TRA wanavyofunga biashara za wazalendo

Mkuu asante kwa ushauri.
Lakini nafikiri unajua fika kuwa kodi kama With Holding Tax na Provisional Tax huwa ni sehemu tu ya Annual Corprate Tax.
Na unajua madudu ambayo yanafanyika katika hili.
Kodi hizi zinakatwa (hasa WHT) kupita na kuzidi makadirio ya Corporate Tax,
Na ikishakatwa hairudishwi.
Nataka neno lako katika hili.

Halafu kwenye Invoicing.
Wafanyabiashara wengi hawalipwi in time, lakini wanapaswa kuwasilisha VAT at source and in time.
Yaani ukimpelekea Invoice na risiti ya EFD mteja wako(mara nyingi Serikali) unatakiwa ulipe a kodi uliyotakiwa kukusanywa ndani ya mwezi mmoja.
Uzoefu unaonyesha kuwa kuna wafanyabiashara hawalipwi hata ndani ya mwaka hivyo kufilisi kampuni.

Haya mambo ya vitabuni wee yaache tu, uhalisia na TRA ni kitu kingine.
 
Wewe ndiyo umejificha kwenye kicha cha ajabu ajabu hujui kuwa baadhi ya maofisa wa TRA huwabambikia kodi kubwa wafanyabiashara kwa makusudi kutengeneza mazingira ya Rushwa, umejitoa fahamu zote na kuwaona maofisa wa TRA ni mungu na malaika hawakosei wapo sahihi kwa kila jambo
 
TRA yafaa ifumuliwe isukwe upya na wale maofisa vinara wa kuwabambikia kodi kubwa wafanyabiashara kuwafungia account kuwafungia biashara watu wachunguzwe na Takukuru juu ya uhalali wa mali zao binafsi
 
Ndani ya miaka 3 nchi itakua hoi sana
Wafanyabiashara wakubwa wamehamishia pesa zao Nchi Jiran kukwepa A/C zao kufungwa na TRA kienyeji kishamba kwa njia haramu za kishetani
 
Nimesoma andiko lake nikabaki kushangaa naona analeta elimu ya darasani ambayo ni tofauti kabisa na uhalisia..Mwambie afungue biashara yake afu a apply hizo theory zake tuone atafika wapi...wasomi wetu ni shida sana
 
Ndio maana hata mabenki sasa hivi wanashindwa kutoaa mikopo sasbabu hamna. Mfanyabiashara mjiinga ataacha pesa yake benki huku akijua kwamba T.R.A wanamnyemelea.kwahio mwisho wa siku ni Tanzania inaingia kwenye great depression.
 
Nimesoma andiko lake nikabaki kushangaa naona analeta elimu ya darasani ambayo ni tofauti kabisa na uhalisia..Mwambie afungue biashara yake afu a apply hizo theory zake tuone atafika wapi...wasomi wetu ni shida sana
Ha ha ha hao wasomi watetea uonevu uovu Rushwa za baadhi ya maofisa wa TRA ni bora wangesalia na Elimu ya darasa la pili kuliko wakajiita wasomi huku wakitetea mateso manyanyaso uonevu kwa wafanyabiashara, hakunaga msomi wa hivyo
 
Hawa jamaa kuanzia kamishina ni ndumi la kuwili sana. Wanapoongea katika vyombo vya habari juu ya taasisi hii na majukumu yake utasema hawa wafanyabiashara ni wakorofi sana na sio waelewa. Ila ukipewa rekodi ya madudu yao wanayofanya ndipo unajua kuwa haujui......

Tazama tu hata makadirio ya kodi ya bidhaa zinazopita bandarini. Yaani magharama yapo juu kweli kweli kuliko hata bei ya bidhaa. Unanunua gari Us dola 2,500, kodi inakuja milioni saba..... Sasa unajiuliza imekuwaje kodi ni zaidi ya 100% ya original price ya bidhaa?!

Tunahitaji kiwakazia wale misukule pale bungeni kujadili upya hizi kanuni za TRA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni wakati Sasa na sisi Tanzania tuwe na Bodi ya Rufaa za Kodi yenye kujielewa
 
Ndio maana hata mabenki sasa hivi wanashindwa kutoaa mikopo sasbabu hamna. Mfanyabiashara mjiinga ataacha pesa yake benki huku akijua kwamba T.R.A wanamnyemelea.kwahio mwisho wa siku ni Tanzania inaingia kwenye great depression.
Wafanyabiashara wengi sasa wanabuni mbinu za kuhifadhi pesa zao Nchi zingine ama hata kuficha ndani mwao, hawana imani na Bank tena, na hii ni hatari kubwa kwa usitawi wa mabenk na mifumo ya mikopo ni vigumu Tanzania kupiga hatua kimaendeleo kwa kuendelea kuwalinda baadhi ya maofisa wa TRA vinara wa kuwabambikia kodi kubwa, kuwafungia Account, kuwafungia biashara wafanyabiashara wengi.
 
Ni wakati Sasa na sisi Tanzania tuwe na Bodi ya Rufaa za Kodi yenye kujielewa
TRA ifumuliwe isukwe upya imejaa wala Rushwa mno akina masamaki wapo wengi sana, Takukuru iwachunguze maofisa wa TRA wale vinara wa kufunga biashara na Account za watu kwa njia haramu za kishetani
 
Njia pekee ya kumaliza Tatizo la usumbufu wa TRA ni kuundwa tume ichunguze mapungufu yote juu ya ukasanyaji kodi na pia wale maofisa wasumbufu wale majanga kwa wafanyabiashara wawajibishwe kwa manufaa ya Taifa
 
Umeandika nn hapa? Mada inahusiana na nn? Unapinga au unakubali? Unapinga nn unakubali nn?

Comment yako ni kama polo haieleweka inasimama wapi, unapinga nn inaafiki nn
 
Umeandika nn hapa? Mada inahusiana na nn? Unapinga au unakubali? Unapinga nn unakubali nn?

Comment yako ni kama polo haieleweka inasimama wapi, unapinga nn inaafiki nn
Ni vigumu kunielewa kwa sababu wewe ni mnufaika wa Rushwa na uonevu wote wa baadhi ya maofisa wa TRA
 
Ni vigumu kunielewa kwa sababu wewe ni mnufaika wa Rushwa na uonevu wote wa baadhi ya maofisa wa TRA

Ume misquote , rudi nenda ka quote ulie tarajia Ku quote

Wazazi wako bora wangetumia condom tu,
Unakua kama nyumbu, unavamia tu kila kinachokuja mbele yako
 
Nilimwona Lissu kwenye kampeni zake akipita kariakoo, mkamwambia mambo yako poa kabisa.

Ni kama vile haya usemayo yanawapata watu wachache sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…