Tiba zenye madhara

Tiba zenye madhara

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,000
Reaction score
828,752
Unapopata tatizo la kiafya...hamu yako ni kupona haraka, hivyo harakati na juhudi za kutafuta tiba huwa kubwa......ni katika hamu hiyo ya kutaka kutibika kwa haraka utapokea ushauri na maelekezo yoyote toka kwa matabibu unaowaamini bila kujali usahihi wa kile wanachokuambia....kidunia tunaambia nusu ya vifo duniani ni kutokana na ushauri wa tabibu.....

Kiroho pia kuna mikanganyiko yake kuanzia kwenye ardhi , makazi, miili yetu mpaka biashara na vitu tunavyomiliki...huku nako kunapata shida ya kiafya lakini kiroho....huku nako kunaugulia na kutafuta tiba...huku nako kuna vita na kuzidiana maarifa....usipokuwa kamili,usipokuwa imara kiroho unapigwa dafrau kubwa usiweze kusimama tena...epuka kuchanganya tiba za kiroho

Ulimwengu wa kiroho ni kitu kikubwa mno na kwa bahati mbaya sana wataalam wajuzi wake ni viumbe waliovaa mwili wa nyama...mwili dhaifu uharibikao...na kwa uoga wao na kutaka sifa hawako tayari kukiri kuwa jambo fulani kwake ni kina kirefu tena kipana
Tunaweka makazi yetu, biashara zetu, ofisi zetu nk juu ya ardhi yenye mambo mengi
Ardhi yenye maagano
Ardhi iliyonajisiwa
Ardhi iliyolaaniwa
Ardhi ambayo ni makazi ya viumberoho
Ardhi iliyofanyiwa kafara ama matambiko
Ardhi ilihobebeshwa roho zilizodhulumiwa, ardhi iliyotwishwa mambo ya ajabu na ya kutisha kabisa
Kwa nia safi kabisa na kwa moyo mweupe unakuja kufanya makazi kwenye ardhi ya namna hiyo ama kufanya biashara

Kwenye mambo kama haya unakumbuka ama unasahau kufanya ibada za kutakasa ardhi na makazi....unaanza biashara yako hapo....lakini pengine tayari kuna wenzako walishaanza kabla yako na kuweka mambo yao sawa
Bila kujua pale unapoingia wewe ndio dampo lililotumika kutupa kila kitu kibaya...unapoanza tu biashara changamoto zinaanza....mwishowe unashauriwa kuwaona wataalam....unakubali na kuanza harakati
Mtaalam wa kwanza anakuja na kufanya yake ...lakini kwa uwezo wake anashindwa kuondoa tatizo bali kuliongeza
Anakuja wa pili na pengine wa tatu....wote hawa kila mmoja ana formula yake...mwisho wa siku bila kujua unakuwa umetengeneza kilinge cha mapambao ya kiroho
Kitakachotokea sasa hapo ni madhara ya kiroho na kimwili kwako wewe, biashara ama makazi yako na hata familia yako kwakuwa kila roho lililopo pale litataka kupigania nafasi yake
Kwenye hizi biashara na makazi yetu, tunapoona mambo hayaendi na changamoto zinakuwa nyingi, rusikimbilie kutafuta na kubadili wataalam...
 
Kuna makazi huwa yana mambo kweli kweli.
Kuna ardhi ukizichungulia rohoni unakuta zinalia, nyingine zina agano la kuondoka na mtu kila mwaka.

Nyingine ni ardhi zinazokataa watu wake na wanakuwa ni watu wa kutanga tanga.

Haya nimesyashuhudia.

Kingine ambacho wanadamu wanakipuuza ni ile laana aliyopewa Nyoka ya kula mavumbi ya ardhi maisha yake yote kipindi cha Anguko la Adam.

Kiroho laana ile inampa Nyoka(Shetani) uhalali wa kutafuna mwili wa mwanadamu(mavumbi) maisha ya nyoka yote.

Kwa hiyo ukijichanganya tu, jamaa anakuja na ana haki hiyo maana alipewa hilo, sema sisi tulipewa pia haki ya kumponda kichwa japo hatuitumii haki hii.

All in all ardhi ina kinywa cha kunena, ardhi ina sikio la kusikia.
Ardhi ikikukataa kwa sababu ya damu zilizomwagwa juu yake au dhuluma iliyofanyika hapo hata ufanye hipi hutoboi....

Na bahati mbaya sana tunamwaga uhai wa vitu(damu) katika ardhi hio hio.

Mungu atusaidie kwa kweli.
 
Kuna makazi huwa yana mambo kweli kweli.
Kuna ardhi ukizichungulia rohoni unakuta zinalia, nyingine zina agano la kuondoka na mtu kila mwaka.

Nyingine ni ardhi zinazokataa watu wake na wanakuwa ni watu wa kutanga tanga.

Haya nimesyashuhudia.

Kingine ambacho wanadamu wanakipuuza ni ile laana aliyopewa Nyoka ya kula mavumbi ya ardhi maisha yake yote kipindi cha Anguko la Adam.

Kiroho laana ile inampa Nyoka(Shetani) uhalali wa kutafuna mwili wa mwanadamu(mavumbi) maisha ya nyoka yote.

Kwa hiyo ukijichanganya tu, jamaa anakuja na ana haki hiyo maana alipewa hilo, sema sisi tulipewa pia haki ya kumponda kichwa japo hatuitumii haki hii.

All in all ardhi ina kinywa cha kunena, ardhi ina sikio la kusikia.
Ardhi ikikukataa kwa sababu ya damu zilizomwagwa juu yake au dhuluma iliyofanyika hapo hata ufanye hipi hutoboi....

Na bahati mbaya sana tunamwaga uhai wa vitu(damu) katika ardhi hio hio.

Mungu atusaidie kwa kweli.
Hili ni la muhumi sana Mshana Jr 'ibada za kutakasa ardhi na makazi'...
Na kwa bahati mbaya sana tunapojaribu kurekebisha mambo...tunazidi kuharibu kwa kuzidi kumwaga damu isiyo hatia ya wanyama na kulisha viumbe vya kuzimu bila kujijua...navyo kwa uroho wao vinapambana
 
.
downloadfile-1.jpg
 
Kiroho hii ndio ardhi iliyolaanika inavyoonekana
b75d76c3a5329e32844167861e6048bb-d5yw0tw.jpg
 
Mkuu umeongea jambo moja safi sana unajua kuna wakati mwingine unaweza kuhisi unaondoa tatizo kumbe unaongeza tatizo
 
Shamba ama kiwanja unachanganya na maji ama kuinyunyiza kama ilivyo kwenye pembe zote nne na katikati ....pia kuzunguka mipaka yote
Kwenye makazi ni hivyo hivyo kuzunguka nyumba nzima ndani na nje
Naweza nuia kupata kitu fulan nanikapata kupitia chumvi
 
Kutakasa ardhi kwa kutumia tiba ya chumvi unaitumia vipi mkuu?
Huo nao ni ushirikina kama ushirikina mwingine tu! Maana mtu anatoka kwa mganga akiwa na hirizi zenye nywele zake na masizi ya zindiko na wewe unatoka kwa nabii ukiwa na kifurushi cha udongo au chumvi iliyofungwa kwenye tambara,ukiwa na chupa yenye maji yaliyonenewa,ukiwa na chupa ya mafuta,ukiwa na chupa ya fruto iliyoombewa,ukiwa na matambara ya nguo za ndugu yako ulizopeleka kwa "NABII"wa kanisa la magunia ili amshughulikie nk!hapo sioni tafauti hata!
 
Huo nao ni ushirikina kama ushirikina mwingine tu! Maana mtu anatoka kwa mganga akiwa na hirizi zenye nywele zake na masizi ya zindiko na wewe unatoka kwa nabii ukiwa na kifurushi cha udongo au chumvi iliyofungwa kwenye tambara,ukiwa na chupa yenye maji yaliyonenewa,ukiwa na chupa ya mafuta,ukiwa na chupa ya fruto iliyoombewa,ukiwa na matambara ya nguo za ndugu yako ulizopeleka kwa "NABII"wa kanisa la magunia ili amshughulikie nk!hapo sioni tafauti hata!
Mimi sio nabii na chumvi sio ushirikina ...hata kwenye Bible inatajwa kama kiua mapooza
 
Mshana nashukuru kwa tiba yako ya kukimbiza wanga usiku, siku hizi nagegeda, siogi mpaka asubuhi.
 
Back
Top Bottom