tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 26,021
- 25,424
Baada ya kudorora kwa huduma za afya hapa nchini, wameibuka waganga wa kienyeji wanaojiita TIBA MBADALA na wamekuwa wakitumia kila mbinu kujitangaza kupitia kwenye vyombo vya habari kama TV, redio, magazeti, mitandao ya kijamii, nk.
Mwaka juzi nilitembelea mganga mmoja aliyeko Temeke kwa lengo la kufanya utafiti. Nilichokipata kule kinasikitisha sana. Aidha, jana nilikuwa nafanya utafiti kupitia redio ya TBCCM. Kuna mganga mmoja alikuwa anaelezea magonjwa ya ngozi akasema kwamba ugonjwa wa candiasis unaathiri hadi ngozi ya miguu na kichwa! Nilimshangaa sana. Hawa watu ni wauaji---ukiwasikia wanaongea utagundua kwamba ni 'weupe' sana....wako shallow sana na ni mbumbumbu wa kutupwa.
Inashangaza pamoja na udhaifu huu wote bado watu wanavyowashobokea. Kwao, kila mmea ni dawa na hakuna ugonjwa watakaosema wanashindwa kuutibu! Serikali inapaswa kuwa makini na makanjanja hawa wasiendelee kuupotosha umma. Dawa zao zifanyiwe uhakiki na watueleze namna dozi ya maji inavyoweza kutibu malaria.
Nawasilisha
:israel:
Mwaka juzi nilitembelea mganga mmoja aliyeko Temeke kwa lengo la kufanya utafiti. Nilichokipata kule kinasikitisha sana. Aidha, jana nilikuwa nafanya utafiti kupitia redio ya TBCCM. Kuna mganga mmoja alikuwa anaelezea magonjwa ya ngozi akasema kwamba ugonjwa wa candiasis unaathiri hadi ngozi ya miguu na kichwa! Nilimshangaa sana. Hawa watu ni wauaji---ukiwasikia wanaongea utagundua kwamba ni 'weupe' sana....wako shallow sana na ni mbumbumbu wa kutupwa.
Inashangaza pamoja na udhaifu huu wote bado watu wanavyowashobokea. Kwao, kila mmea ni dawa na hakuna ugonjwa watakaosema wanashindwa kuutibu! Serikali inapaswa kuwa makini na makanjanja hawa wasiendelee kuupotosha umma. Dawa zao zifanyiwe uhakiki na watueleze namna dozi ya maji inavyoweza kutibu malaria.
Nawasilisha
:israel: