'Think tank' ya Taifa inazidi kuchochora

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,638
697,938
Kwa mazoea vijana ndio tegemeo la taifa kwa
Mawazo mapya
Mawazo chanya
Kwa utayari
Kwa nguvu kazi
Kwa uchapakazi
Weledi
Uzalendo Nknk
Bongo bado ziko timamu, damu zinachemka na miili imejaa nishati.. Kwa muktadha huo na kwa miongozo sahihi na misingi imara vijana ni hazina kubwa kwa maendeleo ya taifa...

Kwa bahati mbaya sana sehemu kubwa ya vijana wa taifa lefu wamekumbwa na utapiamlo mkubwa wa fikra yakinifu, fikra chanya na maono yenye kujenga

Sehemu kubwa ya vijana kwasasa fikra na maono yao kikomo chao ni
Kuwa chawa
Teuzi
Kuendesha ndinga kali
Kuvaa vizuri
Starehe na show offs zisizo na maana yoyote
Kumiliki mali kwa njia za mkato, kuonesha mafanikio feki mitandaoni huku mijadala mikubwa inayowatikisa ni kuhusu kujadili watu na umbea wa kila aina, uzushi na ujinga mwingine

Swala la teuzi serikalini linatengenezewa mijadala ya kila aina na yote si kwa ajili ya kujadili dhana za teuzi husika na manufaa yake la hasha bali nani kateuliwa na kwanini kateuliwa (serikali nayo inapaswa kujitafakari kwenye hili maana teuwa tengua zimekuwa nyingi mno)

Mjadala wa wiki hii ni kuhusu mtangazaji mtanzania aliyerejea nyumbani baada ya kutumikia chombo cha habari ughaibuni kwa miaka mingi.. Wengi wanasema karudi ili kupata uteuzi wa juu serikalini
Kwenye teuzi za hivi karibuni hajateuliwa popote. Hili ndio sasa limekuwa mjadala kwamba kaingizwa mjini, kwamba kaliwa pesa yake kwamba ana bifu na chama chawala nk

Jamani kwani kama taifa hatuna vijana wanaoweza kushika nafasi za juu mpaka tuokoteze watu waliokwisha tumika na kuchoka huko watokako?

Wameteuliwa wangapi waliofanya vizuri sana ughaibuni na hapa wakaboronga mbaya? Hawa hawana maajabu yoyote na si kwamba wana akili kutuzidi la hasha
Mifumo imara, nidhamu ya kazi, masharti, kanuni na miiko ya kazi ndio viliwapaisha na kung'ara.. Wakirudi huku hata wapewe nafasi zilezile zilizowang'arisha kama mifumo yetu ni mibovu wanakuwa wa kawaida mno..

Tuachane ni haya mawazo kimo cha mbilikimo kwamba kila aliyefanya kazi ulaya atafaa kufanya kazi serikalini kwa fikra kwamba anajua na anaweza zaidi yetu tuliobaki nyumbani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiz habar za sijui "think tank" and other blah blah sijui ni nani aliwaamnisha watu..think tank ya taifa? Imagine ... hakunaga kitu kama hiki..ni wajinga wajinga tu hapo wenye mamlaka wanaamua tu kufanya chochote wanachofanya wakijua hakuna wa kuwawajibisha
 
Wameteuliwa wangapi waliofanya vizuri sana ughaibuni na hapa wakaboronga mbaya? Hawa hawana maajabu yoyote na si kwamba wana akili kutuzidi la hasha
Prof Anna Tibaijuka alifaya vema sana tena sana kule makazi UN, akaja hapa akapewa wizara ya makazi (ardhi) aliboronga mpaka dunia ikazimia. Alikuta kila mmoja ni mla rushwa, why not she? akaanza kufuata nyayo ule asali!
 
Kwa mazoea vijana ndio tegemeo la taifa kwa
Mawazo mapya
Mawazo chanya
Kwa utayari
Kwa nguvu kazi
Kwa uchapakazi
Weledi
Uzalendo Nknk
Bongo bado ziko timamu, damu zinachemka na miili imejaa nishati.. Kwa muktadha huo na kwa miongozo sahihi na misingi imara vijana ni hazina kubwa kwa maendeleo ya taifa...

Kwa bahati mbaya sana sehemu kubwa ya vijana wa taifa lefu wamekumbwa na utapiamlo mkubwa wa fikra yakinifu, fikra chanya na maono yenye kujenga

Sehemu kubwa ya vijana kwasasa fikra na maono yao kikomo chao ni
Kuwa chawa
Teuzi
Kuendesha ndinga kali
Kuvaa vizuri
Starehe na show offs zisizo na maana yoyote
Kumiliki mali kwa njia za mkato, kuonesha mafanikio feki mitandaoni huku mijadala mikubwa inayowatikisa ni kuhusu kujadili watu na umbea wa kila aina, uzushi na ujinga mwingine

Swala la teuzi serikalini linatengenezewa mijadala ya kila aina na yote si kwa ajili ya kujadili dhana za teuzi husika na manufaa yake la hasha bali nani kateuliwa na kwanini kateuliwa (serikali nayo inapaswa kujitafakari kwenye hili maana teuwa tengua zimekuwa nyingi mno)

Mjadala wa wiki hii ni kuhusu mtangazaji mtanzania aliyerejea nyumbani baada ya kutumikia chombo cha habari ughaibuni kwa miaka mingi.. Wengi wanasema karudi ili kupata uteuzi wa juu serikalini
Kwenye teuzi za hivi karibuni hajateuliwa popote. Hili ndio sasa limekuwa mjadala kwamba kaingizwa mjini, kwamba kaliwa pesa yake kwamba ana bifu na chama chawala nk

Jamani kwani kama taifa hatuna vijana wanaoweza kushika nafasi za juu mpaka tuokoteze watu waliokwisha tumika na kuchoka huko watokako?

Wameteuliwa wangapi waliofanya vizuri sana ughaibuni na hapa wakaboronga mbaya? Hawa hawana maajabu yoyote na si kwamba wana akili kutuzidi la hasha
Mifumo imara, nidhamu ya kazi, masharti, kanuni na miiko ya kazi ndio viliwapaisha na kung'ara.. Wakirudi huku hata wapewe nafasi zilezile zilizowang'arisha kama mifumo yetu ni mibovu wanakuwa wa kawaida mno..

Tuachane ni haya mawazo kimo cha mbilikimo kwamba kila aliyefanya kazi ulaya atafaa kufanya kazi serikalini kwa fikra kwamba anajua na anaweza zaidi yetu tuliobaki nyumbani

Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo kuu ni moja biashara peke yenye wakika kukutoa kama kijana haraka ni kuingia siasa za uchawa na kupata uteuzi, hapo kijana ataweza kujenga kumiliki gari haraka nk.........Mwijagi ambaye ni chawa ana chances kubwa kua mkuu wa wilaya kuliko dr au lecturer alioko Mzumbe, sasa hapo angalia uwekeze wapi ili utoke mapema. Raisi anaweza kua na namba ya simu yake diamond platform ila ya mkuu wa hospitali ya rufaa ya Bugando anaiomba kwa wasaidizi wake unajua kwa nini? Kati yao wawili nani mhimu zaidi kwa nchi hi?

Hapa nchini uteuzi haufanywi on merit, au academic credentials zako wana angalia utiifu wako na techinical know who not know how. Nani kakuleta,(connection) kwa hali kama hiyo usitegemee vijana kupoteza mda eti wawe think tank wa taifa.
 
Mpaka sasa nilicho ona mm wanangu ni kuwaandaa waje wajiajiri.Unamsomesha mtoto kwa gharama kubwa na anapoteza mda mrefu aje awe chawa na mpuuzi wa kusifia ujinga ujinga ndo apate pesa ???.Kuepusha haya ni kumuuandalia mapema mtoto mazingira aje ajiajiri form 4 inatosha sana kumsaidia vimambo kidogo.
 
Mpaka sasa nilicho ona mm wanangu ni kuwaandaa waje wajiajiri.Unamsomesha mtoto kwa gharama kubwa na anapoteza mda mrefu aje awe chawa na mpuuzi wa kusifia ujinga ujinga ndo apate pesa ???.Kuepusha haya ni kumuuandalia maoema mtoto mazingira aje ajiajiri form 4 inatosha sana kumsaidia vimambo kidogo.
Mkuu elimu ya form six ni muhimu sana kumudu kazi zake za kujiajiri degree ndo aiche kwa elimu yetu form 4 mtoto bado immature sana
 
Kwa mazoea vijana ndio tegemeo la taifa kwa
Mawazo mapya
Mawazo chanya
Kwa utayari
Kwa nguvu kazi
Kwa uchapakazi
Weledi
Uzalendo Nknk
Bongo bado ziko timamu, damu zinachemka na miili imejaa nishati.. Kwa muktadha huo na kwa miongozo sahihi na misingi imara vijana ni hazina kubwa kwa maendeleo ya taifa...

Kwa bahati mbaya sana sehemu kubwa ya vijana wa taifa lefu wamekumbwa na utapiamlo mkubwa wa fikra yakinifu, fikra chanya na maono yenye kujenga

Sehemu kubwa ya vijana kwasasa fikra na maono yao kikomo chao ni
Kuwa chawa
Teuzi
Kuendesha ndinga kali
Kuvaa vizuri
Starehe na show offs zisizo na maana yoyote
Kumiliki mali kwa njia za mkato, kuonesha mafanikio feki mitandaoni huku mijadala mikubwa inayowatikisa ni kuhusu kujadili watu na umbea wa kila aina, uzushi na ujinga mwingine

Swala la teuzi serikalini linatengenezewa mijadala ya kila aina na yote si kwa ajili ya kujadili dhana za teuzi husika na manufaa yake la hasha bali nani kateuliwa na kwanini kateuliwa (serikali nayo inapaswa kujitafakari kwenye hili maana teuwa tengua zimekuwa nyingi mno)

Mjadala wa wiki hii ni kuhusu mtangazaji mtanzania aliyerejea nyumbani baada ya kutumikia chombo cha habari ughaibuni kwa miaka mingi.. Wengi wanasema karudi ili kupata uteuzi wa juu serikalini
Kwenye teuzi za hivi karibuni hajateuliwa popote. Hili ndio sasa limekuwa mjadala kwamba kaingizwa mjini, kwamba kaliwa pesa yake kwamba ana bifu na chama chawala nk

Jamani kwani kama taifa hatuna vijana wanaoweza kushika nafasi za juu mpaka tuokoteze watu waliokwisha tumika na kuchoka huko watokako?

Wameteuliwa wangapi waliofanya vizuri sana ughaibuni na hapa wakaboronga mbaya? Hawa hawana maajabu yoyote na si kwamba wana akili kutuzidi la hasha
Mifumo imara, nidhamu ya kazi, masharti, kanuni na miiko ya kazi ndio viliwapaisha na kung'ara.. Wakirudi huku hata wapewe nafasi zilezile zilizowang'arisha kama mifumo yetu ni mibovu wanakuwa wa kawaida mno..

Tuachane ni haya mawazo kimo cha mbilikimo kwamba kila aliyefanya kazi ulaya atafaa kufanya kazi serikalini kwa fikra kwamba anajua na anaweza zaidi yetu tuliobaki nyumbani

Sent using Jamii Forums mobile app
Ule uzi wako wa kuhusiana na maandamano bdo upo nakaka nikapitie nile nondo kidogo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom