UZUSHI Tohara husababisha upungufu wa nguvu za kiume na kuongeza hatari ya maambukizi ya VVU/UKIMWI

Baada ya tathmini, tumebaini kuwa taarifa hii ni ya uzushi
Kuna baadhi ya watu wanaamini kuwa wanaume waliyofayiwa tohara hupata tatizo la upungufu wa nguvu za kiume pindi wanapokua, na ni kundi ambalo lipo katika hatari ya kupata maambukizi ya VVU kwa urahisi ukilinganisha na wale ambao hawajafanyiwa tohara.

Ukweli upoje?

5D4EB701-4F15-42DC-AAB4-980409146A0C.jpeg
 
Tunachokijua
Tohara ni upasuaji mdogo unaofanyika ili kuondoa ngozi ya mbele inayofunika sehemu za siri za mwanamme.

Asili ya utamaduni huu ni imani za kidini, ambazo baadae zilithibitishwa kuwa na faida kiafya. Leo, watu hutahiri kwa sababu za kiafya, au za kidini.

Mwanamme huzaliwa na ngozi inayofunika kichwa cha sehemu zake za siri hivyo kupitia tohara, ngozi hii huondolewa kwa kufanya upasuaji mdogo usiotumia muda mrefu sana, kati ya dakika 15-30. Kwa sababu za kiusalama, pamoja na kuhakikisha kuwa tendo hili linafanyika kwa ufanisi mkubwa, ni vizuri kama likifanywa hospitalini.

Watoto wadogo wanaofanyiwa tohara huwa na faida kubwa ya kutokupata maumivu makubwa kama watu wazima, kutumia muda mchache zaidi kwenye upasuaji pia uponaji wa kidonda huchukua muda mfupi sana kati ya siku 7-10 pekee.

Kwa mujibu wa WHO na Kituo cha Udhibiti na Kinga ya Magonjwa cha Marekani, CDC, tohara huwa na faida kubwa kwa mwanamme ikiwemo kupunguza nafasi ya kuugua Saratani ya uume pamoja na magonjwa mengine ya zinaa hasa VVU/UKIMWI.

Hii inatoa maana kuwa tohara haiongezi nafasi ya kupata maambukizi ya VVU/UKIMWI bali hupunguza nafasi hiyo. Ikumbukwe kuwa ngozi inayofunika umme huwa ni laini na nyepesi sana kuchanika panapotokea msuguano wakati wa tendo la ndoa, hii ni hatari kwa afya na inaweza kuongeza maambukizi ya magonjwa ya zinaa, VVU ikiwemo.

Kuhusu kupunguza nguvu za kiume, ni muhimu kwanza kufahamu kuwa kinachoondolewa wakati wa tohara ni ngozi tu isiyo na athari yoyote kwa ukuaji wa via vya uzazi wa mwanamme, pamoja na ufanisi wake katika kushiriki tendo la ndoa.

Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali za kisayansi, upungufu wa nguvu za kiume huchangiwa na mambo mengi sana, lakini tunaweza kuyagawa kwenye makundi makubwa mawili ambayo ni-
  1. Sababu za kisaikolojia na kihisia
  2. Sababu za kibaiolojia, ambazo huhusisha uwepo wa magonjwa mengine pamoja na baadhi ya changamoto kwenye mfumo wa homoni, au neva za fahamu.
Hadi sasa, hakuna tafiti wa kisayansi unaoonesha kuwa tohara hupunguza nguvu za kiume. Uvumi uliopo mtaani hauna mashiko kisayansi kwa kuwa hauna uthibitisho wa wazi.
MADAI
Kuna baadhi ya watu wanaamini kuwa wanaume waliyofayiwa tohara hupata tatizo la upungufu wa nguvu za kiume pindi wanapokua, na ni kundi ambalo lipo katika hatari ya kupata maambukizi ya VVU kwa urahisi ukilinganisha na wale ambao hawajafanyiwa tohara.

Ukweli upoje?

View attachment 2417307

Tohara inapunguza nafasi ya kupata ukimwi kwa asilimia zaidi ya 60. This is scientifically proven.
Ndio maana mashirika yanadeal na ukimwi yanahusika pia na tohara ili kumfanya mtu asipate ukimwi kwa urahisi.

Tatizo la nguvu za kiume pia si kweli kwa kua wengi wametahiriwa na wanapiga shoo mujarabu kabisa japo hii sina scientific evidence.
 
Tohara inapunguza nafasi ya kupata ukimwi kwa asilimia zaidi ya 60. This is scientifically proven.
Ndio maana mashirika yanadeal na ukimwi yanahusika pia na tohara ili kumfanya mtu asipate ukimwi kwa urahisi.
Tatizo la nguvu za kiume pia si kweli kwa kua wengi wametahiriwa na wanapiga shoo mujarabu kabisa japo hii sina scientific evidence.

Uko sahihi.

Nguvu za kiume hazina uhusiano na kuwepo au kutokuwepo kwa govi.
 
Kuhusu tohara kupunguza nguvu za kiume ni kweli kabisa ingawa kamwe haiwezi kuwekwa wazi. Kwa wale waliofanya tohara wakiwa watu wazima (miaka 18+) wanaweza kuthibitisha hili. Kwamba kinachoathirika zaidi ni uwezo wa kusimamisha uume na siyo uwezo wa kutungisha mimba.

Hivyo ni kweli uwezo wa kusimamisha uume hupungua na huwezi kupiga mfululizo kama ambaye hajafanyiwa tohara ingawa hakuathiri uzazi (fertility).
 
Kuhusu tohara kupunguza nguvu za kiume ni kweli kabisa ingawa kamwe haiwezi kuwekwa wazi. Kwa wale waliofanya tohara wakiwa watu wazima (miaka 18+) wanaweza kuthibitisha hili. Kwamba kinachoathirika zaidi ni uwezo wa kusimamisha uume na siyo uwezo wa kutungisha mimba.

Hivyo ni kweli uwezo wa kusimamisha uume hupungua na huwezi kupiga mfululizo kama ambaye hajafanyiwa tohara ingawa hakuathiri uzazi (fertility).
Si kweli Mkuu, Mimi nilifanyiwa tohara at the age of 19, na Sasa Niko na 40+ year lakini naweza piga miti fora 3 hour bila uume kuanguka,
 
Hivi kwann jf msitulete interface nzuri kama hizi wewe Payge mshauri melo afanye hivyo mkuuu nimeipenda sana hii ramgi umenisikia au
 

Attachments

  • Screenshot_20230324-223210.png
    Screenshot_20230324-223210.png
    47 KB · Views: 14
Kukosa nguvu za kiume waty wengi hawajui tuu sasa wewe una madeni Hadi kupita nje unaogopa au unamawazo mpk unais dunia ndogo sasa utapataje nguvu za Kiume kula vizuri Milo inayotakiwa fanya mazoea then utanipa majibu
 
Shuleni boarding tuliamini alotahiriwa angali mtoto hajitambui ka uume kanakuwa kadogo.

Ila alotahiriwa mkubwa anajitambua ndio anakuwa na mashine haswa.

So timing inaweza kuchangia pia. Lakini hili nalo lichunguzwe. Ili ifahamike umri gani ni sahihi kutahiri mtoto kuepuka kibamia baadae. Tafiti zifadhiliwe na serikali, mzungu hawezi wekeza kwenye hayo mambo labda ukimwi.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom