The Zanzibar Echo
JF-Expert Member
- Apr 21, 2025
- 490
- 836
Rais wa Marekani Donald Trump ameashiria kauli "kuu" kuhusu Ukraine hii leo, huku kukiwa na kile kinachoonekana kuzidi kukasirishwa na Rais wa Urusi Vladimir Putin.
Siku ya Jumapili usiku, Trump alisema kuwa vifaa vya kijeshi "vya kisasa" vitaelekea Ukraine, ikiwa ni pamoja na makombora ya ulinzi wa anga ya Patriot.
Na rais wa Marekani alionekana kukerwa na kutochukua hatua kwa Moscow kuelekea usitishaji mapigano nchini Ukraine, akiwaambia waandishi wa habari kwamba "Putin ... anazungumza vizuri na kisha anapiga kila mtu jioni".
Maoni yake yanafuatia mahojiano siku ya Alhamisi, ambapo aliahidi kutoa "taarifa kuu" leo.
Chombo cha habari cha Marekani Axios kiliripoti jana usiku kwamba rais anafikiria kutuma silaha za mashambulizi nchini Ukraine.
Kufikia sasa, Trump ametoa silaha za kujihami pekee kwa taifa - kama vile mfumo wa Patriot.
Trump atakutana na mkuu wa Nato Mark Rutte leo katika Ikulu ya White House, na mjumbe maalum wa Marekani nchini Ukraine, Keith Kellogg, yuko Kyiv wiki hii kwa mazungumzo.
Siku ya Jumapili usiku, Trump alisema kuwa vifaa vya kijeshi "vya kisasa" vitaelekea Ukraine, ikiwa ni pamoja na makombora ya ulinzi wa anga ya Patriot.
Na rais wa Marekani alionekana kukerwa na kutochukua hatua kwa Moscow kuelekea usitishaji mapigano nchini Ukraine, akiwaambia waandishi wa habari kwamba "Putin ... anazungumza vizuri na kisha anapiga kila mtu jioni".
Maoni yake yanafuatia mahojiano siku ya Alhamisi, ambapo aliahidi kutoa "taarifa kuu" leo.
Chombo cha habari cha Marekani Axios kiliripoti jana usiku kwamba rais anafikiria kutuma silaha za mashambulizi nchini Ukraine.
Kufikia sasa, Trump ametoa silaha za kujihami pekee kwa taifa - kama vile mfumo wa Patriot.
Trump atakutana na mkuu wa Nato Mark Rutte leo katika Ikulu ya White House, na mjumbe maalum wa Marekani nchini Ukraine, Keith Kellogg, yuko Kyiv wiki hii kwa mazungumzo.