Timu ya kampeni ya Lowassa hii hapa

Timu ya kampeni ya Lowassa hii hapa

Umesifia sana kuwa kundi lenu lina nguvu ya kifedha. Nakukumbusha uyanukuu maneno ya marehemu Baba wa Taifa, Mwl. Julius Kambarage Nyerere alisema nini juu ya wagombea wanaotaka kuingia Ikulu kwa kuhonga pesa.

Pia utafakari kwanini Edward Lowassa alijiuzuru nafasi yake ya Uwaziri Mkuu? Ni uchaguzi upi Bashe aliishawahi kushinda hata leo hii ukataka kututhibitishia kuwa hashindwi kwa kila jambo analolitaka? Hivi unaona ni sahihi kwa Mzee Apson kuingia ktk siasa kupitia timu uliyoitaja? Karamagi yupo wapi leo hii?

Unaamini kuwa Peter Serukamba yupo sawa sawa jimboni kwake? Unajua Sophia Simba alipataje nafasi anazoshikilia? Rostam yupo wapi ktk medani za siasa nchini? Kwa kuwa hujui siasa ndio manna unasema kuwa JK hana nguvu ya ushawishi, subiri uone wakati utakapofika, na kwa tathmini hii naimani vijana wake watampelekea, na siku mona atatuonesha nguvu alizonazo.

Kama mulidhani kumuandika ktk magazeti Pinda ni kumbomoa, basi ile taarifa iliyotoka juzi imemjenga sana. Mujitahidi kufikiria kabla hamjafanya, na sio kufanya kwanza halafu ndio mufikirie.
 
Hivi nguvu unazosema kuwa Edward Lowassa anazo ndani ya Chama zipo wapi? Kwanini alikimbilia kugombea nafasi ya ujumbe wa Halmashauri Kuu ktk Wilaya yake wakati anajua kuwa wajumbe watakaopiga kura za kumchagua mgombea kiti cha Urais ni wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa? Huu ulikuwa ushauri mzuri kweli kwa mtu aliyeanza kufanya maandalizi mwaka 2008 kama unavyotaka kutuaminisha humu jamvini?

Kama ana nguvu kweli, kwanini alishindwa kumzuia Bernard Membe aliyeshinda ktk viti 10 vya Taifa pamoja na nguvu kubwa muliyotumia kuwashawishi wajumbe munaodai kuwa ni wenu? Hivi bado munaamini kuwa muna nguvu kweli? Kaeni chini, bila kudanganyana fanyeni tathmini mutaona kuwa, muna vivuli vingi kuliko watu.
 
Hizi ni habari njema kusikia kuwa eti Bernard Membe amejiunga na timu ya Mizengo Pinda. je Edward Lowassa amejiunga na kambi ya nani? Chadema? UKAWA? au UAMSHO?
 
9. Wanndishi wa habari
hili ni group muhimu sana wakiongozwa na Kibanda, Msaki, Pasco, Bakari na kwa sasa bbc iliyoanzishwa hapa nchini.

Hii ni dharau kubwa sana. Bahati nzuri hawa wore nawafahamu, na nina waheshimu sana, lkn kwa mwendo huu naanza kujiuliza kama nilikuwa sahihi.
 
7. Asian Group
Hili group lilijitoa kwa hali na mali kufanikisha kampeni za JK 2005 kwa kutoa fedha nyingi sana sana kama wakina Patel et all....... ila baadaye jamaa waliwageuka na kuwapa mashataka ya EPA wakati dhumuni la fedha hizo zilikuwa za kampeni, kwa hiyo majamaa wamekasirika sana na sasa wamehamisha majeshi kwa Lweiganan... hawa watu kama tunavyojua ni wazuri sana wa kutoa fedha hasa kwa ajili za kampeni Moja wao nilimsikia ofisini kwake akiwaeleza wenzake "huyu mtu sio mtu iko nafiki sana, tumesaidia sana sana ila saizi aacha sisi, iko hakuna shida sisi 2015 iko shinda tena bila problem".

Kawaulize ndugu zako wanaofanya kazi ktk nyumba au makampuni ya kundi hili kama wanapata mshahara sawa na jasho lao. Hivi unaona ni fahari kusifia jambo hili la kipumbavu? Kumbe mukipewa ridhaa ya kutuongoza munataka kuikabidhi nchi hii kwa kundi hili…
 
4. Mzee Chizi
kama umekulia ndani ya ccm uwezi kutofahamu uwezo na umahiri wa mzee chizi..amekuwa mkufunzi wa chama katika miaka mingi sana hivyo ni mtaaluma wa chama anayejua chama vizuri, anayejua misingi ya chama, anayejua conceptual za chama, anayejua theories za chama, anawajua wanachama na misimamo yao... kwa kifupi ni mwanachama wa muda mrefu anayeheshimika katika chama.

Kujua hesabu hakumaananishi kuwa wewe ni mhasibu mzuri. Huyu nitamchambua vizuri ktk taarifa yangu ya sifa za hao uliowataja.
 
Ogepeni saaaana mtu anayepigana vita kimya kimya. Mutashangaa siku ya mwisho hata mkeo atakugeuka. Kama maneno yangekuwa ni ushindi, basi sadam hussein angeshinda vita dhidi ya wamarekani kwa kupitia waziri wake wa mambo ya nje wakati wa utawala wake.
 
ogepeni saaaana mtu anayepigana vita kimya kimya. Mutashangaa siku ya mwisho hata mkeo atakugeuka. Kama maneno yangekuwa ni ushindi, basi sadam hussein angeshinda vita dhidi ya wamarekani kwa kupitia waziri wake wa mambo ya nje wakati wa utawala wake.

team wasira 2015 kama unabisha andamana
 

1. Mzee Apson
Huyu kila mtu anafahamu umahiri wake, amekuwa mkurugenzi wa usalama na ndicho kipindi usalama wa taifa wa Tanzania ulikuwa imara sio tu Tanzania ila na nchi za Africa kote...ni kipindi hichi usalama wa taifa uliweza kulisaidia dunia katika vita ya ugaidi katika kanda hii yote ya Africa na Latin America, na ukisoma kitabu cha Ogot (2012), katika kitabu chake cha current African story to the World anasema pamoja na Tanzania kupata hizo sifa lakini Mzee Apson Mwangonda alistahili pongezi zaidi na zaidi kwa kazi aliyofanya ya kuimarisha amani katika maziwa makuu na kujenga imani kwa nchi za magharibi kwamba africa mashariki kwa ujumla imekomaa katika usalama hasa wa ushushushu; sasa huyo ndio leo ni mwenyekiti wa kampeni ya Lowassa ebu jaribu kupata picha ninayopata sasa hivi...

Duh!
Watalamu ebu shusheni data za huyu Mzee Apson!
1.Ufisadi yumo au hapana?
2.Je hizi sifa anazomwagiwa zina ukweli?
3.Je mtu msafi anawezaje kumsapoti mtuhumiwa?

4. Mzee Chizi
kama umekulia ndani ya ccm uwezi kutofahamu uwezo na umahiri wa mzee chizi..amekuwa mkufunzi wa chama katika miaka mingi sana hivyo ni mtaaluma wa chama anayejua chama vizuri, anayejua misingi ya chama, anayejua conceptual za chama, anayejua theories za chama, anawajua wanachama na misimamo yao... kwa kifupi ni mwanachama wa muda mrefu anayeheshimika katika chama.


Mzee Chizi ndiyo nani tena?


- Membe sasa kanyosha mikono hawezi gemu na sasa kumsapoti Pinda, hii ni baada ya familia ya JK kuacha kumsapoti kwa kuwa jamaa hauziki hata kidogo, hana mvuto wa kisiasa, na zaidi kusapotiwa na familia ya salma imemfanya aonekane ni mtu wa kubebwa bebwa tu wakati wanaume wanapigana wenyewe...Hatuwezi kumpa nchi mtu dhaifu tena na tena...........

Hapa kuna njama kubwa tu na lengo kubwa ni kujaribu kupunguza Nguvu ya Lowasa ndani ya CCM!

Ila kuna taabu mbele ya safari na huu mchezo Wazanzibar ndiyo watakuwa washika Mpini.

Wapinzani wanatakiwa kuanza kufanya utafiti hasa kupitia UKAWA-maana kipindi hiki ni cha Usajili na ni vizuri kuanza mapema na kuwa na Majina tayari kwenye mikoba ili siku ya ufunguzi wa zoezi lenyewe hakuna kupoteza muda mwingi kutafuta taarifa ya wahusika walioomba na wanaofaa kushawishi.
 
Hii timu asilimia kubwa ni wezi wote sijui wakishika uongozi itakuwaje.
genge la wahalifu akina rostam na watoa rushwa wenzake wapeni utawala muwajue,nyie zenu si laki tatu wenzenu wanapiga mabilioni shabikieni sana, nchi hi bado inao watu wazuri wanaoweza kuongoza bila mambo ya rushwa ingawa mmeanza kuwapiga vita
 
Hizi ni habari njema kusikia kuwa eti Bernard Membe amejiunga na timu ya Mizengo Pinda. je Edward Lowassa amejiunga na kambi ya nani? Chadema? UKAWA? au UAMSHO?

Labda ajiunge na ukawa!! Na wakati huo ahamie chadema.
 
Mzee Apson
Huyu kila mtu anafahamu umahiri wake, amekuwa mkurugenzi wa usalama na ndicho kipindi usalama wa taifa wa Tanzania ulikuwa imara sio tu Tanzania ila na nchi za Africa kote...ni kipindi hichi usalama wa taifa uliweza kulisaidia dunia katika vita ya ugaidi katika kanda hii yote ya Africa na Latin America, na ukisoma kitabu cha Ogot (2012), katika kitabu chake cha current African story to the World anasema pamoja na Tanzania kupata hizo sifa lakini Mzee Apson Mwangonda alistahili pongezi zaidi na zaidi kwa kazi aliyofanya ya kuimarisha amani katika maziwa makuu na kujenga imani kwa nchi za magharibi kwamba africa mashariki kwa ujumla imekomaa katika usalama hasa wa ushushushu; sasa huyo ndio leo ni mwenyekiti wa kampeni ya Lowassa ebu jaribu kupata picha ninayopata sasa hivi...


Kamuulize mzee huyu kama yupo tayari tumchambue kwa sifa hizo zilizotajwa hapo juu.
 
Urafik wa watu na uhusiano msipende kugeuza kuwa jukwaa la kisiasa.hata hivyo juhudi hizi zenu za kuchafuana zimeendelea lengo ni kuwa kujenga dhana potofu kwamba edward ameanza kampeni na kujitengenezea kundi lake kabla ya wakati.lkn ukwel ni kwamba ni upofu wa fikra na uoga kujenga mazingira ya kuwapungaza washindani wako kwa kuwaundiza zengwe badala ya kwenda uwanjan na kushindana kwa hoja.acheni siasa za chuki mbona hamwandiki za wengine
 
Back
Top Bottom