Migomba
JF-Expert Member
- Nov 30, 2013
- 945
- 1,339
History inatuonyesha kuwa miaka ya nyuma kabla ya kugunduliwa pesa watu waliuziana kwa mtindo wa kitu kwa kitu (barter trade) ambapo kama wewe ni mvuvi ambaye una samaki na unahitaji mbuzi basi itabidi utafute mtu ambaye ana mbuzi na wakati huo huo anahitaji samaki. Hivyo kupata tu mwenye mbuzi sio ishu, ishu ni kwamba naye awe anataka samaki tena aina ile ambayo wewe unayo na kwa kiasi cha kutosha kutoa mbuzi wake. Jambo hilo linaweza kuwa mfano mzuri kwenye mapenzi.
Bwana Nyangema labda interest yako ni mwanamke mweusi, mrefu, aliyejazia, mwenye elimu ya chuo, anayejua kupika na kutunza familia.
Bibie Mrembolisious anataka handsome boy, mwenye kazi nzuri, mwenye huruma, awe mrefu, mwenye umbo la kimazoezi na anayejua kuvaa.
Sasa hapo tabu ni Nyangema aliye single kukutana na Mrembolisious aliye single. Utaona ni rahisi kumpata mwenye sifa zako lakini asipende za kwako au mkawa na sifa lakini tayari mna uhusiano. Au ikakulazimu kuvumilia hizo chache alizonazo na ukiwa kwenye uhusiano ukajikuta unakutana na yule haswaa mwenye sifa zako na ukashindwa kuvumilia (mchepuko)
Kwa kuliona hilo wazungu wamejaribu kutengeneza hadi mitandao ya ku-date ili kuweka medium ya kukutanisha hizo sifa (kama pesa inavyotumika kutatua changamoto za barter trade) lakini bado humo namo kumejaa uongo na biashara.
Hivyo kiujumla kupata anayekupenda na ukampenda ni ngumu sana, ishu ni kukubaliana/kuridhika na kile ulichopata.
Bwana Nyangema labda interest yako ni mwanamke mweusi, mrefu, aliyejazia, mwenye elimu ya chuo, anayejua kupika na kutunza familia.
Bibie Mrembolisious anataka handsome boy, mwenye kazi nzuri, mwenye huruma, awe mrefu, mwenye umbo la kimazoezi na anayejua kuvaa.
Sasa hapo tabu ni Nyangema aliye single kukutana na Mrembolisious aliye single. Utaona ni rahisi kumpata mwenye sifa zako lakini asipende za kwako au mkawa na sifa lakini tayari mna uhusiano. Au ikakulazimu kuvumilia hizo chache alizonazo na ukiwa kwenye uhusiano ukajikuta unakutana na yule haswaa mwenye sifa zako na ukashindwa kuvumilia (mchepuko)
Kwa kuliona hilo wazungu wamejaribu kutengeneza hadi mitandao ya ku-date ili kuweka medium ya kukutanisha hizo sifa (kama pesa inavyotumika kutatua changamoto za barter trade) lakini bado humo namo kumejaa uongo na biashara.
Hivyo kiujumla kupata anayekupenda na ukampenda ni ngumu sana, ishu ni kukubaliana/kuridhika na kile ulichopata.