Maana hii mada imeenda sana na tumeleana sana, nataka kumaliza hili kwa mtindo huu.
Anasema Allah aloye juu :
5. Ameumba mbingu na ardhi kwa Haki. Hufunika usiku juu ya mchana, na hufunika mchana juu ya usiku. Na amefanya jua na mwezi vitumike. Kila kimojapo kinakwenda kwa kipindi kilicho wekewa. Jueni mtanabahi! Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe! (Azzumar : 5 )
Hili andiko ukilisoma vizuri linaonyesha ya kuwa dunia duara, ukisoma matini ya tamko hilo utaona neno "yuqawirru" maana yake "wrap around" na kinacho bi "wrapped" ni Dunia.
Akasema tena Allah aliye juu :
19. Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi chake. (al Hijri : 19 )
Hapa aya inasema ardhi imefanywa kama tandiko, yaani baada ya kuumbwa dunia ikatandikwa ardhi juu yake. Hapa ndio tunauzungumzia huo utambarare wa Dunia duara.
Akasema tena Allah aliye juu :
19. Na Mwenyezi Mungu amekukunjulieni ardhi kama busati.
20. Ili mtembee humo katika njia zilizo pana. (Nuhu : 19 - 20)
Ardhi imefanywa kama busati, ili tutembee katika njia pana.
Akasema tena Allah mtukufu aliye takasika :
6. Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
7. Na milima kama vigingi?
8. Na tukakuumbeni kwa jozi?
9. Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko? (an Nabaa : 6 - 9 )
Kwahiyo kwa jumla ya aya hizo tunaona ya kuwa Dunia kwa umbile lake ni duara ila ni tambarare kwa juu.