DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,152
Kada wa Chama Cha Mapinduzi CCM, Mtaalamu wa ardhi na Mjasiriamali Kijana Bw. Thom Mnkondya, Leo Jumanne Julai Mosi, 2025, amechukua rasmi fomu ya kuwania nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Tunduma kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika Ofisi za CCM Wilaya ya Momba.
Thom, ambaye amejizolea heshima kutokana na mchango wake mkubwa katika sekta ya ardhi, upimaji na uwezeshaji wa jamii kupitia elimu na uwekezaji, anaingia kwenye kinyang’anyiro hicho akiwa na ajenda ya maendeleo jumuishi na ushirikishwaji wa vijana na makundi yote ya jamii.
Kupitia taasisi alizozianzisha na kuziongoza, zikiwemo LAPEX Group Ltd na LAPEX Properties, Thom amekuwa mstari wa mbele katika kutatua changamoto za ardhi, kutoa ajira, na kuhamasisha matumizi bora ya ardhi kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Hatua yake hii ya leo imepokelewa kwa hamasa kubwa na wananchi, hasa vijana, ambao wamekuwa mstari wa mbele kumuunga mkono wakiamini kuwa ana dira sahihi kwa mustakabali wa Tunduma.
Kupitia taasisi alizozianzisha na kuziongoza, zikiwemo LAPEX Group Ltd na LAPEX Properties, Thom amekuwa mstari wa mbele katika kutatua changamoto za ardhi, kutoa ajira, na kuhamasisha matumizi bora ya ardhi kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Hatua yake hii ya leo imepokelewa kwa hamasa kubwa na wananchi, hasa vijana, ambao wamekuwa mstari wa mbele kumuunga mkono wakiamini kuwa ana dira sahihi kwa mustakabali wa Tunduma.