TLS yaingilia kati sakata la Mbowe

TLS yaingilia kati sakata la Mbowe

"Kufanya kongamano haijawahi kuwa kosa la jinai kwa mujibu wa Katiba na Sheria za nchi.

Katiba yetu ibara ya 21(1) inatoa haki ya kujumuika na ibara ya 13(1) inatoa masharti ya watu wote kuwa sawa mbele ya Sheria.

Kitendo cha kumkamata usiku wa manane Mheshimiwa Freeman Mbowe na wenzake, kwa sababu ya kuandaa kongamano ni ukiukwaji wa Katiba na Sheria za nchi yetu.

Ikiwa kuna tuhuma nyingine dhidi yake bado kwa sheria zetu alipaswa kuwa amefikishwa kwenye mamlaka za kisheria na si kuendelea kuzuiliwa.

Natoa mwito kwa mamlaka kumwachia huru kwa sababu kuendelea kumshikilia ni kukiuka utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa Sheria.

Chama cha Mawakili wa Tanganyika tunaendelea kufuatilia kwa ukaribu suala hili na tutatoa msimamo wetu na mwelekeo baada ya mashauriano kufanyika kupitia Baraza la Uongozi".

Rais wa TLS.
Edward HoseahView attachment 1867618
Hi katiba ya Ndungai inawatesa sana watanzania. Safi sana mwenyekiti imarisheni vijana wajiamini zaidi sio kuogopana na kutishiana.

Hili kundi la kukomoana badala ya kutoa na kujibu hoja watasambaratika tu.
 
Hi katiba ya Ndungai inawatesa sana watanzania. Safi sana mwenyekiti imarisheni vijana wajiamini zaidi sio kuogopana na kutishiana.

Hili kundi la kukomoana badala ya kutoa na kujibu hoja watasambaratika tu.
Saana acha tukomae ibadilishwe
 
Hawa TLS wapuuzi Sana wameambiwa mbowe amekamatwa kwa kuandaa kongamano,kwani hawajui kuwa walk kamatwa kwa kongamano wameachiwa mbowe amekamatwa kwa ugaidi


USSR
Mpuuzi ni yule Zulumati NSSF ...kaambulia nini sasa huko alipo...
 
Gaidi Mbowe yupo chini ya ulinzi salama wa Polisi, nchi nzima imetulia hakuna matukio ya ajabu ajabu kama Uamsho walivyowekwa sehemu salama na Zenji ikatulia.
 
"Kufanya kongamano haijawahi kuwa kosa la jinai kwa mujibu wa Katiba na Sheria za nchi.

Katiba yetu ibara ya 21(1) inatoa haki ya kujumuika na ibara ya 13(1) inatoa masharti ya watu wote kuwa sawa mbele ya Sheria.

Kitendo cha kumkamata usiku wa manane Mheshimiwa Freeman Mbowe na wenzake, kwa sababu ya kuandaa kongamano ni ukiukwaji wa Katiba na Sheria za nchi yetu.

Ikiwa kuna tuhuma nyingine dhidi yake bado kwa sheria zetu alipaswa kuwa amefikishwa kwenye mamlaka za kisheria na si kuendelea kuzuiliwa.

Natoa mwito kwa mamlaka kumwachia huru kwa sababu kuendelea kumshikilia ni kukiuka utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa Sheria.

Chama cha Mawakili wa Tanganyika tunaendelea kufuatilia kwa ukaribu suala hili na tutatoa msimamo wetu na mwelekeo baada ya mashauriano kufanyika kupitia Baraza la Uongozi".

Rais wa TLS.
Edward HoseahView attachment 1867618
Waliomshikilia hawapo mitandaoni na wanajua walipo ni vyema mkaenda kuwaambia na kutaja hivyo vifungu vya sheria
 
Ety katiba ya sasa imepitwa na wakati halafu bado mnaendelea kufuata kilichoandikwa humo, kama kawaida ukiitwa mpinzani bc kazi yako ni kupinga-pinga
Kwanini kuna kuwa na Constitution ammandment kila leo bungeni Kama hii haina mapungufu?
Mengi mazuri yapo kwenye hii katiba iliyopitwa na wakati.

Hebu vuta picha sifa za mkuu wa wilaya mbunge kwa mujibu wa katiba jinsi ilivyo upumbavu.
Katiba imesema ajue kusoma na kuandika huku haijasema lugha ipi.
 
Back
Top Bottom