Tommy Flavour: Kuwa chini ya Kiba

Tommy Flavour: Kuwa chini ya Kiba

Gustavo Gaviria

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2018
Posts
633
Reaction score
1,119
Huyu Tommy flavour, ana uwezo mkubwa sana kimuziki, kwa maoni yangu sioni kama ni movement sahihi kuwa chini ya ali kiba, itakuwa ngumu sana kupanda chati na kukuza muziki wake

Naona alipaswa awe msanii wa kujitegemea na management yake, na mbinu zake za kimuziki

Tommy Flavour ft Alikiba-Omukwano



Tommy flavour- She got a gwan(Ngwair Tribute)

 
Kiba mwenyewe kushindwa kujimanage atawezaje kummanage mtu mwingine.

Wasanii wa bongo wajitafutie managers ambao sio wasanii ndo watakuwa stable
 
Wasanii wote wanaoanzisha hz leble wasiogope kuuliza kwa WCB wamewezaje kufanikiwa.
High table sound ipoipoipo tu
Mdee music wanajikongoja tu
 
Leo ndo umemjua tommy? tulieni Dawa Iwaingie Acheni kupiga Ramli. Kwamba wewe una Akili kumzidi Tommy aliyeamua kua chini ya kings Music,.

Tulieni Kings Music Wanakuja kivingine Ni mawe Juu ya mawe, hit baada ya hit
 
Kiba namkubali sana lakini nahisi atakuwa mchawi yule jamaa kwa anachomfanyia huyo dogo!

Tommy yupo chini ya kiba anatoa ngoma tamu kabisa chakushangaza ndani ya siku tatu haijaingia hata kwenye trending videos

Huyo boss wake tangu apost inavyotoka kaingia mitini, Kiba abadirike aache kuona mziki kama mazoea
 
Nadhani ni mtu mzima usimchagulie maamuzi kwenda kwa kiba yeye ndio kaona sahihi kwake
 
Kiba namkubali sana lakini nahisi atakuwa mchawi yule jamaa kwa anachomfanyia huyo dogo!

Tommy yupo chini ya kiba anatoa ngoma tamu kabisa chakushangaza ndani ya siku tatu haijaingia hata kwenye trending videos

Huyo boss wake tangu apost inavyotoka kaingia mitini, Kiba abadirike aache kuona mziki kama mazoea
Kweli mkuu

Kuna uwezekano wa yeye kudidimia
 
Leo ndo umemjua tommy? tulieni Dawa Iwaingie Acheni kupiga Ramli. Kwamba wewe una Akili kumzidi Tommy aliyeamua kua chini ya kings Music,.

Tulieni Kings Music Wanakuja kivingine Ni mawe Juu ya mawe, hit baada ya hit
Tommy ni mkali tangu hajaingia kwa kiba
 
Kiba mwenyewe kushindwa kujimanage atawezaje kummanage mtu mwingine.

Wasanii wa bongo wajitafutie managers ambao sio wasanii ndo watakuwa stable
Kabisa mkuu

Kuwa chini ya mtu aliyeshindwa kujimanage mwenyewe ni tatizo
 
Tommy ni mkali tangu hajaingia kwa kiba
Uliwai kumzungumzia popote kuhusu ukali wake? Tommy hajawai kuwa kwenye Level hii aliyopo sasa, sana alikua kajikita kwenye Uhadishi..

Tulieni ndo Kwanza kunapambazuka kwa Tommy Anakuja na EP kaa mkao wa Kula
 
Kabisa mkuu

Kuwa chini ya mtu aliyeshindwa kujimanage mwenyewe ni tatizo
Mmekalilishwa ka msemo ka kushindwa kujimanage basi mnakaropoka kama watoto wanaokalilishwa neno

Mtu yupo kwenye game miaka karibu 20 na yupo top Level mpaka leo. Unaropoka eti kashindwa kujimanage?

Kule kwa Diamond Mna wasifia mameneja huku kwa kiba ana mameneja ila hamlaumu mameneja mnamlaumu yeye, mnakalilishwa kama mapopoma vimisemo vya miaka nenda rudi..

Kashindwaje kujimanage?
 
Leo ndo umemjua tommy? tulieni Dawa Iwaingie Acheni kupiga Ramli. Kwamba wewe una Akili kumzidi Tommy aliyeamua kua chini ya kings Music,.

Tulieni Kings Music Wanakuja kivingine Ni mawe Juu ya mawe, hit baada ya hit
Kiba mwenyewe hajatoka, halafu msanii ukae chini yake unategemea nn?
 
Ali kiba ni msanii mzuri akiacha
1. Dharau
2. Majivuno
3. Kujiona anajua na kujifanya hapendi show of
4. Kubadilika kulingana na nyakati
5. Kuacha kujijaza upepo kuwa yeye ni king wakati yeye siyo baba ake nandy (princess 😀 just kidding)
6. Akishirikishwa afanye kweli (katika nyimbo mbovu ambazo hakufanya cha maana ni NAI NAI ya dimpoz zaidi ya kuipaisha kwa jina)
7. Atafute management iliyokaa kibiashara.
8. Asitafute mchawi maana anajiroga mwenyewe.
9. Ajifunze kujibu maswali kwenye interview.
10. Kusikiliza ushauri na kuacha bifu zisizona maana. Akumbuke tu kuna mwenzie Bob junyo😀 walianza kugombania urais na diamond enzi za kikwete, ati wao ni marais wa wasafi. Nikajiuliza mbona hata mimi ni msafi na sijawahi kushiriki uchaguzi? Leo hii hata sijui mheshimiwa ndugu Jr yuko wapi.

Team king kiba na wenye baba yao msinipige mawe.
 
[emoji23][emoji23][emoji23]
Ali kiba ni msanii mzuri akiacha
1. Dharau
2. Majivuno
3. Kujiona anajua na kujifanya hapendi show of
4. Kubadilika kulingana na nyakati
5. Kuacha kujijaza upepo kuwa yeye ni king wakati yeye siyo baba ake nandy (princess [emoji3] just kidding)
6. Akishirikishwa afanye kweli (katika nyimbo mbovu ambazo hakufanya cha maana ni NAI NAI ya dimpoz zaidi ya kuipaisha kwa jina)
7. Atafute management iliyokaa kibiashara.
8. Asitafute mchawi maana anajiroga mwenyewe.
9. Ajifunze kujibu maswali kwenye interview.
10. Kusikiliza ushauri na kuacha bifu zisizona maana. Akumbuke tu kuna mwenzie Bob junyo[emoji3] walianza kugombania urais na diamond enzi za kikwete, ati wao ni marais wa wasafi. Nikajiuliza mbona hata mimi ni msafi na sijawahi kushiriki uchaguzi? Leo hii hata sijui mheshimiwa ndugu Jr yuko wapi.

Team king kiba na wenye baba yao msinipige mawe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom