Kuna makazi huwa yana mambo kweli kweli.
Kuna ardhi ukizichungulia rohoni unakuta zinalia, nyingine zina agano la kuondoka na mtu kila mwaka.
Nyingine ni ardhi zinazokataa watu wake na wanakuwa ni watu wa kutanga tanga.
Haya nimesyashuhudia.
Kingine ambacho wanadamu wanakipuuza ni ile laana aliyopewa Nyoka ya kula mavumbi ya ardhi maisha yake yote kipindi cha Anguko la Adam.
Kiroho laana ile inampa Nyoka(Shetani) uhalali wa kutafuna mwili wa mwanadamu(mavumbi) maisha ya nyoka yote.
Kwa hiyo ukijichanganya tu, jamaa anakuja na ana haki hiyo maana alipewa hilo, sema sisi tulipewa pia haki ya kumponda kichwa japo hatuitumii haki hii.
All in all ardhi ina kinywa cha kunena, ardhi ina sikio la kusikia.
Ardhi ikikukataa kwa sababu ya damu zilizomwagwa juu yake au dhuluma iliyofanyika hapo hata ufanye hipi hutoboi....
Na bahati mbaya sana tunamwaga uhai wa vitu(damu) katika ardhi hio hio.
Mungu atusaidie kwa kweli.