Tozo zimehamia kwenye Ma-Benki

Tozo zimehamia kwenye Ma-Benki

Naichukia sana hii serikali, yumkini kuliko serikali yoyote ile. Nahisi imekuja kunipa stress zaidi za maisha....

Juzi nilikamatwa na watoza ushuru, wakinishuku sitoi receipt..Tukaenda ofisini kwao..baadaye wakasema nilete document zote nikapeleka..Mzee kitengoni akasema...enyi vijana mbona sioni shida kwa huyu? Akawaita ofisini, wamekaa kama dakika 5 hivi wakarudi kusema...tumeongea tumeona tu tukuruhusu tumekusamehe...ila usirudie...Nilibaki nashangaa sana. Nilijikuta machozi yanatoka.

Jirani yangu alitoa 1.3M kuhonga asipogwe faini ya 3M ukiangalia mazingira aliyokamatiwa unashangaaa....eti radio subwoofer ameandika receipt ndogo ya 120,000 badala ya 160,000 yaani yaani ndo ulipe 1.3M tena si kwa controll number??? Kweli jamani kweli Haya mambo haya!!!

Hivi watanzania wenzangu, hatuyaoni haya/kila mtu achukue zake???? Awamu hii imekuwa ya shida kila mahali... Ukiagiza bidhaa Dsm gharama ya usafiri imepanda karibu mara mbili.

Halafu leo waziri wa biashara sijui anasema cement imeshuka bei....wakati mtaani bei ndo zinapanda yaani

Kama ni mfanya biashara ukisema uende somoni vyakula vimepanda bei utafikiri tunakomolewa yaani

Baadhi ya taasisi ukienda sasa baadhi ya watumishi yaani ni maringooo tu, unawabembeleza kulipa mapato ya serikali hawajali yaani..ni kama wao nao wamechoka yaani...


Yule Mzee alikuwa na mapungufu yake lakini, hatukuwa huku tulikofika tuliheshimiana, hakukuwa na inflation kama hii tuionayo!!!


Umeharibu hapo mwishoni. Yule mzee tena?
 
Naona baadhi ya watanzania wenzangu limeanza kuwachosha hili.
 
Cha ajabu bunge likabariki huu upuuzi, tusipoamka hawa wanasiasa wataendelea kutukandamiza milele, haiwezkani nime hustle kivyangu sio mtumishi wa serikali nikapata vipesa vyangu nikaviifadhi bank alafu uje unikate, serikali gani hii inayonyanyasa raia wake kiasi hichi?
 
20220730_154221.jpg
 
Ujambazi utaongezeka hawa Viongozi hawaajali kulinda usalama wa Wa Watanzania wapo kwa ajili ya kuwaumiza hata wakitaka wafe wafe ili mradi wachangie Tozo zao..
 
Back
Top Bottom