Mwingereza
JF-Expert Member
- Jan 21, 2014
- 1,115
- 2,771
Kwa makusudi Kabisa, TRA inahujumu (Sabotage) Jitihada za Rais Magufuli kuelekea Uchumi wa Viwanda.
Kwa kipindi kirefu, TRA wamekuwa ni wababe, wamelalamikiwa sana. Hawamskilizi mtu, wamekuwa wakifanya mambo kwa kukurupuka na kukomoa. Unafungua biashara wanakuja na kukupa makadiro ya kutisha kabla ya kuanza biashara. Wafanya biashara wakaanza kwenda nchi jirani
Unaleta bidhaa bandarini, wanakupa ushuru mkubwa kuliko thamani ya bidhaa, unapobisha, unaombwa rushwa kubwa ili amigo wako utoke. Mwisho wa siku wafanya biashara wakaanza kusita kuagiza.Na ndio maana mizigo nayo ikapungua. Hapa mchawi ni nani?
Wafanya biashaa wadogowadogo wanalaimishwa kununua EFD machine wakati mitanni yao ni midogo kuliko thamani ya EFD. Kwa nini wasifunge biashara? Hapa Mchawi ni Nani?
Sehemu zingine kama mabaa na grocery, TRA wanajificha wakihesabu umeuza nini, hata beer na chakula wnahesabu umeuza ngapi kisha wanakuvamia wanataka kodi. Hii inafanyika wapi? Mfuga kuku anavamiwa nyumbani kwake alipe kodi. Kwa nini wasifunge, wakati wanahangaika na kuku wanaokufa?
Kodi nchini Tanzania inatumika kama adhabu na kukomoana. TRA inaajiri vijana wasiojitambua, wanatishia walipa kodi. wanatisha kuifunga biashara yako na kupiga mnada ulivyo navyo kama hukubali kulipa kodi waitakayo. hasa wakinyimwa rushwa wanayoitaka wao. Duniani kote, hakuna serikali inayokusanya kodi kwa mtu ambaye hajauza hata chupi. Makadirio ya kodi, hiyo kodi inatoka wap wakati biashara hata bado? Anafanya tathmini, hata ya mwaka, wakati mwingine hata mwaka haufiki?
Uchumi wa Nchi hauendeshwi na kodi.Uchumi unaendeshwa na uzalishaji
Kwa kipindi kirefu, TRA wamekuwa ni wababe, wamelalamikiwa sana. Hawamskilizi mtu, wamekuwa wakifanya mambo kwa kukurupuka na kukomoa. Unafungua biashara wanakuja na kukupa makadiro ya kutisha kabla ya kuanza biashara. Wafanya biashara wakaanza kwenda nchi jirani
Unaleta bidhaa bandarini, wanakupa ushuru mkubwa kuliko thamani ya bidhaa, unapobisha, unaombwa rushwa kubwa ili amigo wako utoke. Mwisho wa siku wafanya biashara wakaanza kusita kuagiza.Na ndio maana mizigo nayo ikapungua. Hapa mchawi ni nani?
Wafanya biashaa wadogowadogo wanalaimishwa kununua EFD machine wakati mitanni yao ni midogo kuliko thamani ya EFD. Kwa nini wasifunge biashara? Hapa Mchawi ni Nani?
Sehemu zingine kama mabaa na grocery, TRA wanajificha wakihesabu umeuza nini, hata beer na chakula wnahesabu umeuza ngapi kisha wanakuvamia wanataka kodi. Hii inafanyika wapi? Mfuga kuku anavamiwa nyumbani kwake alipe kodi. Kwa nini wasifunge, wakati wanahangaika na kuku wanaokufa?
Kodi nchini Tanzania inatumika kama adhabu na kukomoana. TRA inaajiri vijana wasiojitambua, wanatishia walipa kodi. wanatisha kuifunga biashara yako na kupiga mnada ulivyo navyo kama hukubali kulipa kodi waitakayo. hasa wakinyimwa rushwa wanayoitaka wao. Duniani kote, hakuna serikali inayokusanya kodi kwa mtu ambaye hajauza hata chupi. Makadirio ya kodi, hiyo kodi inatoka wap wakati biashara hata bado? Anafanya tathmini, hata ya mwaka, wakati mwingine hata mwaka haufiki?
Uchumi wa Nchi hauendeshwi na kodi.Uchumi unaendeshwa na uzalishaji