Trump asema Marekani itaipa Ukraine silaha hatari na za kisasa huku akimkosoa Putin

Trump asema Marekani itaipa Ukraine silaha hatari na za kisasa huku akimkosoa Putin

The Zanzibar Echo

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2025
Posts
490
Reaction score
836
Rais wa Marekani Donald Trump ameashiria kauli "kuu" kuhusu Ukraine hii leo, huku kukiwa na kile kinachoonekana kuzidi kukasirishwa na Rais wa Urusi Vladimir Putin.

Siku ya Jumapili usiku, Trump alisema kuwa vifaa vya kijeshi "vya kisasa" vitaelekea Ukraine, ikiwa ni pamoja na makombora ya ulinzi wa anga ya Patriot.

Na rais wa Marekani alionekana kukerwa na kutochukua hatua kwa Moscow kuelekea usitishaji mapigano nchini Ukraine, akiwaambia waandishi wa habari kwamba "Putin ... anazungumza vizuri na kisha anapiga kila mtu jioni".

Maoni yake yanafuatia mahojiano siku ya Alhamisi, ambapo aliahidi kutoa "taarifa kuu" leo.

Chombo cha habari cha Marekani Axios kiliripoti jana usiku kwamba rais anafikiria kutuma silaha za mashambulizi nchini Ukraine.

Kufikia sasa, Trump ametoa silaha za kujihami pekee kwa taifa - kama vile mfumo wa Patriot.

Trump atakutana na mkuu wa Nato Mark Rutte leo katika Ikulu ya White House, na mjumbe maalum wa Marekani nchini Ukraine, Keith Kellogg, yuko Kyiv wiki hii kwa mazungumzo.
 
Hakuna kipya kwenye vita ya Ukraine na Urusi ambacho magharibi hawajakifanya. Walianza kuvisifia vifaru vya Bradley mara Abrahams, Leo viko wapi? Zelenskiy aliomba mifumo ya ulinzi ya anga c alipewa? Vimesaidia nini? Kaomba ndege za F-16 nazo c alipewa? Mbona zinazidi kupukutishwa?


Huu mgogoro usingelipuka na kuwa hapa endapo magharibi wangendelea kuheshimu mkataba waliowekeana na Urusi kuwa hakuna nchi kubwa mbili hizi kujitanua kuelekea kwa mwenziye. Diplomasia imeshindikana kwa sababu Putin amesimamia mkataba wao unavyodai huku wao wakiitaka Ukraine iwe mwanachama wao ili wakae karibu na Urusi kitu ambacho kwa usalama wa Urusi ni hatari.


Hata hizi silaha wanazotangaza kuwa za kisasa haziendi kutatua lolote pale ulaya mashariki. Muda utaongea, ngoja tuone.
 
Hakuna kipya kwenye vita ya Ukraine na Urusi ambacho magharibi hawajakifanya. Walianza kuvisifia vifaru vya Bradley mara Abrahams, Leo viko wapi? Zelenskiy aliomba mifumo ya ulinzi ya anga c alipewa? Vimesaidia nini? Kaomba ndege za F-16 nazo c alipewa? Mbona zinazidi kupukutishwa?


Huu mgogoro usingelipuka na kuwa hapa endapo magharibi wangendelea kuheshimu mkataba waliowekeana na Urusi kuwa hakuna nchi kubwa mbili hizi kujitanua kuelekea kwa mwenziye. Diplomasia imeshindikana kwa sababu Putin amesimamia mkataba wao unavyodai huku wao wakiitaka Ukraine iwe mwanachama wao ili wakae karibu na Urusi kitu ambacho kwa usalama wa Urusi ni hatari.


Hata hizi silaha wanazotangaza kuwa za kisasa haziendi kutatua lolote pale ulaya mashariki. Muda utaongea, ngoja tuone.


Usiwe unaandika vitu usivyo na uelewa navyo. Jibu maswali yafuatayo:

1. Ukraine imeomba lini kuwa mwanachama wa NATO?

2. Urusi ilianza lini kuyateka maeneo Ukraine?

Kama hujui Urusi kwa mara ya kwanza iliyachukua maeneo ya Ukraine, Crimea, Donetsk na Luhansk mwaka 2014. iliivamia Ukraine kwa mara ya kwanza mwaka 2014.

Kama hujui, Ukraine iliomba kujiunga na NATO ili kujilinda na uvamizi wa Putin, baada ya kudhihirika wazi kuwa Putin baada ya kuyachukua maeneo ya Crimea, Donetsk na Luhansk, bado alikuwa na tamaa ya kuchukua maeneo mengine ya Ukraine.

Chanzo cha tatizo ni Putin kuyachukua maeneo ya Ukraine na kuyafanya sehemu ya Urusi.
 
Marekani haijawahi kusitisha Upelekaji wa Silaha Ukraine tangu vita vianze, licha kelele za Trump huenda ndiyo maana Putin hataki kusikia.
US ilichofanya ni kuendelea kufanya biashara ya silaha na nchi za NATO ambazo kwa sababu ni vibaraka wake zikapigane na Russia.
Hata hivyo hata US ingeisaidiaje Ukrain haitabadilisha cho chote sana sana itarefusha vita.
 
Usiwe unaandika vitu usivyo na uelewa navyo. Jibu maswali yafuatayo:

1. Ukraine imeomba lini kuwa mwanachama wa NATO?

2. Urusi ilianza lini kuyateka maeneo Ukraine?

Kama hujui Urusi kwa mara ya kwanza iliyachukua maeneo ya Ukraine, Crimea, Donetsk na Luhansk mwaka 2014. iliivamia Ukraine kwa mara ya kwanza mwaka 2014.

Kama hujui, Ukraine iliomba kujiunga na NATO ili kujilinda na uvamizi wa Putin, baada ya kudhihirika wazi kuwa Putin baada ya kuyachukua maeneo ya Crimea, Donetsk na Luhansk, bado alikuwa na tamaa ya kuchukua maeneo mengine ya Ukraine.

Chanzo cha tatizo ni Putin kuyachukua maeneo ya Ukraine na kuyafanya sehemu ya Urusi.
Nashauri asikujibu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom