pa1985
Senior Member
- Feb 18, 2015
- 166
- 43
Nauliza kidogo, naona watu wanazichangamkia sana hizi gari aina ya TOYOTA BREVIS. Kuna nini cha ziada?
============
============
![]()
![]()
The Toyota Brevis is a mid-sized luxury sedan introduced in May 2001 and sold only in Japan. The Brevis has some styling cues from the Lexus LS 430. The Brevis had been discontinued in 2007. Sales started in June, 2001. The cars finishing gives composure and a feeling of luxury although performance wise it is similar to the Progres and both having similar medium size bodies.
![]()
Kwa kifupi inavutia, ni la ukubwa wa kati na lilitengenezwa kati ya mwaka 2001 hadi 2007 kwa soko la Japan tu. Halitengenezwi tena kwa hiyo angalia uendeshaji na matengenezo yake
Brevis mashine kubwa man! Kwanza jua kuwa Brevis zote zinatumia engine ya Jz ambayo ni engine inayotumika katika sport car za toyota mfano toyota Supra.
Engine ya Brevis imegawanyika katika mifumo na ukubwa;
2.5L 1JZ-GE I6
2.5L 1JZ-FSE I6
3.0L 2JZ-GE I6
3.0L 2JZ-FSE I6
Sasa hiyo ya 3.0 ni balaa, yani sijui gari gani linaweza kukimbiza hiyo mashine. Kinachowafaya watu wanunue Brevis ni perfomance yake yaani engine, kama unapenda mbio basi nakushauri nunua Brevis utafurahi.
Brevis ni ugonjwa wa moyo. Kwa gari ndogo kama hiyo with a CC 2500 engine capacity ni kujipa gharama za ziada.
Vp mafuta unywaji wake?
Mzee si unaona izo ccc 2.5 na 3.0 halafu petrol, inakula wese sana tu yaani sana 2, kama huna hela ya mafuta endesha Vitz ndio hazili mafuta, lakini gari ya zaidi ya CC 2.5 halafu ikiwa inatumia Petrol, lazima ile mafuta
Bei inategemeana kama wataka brand new, used both Bongo and nje ya nchi.. Nyingi zinazokuja Bongo ni used tayari, si unajua wenzetu matumizi yao kidogo yako poa hata kama used inaonekana iko powa tu. Tatizo kubwa hizi brand mfano kuipata Brevis latest brand kwa maisha yetu ni ngumu. Ndio maana tunabase za kati ya 2001 or 2003.
Yangu nilichukua million 13 Japanese used milage 68000, Saa hizi hata million 11 unapata ila kama mwoga wa maisha kama wengine hao hii gari inanyonya wese hatari! Kwa spidi utapenda, Six Valve hata new force utampumulia kwa nyuma.
Kuna vitu vitatu lazima tuvielewe tunapoendesha magari, kwanza performance ya gari kwa jinsi ilivyotengenezwa, na hili linahusishwa na service ya gari husika. Cha pili na muhimu ni uwezo wa mtu binafsi katika kuendesha gari (mfano kuna watu wanatumia Carina, Premio na wengine wanatumia Prado, Alteza Subaru; lakini wanaotumia Carina, Premio ndio wanawahi kufika.)
Hii nina maana kuwa hata kama gari ina performance gani kama ni muoga huwezi shindana na mtu ambaye si mwoga na ana gari ambayo performance yake ni ndogo.
Cha mwisho ni uenyeji wa njia husika..