Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
Rais Trump ametishia kufanya mashambulizi kadhaa dhidi ya Iraq baada ya bunge lake kutaka Marekani kuondoa majeshi yake nchini humo.
"Tumewekeza kiasi kikubwa sana cha fedha katika jeshi la anga huko. Kujenga msingi wake imetugharimu mabilioni ya dola. Hatutaondoka labda kama watatulipa gharama tuliyotumia", aliwaambia waandishi wa habarai.
Akizungumza akiwa katika ndege ya rais, Trump alisema kuwa kama Iraq inataka majeshi ya Mareani yaondoke nchini mwake kwa nguvu, "Tutalipiza kwa kufanya mashambulizi ambayo hayajawahi kutokea kabla . Na kufanya vikwazo ambavyo Iran imeviweka kuwa vya kawaida sana."
Wanajeshi wa Marekani wapatao 5,000 wapo Iraq kama sehemu ya makubaliano ya kimataifa ya kupambana na kundi la kigaidi la kiislamu 'Islamic State' (IS).
Siku ya jumapili, azimio lilifikiwa na wabunge wa Iraqi kuwa majeshi yote ya kigeni yaondoke nchini humo.
Mvutano bado ni mkubwa baada ya Marekani kuusika kumuua kiongozi wa jeshi wa Marekani jenerali Qasem Soleimani huko Baghdad wiki iliyopita. Iran iliapa kulipiza kisasi.
Soleimani ambaye alifariki akiwa na umri wa miaka 62, alikuwa akiongoza operesheni za vita katika nchi za mashariki ya kati na alikuwa anatambuliwa na wamarekani kama gaidi.
Mabaki ya mwili wa jenerali sasa yamerejeshwa katika nchi yake Iran, eneo ambalo waombolezaji wamekusanyika barabarani katika mitaa ya Tehran.
Kiongozi mpya wa kikosi cha jeshi la Iran la Quds - ambacho Soleimani aliongoza - aliapa kuwaondoa Wamarekani katika mataifa ya mashariki ya kati.
"Tumehaidi kuendelea kuwa mashaidi wa Soleimani kwa kufuata muongozo wake... na kile ambacho tunaweza kukifidia dhidi ya kifo chake ni kuwaondoa wamarekani katika ukanda wetu,"radio ya taifa ilimnukuu Esmail Ghaani.
Pia soma;
"Tumewekeza kiasi kikubwa sana cha fedha katika jeshi la anga huko. Kujenga msingi wake imetugharimu mabilioni ya dola. Hatutaondoka labda kama watatulipa gharama tuliyotumia", aliwaambia waandishi wa habarai.
Akizungumza akiwa katika ndege ya rais, Trump alisema kuwa kama Iraq inataka majeshi ya Mareani yaondoke nchini mwake kwa nguvu, "Tutalipiza kwa kufanya mashambulizi ambayo hayajawahi kutokea kabla . Na kufanya vikwazo ambavyo Iran imeviweka kuwa vya kawaida sana."
Wanajeshi wa Marekani wapatao 5,000 wapo Iraq kama sehemu ya makubaliano ya kimataifa ya kupambana na kundi la kigaidi la kiislamu 'Islamic State' (IS).
Siku ya jumapili, azimio lilifikiwa na wabunge wa Iraqi kuwa majeshi yote ya kigeni yaondoke nchini humo.
Mvutano bado ni mkubwa baada ya Marekani kuusika kumuua kiongozi wa jeshi wa Marekani jenerali Qasem Soleimani huko Baghdad wiki iliyopita. Iran iliapa kulipiza kisasi.
Soleimani ambaye alifariki akiwa na umri wa miaka 62, alikuwa akiongoza operesheni za vita katika nchi za mashariki ya kati na alikuwa anatambuliwa na wamarekani kama gaidi.
Mabaki ya mwili wa jenerali sasa yamerejeshwa katika nchi yake Iran, eneo ambalo waombolezaji wamekusanyika barabarani katika mitaa ya Tehran.
Kiongozi mpya wa kikosi cha jeshi la Iran la Quds - ambacho Soleimani aliongoza - aliapa kuwaondoa Wamarekani katika mataifa ya mashariki ya kati.
"Tumehaidi kuendelea kuwa mashaidi wa Soleimani kwa kufuata muongozo wake... na kile ambacho tunaweza kukifidia dhidi ya kifo chake ni kuwaondoa wamarekani katika ukanda wetu,"radio ya taifa ilimnukuu Esmail Ghaani.
Pia soma;
Bunge la Iraq kupiga kura ya dharura kuviondoa vikosi vya Marekani nchini humo
Bunge la Iraq leo linapiga kura ya kuviamrisha vikosi vya USA kuondoka nchini humo. Wakati huo huo vikosi vya Iran vimetishia kushambulia vituo muhimu vya USA vilivyoko Europe.
www.jamiiforums.com