The World is a flat plane and not a globe

The World is a flat plane and not a globe

kuwa serious eti ndani ya jua nimecheka duh watu ni shida
We unavyofikiri nje ya dunia ni kuanzia wapi? Juzi tu mwaka jana kuna chombo imetumwa inaenda kuingia ndani ya jua kabisa!!Nyie mnakazana kujadili nadharia ambazo watu walikomaa nazo mpaka wakapoteza maisha kwa kuzipinga.Yani hamkubali efforts alizofanya Gallileo mpaka mamlaka ya Roma iliyokuwa inaamini dunia ni tambarare kama meza ikamuhukumu kifo,kabla ya baadae kuja kuthibitika kuwa ni ya mfano wa duara.Kabisa mtu unakazana eti hakuna picha iliyopigwa nje ya dunia, wakati hata drone na rockets zinakuwa launched zinaenda katika space na outer space, mtu unapinga kwa vitu ambavyo hakuna taasisi yoyote ya kielimu wala kitaalamu inayokubaliana!!! Wachina nao walishafanya route za mwezini, nadhani hata russia.Wakenya hapo jirani zetu washarusha sattelite yao kwa mafanikio outer space, na hawako katika hizo contracts zq nchi 14 mlizosema.Haya ndio matatizo ya kuwa vizuri kichwani kwa sababu ya long extended memory na uwezo mkubwa wa kukariri,lakini analysis 0. Yani unafaulu mitihani tu lakini hauwezi kufanya analysis.Na ndio mnakuja kuwa ma Professor mnaotukwamisha tukiwaamini na kuwapa nafasi za kutuongoza.Yani unakataa kabisa kuwa hakuna sattelite katika space tehee tehee yani kwa point hiyo tu inabidi tukiri "nyinyi hamna kitu" yani Sattelite hakuna ila katika mchoro mmoja wa evidence heaven, na heaven of heaven na destination ya God ipo.Wakati katika vitabu vyote hakuna mtu kawahi kumwona Mungu looh!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Alivyoandika tu kaona Alliens, hata sikuhangaika ku reply pale.Kisha akasema aliona Alliens wakati anafunga dish.Nikawa nawaza, Nigga is seeing things, huenda anatakiwa kucheki wale mnaowaita psychiatrist sijui
Hivi umesoma nilichoandika ,na elimu si ushindani very shamefull.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
..
Nilitegemea unijibu maswali yangu lakini naona unaleta maswali zaidi....

Anyway...kukujibu swali lako ni kuwa dunia iko tilted to kwenye angle ya degree 23.4 kwenye mhimili wake na hiyo hali ndiyo inafanya maeneo ya artic yapate mwanga wa jua kwa muda mrefu kuliko kawaida. Na hali hii inatokea kwa sababu dunia ni sphere. Kama dunia ingekuwa flat plane hali kama hiyo isingetokea kwa maeneo ya arctic.

View attachment 1336232
thesunandmoonabovetheearth%20(1).gif


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tuliza akili kijana.
Hehehe mtu anakwambia hii ni evidence, aisee yule Professor ambae ni governor kuna time aliwahi kutuambia kuwa "mtu anapaswa kuwa respnsible na knowledge anayopewa vinginevyo anaweza kuharibu au kuvuruga jamii".
Mwamba anakazana kuna gate anatarctica ukivuka kwenda kule unakuta viumbe wana macho ya blue, na haelezi hao viumbe ni ng'ombe,watu,au mbuzi au wanaitwaje? Wanaongelea free energy,sijui tumetekwa na kutengenezewa routine ya kudhani maisha ni kula kulala na kufa blah blah mingiii, leta proof.Unaambiwa sijui High Jump Admiral sijui alileta results.Bwana wee "walongo" kama hawa bwana huwa wanatupoteza sana, sioni tofauti ya hawa sijui kina Zurri na the likes of "Dr Shika" "Nabii Tito" "Babu Wa Loliondo" na wale wanaosaka "mali zilizoachwa na wajerumani"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaha mkuu bora unisaidie unayoyasema ni flat earth inayo na nembo ni ya wakuu wao
Kama dunia duara kwanini nchi zilizo kizio cha kaskazini zipo karibu karibu lakini zilizo kizio cha kusini ziko mbali mbali sanaaa?

Na kwanini hakuna ramani ya kizio kusini kilivyo ila ramani ya kaskazini ipo?

Sent using Jamii Forums mobile app
images%20(1).jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu huyu Jamaa anafananisha Dunia na Sinia, Jua analifananisha na torch inayo mlika mwanga wake kwa kuzunguka kingo za Sinia!
 
Kama dunia ingekuwa flat. Ilitakiwa nikiwa hapa niuone Mlima Kilimanjaro uleeeeeeeeeeeeeeeeeee. Au nikigeuka kwa hivi niuone Mlima Everest Uleeeeeeeee. Ila siri ya dunia aijuae ni yule aliyeiumba ambaye ni Mungu.
 
Kama dunia ingekuwa flat. Ilitakiwa nikiwa hapa niuone Mlima Kilimanjaro uleeeeeeeeeeeeeeeeeee. Au nikigeuka kwa hivi niuone Mlima Everest Uleeeeeeeee. Ila siri ya dunia aijuae ni yule aliyeiumba ambaye ni Mungu.
Huwezi kuona kutokana na vizuizi vinavyofanya macho yako yasipate taswira kamilifu kama vumbi,ukungu n.k

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom