Tiba ya Dr. Ndodi utapeli mwingine chini ya mwavuli wa Biblia

Dumelambegu

JF-Expert Member
Jan 28, 2011
1,052
257
Ndugu zangu,

Nime-ipost thread hii kwenye Jukwaa la Siasa siyo kwa sababu sijui jukwaa lake muafaka bali ni kwa sababu naamini hili ndilo jukwaa ambalo watu wengi na hususan viongozi wetu wenye dhamana ya uongozi huwa wanasoma na kujumuika nasi. Nimeamua kuandika mambo kadhaa yanayomhusu anayejiita Dr. Ndodi kwa sababu nilivyomfahamu tangu nianze kumsikiliza kupitia kwenye TV sivyo nilivyomshuhudia mwenyewe. Kwa ufupi ni kwamba tiba ya Ndodi ina utapeli uliojificha na bahati mbaya sana Biblia imegeuzwa kuwa kichaka cha kuficha utapeli huo.

Hivi karibuni nilimsikia akiongea kwenye TV kwamba anagawa dawa ya pumu bure na aliwakaribisha wagonjwa kufika kwenye vituo vyake vya Dar, Mwz na Arusha. Mimi ni mmojawapo wa watu waliohamasika na tangazo lake hilo. Nilikwenda kwenye clinic yake ya Magomeni Mwembechai na kukutana na mambo ya ajabu. Kwanza niliambiwa kwamba dawa inauzwa kwa bei ndogo sana ya Sh. 70,000 ambayo ni sawa na bure. Halafu mgonjwa hahitaji kujiandikisha. Nilishtushwa sana na kauli ile lakini kwa sababu ya ugonjwa wa ndugu yangu mmoja ilibidi ninunue hiyo dawa. Baada ya kulipa Sh. 70,000 niliambiwa nimwone Dokta anipe maelekezo ya namna ya kutumia dawa. Hapo ndipo nilipoishiwa nguvu. Niliambiwa na dokta kuwa hiyo ni dawa ya wiki moja na dozi nzima ni wiki 10. Kwa hiyo, nitatakiwa kurudi baada ya wiki moja nichukue dozi nyingine na nitafanya hivyo kwa wiki kumi. Kwa maneno mengine, dozi ya pumu inaiuzwa Sh. 700,000. Maneno hayo yalinishtua sana. Nilimwambia dokta kwamba sitakuwa na uwezo wa kulipa dawa yote. Yeye akaniambia hawezi kurejesha hela na mbaya zaidi eti hata dawa niliyonunua haiwezi kunifikisha mbali kwani ni moja ya kumi tu ya dozi nzima.

Jambo nalojiuliza ni kwamba kwa nini Ndodi hawi mkweli anapotangaza dawa zake kuhusu dawa zake? Jambo la pili ni je, gharama hizo zinatokana na nini? Je, maandalizi ya dawa yanamgharimu kiasi hicho?!

Ukweli ni kuwa huu utitiri wa watu waojiita madokta na wanakuja kwa njia ya kidini inabidi Serikali iingilie kati. Naona kuna utapeli fulani unafanywa kwa kupitia afya za watanzania. Serikali lazima iwabane watu kama akina Ndodi ili kunusuru wagonjwa wanaofanyiwa utapeli mkubwa wa aina hii. Imefika mahali nawaza kwamba kwa nini Sekta ya Afya nayo isiwe na Mdhibiti kama ilivyo kwenye sekta zingine. Viongozi mnaosoma jukwaa hili tusaidieni tafadhali.
 
Ndugu zangu,

Nime-ipost thread hii kwenye Jukwaa la Siasa siyo kwa sababu sijui jukwaa lake muafaka bali ni kwa sababu naamini hili ndilo jukwaa ambalo watu wengi na hususan viongozi wetu wenye dhamana ya uongozi huwa wanasoma na kujumuika nasi. Nimeamua kuandika mambo kadhaa yanayomhusu anayejiita Dr. Ndodi kwa sababu nilivyomfahamu tangu nianze kumsikiliza kupitia kwenye TV sivyo nilivyomshuhudia mwenyewe. Kwa ufupi ni kwamba tiba ya Ndodi ina utapeli uliojificha na bahati mbaya sana Biblia imegeuzwa kuwa kichaka cha kuficha utapeli huo.

Hivi karibuni nilimsikia akiongea kwenye TV kwamba anagawa dawa ya pumu bure na aliwakaribisha wagonjwa kufika kwenye vituo vyake vya Dar, Mwz na Arusha. Mimi ni mmojawapo wa watu waliohamasika na tangazo lake hilo. Nilikwenda kwenye clinic yake ya Magomeni Mwembechai na kukutana na mambo ya ajabu. Kwanza niliambiwa kwamba dawa inauzwa kwa bei ndogo sana ya Sh. 70,000 ambayo ni sawa na bure. Halafu mgonjwa hahitaji kujiandikisha. Nilishtushwa sana na kauli ile lakini kwa sababu ya ugonjwa wa ndugu yangu mmoja ilibidi ninunue hiyo dawa. Baada ya kulipa Sh. 70,000 niliambiwa nimwone Dokta anipe maelekezo ya namna ya kutumia dawa. Hapo ndipo nilipoishiwa nguvu. Niliambiwa na dokta kuwa hiyo ni dawa ya wiki moja na dozi nzima ni wiki 10. Kwa hiyo, nitatakiwa kurudi baada ya wiki moja nichukue dozi nyingine na nitafanya hivyo kwa wiki kumi. Kwa maneno mengine, dozi ya pumu inaiuzwa Sh. 700,000. Maneno hayo yalinishtua sana. Nilimwambia dokta kwamba sitakuwa na uwezo wa kulipa dawa yote. Yeye akaniambia hawezi kurejesha hela na mbaya zaidi eti hata dawa niliyonunua haiwezi kunifikisha mbali kwani ni moja ya kumi tu ya dozi nzima.

Jambo nalojiuliza ni kwamba kwa nini Ndodi hawi mkweli anapotangaza dawa zake kuhusu dawa zake? Jambo la pili ni je, gharama hizo zinatokana na nini? Je, maandalizi ya dawa yanamgharimu kiasi hicho?!

Ukweli ni kuwa huu utitiri wa watu waojiita madokta na wanakuja kwa njia ya kidini inabidi Serikali iingilie kati. Naona kuna utapeli fulani unafanywa kwa kupitia afya za watanzania. Serikali lazima iwabane watu kama akina Ndodi ili kunusuru wagonjwa wanaofanyiwa utapeli mkubwa wa aina hii. Imefika mahali nawaza kwamba kwa nini Sekta ya Afya nayo isiwe na Mdhibiti kama ilivyo kwenye sekta zingine. Viongozi mnaosoma jukwaa hili tusaidieni tafadhali.

Pole wee! unategemea anapata wapi fedha za kusafiri kwa ndege mkoa kwa mkoa na kulipia vipindi kwenye TV zote nchini? Tafakari!
 
Hata mm ninamashaka na uendeshaji wa biashara yake japo sina uhakika na kama dawa zinatibu kweli.Kwa jinsi nilivokuwa namsikia kwenye TV na nilivoenda pale kuulizia dawa niliona tofauti kubwa.Mpka leo siangalii tena vipindi vyake.
 
nenda mahakamani bwana , huu ni wizi wa wazi wazi kabisa

Nadhani hilo ni wazo zuri. Labda nitakachokosa ni evidence ya kipindi cha TV alichosema anatoa dawa bure. Nimeendela kumtafakari huyu Ndodi kiasi cha kuanza kushawishika kuwa huenda pia anakula na watu wa vyombo vya habari hususan StarTV. Zile picha zinazoonyesha wananchi wengi wamejaa kwenye viwanja wanamsikiliza huenda huwa zinachakachuliwa kwa mnajili ya kumpromote.
 
Changa la macho hilo....hapo ushapigwa mtu wangu!.... kaka mjini si shule,mjini ni akili kum-kichwa
 
mwiz tu, afu ana elimu ndogo. kaz kujichkesha tuu star tv. kwel mjin pagumu, duh
 
Ndodi mwizi na mshenzi mkubwa. Anawaibia sana wagonjwa. Kazi yake kujichekeshachekesha kama yupo mitaa ya ohio na kinondoni.
 
Watanzania wenzangu tafakarini jambo kabla ya kutenda. Mimi nilijua tangu awali kwamba Ndodi ni tapeli anayetumia Biblia kurubuni watu ili wateja wawe wengi. Kuna wakati huwa wanaonyesha mikutano yake ya hadhara anayoifanya maeneo anayotembelea. Baadhi ya picha ni za kuchakachua. Anachanganya na picha za matukio mengine ili kuwavuta watu. Ni mwizi mkubwa sana huyo.
 
Pole sana ndg yangu!Hp Tz ubinadamu ulikwisha wekwa rehani,Dk Ndodi hana hata huruma na walalhoi hata kidogo,ukimfuatilia sana zamani alikuwa anasafiri mwenyewe kwa ndege DAR -MWZ,DAR-AR,siku hizi anasema ana wawaklishi wake ktk mikoa hiyo.

KWA NINI TIBA NYUMA YA PAZIA YA IMANI?
Ili aweze kupat soko la uhakika,waumini ni watu rahisi na muhimusana kuwateka kupitia biblia!

SERIKALI KUTOKUWA MAKINI
Si Ndodi tu,hapa Tz tiba imekuwa biashara huria sana kuliko nyingine.Kuna vi-dispensari vidogo kama VIBANDA VYA SIMU ambavyo havina hata anuani!Ni kweli ukaguzi huwa unafanyika lakini sote tumekuwa mashahidi bado vinaendelea kutoa TIBA feki na duni kwa wananchi.

ANGALIA MATANGAZO
Ukipita mitaani utakutana na matangazo ya ajabu ajabu!Mbaya zaidi yanaandikwa kwenye MAGAZETI YA UKWELI/ UDAKU!WAGANGA WANATANGAZA KUTIBU HADI UKIMWI,na wakati huo serikali iko kimya,KWA NINI HAIPIGI MARUFUKU MATANGAZO HAYO?Je huo siyo wizi wa pesa za wananchi ambao wanasumbuliwa na magonjwa sugu?

HATA WEWE NI DK MUULIZE BABU YAKO MTI WENYE DAWA YA KWELI NA UHAKIKI.
 
Pole sana ndg yangu!Hp Tz ubinadamu ulikwisha wekwa rehani,Dk Ndodi hana hata huruma na walalhoi hata kidogo,ukimfuatilia sana zamani alikuwa anasafiri mwenyewe kwa ndege DAR -MWZ,DAR-AR,siku hizi anasema ana wawaklishi wake ktk mikoa hiyo.

KWA NINI TIBA NYUMA YA PAZIA YA IMANI?
Ili aweze kupat soko la uhakika,waumini ni watu rahisi na muhimusana kuwateka kupitia biblia!

SERIKALI KUTOKUWA MAKINI
Si Ndodi tu,hapa Tz tiba imekuwa biashara huria sana kuliko nyingine.Kuna vi-dispensari vidogo kama VIBANDA VYA SIMU ambavyo havina hata anuani!Ni kweli ukaguzi huwa unafanyika lakini sote tumekuwa mashahidi bado vinaendelea kutoa TIBA feki na duni kwa wananchi.

ANGALIA MATANGAZO
Ukipita mitaani utakutana na matangazo ya ajabu ajabu!Mbaya zaidi yanaandikwa kwenye MAGAZETI YA UKWELI/ UDAKU!WAGANGA WANATANGAZA KUTIBU HADI UKIMWI,na wakati huo serikali iko kimya,KWA NINI HAIPIGI MARUFUKU MATANGAZO HAYO?Je huo siyo wizi wa pesa za wananchi ambao wanasumbuliwa na magonjwa sugu?

HATA WEWE NI DK MUULIZE BABU YAKO MTI WENYE DAWA YA KWELI NA UHAKIKI.

Tunahitaji viongozi wenye uchungu na wananchi wake. Kama viongozi wanasoma threads hizi tunawaomba sana wachukue hatua madhubuti ili kuwadhibiti matepeli kama akina Ndodi.
 
Mwanzoni alivyaanza, katibu wa wizara ya afya alisema kupitia kipindi cha asubuhi TBC kuwa alipigwa marufuku kwa kukiukwa maadili ya utabibu ya kutangaza dawa zake kwenye vyombo vya habari.
Kwa muda hakuonekana akiwahadaa wananchi, mara ghafla akaanza tena kuonekana,sijui ni nini kilifanyika,,huenda mlungula ulitembea, make hakuna kinachoshindikana tz.
 
Huo ni wizi wa mchana.Inawezekana TRA nayo imezubaa kwa kutomtoza kodi ya mapato mtu huyu!
 
Ndodi ni mwizi wa kutupa, ukiona mwanaume anaongea maneno mia tatu kwa sekunde moja ujue kuna kasoro. Kila kitu anakijua yeye ni nani? hivi jamani hawa watu wanakuja kwa gear hizo basi tufunge mahospitali au hatuna haja ya kuwa na madactari bingwa. Ndodi nafikiri kitu asichokiweza ni Operation vilivyosalia vyote yeye anajua.

Mungu tunusuru, hawa vibaka wanaokuja kwa njia hiyo wakomeshwe, wanatupeleka kusiko.

Asante sana kwa kutuzindua mzee. Huyo sasa hivi atachekea TRA we ngoja.
 
Viongozi wenye dhamana ya kuongoza nchi hii tafadhali tusaidieni kuwafutilia mbali matapeli aina ya akina Ndodi. Hawana hata huruma kutapeli wagonjwa ambao kimsingi walipaswa wasaidiwe. Tunaomba Mamlaka husika ziingilie kati kufanya uchunguzi wa kina wa dawa na gharama anazowatoza wagonjwa na hatua stahili zichukuliwe.
 
WaTZ ni wagonjwa na mfumo wa tiba ni mbovu. Tumemiminika kwwa wingi kwa waota ndoto, wapiga ramli na wajanja wa mjini na vijijini. Na bahati nzuri serikali imetoa baraka zote. Ilianzia kwa Shehe Yahaya kwa kumruhusu kutoa ulinzi wa majini kwa Bwana Mkubwa Kabisa. Hakuna cha kushangaa, kwani si kuna wakati tuliletewa waganga wa mvua kutoka Thailand? Sasa Ndugu Nape, mtavua magamba mangapi?
 
Back
Top Bottom