Kyokola
JF-Expert Member
- Sep 5, 2014
- 1,402
- 1,894
Kaka, hii story sio ya kutunga, sina sababu ya kumpa Mungu utukufu kwa kitu ambacho hakukifanya kwenye maisha yangu, ujue Mungu hajibembelezi tumtungie sifa na utukufu, na ni dhihaka mbele za Mungu ambayo siwezi kuifanya, Mungu hadhhakiwi wala hahitaji msaada wa wanadamu kupata utukufu, na katu hawezi kuruhusu wala kukubali icho kitu. story hii imenitokea maishani mwangu. vilevile, nawaonya wale ambao hawajaoa au kuolewa, muwe makini sana na zawazi wanazoleta watu, muwe makini na vyakula na kila kitu wakati wa sherehe, muwe makini na ndugu...sio wote wanakuja kwenye ndoa wanawapenda, wengine wanawaonea wivu....kuna mengi huwa yanatokea, niliandika tu harakaharaka nikitoa kichwani yale yaliyotokea, na sijaandika yote, ningeandika yote hapa na kuweka mifano yote, kuna watu hapa wangeshataja hadi jina langu hapa...yapo kadhaa nimeyaacha, nitasimulia siku nyingine, lakini Mungu ni shahidi yangu, haya maisha nimeyapitia kabisa.
Ashukuriwe Mungu atufanyiaye njia pale pasipokua na njia. Mungu hufungua milango iliyofungwa na adui. Yeye ndiye mwenye ufunguo wa Daudi, yeye afunguaye na hapana afungaye. Wao walipokuvuruga walijua wamekuweza, hawakujua Mungu atakukumbuka na kuwaumbua siku moja.