Nani anajua kitu ambacho huwa wanajadili?Kuna wakati huwa wanajadili sana maisha ya watanzania.Wamesahau kuwa watanzania weng hawajui kingereza.Nadhani ni bora wabadili lugha na kuwa kiswahili.
Kwa mfano mdahalo gani wa kiswahili unaendeshwa na TBC Huwa na hoja nzito zenye maana?Tatizo hapa ni lugha? Hiki kipindi wanalenga kundi la watazamaji wanaojua kiingereza, mbona wanayo midahalo mingi ya Kiswahili?
Pamoja na mapungufu yaliyoainishwa hapo juu, kubwa zaidi ni pale mwenyekiti anapoonesha kuwa anajua kila kitu, kwa ujumla hata kwa kiingereza kipindi hakina mvuto.
Tizo1, kasumba ya matumizi ya lugha ya Kiingereza imetufikisha pabaya, mikutano yote ya maana, semina, warsha na makongamano, yote huendeshwa kwa Kiingereza.
Juzi juzi nimehudhuria mkutano wa uwekezaji Ziwa Tanganyika uliofanyikia Sumbawanga, waliwahamasisha wakazi wa kanda yote hiyo kujitokeza kwa wingi, watu walijitokeza mamia kwa maelfu, wakawafungia vipaza sauti. Mkutano kuanza, eti unaendeshwa Kiingereza huku ukitangazwa live na TBC!, kisa, eti tumewaalika mabalozi na wawekezaji wakubwa!. Mada karibu zote zimeandikwa Kiingereza!.
Kwa mfano mdahalo gani wa kiswahili unaendeshwa na TBC Huwa na hoja nzito zenye maana?
Acheni mambo yenu kujifanya hamjui hku mnajua hta mahakamani hukumu inaandikwa kwa kiingereza
Wabadilishe lugha wengi wanufaike, sababu kama wamelenga ujumbe uwafikie mpaka walioko mashambani itakuwa rahisi zaidi
mimi huwa sikosi hiki kipindi, vijana wengi wanaangamia kwa kukosa maarifa ya wazee!