Nundu_Tanzania
JF-Expert Member
- Apr 19, 2019
- 811
- 349
Mashaka yangu ni kwamba, unatafsiri na kuelewa maandiko matakatifu: Biblia na Quran kama elimu ya historia. Kama unafikiri maandiko matakatifu ni historia unapotoka.Hakuna historia ya kale iliyonukuliwa nje ya DINI,hili hakuna ndio maana hata wewe unashindwa kunyoosha maelezo na kulenga shabaha katika lengo. Sio tu kuumbwa mwanadamu kulikuja baadae,bali Adam ndio kiumbe wa mwisho kuumbwa na kuumbwa kwake mwishoni hakuonyeshi ya kuwa kabla yake kulikuwa na mtu.
Ni makosa kuelewa moja kwa moja na wakati wote kwamba, Quran na Biblia ni elimu ya historia.
Hivi vitabu ni teolojia na siyo elimu ya historia. Kila simulizi katika Biblia au Quran linakusudia teolojia: Mungu na mwanadamu.