Wizara ya Afya Tanzania
Official Account
- Oct 1, 2020
- 58
- 124
Wajawazito wapo katika hatari kubwa zaidi ya kupata ugonjwa wa Malaria katika Jamii. Dawa ya SP hutolewa kukinga madhara ya Malaria kwa kuua vimelea vinavyojificha kwenye kondo la nyuma.
TIBA KINGA YA MALARIA KWA WAJAWAZITO (SP)
Malaria wakati wa ujauzito ni hatari zaidi kwa mama na mtoto aliye tumboni mwake. Tiba kinga wakati wa ujauzito, matumizi ya vyandarua vyenye dawa pamoja na tiba sahihi pale mjamzito anapougua malaria ndizo mbinu zinazoainisha kuwa na ufanisi katika kujikinga dhidi ya malaria na madhara yake wakati wa ujauzito
Tiba Kinga kwa kutumia dawa ya SP hutolewa kwa vipindi wakati wa ujauzito. Mjamzito anatakiwa apate dozi 3 au zaidi katika kipindi chake chote cha ujauzito.
Tafiti zinazonesha kuwa idadi kubwa ya Wajawazito wanachelewa kuanza mahudhurio ya Kliniki na hivyo kusababisha kutomaliza dozi zote za tiba kinga zinazotakiwa kwa mjamzito.
Madhara ya Malaria kwa Mjamzito
Malaria wakati wa ujauzito huweza kusababisha madhara yafuatayo;
Tiba Kinga kwa kutumia dawa ya SP hutolewa kwa vipindi wakati wa ujauzito. Mjamzito anatakiwa apate dozi 3 au zaidi katika kipindi chake chote cha ujauzito.
Tafiti zinazonesha kuwa idadi kubwa ya Wajawazito wanachelewa kuanza mahudhurio ya Kliniki na hivyo kusababisha kutomaliza dozi zote za tiba kinga zinazotakiwa kwa mjamzito.
Madhara ya Malaria kwa Mjamzito
Malaria wakati wa ujauzito huweza kusababisha madhara yafuatayo;
- Upungufu mkubwa wa damu mwilini
- Mimba kuharibika
- Kujifungua mtoto njiti au mtoto mwenye uzito pungufu (Chini ya kilo mbili na nusu)
- Kujifungua mtoto mfu
- Afya ya Mama kudhoofika
- Kifo huweza kutokea kwa mama na mtoto
UJUMBE MUHIMU JUU YA TIBA KINGA YA MALARIA KWA WAJAWAZITO
- Wajawazito wapo katika hatari zaidi ya kupata maambukizi ya ugonjwa wa malaria kuliko watu wengine kwa sababu mwili wa mjamzito unapungua nguvu ya kupambana na magonjwa
- Vimelea vya malaria vinaweza kujificha kwenye kondo la nyuma la mama na hivyo kuathiri ukiaji wa mtoto ingawaje mama anaweza kuonekana mwenye afya
- Kwa sasa inashauriwa kutumia dozi tatu au zaidi za SP wakati wa ujauzito ili kuzuia maambukizi ya malaria kwa mama na mtoto aliye tumboni
- Ugonjwa wa malaria wakati wa ujazito unaweza kusababisha mtoto kuzaliwa na uzoto mdogo au mimba kuharibika
- Weka wazi hali yako ya ujauzito na wahi Kliniki ili uweze kupata huduma stahiki za pamoja zinazotolewa
- Wajawazito wafuate ushauri na maelekezo ya mtoa huduma za afya
- Huduma ya Tiba Kinga dhidi ya Malaria kwa Wajawazito kwa kutumia SP hutolewa katika vituo vya kutolea huduma za Afya bila malipo
Ujue Ugonjwa wa Malaria: Dalili, Madhara, Kinga, Tiba, Malaria kwa Wajawazito na Mpango wa Serikali katika kuzuia Malaria
Malaria ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea vinavyojulikana kama 'Plasmodium' ambavyo huenezwa na mbu jike aina ya Anofelesi. Ugonjwa wa Malaria huenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine pale mbu mwenye vimelea vya malaria anapomuuma mtu mwingine na kuacha vimelea mwilini mwake. DALILI...
www.jamiiforums.com
Mambo ya kuzingatia katika Kudhibiti Mbu waenezao Malaria, Uchunguzi wa Ugonjwa na Tiba sahihi ya Malaria
Mambo muhimu juu ya udhibiti wa Mbu waenezao Malaria kwa njia za Utangamano; Matumizi sahihi ya Vyandarua vyenye dawa kwa kila mwanajamii kila siku Upulizaji viuatilifu ukoko kwenye kuta ndani ya nyumba ni njia fanisi ya kuua mbu waenezao malaria na hivyo kupunguza maambukizi ya malaria...
www.jamiiforums.com