Tofauti kubwa ya Mwafrika na Mzungu

Umetumia njia zipi za kitafiti (research methodology) au ni kwa mujibu wa maoni yako!

Usitake kupandikiza udhaifu waku Binafsi kwa watu wengine!

Katika kufanya tafiti ya jumla nimegundua moja ya tofauti kubwa kati ya Mwafrika na Mzungu ni kwamba, Sisi waafrika tuna ungana na kushirikiana zaidi kimwili wakati wenzetu wanashirikiana na kuungana zaidi kimawazo na kiakili.

Mzungu akipata elimu, ataandika vitabu ili mwenzake asome aendeleze pale yeye alipo ishia, ataunganisha mawazo yake na ya mwenzake wataunda ama watatengeneza kitu au machine fulani. Ndiyo maana utakuta kifaa kimoja kimetengenezwa na watu wa fani mbalimbali ili kiweze kufanya kazi kwa ufanisi.

Wazungu hawashirikiani kimwili zaidi, ni vigumu kukuta wanapelekeana mialiko kama ya kitchen party au misiba, ni vigumu kujua jirani yake ni nani na anafanya nini. Hata akitoka out na girlfriend wake, kila mtu anatalipia bili yake kwa mfuko wake. Harusi zao hazikusanyi watu wengi na kutumia siku nzima wakila na kunywa labda awe ni mtu maarufu sana!

Sisi waafrika hatuko pamoja kiakili, hata mtu akiwa nawazo zuri kivipi, litadharauliwa na kila mtu kubaki na mambo yake. Tumekuwa wajinga wa kuwa achia wanasiasa kutuamulia nini cha kufanya na nini tusifanye hata kwenye mambo ya kisayansi na utafiti kwa mambo ya kawaida. Wasomi wazuri hawatungi vitabu bali wanakimbilia kwenye siasa, sii ajabu ukakuta profesa haandika kitabu chochote kwa miaka 20 na bado anajiita Profesa!

Waafika tunashindwa kuunganisha tafiti za kisayansi za fani mbalimbali ili kupata kitu bora kwa matumizi ya kila siku na tumebaki kununua vilivyotengenezwa na wazungu. Watunga sera wamekuwa wakidharau hata mawazo ya wengine na kuona ya wazungu ndo bora kuliko ya mwafrika mwenzao. Lakini likija swala la kuzikana, harusi na mengi yanayofanana na hayo, utakuta waafrika wamerundikana utafikiri wana umoja wa kweli!
 
na wewe unaishia kumwambia mwenzako analalamika badala kusema nini kifanyike!

Na wewe pia umeishia kumwambia mwenzio analalamika mwisho ujasema nini kifanyike.
My take:
duniani tunaishi kwa kutegemeana,sio lazima wote wafanye utafiti.
 
mkuu, kabla hatujaendelea na mchango wa uzi wako, naomba ufafanuzi toka kwako. Mzungu ni mtu wa aina gani?
Wewe unafikiri kila mtu mweupe ni mzungu?

mtu mweupe sio mzungu.Mzungu ni yule mtu mwenye pua ndefu kama embasi/sigara
 
Kweli kumwelimisha mwafrika yataka moyo na uvumilivu mwangi sana maana ni kichwa maji
 
Tumeutupa Utamaduni wetu hivyo kupoteza Identity yetu.. Imefikia hata watu kubishana juu ya nani Mwafrika! - Yale yaleeee!. Na kweli maana siku hizi ukitaka kuzungumzia waafrika ni lazima useme - Kusini mwa Jangwa!
 
tatizo hapa kuna watu wako huku kwa ajili ya kupinga hoja za wengine,,, kimsingi hata kama mtu kaleta hoja menzani ni vyema ukamcritisize kwa kutoa arguments zenye mashiko ili ajifunze kupitia wewe... kimsingi ninaueshimu mchango wa mwanajamii MKANDARA maana amejielekeza kutoa argument yenye mantiki....
ninamuunga mtoa hoja kwa sababu zifuatazo:
1. je tanzania tuna maprofesa wanagapi? nafikiri ni wengi lakini kila siku wadau wa elimu wanalia kuwa hakuna vitabu vya kutosha, sasa utaniambia kuwa maprofesa wamefanya kazi ya kutunga vitabu.... na hii inatokana na maprofesa wetu kuwa affected na mfumo wa kisiasa
2. mtanzania ukimwambia akuchangie ili ukasome sahau kabisa lakini ukimwambia ni sherehe basi hata laki kadhaa anatoa? maana yake hatuthamini maendeleo ya wenzetu kwa uoga wa kuzzidiwa na hoja ya kwanini nimsaidie mtu ambaye si ndugu yangu... kwa maana nyingine sisi ni wabinafsi wa maendeleo
zingine zitafuata hapo baadae
 
Umetumia njia zipi za kitafiti (research methodology) au ni kwa mujibu wa maoni yako!

Usitake kupandikiza udhaifu waku Binafsi kwa watu wengine!

Ulivyo andika inaonekana umekurupuka, kama ukipenda fuatilia mtililiko wa thread utapata jibu la wasiwasi wako humo humo, ila kama ukiwa na mtazamo hasi basi ujinga hauta kutoka, utaendelea kuishi vivyo hivyo, na waafrika hatuwezi kuendeleza nchi zetu!
 
Refer the following case study;
American Presidency vs. Tanzanian Presidency, majibu yote utayapata.
 
tatizo hapa kuna watu wako huku kwa ajili ya kupinga hoja za wengine,,, kimsingi hata kama mtu kaleta hoja menzani ni vyema ukamcritisize kwa kutoa arguments zenye mashiko ili ajifunze kupitia wewe... kimsingi ninaueshimu mchango wa mwanajamii MKANDARA maana amejielekeza kutoa argument yenye mantiki....
ninamuunga mtoa hoja kwa sababu zifuatazo:
1. je tanzania tuna maprofesa wanagapi? nafikiri ni wengi lakini kila siku wadau wa elimu wanalia kuwa hakuna vitabu vya kutosha, sasa utaniambia kuwa maprofesa wamefanya kazi ya kutunga vitabu.... na hii inatokana na maprofesa wetu kuwa affected na mfumo wa kisiasa
2. mtanzania ukimwambia akuchangie ili ukasome sahau kabisa lakini ukimwambia ni sherehe basi hata laki kadhaa anatoa? maana yake hatuthamini maendeleo ya wenzetu kwa uoga wa kuzzidiwa na hoja ya kwanini nimsaidie mtu ambaye si ndugu yangu... kwa maana nyingine sisi ni wabinafsi wa maendeleo
zingine zitafuata hapo baadae
Mkuu, hilo la Maprofesa wetu hawawezi kuandika vitabu ikiwa lengo letu ni kuwa kama Ulaya ndio maana tunatumia vitabu vya Ulaya zaidi. Wakiandika vitabu vinavyohusiana na mazingira yetu wananchi hawavitaki isipokuwa vile vilivyoandikwa na wazungu kwa sababu sisi tunataka kuwa kama wao na sii sisi kama sisi..

Kwa hiyo ndio maana utasikia shule haina vitabu vya kusomea (vitabu vya wazungu) na tunaletewa misaada kutoka nje na NGOs. Na ndio maana tumeshindwa, tumeshindwa kuelekeza nguvu zetu kufanikisha mahitaji yetu ktk mazingira tuliyopo isipokuwa kuichubua Afrika iwe kama Ulaya sawa na mawazo ya mdada anayejichubua ngozi ili awe mweupe!..Hivyo, sabuni isiyochua ngozi haina soko.
 
Refer the following case study;
American Presidency vs. Tanzanian Presidency, majibu yote utayapata.

Samaki hawezi kuzaa nyoka, vivyo hivyo jinsi Rais alivyo na Taifa lake vivyo hivyo kwa vile Rais ametoka kwenye jamii hiyo hiyo! Thanks!
 
Mkuu, hilo la Maprofesa wetu hawawezi kuandika vitabu ikiwa lengo letu ni kuwa kama Ulaya ndio maana tunatumia vitabu vya Ulaya zaidi. Wakiandika vitabu vinavyohusiana ana mazingira yetui wananchi hawavitaki isipokuwa vile vilivyoandikwa na wazungu kwa sababu sisi tunatakja kuwa kama wao na sii sisi kama sisi..

Kwa hiyo ndio maana utasikia shule haina vitabu vya kusomea na tunaletewa misaada kutoka nje na NGOs. Na ndio maana tumeshindwa, tumeshindwa kuelekeza nguvu zetu kufanikisha mahitaji yetu krk mazingira tuliyopo isipokuwa kuichubua Afrika iwe kama Ulaya sawa na mawazo ya mdada anayejichubua ngozi ili awe mweupe!..Hivyo, sabuni isiyochua ngozi haina soko.

Tatizo jingine kama ulivyosema ni kwamba tunavidharau vya kwetu na kupenda vya wenzetu. Hatutaki kutumia lugha, utamaduni na hata dini zetu zote tumetupilia mbali tukaona vya kishenzi! Profesa wa kiafrika kiandika kitabu utachoka mwenyewe, utakuta akijitahidi sana ataandika page 300 hata Shigongo anawazidi jinsi anavyo andika hadhidhi za kubuni.

Wachina, wajapan, nk walikataa kulishwa kila kitu, mambo mengine waliaply kwa tamaduni na desturi zao leo wameendelea. Hata haya mambo ya kubuni namna nzuri ya kuongoza nchi wali-implement kwa tamaduni zao, yaani ukikiuka wanakupotezea.

Sisi leo mtu ana Ph D ana rubuniwa na 10% ana tengeneza mkataba wa kuliangamiza Taifa, rasilimali zote anawaachia wazungu na bado yuko kwenye system. Ubinafsi umetawala. Wenzetu fanya ufanyalo lakini ikifika kwa maslahi ya Taifa wanakuwa na msimamo mmoja!
 
Nakubaliana na hiyo tofauti lakini tufanye ni ni?????????

Sija malizia utafiti wangu, lakini kwa hatua za haraka, TUJIKUBALI kwanza kuwa na SISI WAAFRIKA TUNAWEZA kama wao kwani SABABU TUNAZO na UWEZO TUNAO kwani rasilimali nyingi zipo zinazoweza kubadilishwa kwa teknolojia rahisi ili kumudu maisha yetu, japo tutapata taabu mwanzo lakini baada ya miaka kadhaa ya kujichimbia kama walivyofanya wachina tutakuwa na mawazo yetu siyo yao. Tatizo NIA hatuna, tukisha kuwa na NIA ya DHATI tunaweza kuweka mipango yetu bila kutegemea sana wao na tukaweza. Tuwe na NIA ya KUIBA teknolojia na kuzifanyia kazi.

Mtu akigundua namna ya kutengeneza silaha tusimkamate na kufunga tumpe support kwa kuanzia pale alipofikia, atakae gundua madini sehemu tusimfukuze bali tumshirikishe katika kuyachimba, atakae kuwa nanjia bora zaidi namna ya kuwadhibiti majambazi na mafisadi, tumsupport hata kama njia yenyewe ni chungu kwa wahusika. Atakae kuwa na njia ya kuleta mvua kwa njia ya kisayansi asikatazwe bali afundishe na wengine, atakaekuwa na ujuzi wa kuunga mifupa kwa njia salama, asaidiwe kujengewa na hospitali ya kuunga watu mifupa, afundishe wengine na vitabu viandikwe juu ya kuutumia ujuzi huo nk.

Lakini kama tutaona kila kitu chetu ni cha kishenzi ama tukibaki na ubinafsi wa hiki changu, hatutafika mbali. Hapa sisemei ushirikina na uchawi, hayo yabaki kwenye mazingaombwe na sarakasi za maonyesho ili wajipatie kipato. Mtu akigundilika na rudisha nyuma maendeleo kwa kuchawia wenzake-asibaki katika uso wa nchi. Tukienda kwa mtindo huo baada ya karne moja lazima mabadiriko ya wazi yataonekana.
 
Your Thread is Lacking the Following:


  • Relevance,
  • Comprehensiveness, and
  • Reference.

Hili ni jamvi la kuelimishana kiujumla jumla, unataka niweke kila kitu hapa si itakuwa balaa. Watu watachoka kusoma na haitakuwa effective kupata nonacho hitaji. Twende hivi hivi ntakuwa nachambua mwenyewe na kuyaweka kwenye tafiti yangu. Thanks.
 
Analysis yako, Anko Sam, nimeipenda. Tafiti nyingi zimekwishaonesha nini tufanye siyo lazima ueleze wewe kila kitu.Tatizo ni utashi wa kufanya yaliyo sahihi (make tayari yanaeleweka)
 
Back
Top Bottom