Tiba ya chunusi

Tiba ya chunusi

clinician

JF-Expert Member
Joined
Mar 5, 2014
Posts
2,334
Reaction score
5,527
Wakuu, binafsi ni muathirika mkubwa wa chunusi. Ni wazi kuwa dawa nyingi zinazopatikana madukani either hazisaidii ama huondoa tatizo hili kwa muda tu kisha linarudi palepale.Kwa waathirika wa chunusi hamna haja ya kuelezea kero tunayokumbana nao.

Well kwa mara ya kwanza inaonekana kuna solution imepatikana itakayomaliza kabisa tatizo la chunusi. Ni kitabu cha mike walden kiitwaco acne no more, anaelezea kuhusu mabadiliko katika mfumo wa maisha haswa vyakula mazoezi n.k katika kupata solution ya kudumu ya chunusi.

Nimekuwa nikisoma review ya kutabu hiki mtandaoni kwa muda mrefu sasa na nimeshawishika kujaribu.Tatizo ni kwamba kwa sasa sina uwezo wa kukinunua kitabu hiki kwa kuwa kinauzwa dola 37.

Pili kinauzwa mtandaoni na sina uzoefu wa manunuzi ya online.Hivyo basi kwakuwa nafahamu tatizo la chunusi ni la watu wengi na humu ndani kuna watu wenye uwezo wa kukinunua kitabu hicho online.

Nimelileta kwenu hili kwa msaada. Ni kitabu cha soft copy hivyo atakayekinunua ana uwezo wa kunipa then nikamchangia gharama ya manunuzi.

Kwa yeyote atakayekubali kununua kitabu hiki kina guarantee ya kurudishiwa pesa yako kama utahisi umedanganywa.Kuhusu matokeo utakayoyapata kulingana na review nilizosoma ni kwamba usiwe na mashaka kabisa tatizo ni kwamba baadha ya watu wamekuwa wakikosoa mfumo mgumu wa maisha haswa ulaji ulioelekezwa kwenye kitabu hiko.

Hivyo basi kitabu hiku ni kwa watu ambao wapo serious na tayari kufuata program hii inayodaiwa kuwa ngumu kiasi ili kumaliza kabisa chunusi zao.

Kwa maelezo zaidi tembelea www.acnenomore.com.
 
Wamekulipa sh. ngapi kuja kuwatangazia hicho kitabu hapa? Eti umesoma review mtandaoni. Hizo review si wanaandika wenyewe tu hawa matapeli? Kuna free information tena kutoka reputable sources mtandaoni kuhusu tiba na prevention ya chunusi. Just Google but always be careful. Nitarudi baadaye na kuweka links nzuri tu za institutes mbalimbali. Kweli na akili yako unategemea mtu atoe dola 37 kununua soft copy ya kitabu cha chunusi? At this time and age?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom