Anko Sam
JF-Expert Member
- Jun 30, 2010
- 3,200
- 820
Katika kufanya tafiti ya jumla nimegundua moja ya tofauti kubwa kati ya Mwafrika na Mzungu ni kwamba, Sisi waafrika tuna ungana na kushirikiana zaidi kimwili wakati wenzetu wanashirikiana na kuungana zaidi kimawazo na kiakili.
Mzungu akipata elimu, ataandika vitabu ili mwenzake asome aendeleze pale yeye alipo ishia, ataunganisha mawazo yake na ya mwenzake wataunda ama watatengeneza kitu au machine fulani. Ndiyo maana utakuta kifaa kimoja kimetengenezwa na watu wa fani mbalimbali ili kiweze kufanya kazi kwa ufanisi.
Wazungu hawashirikiani kimwili zaidi, ni vigumu kukuta wanapelekeana mialiko kama ya kitchen party au misiba, ni vigumu kujua jirani yake ni nani na anafanya nini. Hata akitoka out na girlfriend wake, kila mtu anatalipia bili yake kwa mfuko wake. Harusi zao hazikusanyi watu wengi na kutumia siku nzima wakila na kunywa labda awe ni mtu maarufu sana!
Sisi waafrika hatuko pamoja kiakili, hata mtu akiwa nawazo zuri kivipi, litadharauliwa na kila mtu kubaki na mambo yake. Tumekuwa wajinga wa kuwa achia wanasiasa kutuamulia nini cha kufanya na nini tusifanye hata kwenye mambo ya kisayansi na utafiti kwa mambo ya kawaida. Wasomi wazuri hawatungi vitabu bali wanakimbilia kwenye siasa, sii ajabu ukakuta profesa haandika kitabu chochote kwa miaka 20 na bado anajiita Profesa!
Waafika tunashindwa kuunganisha tafiti za kisayansi za fani mbalimbali ili kupata kitu bora kwa matumizi ya kila siku na tumebaki kununua vilivyotengenezwa na wazungu. Watunga sera wamekuwa wakidharau hata mawazo ya wengine na kuona ya wazungu ndo bora kuliko ya mwafrika mwenzao. Lakini likija swala la kuzikana, harusi na mengi yanayofanana na hayo, utakuta waafrika wamerundikana utafikiri wana umoja wa kweli!
Mzungu akipata elimu, ataandika vitabu ili mwenzake asome aendeleze pale yeye alipo ishia, ataunganisha mawazo yake na ya mwenzake wataunda ama watatengeneza kitu au machine fulani. Ndiyo maana utakuta kifaa kimoja kimetengenezwa na watu wa fani mbalimbali ili kiweze kufanya kazi kwa ufanisi.
Wazungu hawashirikiani kimwili zaidi, ni vigumu kukuta wanapelekeana mialiko kama ya kitchen party au misiba, ni vigumu kujua jirani yake ni nani na anafanya nini. Hata akitoka out na girlfriend wake, kila mtu anatalipia bili yake kwa mfuko wake. Harusi zao hazikusanyi watu wengi na kutumia siku nzima wakila na kunywa labda awe ni mtu maarufu sana!
Sisi waafrika hatuko pamoja kiakili, hata mtu akiwa nawazo zuri kivipi, litadharauliwa na kila mtu kubaki na mambo yake. Tumekuwa wajinga wa kuwa achia wanasiasa kutuamulia nini cha kufanya na nini tusifanye hata kwenye mambo ya kisayansi na utafiti kwa mambo ya kawaida. Wasomi wazuri hawatungi vitabu bali wanakimbilia kwenye siasa, sii ajabu ukakuta profesa haandika kitabu chochote kwa miaka 20 na bado anajiita Profesa!
Waafika tunashindwa kuunganisha tafiti za kisayansi za fani mbalimbali ili kupata kitu bora kwa matumizi ya kila siku na tumebaki kununua vilivyotengenezwa na wazungu. Watunga sera wamekuwa wakidharau hata mawazo ya wengine na kuona ya wazungu ndo bora kuliko ya mwafrika mwenzao. Lakini likija swala la kuzikana, harusi na mengi yanayofanana na hayo, utakuta waafrika wamerundikana utafikiri wana umoja wa kweli!