TLS: Mifumo ya Haki Jinai bado haiwezi kuthibitisha Makosa ya Mauaji, Hukumu ya Kifo ifutwe

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,377
8,121
Akizungumza katika kongamano lililowakutanisha wadau kujadili kuhusu adhabu ya Kifo, Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Harold Sungusia amesema mifumo ya haki haipo madhubuti na kuweza kuthibitisha bila kuacha shaka kuwa aliyetiwa hatiani ana kosa

Ameongeza kubwa “Adhabu hii ni hatarishi kwa uhai wa watu ambao hawana hatia, pia ni adhabu ambayo imepitwa na wakati kwa kuwa imejengwa katika mfumo wa kisasi kwamba anayeua na yeye auwawe. Ukitengeneza mfumo wa Haki kwa utaratibu huu hauwezi kubadili makosa ya mkosaji

Sungusia amependekeza kuwepo adhabu mbadala, mtu akitiwa hatiani kwa kosa la kuua apewe kifungo maalumu na ikiwezekana akae kwenye Gereza maalumu la kuzalisha mali na Serikali isitumie fedha zake kuwahudumia ili Wafungwa wafanye shughuli za uzalishaji.

=========
 
Naunga mkono hoja,futa death sentence, utafiti wa kisayansi umethibitisha kuwa sentence hii haileti matokeo chanya, long term in jail ndio inaweza kuondoa tatizo
 
Akizungumza katika kongamano lililowakutanisha wadau kujadili kuhusu adhabu ya Kifo, Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Harold Sungusia amesema mifumo ya haki haipo madhubuti na kuweza kuthibitisha bila kuacha shaka kuwa aliyetiwa hatiani ana kosa

Ameongeza kubwa “Adhabu hii ni hatarishi kwa uhai wa watu ambao hawana hatia, pia ni adhabu ambayo imepitwa na wakati kwa kuwa imejengwa katika mfumo wa kisasi kwamba anayeua na yeye auwawe. Ukitengeneza mfumo wa Haki kwa utaratibu huu hauwezi kubadili makosa ya mkosaji

Sungusia amependekeza kuwepo adhabu mbadala, mtu akitiwa hatiani kwa kosa la kuua apewe kifungo maalumu na ikiwezekana akae kwenye Gereza maalumu la kuzalisha mali na Serikali isitumie fedha zake kuwahudumia ili Wafungwa wafanye shughuli za uzalishaji.

=========
Mean unaua kwa makusudi then unawekwa kwenye Gereza la kuzalisha Mali za serikali?sijawahi kuona upuuzi wa namna hii ,ukiua kwa kukusudia na wewe unyongwe tu dawa ya moto ni moto
 
Wengi wanaopinga adhabu ya kifo ni "wauawaji" tu hivyo wanaogopa adhabu hiyo.
Ebu angalia utakuta wengi wao wanamiliki bunduki na wapo tayari kuzitumia kuua wenzao(hutoa adhabu ya kifo) kwa visingizio mbalimbali lakini wao hawataki kupewa adhabu stahiki bali wanataka wahukumiwe kwa huruma.
 
Back
Top Bottom