Fafanua kwanza haya ndo tuendelee:
1. Inawezekanaje watu na wanyama kuishi na kufanya shughuli zao ktk dunia duara kama tufe inayoning'inia angani wakiwa wamenata na kutembea upandeupande, wameegama na wengine miguu juu kichwa chini ili hali wao ni non magenital.?
2. Inakuingia akilini vitu, watu na wanyama kunatishwa pembezoni mwa dunia eti kwa kisingizio cha gravity akati vitu hivyo ni non magnetic substance.
3. Ni ngumu kwa maji ya bahari na maziwa ku-bend ili kuleta dhana ya uduwara wa dunia.
4. Huoni kama ni rahisi kwa a Plate earth ku-hold kila kitu without any assist of gravity. The more denser you are, the more you prevail.
Refer the evidence below so that you can come up with new vision


View attachment 1346771View attachment 1346772View attachment 1346774View attachment 1346779View attachment 1346784View attachment 1346786View attachment 1346792
Sent using
Jamii Forums mobile app
Je wewe ni mfuatiliaji na upo updated katika masuala yote yahusuyo 'Flat Earth' na 'flat-earthers' duniani? Maana kuna taarifa nyingi yaonesha bado hunazo.
Je, wewe ni flat-earther?
Je, ni flat-earther wa namna gani?
Usishangae kwa mimi kukuuliza maswali hayo maana kuna baadhi ya maswali hujibiwa kwa maswali kwanza kabla ya muendelezo wa mambo mengine.
Kuhusu swali lako la kwanza;
Watu wanatembea upandeupande kwa namna gani? Wameegama kiaje?
Miguu juu kichwa chini? Juu ni wapi na chini ni wapi?
Kabla sijajibu swali lako la pili, "kisingizio cha gravity"? "Kisingizio" then what? Ili iweje? Kwa faida ya nani?
Kuna wachangiaji wengi wamekwisha kuuliza huko mwanzoni kuwa hayo yote ya "kuficha ukweli" na "kusingizia" yanafanyika ili iweje katika ulimwengu huu wa utandawazi na teknolojia ya hali ya juu?
Kuna ulazima gani wa kufanya miradi mikubwa ya mabilioni ya fedha ili tu "kuwadanganya" wakaao duniani kuwa dunia ni duara (spherical)?
Swali lako la pili na la tatu;
Awali nilitoa mfano kuwa, mtu anayeamini kuwa chombo pekee kinachosafiri baharini ni meli. Siku ukija kumuambia kuhusu uwepo wa submarines zinazopita chini ya bahari anaweza kukukatalia kata kata.
Naomba nikuulize swali jingine;
Je wajua kuwa nguvu ya mvutano si katika sumaku kwa vitu vya chuma pekee?
Je unafahamu kuhusu uwepo wa interaction kati ya electric charges?
Je unakubaliana na kipi na pia kipi hutaki kukubaliana nacho?
Swali lako la nne;
Madai ya flat Earthers kwamba Density ndiyo chanzo cha kuvipeleka vitu kuelekea katika uso wa dunia ni irrelevant.
Density ni amount of matter an object has to its volume au kwa kifupi amount of mass within a volume.
Density si force na automatically has nothing to do with acceleretion ya vitu kuuelekea uso wa dunia.
Swali jingine! Kwanini Density iwe ndiyo chanzo cha kuvifanya vitu viiangukie dunia na si kuiangukia tu bali kuanguka katika muelekeo uleule maalumu (same specific direction towards the earth).
Kwanini Density ivifanye vitu vihame kwa namna hiyo tu na si nyingineyo?
Ni Density ya namna gani hiyo?
Je hilo lina make sense kwako? Kwa misingi gani?
Karibu kwa majibu!