Tra huu mnaofanya ni wizi

Kiherehere

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
1,806
621
1.Kwanza nataka kuuliza? ni sababu gani MNACHUKUA malipo ya DOLA kwa ulipaji wa leseni za kampuni za FREIGHT FOWARD (clearing & fowarding)?
Kama tunataka kukuza thamani ya shilingi, na TRA ni agent wa serikali ta Tanzania, hizi DOLA mnapeleka wapi na ni za nani? ikiwa walipaji ni watanzania?

2.Kwanini mnaweka limiti ya kutoa LESENI kwa makampuni ya FREIGHT FOWARD?? mbona leseni nyingine haziwekewe limitation? kama leseni za Mabar,Clubs,Maduka nk.nk?
Hii ni kufanya ushindani usiwepo dhidi ya makampuni yanayofunguliwa na wafanyakazi wa TRA? Pia makampuni ya wageni yanayo wahonga pesa msitoe leseni kwa watanzania wanaotaka kufanya hivyo, kwakuwa wao watacharge gharama ndogo kulinganisha na wao na kuwapotezea wateja wageni, ambao wao wakiomba ni rahisi kupewa baada ya KUFUNGIA KAMPUNI ZINGINE ZA RAIA.

3.Kwa mtindo huo, hamuoni kama mnaikoseha serikali mapato? ikiwa kampuni moja inaweza kulipia $400 kwa mwaka, je ni makampuni mangapi yangekuwepo na kulipa kiasi hicho kwa mwaka, ikiwa atashindwa kulipia au kuwa na matatizo mengine ndo mumfungie?

Huu ni wizi na dhuluma kwa watanzania walio na uwezo wa kufanya kazi hiyo.kama ilivyoainishwa na katiba, kwa nini nyie mnaweka limiti za umiliki ktk secta hiyo, na kwa nini leseni ZITOLEWE KWA MKUPUO MWIZHO WA MWAKA TU!!
Zingatia
22​
.-(2) Kila raia anasta hili fursa na haki sawa, kwa masharti ya
usawa, ya kushika nafasi yoyote ya kazi na shughuli yoyote iliyo

chini ya Mamlaka ya Nchi.
 
Back
Top Bottom