This Mchepuko is another level to my wife, mpaka najuta

This Mchepuko is another level to my wife, mpaka najuta

Lara 1 kila mtu anamapokeo tofauti sio kila mwanamke ni muelewa wengine akiona kapewa lifti mwanamke mwenzie nyumbani hapalaliki
 
Basi nikawa nasoma haraka haraka ili nijue unataka ushauri kuhusu nini. Nilichokutana nacho kimenivunja mbavu. Eti liwalo na liwe. Michepuko siyo dili jamani. Usingekuwa na mchepuko ungetumia bidii zako zote kumuelimisha mkeo hayo mambo ya kiyosaki.

Lakini kwa kuwa tayari kuna mchepuko unaona uvivu. Nimewahi kusoma kanuni moja ya T.D. Jakes ya 80 kwa 20 na ina ukweli mkubwa. Unapomuoa barafu wako wa moyo anakuwa na mazuri 80% na 20% unayavumilia.

Mahaba yakipungua kama ilivyo kawaida ya mahusiano yote unaanza ku-focus kwenye ile 20% ya mapungufu. Ukikutana na mchepuko unaangalia tu ile 20% unayoikosa kwa mwenzio unaiona kama 100%. 80% ya mapungufu yake huioni. Ndo wewe sasa. We endelea tu. Liwalo na liwe.
 
Na ww kwa uchoyo mbona husemi ni.biashara gani ama ni
 
Hahaha aisee nimecheka sana..ila ni kweli kuna michepuko.mingine inakuwaga makini na maendeleo kuliko hata mwenza wa ndoa
 
Kama hamjazaa piga chini mkeo nenda kwa mchepuko, ila tahadhali baada ya mda jua utakutana na next mchepuko ambapo utaona the current mchepuko pia una madhaifu.
Ila pia hujaeleza madhaifu ya huo mchepuko tupime kama ulivyofanya kwa mkeo kuweka bayana madhaifu yake
 
Me nikuambie tu acha ufala...huyo ni mkeo na yule ni mpita njia,wewe jukumu lako nikumhudumia mkeo hata kama hana kazi,upendo ni zaidi ya pesa au uwezo wakutafuta pesa,..huyo unayefanya nae biashara atakuja kukufanyia biashara na wewe ndivyo tofauti ya watu walivyoumbwa...acha ufala...tulia na mkeo mueleze ukweli kwa sababu hata huyo mwanamke anajua kuwa una mke....
 
Unamzibia risiki tu huyo msichana atakuwa mchepuko wako wewe forever??Ulishajiuliza hilo??Wewe upo na ndoa yako na mchepuko unae unataka upate kote kote mkuu?? Au una mustakabali gani na huo mchepuko?
A REMINDER:KILA MTU NA MAPUNGUFU YAKE HATA HUYO MCHEPUKO!!
Na ingelikuwa umemuoa huyo ungekuja kulalama hapa kazaa sijui "left over" nna wasiwasi anampenda alozaa nae blah blah blah:A S confused::A S confused::A S confused:Hamjielewi kabisa nyinyi viumbe!!
 
Wewe na mkeo akili zenu moja.Sasa kama unahisi umepaniki kimawazo kwanini uendelee kuganda nakusubir takrima kutok kw mchepuko...ptuuuu ....ndo waleee wanaume suruali jichanganye fany yko mfunfishe mkeo nae atajichangany2.
 
1000000+300000=1300000 haifiki hata tarehe 10,
1500000 ya mchepuko+1300000=2800000
hii amount kwa makadirio ni siku 20 tu na mwezi una siku 30/31.
Hizi siku zinazobaki unaishije??!! Pesa ya akiba??!!
Kusaidiwa siku kumi tu za kutunza familia ndio unachanganyikiwa?! Acha upuuzi.
 
Jiitahidi mkeo aijue hiyo biashara na yatokanayo lakini asijue uhusiano,Siku mchepuko ukitaka kuolewa hakikisha unauelewa na usilete noma na hapo uwe mwisho wa mapenzi yenu.In the mean time..have a good tym mkuu
 
Aaahh na wachepuke tu mana hamna namna sasa..tumechoka
 
Mshahara hata wa Mwalimu Grade III A anayeanza kazi leo ni zaidi ya hiyo Laki tatu, acha kudanganya watu.
 
Back
Top Bottom