kama kweli mpenzi ataamini kuwa ulikuwa kwa shangazi, utakuwa umejenga hisia gani kwake kuhusu wewe? kwa nini umdanganye?
Wenzangu mnalizungumziaje hili?

Karibuni kwa mjadala
 
FP Huo sasa ni Uongo wa ajabu we unaenda saloon unasema unaenda sokoni?
unaogopa kusema kweli utadhani ni dhambi?

Mie najua uaminifu mwingi unakuwa mgumu kwenye mahusiano ya mapenzi ndo hapo watu wanadanganya
Ila ngoja nipate lunch huku natafakari ili nipate Point za kuweka hapo
NB:Ukimuona @MJ1 msalimie sana
 
Last edited by a moderator:
Kuna mwingine anadanganya kwenye simu tena bila aibu yupo kwenye dala dala anakuja ubungo utasikia niko kariakoo kumbe yupo mbagaraa
hili hapa pia nilitaka kuliandika ila sasa nikaona hadithi itakuwa ndefu sana na kuwachosha wasomaji.
mwingine yupo kwenye basi la Iringa tena mmeshapita Morogoro anasema yupo njiani anaelekea Tanga......

Nilishasema sisemi uongo usio na tija, maana nikikudanganya ni sign kwamba nakuogopa; so kama kungekuwa na uwezekano wa kumdanganya Mungu (ninayemuogopa) huenda ningefanya hivyo lakini there is now way naweza mdanganya yeye anijuaye kuliko ninavyojijua mwenyewe. Hivyo sioni na sitakaa kuona umuhimu wa uongo uso na faida. halafu kwenye mahusiano, mimi naamini ni vyema mtu akujue tangia mapema udhaifu na mapungufu yako ili afanye informed decision lakini pia inakusaidia wewe usiishi maisha ya kupretend.
ha haaa, siku moja nimemwambia hubby naenda disco na rafiki zangu, wakati huo yeye alisafiri. basi usiku wa manane tunajirusha zetu hubby anapigiwa simu "namwona shem hapa ........ upo naye?" Imagine ningekuwa sijaaga ingekuwaje?
 
Nilishasema sisemi uongo usio na tija, maana nikikudanganya ni sign kwamba nakuogopa; so kama kungekuwa na uwezekano wa kumdanganya Mungu (ninayemuogopa) huenda ningefanya hivyo lakini there is now way naweza mdanganya yeye anijuaye kuliko ninavyojijua mwenyewe.

Hivyo sioni na sitakaa kuona umuhimu wa uongo uso na faida. halafu kwenye mahusiano, mimi naamini ni vyema mtu akujue tangia mapema udhaifu na mapungufu yako ili afanye informed decision lakini pia inakusaidia wewe usiishi maisha ya kupretend.
 
Da Mkubwa @FP........... mada nzuri sana. Ninaomba kusema kitu kimoja tu, inapofikia mtu anamdanganya mpenzi wake kwa mambo ya kawaida kama uliyoyataja hapo juu jua kuwa tatizo linawezakuwa kwa mpenzi wake ambaye pengine sio mwelewa. Mara nyingi unapokuwa na mtu ambaye sio mwelewa, mwenye wivu na mafikra yake na ambaye anaamini kila akiwazacho yeye ndio sahihi, basi mahusiano huwa magumu sana hata ufanyeje kumu-assure inakuwa kazi bure. Mie nakumbuka niliskhawahi kuwa na mtu ambaye for no reason aliamua tu nisiwe nakwenda nyumbani kwetu kusalimia. Yaani bila kuambiwa kuwa kuna mgonjwa basi hakuna kwenda na hata ukimwelewesha vipi ukienda ukirudi ni ugomvi. Mwishowe nlijikuta kila mara nilitamani kumsalimia mamangu, natafuta mtu wa kumwuuguza..leo baba anaumwa, kesho mama hajisikii vizuri kesho kutwa mdogo wangu ni mgonjwa mpaka pale nilipoamua basi kama n'mbwai nmbwai....ntawauguza mpaka lini. Ikafika tu mahali nkawa namwambia leo nakwenda msalimia mama, akiprotest bado ninakwenda ila ndio najiandaa na vagi la kufa mtu......................
 
Nilishasema sisemi uongo usio na tija, maana nikikudanganya ni sign kwamba nakuogopa; so kama kungekuwa na uwezekano wa kumdanganya Mungu (ninayemuogopa) huenda ningefanya hivyo lakini there is now way naweza mdanganya yeye anijuaye kuliko ninavyojijua mwenyewe.

Hivyo sioni na sitakaa kuona umuhimu wa uongo uso na faida. halafu kwenye mahusiano, mimi naamini ni vyema mtu akujue tangia mapema udhaifu na mapungufu yako ili afanye informed decision lakini pia inakusaidia wewe usiishi maisha ya kupretend.

Kweli Kaunga, huo uongo anaoongelea FP hauna tija kabisa....

Ila nilishasema kwamba, uongo mtakatifu au kutosema baadhi ya mambo ni vitu vya muhimu na haviepukiki katika mahusiano.

Mfano, kwa nini umweleze mpenzi wako kwamba umekutana na ex-BF/GF mahali wakati unajua itamuumiza?

Kwa nini umweleze kuwa utapita kwa rafiki yako John/Amina wakati unajua hampendi?

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
Da Mkubwa @FP........... mada nzuri sana. Ninaomba kusema kitu kimoja tu, inapofikia mtu anamdanganya mpenzi wake kwa mambo ya kawaida kama uliyoyataja hapo juu jua kuwa tatizo linawezakuwa kwa mpenzi wake ambaye pengine sio mwelewa. Mara nyingi unapokuwa na mtu ambaye sio mwelewa, mwenye wivu na mafikra yake na ambaye anaamini kila akiwazacho yeye ndio sahihi, basi mahusiano huwa magumu sana hata ufanyeje kumu-assure inakuwa kazi bure. Mie nakumbuka niliskhawahi kuwa na mtu ambaye for no reason aliamua tu nisiwe nakwenda nyumbani kwetu kusalimia. Yaani bila kuambiwa kuwa kuna mgonjwa basi hakuna kwenda na hata ukimwelewesha vipi ukienda ukirudi ni ugomvi. Mwishowe nlijikuta kila mara nilitamani kumsalimia mamangu, natafuta mtu wa kumwuuguza..leo baba anaumwa, kesho mama hajisikii vizuri kesho kutwa mdogo wangu ni mgonjwa mpaka pale nilipoamua basi kama n'mbwai nmbwai....ntawauguza mpaka lini. Ikafika tu mahali nkawa namwambia leo nakwenda msalimia mama, akiprotest bado ninakwenda ila ndio najiandaa na vagi la kufa mtu......................
Da Mdogo MJ1, kwanza salamu zako sana toka kwa FirstLady1 hapo juu.... ujue tunakumiss sana......
nakubaliana kabisa na wewe hapo kwenye RED, kama si mwelewa........
Vipi kama mwenzio ni mwelewa? unakuwa unamkinga na nini kwa kumdanganya?
 
Last edited by a moderator:
ha haaa, siku moja nimemwambia hubby naenda disco na rafiki zangu, wakati huo yeye alisafiri. basi usiku wa manane tunajirusha zetu hubby anapigiwa simu "namwona shem hapa ........ upo naye?" Imagine ningekuwa sijaaga ingekuwaje?

Umeona eeh, yaani ukweli unakuweka huru kabisa yaani. Hii ilitokea nilienda Bujumbura na rafiki zangu, mmoja wa rafiki ni mume wa rafiki yangu. Badi baada ya muda, shosti wangu anaambiwa, Kaunga alienda kuspend weekend na mumeo...Yaani tulicheka tu, maana hakujua kazi yangu kule Buja ilikuwa ni pamoja na kukaba hadi penati ili watoto wa kitusi, wasipate nafasi; ingawa ilinicost maana naye alinikaba nisizile za mapedejee wa kikongo. LOL
 
Hakuna mtu ambae hapendi trust kati ya mahusiano. Kila mmoja anapenda siku zote aambiwe ukweli. Upande wa mahusiano kutokuwepo na trust (nazungumza strictly nje ya) husababishwa na aidha mtu wako mwenyewe ama wewe mwenyewe. Kuna mwingine kweli anaweza sema anapenda awe anaambiwa ukweli no matter what! Cha ajabu ukweli ukitoka hapo si Drama hiyo itakayofuata - Kiasi kwamba huyo mtu anajuta anaona heri kuongopa. Take note sihalalishi kukosekana kwa uaminifu, ila najaribu kueleza why kwa wengine hua hawawi waaminifu.

Kikubwa cha kuelewa mahala ambapo hakuna trust ni ‘Kwa nini huyo mtu asiwe wazi na aongope katika suala ambalo ni la kawaida?"

Kukosekana kwa uaminifu kwa misingi ya wewe (ulie mpenzi wake)

Mara nyingi kuna masuala ambayo kimsingi ukiyaangalia yanaonekana madogo sana. Kama mfano uliotoa kwa kujifanya waenda Sokoni na hali waenda Salon. Hapo ni wazi kuwa sababu kubwa moja wapo inaweza kuwa huyo mwanamke huwa na matumizi makubwa na kuwa moja ya eneo ambayo anatumia sana pesa ni Saloon. Na wajua siye wanawake, kuna style inakuhiraji uende Saloon walau mara tatu kwa wiki. Inapotokea J/2 ulienda Saloon, J/5 ulienda Saloon na Leo Ijumaa unataka kwenda Saaloon na pengine ulishawahi ongea na mtu wako safari za Saloon zipungue (or hata hamjawahi ongea but wajishuku); the safest unaweza kuaga ni kuwa unaenda Sokoni badala ya Saloon.

Yes kaongopa it's a bad thing, but ukiliangalia kwa upande mwingine unatkuta anaongopa tokana na kuwa Mpenzi wake kamuona si mwelewa, ama tu hataji kuonyesha ni to what extent hilo tendo la Saloon limepewa kipaumbele na the like.
Uongo wa disaini hii kati ya wapenzi wengi hauepkiki.

Kukosekana kwa uaminifu kwa misingi ya mpenzi wako

Kuna wengine siku zote wao kuongopa ama kutokuwa wazi ni hulka yao… Tena pengine inasukumwa saana na selfishness.. Kutotaka ajue vitu vyote anavyomiliki, Kutoka ajue wapi hua anaenda, kutoka ujue tu kwa sababu yoyote ile! Na mara nyingi pia pamoja na kuwa cheating imetolewa katika kuelewa kukosekana kwa uaminifu wa hivi – Mara nyingi cheating ndiyo sababu kubwa sana ya wapenzi kuwa waongo kwa wenza/partners wao.

Mfano kama mliwahi gombana kwa ajili ya mtu uliyemhisi ana interest na huyo mtu anafanya Hotel Magongo, siku akiwa Hotel Magongo si rahisi kusema kuwa yupo hapo. Ama anapokuwekea silent simu ama kutoweza kupokea sababu yupo faragha na mpango wa kando akipokea hawezi sema nilikuwa faragha, atasema lingine lolote ambalo mpenzi wake atalikubali bila shida.
 
Kweli Kaunga, huo uongo anaoongelea FP hauna tija kabisa....

Ila nilishasema kwamba, uongo mtakatifu au kutosema baadhi ya mambo ni vitu vya muhimu na haviepukiki katika mahusiano.

Mfano, kwa nini umweleze mpenzi wako kwamba umekutana na ex-BF/GF mahali wakati unajua itamuumiza?

Kwa nini umweleze kuwa utapita kwa rafiki yako John/Amina wakati unajua hampendi?

Babu DC!!

Yes kuna kweli zingine ni very unpleasant au damaging. Mzazi mwenzangu aliniambiaga baada ya kuona jinsi gani nilivyohonest kuwa "kutosema ukweli wote hakumaanishi unasema uongo", so kwa couple sio vizuri kudig sana past za mtu maana waweza sababisha akudanganye kwa ajili ya kuprotect relationship yenu. Kuna vitu kama mtoto ni muhimu kuuliza lakini sijui umeshatembea na wanawake wangapi it is irrelevant IMO.
 
Kweli Kaunga, huo uongo anaoongelea FP hauna tija kabisa....

Ila nilishasema kwamba, uongo mtakatifu au kutosema baadhi ya mambo ni vitu vya muhimu na haviepukiki katika mahusiano.

Mfano, kwa nini umweleze mpenzi wako kwamba umekutana na ex-BF/GF mahali wakati unajua itamuumiza?

Kwa nini umweleze kuwa utapita kwa rafiki yako John/Amina wakati unajua hampendi?

Babu DC!!
ha haaa, babu huo uongo usio na tija ndo haswa ninaotamani kuujadili hapa.....
unajua tunaweza ona hauna tija lakini labda sababu za huo uongo zina tija..... ndo maana nauliza kwa nini uuseme huo uongo ambao unaonekana kabisa hauna tija?
kama mwenzio hapendi wewe uonane na John, unadanganya na unaenda kumwona John, akigundua ulienda kumwona itakuwaje?
 
Umeona eeh, yaani ukweli unakuweka huru kabisa yaani. Hii ilitokea nilienda Bujumbura na rafiki zangu, mmoja wa rafiki ni mume wa rafiki yangu. Badi baada ya muda, shosti wangu anaambiwa, Kaunga alienda kuspend weekend na mumeo...Yaani tulicheka tu, maana hakujua kazi yangu kule Buja ilikuwa ni pamoja na kukaba hadi penati ili watoto wa kitusi, wasipate nafasi; ingawa ilinicost maana naye alinikaba nisizile za mapedejee wa kikongo. LOL
ha haaaa, mlikosa wote, ndo cost ya urafiki hiyo.......
hilo zali lilishawahi kunitokea ila naomba nisilisimulie hapa, lol!
 
Yes kuna kweli zingine ni very unpleasant au damaging. Mzazi mwenzangu aliniambiaga baada ya kuona jinsi gani nilivyohonest kuwa "kutosema ukweli wote hakumaanishi unasema uongo", so kwa couple sio vizuri kudig sana past za mtu maana waweza sababisha akudanganye kwa ajili ya kuprotect relationship yenu. Kuna vitu kama mtoto ni muhimu kuuliza lakini sijui umeshatembea na wanawake wangapi it is irrelevant IMO.

Hilo swali kama kuna mwanamume haulizi basi huyo kabarikiwa....

Ila mwisho wake huwaumiza sana rohoni....from the man's perspective..!

Babu DC!1
 
ha haaa, babu huo uongo usio na tija ndo haswa ninaotamani kuujadili hapa.....
unajua tunaweza ona hauna tija lakini labda sababu za huo uongo zina tija..... ndo maana nauliza kwa nini uuseme huo uongo ambao unaonekana kabisa hauna tija?
kama mwenzio hapendi wewe uonane na John, unadanganya na unaenda kumwona John, akigundua ulienda kumwona itakuwaje?

Relationship is about compromise, sasa kama sababu za kutomuona John hazina mshiko na kama sitakufa nisipomuona John; basi for the sake of mahusiano na kumjengea confidence hubby basi sintamuona John. Ila kama ni lazima nimuone, nitamwambia na kumfanya aelewe kwanini l had to go n see john.

Mazingira ya kuaminiana yanakuwa cultivated kwakweli; lkn kukiwa na maswali mengi sana kwa tuvitu tudogo basi kunatoa room ya kudanganyana.

Katika swali linaloongoza kwa majibu ya UONGO ni UKO WAPI SASA HIVI?
well some people may see that question as very romantic lakini lina dalili ya kutokumuamini mtu kidizaini hivi.
 
Hakuna mtu ambae hapendi trust kati ya mahusiano. Kila mmoja anapenda siku zote aambiwe ukweli. Upande wa mahusiano kutokuwepo na trust (nazungumza strictly nje ya) husababishwa na aidha mtu wako mwenyewe ama wewe mwenyewe. Kuna mwingine kweli anaweza sema anapenda awe anaambiwa ukweli no matter what! Cha ajabu ukweli ukitoka hapo si Drama hiyo itakayofuata - Kiasi kwamba huyo mtu anajuta anaona heri kuongopa. Take note sihalalishi kukosekana kwa uaminifu, ila najaribu kueleza why kwa wengine hua hawawi waaminifu.

Kikubwa cha kuelewa mahala ambapo hakuna trust ni ‘Kwa nini huyo mtu asiwe wazi na aongope katika suala ambalo ni la kawaida?"

Kukosekana kwa uaminifu kwa misingi ya wewe (ulie mpenzi wake)

Mara nyingi kuna masuala ambayo kimsingi ukiyaangalia yanaonekana madogo sana. Kama mfano uliotoa kwa kujifanya waenda Sokoni na hali waenda Salon. Hapo ni wazi kuwa sababu kubwa moja wapo inaweza kuwa huyo mwanamke huwa na matumizi makubwa na kuwa moja ya eneo ambayo anatumia sana pesa ni Saloon. Na wajua siye wanawake, kuna style inakuhiraji uende Saloon walau mara tatu kwa wiki. Inapotokea J/2 ulienda Saloon, J/5 ulienda Saloon na Leo Ijumaa unataka kwenda Saaloon na pengine ulishawahi ongea na mtu wako safari za Saloon zipungue (or hata hamjawahi ongea but wajishuku); the safest unaweza kuaga ni kuwa unaenda Sokoni badala ya Saloon.

Yes kaongopa it's a bad thing, but ukiliangalia kwa upande mwingine unatkuta anaongopa tokana na kuwa Mpenzi wake kamuona si mwelewa, ama tu hataji kuonyesha ni to what extent hilo tendo la Saloon limepewa kipaumbele na the like.
Uongo wa disaini hii kati ya wapenzi wengi hauepkiki.

Kukosekana kwa uaminifu kwa misingi ya mpenzi wako

Kuna wengine siku zote wao kuongopa ama kutokuwa wazi ni hulka yao… Tena pengine inasukumwa saana na selfishness.. Kutotaka ajue vitu vyote anavyomiliki, Kutoka ajue wapi hua anaenda, kutoka ujue tu kwa sababu yoyote ile! Na mara nyingi pia pamoja na kuwa cheating imetolewa katika kuelewa kukosekana kwa uaminifu wa hivi – Mara nyingi cheating ndiyo sababu kubwa sana ya wapenzi kuwa waongo kwa wenza/partners wao.

Mfano kama mliwahi gombana kwa ajili ya mtu uliyemhisi ana interest na huyo mtu anafanya Hotel Magongo, siku akiwa Hotel Magongo si rahisi kusema kuwa yupo hapo. Ama anapokuwekea silent simu ama kutoweza kupokea sababu yupo faragha na mpango wa kando akipokea hawezi sema nilikuwa faragha, atasema lingine lolote ambalo mpenzi wake atalikubali bila shida.
Umeeleza kwa kirefu sana rafiki na mengi ni ya msingi.......
ninachojaribu kukiangalia hapa ni je kama katika kudanganya kwako, kwa sababu yoyote ile ukakamatwa...... unakuwa umeweka wapi uaminifu wake kwako (wako kwake? kiswahili nacho kigumu!)?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Yes kuna kweli zingine ni very unpleasant au damaging. Mzazi mwenzangu aliniambiaga baada ya kuona jinsi gani nilivyohonest kuwa "kutosema ukweli wote hakumaanishi unasema uongo", so kwa couple sio vizuri kudig sana past za mtu maana waweza sababisha akudanganye kwa ajili ya kuprotect relationship yenu. Kuna vitu kama mtoto ni muhimu kuuliza lakini sijui umeshatembea na wanawake wangapi it is irrelevant IMO.
ha haaa, ndo maana sikutaka kabisa kuzungumzia uongo kuhusu mipango ya kando..... kwenye hilo, wooooteeeee tunasema uongo. siwezi kubali kwa mpenzi wangu kuwa nina mpango wa kando, labda anikamate, lol!
 
ha haaa, babu huo uongo usio na tija ndo haswa ninaotamani kuujadili hapa.....
unajua tunaweza ona hauna tija lakini labda sababu za huo uongo zina tija..... ndo maana nauliza kwa nini uuseme huo uongo ambao unaonekana kabisa hauna tija?
kama mwenzio hapendi wewe uonane na John, unadanganya na unaenda kumwona John, akigundua ulienda kumwona itakuwaje?

Bahati mbaya mimi siyo mdau wa uongo usio na tija...

Huo wenye tija hata ukinaswa unasema kweli kwamba sikutaka kukuharibia mood...and you now that we have a great appointment tonight.....ni rahisi kueleweka IMO!!

Babu DC!!
 
Hilo swali kama kuna mwanamume haulizi basi huyo kabarikiwa....

Ila mwisho wazi huwaumiza sana rohoni....from the man's perspective..!

Babu DC!1
na hilo swali kama kuna mwanamke anajibu ukweli basi huyo kabarikiwa.......
mpaka uniulize hilo swali maana yake hujanikuta sealed.... the max number mdada anaweza kutaja ni 2, got you!
 
Hivyo sioni na sitakaa kuona umuhimu wa uongo uso na faida. halafu kwenye mahusiano, mimi naamini ni vyema mtu akujue tangia mapema udhaifu na mapungufu yako ili afanye informed decision lakini pia inakusaidia wewe usiishi maisha ya kupretend.

Kaunga no matter unamfahamu vipi mtu wako... Kwa kiasi kikubwa with time, circumstances with a combination of other forces wengine hubadilika. Kwa mfano tukio kama hili wewe unatoa ushauri upi?

Kuna wanandoa nawafahamu... The wife hana kasoro kama ideal wife anapaswa kuwa kwa mising ya vile ambavyo wengi huangalia... Ni msafi, mtulivu si mtu wa kuzurula, ni mpishi mzuri, a good mom and wife na mengine mengi. To the extent kuwa ndugu wa upande wa mke na mume wote wanampenda na kumridhia. Ana kasoro moja tu huyu dada - Tamaa! Na she has tastes ya expensive things... Ni spender mzuri sana. Tatizo lake hilo linafanya hata mumewe akimpa pesa ahifadhi; akiulizia hiyo pesa inakuwa imetumika on things ambazo si za msingi... Na haijalishe pesa ilikuwa kiasi kikubwa vipi.

Vikao vimekaliwa, utatuzi umetafutwa, 10 years in marriage mwanaume kaamua kukubali kuwa the wife ndivyo alivyo hawezi change. Kilicho baki sasa mumewe ana pesa sana, mkewe hana access hadi apewe na mwanaume hayupo open kabisa the money he has maana ikiwa tu disclosed tayari lazima pesa kubwa iombwe. Kuna cases nyingi but sasa hili ni baya saana, kuwa yule mtu ambaye ndiye alipaswa aelewe all the details ndiye anafichwa kuliko wote! WHY? Sababu ya mwenza na si mwanaume mwenyewe.
 
Back
Top Bottom