Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 56,744
- 46,268
Wanaukumbi.
Rais wa Marekani Donald Trump amekataa pendekezo lililoripotiwa ambapo Oman na Iran walikuwa wakijadili mpango wa kutoza ushuru meli zinazopita kwenye Mlango wa bahari wa Hormuz.
"Oman haina budi kufuta mkondo wa watu wengine, la sivyo tutawaangamiza. Wanafikiri kila kitu kitakuwa sawa," Trump aliwaambia waandishi wa habari wakati wa mkutano wa baraza la mawaziri katika Ikulu ya White House siku ya Jumatano.
Bloomberg iliripoti kwa mara ya kwanza mnamo Mei 21 kwamba Iran ilikuwa katika mazungumzo na Oman kuhusu utozaji ushuru wa meli zinazopita kwenye Mlango-Bahari wa Hormuz.
Gazeti la New York Times baadaye liliripoti, likinukuu vyanzo viwili vinavyofahamu mazungumzo hayo, kwamba majadiliano hayakuwa juu ya kutoza ushuru wa moja kwa moja kwenye njia ya kupita Hormuz, bali kuhusu kutoza meli kwa huduma.
SOuRCE: BBC
Rais wa Marekani Donald Trump amekataa pendekezo lililoripotiwa ambapo Oman na Iran walikuwa wakijadili mpango wa kutoza ushuru meli zinazopita kwenye Mlango wa bahari wa Hormuz.
"Oman haina budi kufuta mkondo wa watu wengine, la sivyo tutawaangamiza. Wanafikiri kila kitu kitakuwa sawa," Trump aliwaambia waandishi wa habari wakati wa mkutano wa baraza la mawaziri katika Ikulu ya White House siku ya Jumatano.
Bloomberg iliripoti kwa mara ya kwanza mnamo Mei 21 kwamba Iran ilikuwa katika mazungumzo na Oman kuhusu utozaji ushuru wa meli zinazopita kwenye Mlango-Bahari wa Hormuz.
Gazeti la New York Times baadaye liliripoti, likinukuu vyanzo viwili vinavyofahamu mazungumzo hayo, kwamba majadiliano hayakuwa juu ya kutoza ushuru wa moja kwa moja kwenye njia ya kupita Hormuz, bali kuhusu kutoza meli kwa huduma.
SOuRCE: BBC