Tigo..... Zawadi zenu feki

Kiranja Mkuu

JF-Expert Member
Feb 18, 2010
4,066
4,085
Tigo wamekuja na wazo zuri la kutoa zawadi.
Lakini wafanyakazi wake wa idara ya i t sio waaminifu hata kidogo.
Wanagawa hizo zawadi kwa marafaiki zao, na wana namba zao za sh. Miamia ambazo huwa wanazitumia kuwasiliana na hao washindi feki.
Naomba kama kuna uwezekano taasisis ya kuzuia na kudhibiti rushwa takukuru ikimulike kitengo cha it cha kampuni hiyo na itaona jinsi haki za watu zinavyodhulumiwa na vihuni vichache.
 
Kiranja Mkuu,

Naamini huna ugomvi na mtu fulani wa TiGO kwenye idara ya IT?
 
Mi sio ndio maana nikasema idara ya i.t ichunguzwe? Laiti ningekuwa na ugomvi na mtu, ningesema fulani achunguzwe
 
hivi we unafikiri kuna bahati nasibu bongo...uwizi mtupu...si cha tigo wala vodacom wala zain...kwanini utakuta leo akishinda mtu wa moshi, siku inayofuata atakuwa wa sumbawanga, siku ingine atakuwa wa tanga, siku ingine atakuwa wa morogoro, siku ingine atakuwa wa dsm...etc, wanapanga kwa kuchagua kabisa kuwa kwa leo ngoja ashinde wa dsm, kwa leo ashinde wa moro etc...hata kama hawasemi, wajuzi wa mambo tunaelewa ndo maana huwa hatuhangaiki na kitu kama icho..nendeni ulaya muone lotto zao zilivyo na uhakika...mtu anashinda kwa uhalali..lakini hapo bongo, ukwizi mtupu...
 
kweli eeehe basi tugomeni kushiriki maana wanatuona sisi ni mabahau.
 
haya mambo bwana .....nakumbuka namba iliyo shinda gari utadhani kama imepangwa ni namba nzuri nadhani nikisema namba nzuri mnaelewa mf: 0713****** huo mfano tu!
 
Nakumbuka mzee wangu aliwahi kuniambia kuwa alicheza bahati nasibu miaka 60 akashinda kret 1 ya bia alipo kwenda kukabidhiwa zawadi yake akapewa bia 2 tu akauliza kulikoni mnipe bia mbili ingali nimeshinda kret moja? akaambiwa umefanya kazi gani hadi tukupe kret ya bia? alikuwa mpole akaondoka zake kimya kimya.....

Kama ni kweli tigo kuna mchezo huu wanatakiwa kuchungunzwa na takukuru mara moja, nimepoteza imani nao hawa jamaa!
 
Mimi nilisha fuatwa mara kadhaa na kuwadi wa hao watu wa i.t, nishiriki lile shindano la milioni moja,
nikichukua hiyo milioni moja nimpehuyo kuwadi laki tisa unusu kisha mi nibaki na hamsini elfu,
nikasema sifanyi dhuluma. Wapeni wanaostahili.

Ikatokea bahati nasibu ya kugombea tv na dish, nikafuatwa nikakataaa.

Leo kaja tena dalali mwingine, anasema wanipe line mpya kisha wanipigie kuwa nimeshinda shilingi millioni mbili.
Nimegoma nimewaambia kuwa mie sio dhulumati...
Wakatafute wahuni kariakoo wawape dili
 
Mimi nilisha fuatwa mara kadhaa na kuwadi wa hao watu wa i.t, nishiriki lile shindano la milioni moja,
nikichukua hiyo milioni moja nimpehuyo kuwadi laki tisa unusu kisha mi nibaki na hamsini elfu,
nikasema sifanyi dhuluma. Wapeni wanaostahili.

Ikatokea bahati nasibu ya kugombea tv na dish, nikafuatwa nikakataaa.

Leo kaja tena dalali mwingine, anasema wanipe line mpya kisha wanipigie kuwa nimeshinda shilingi millioni mbili.
Nimegoma nimewaambia kuwa mie sio dhulumati...
Wakatafute wahuni kariakoo wawape dili
Sasa kiranja mkuu, kwa nini usiwakamatishe kwa jamaa wa takukuru? maana inatia hasira sana unadhani mtu ameshinda kumbe ni usanii tu.... yaani umpe laki tisa na nusu? mmhh aisee ingekuwa ni mimi ningekubali baada ya kutanganza kuwa ni mshindi simpi hata sent tano kiushenzi ili next time hakome kufanya huo uchafu wao!
 
Jamani haya mambo ya bahati na sibu sijui ya milioni 100 sijui gari waachieni wenyewe wanajua wanafanya nini. Hakuna biashara ya hasara ulimwengu huu. Kibaya zaidi ni afrika ambako wizi ni 200%.

Mimi nilishajiwekea utaratibu kwamba ktk maisha yangu ni bidii yangu na baraka za mungu tu ndo vitaniwezesha nifanikiwe maisha na siyo bahati na sibu. Watanzania kama umebahatika kusoma walau hadi degree level jaribuni kuwaelimisha wengine kwamba bahati na sibu za bongo ni wizi mtupu.
 
Hii mii naunga mkono kuwa zawadi za tiGO ni feki.

Kuna jamaa yangu ambaye ana mama yake mdogo anafanya kazi tiGO, aliwahi kupigiwa simu wakati ule tiGO wanatoa zawadi za milioni moja. Mama yake alimwambia anunue vocha ya TZS 10,000 halafu atume ujumbe mara nyingi mpaka hiyo pesa iiishe, halafu yeye atajua jinsi ya kuseti kule tiGO. Aiseee, baada ya muda yule kijana akapigiwa simu kuwa ameshinda milioni moja ya tiGO. Tangu siku hiyo nikiona tiGO wanatangaza zawadi inanijia hisia ya mchezo huo mchafu.

Kweli kama IT wa tiGO wanafanya hivyo waache mara moja.
 
Hii mii naunga mkono kuwa zawadi za tiGO ni feki.

Kuna jamaa yangu ambaye ana mama yake mdogo anafanya kazi tiGO, aliwahi kupigiwa simu wakati ule tiGO wanatoa zawadi za milioni moja. Mama yake alimwambia anunue vocha ya TZS 10,000 halafu atume ujumbe mara nyingi mpaka hiyo pesa iiishe, halafu yeye atajua jinsi ya kuseti kule tiGO. Aiseee, baada ya muda yule kijana akapigiwa simu kuwa ameshinda milioni moja ya tiGO. Tangu siku hiyo nikiona tiGO wanatangaza zawadi inanijia hisia ya mchezo huo mchafu.


Kweli kama IT wa tiGO wanafanya hivyo waache mara moja.


I see!!!
Unajua masikini kuna ndugu yangu amekuwa anatumia nguvu kubwa kucheza hizi bahati nasibu , masikini wa mungu akiamini kuwa iko siku atashinda... mimi nimekuwa mzito sana kuingia kwenye kwenye michezo hii ya bahati nasibu... sasa ndo napata mshtuko zaidi kama kuna uhuni kama huu unaendelea....duu shukrani sana wachangiaji , nitamwonyesha jamaa yangu aone anayoumia bure...
 
Kweli imani imekwisha.
Hivi hao wakulu wa kitengo hicho cha I.T kwani hawaijui michezo hii michafu?
Wanaijua, ila wananufaika nayo.
Maaana haiwezekani vijana wakawa wanacheza rafu, halafu mabosi wao wasijue.
 
Kweli imani imekwisha.
Hivi hao wakulu wa kitengo hicho cha I.T kwani hawaijui michezo hii michafu?
Wanaijua, ila wananufaika nayo.
Maaana haiwezekani vijana wakawa wanacheza rafu, halafu mabosi wao wasijue.

Mimi nahisi watakuwa wanashirikiana... just imagine kitita cha sh. 100M au nyumba au gari... lazima kuna namna..

So disgusting!!
 
Daaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaamn Tigo Daaaaaaaaaaaaaaamn Tigo

Didnt know tiz rubbish business............I have been wasting ma Money a lot wit a hope to WIN

Daaaaaaaaaaaaaaaaaamn Tigo
 
Dah bongo bana yaani kila kitu lazima kipigwe dili.
Ticket za Brazil mtaani watu wanauza kwa dili.
Bahati nasibu nayo dili, tiGo kuweni makini mnaweza mkachafuka.
 
Back
Top Bottom