The World is a flat plane and not a globe

The World is a flat plane and not a globe

Ukitazama hapo Jua ni mviringo nasiyo nusu duara lakini lina toa mwanga wake kuelekea kwenye uso wa Dunia kwa mfumo wa nusu duara iliyo na nusu kipenyo kumbuka mwanga usafiri kwa kunyooka na jua haliwezi kufikisha mwanga wake chini kwa mwonekano wa mstatili au mraba! Swali :Kwanini Jua lisitoe mwanga wake kwa Mzunguko kutokana na umviringo wake na center ya sehemu yenye giza ikeviwe na mwanga wa jua sio huo mwanga wa nusu duara tunao uona hapo kwenye hiyo flat Earth yenu?! Na ukitaka kuthibitisha kuna sehemu mnakwama,Wewe chukua tochi yenye kioo cha duara mlika chini uone chini kama mwanga sio wa duara!Kama umeshindwa kuliona hilo mapema na Wewe pia ni miongoni mwa Watu wasio tumia vema akili zao kufikilia vema?!
Swali hilo haliwezi kujibiwa na flat-earthers sababu muundo mzima wa flat-earth ni illogical. Hilo swali watalikimbia tu!

Jua hilo hilo katika nyakati tofauti linabadili sura ya mwangaza wake, linabadili njia katika mzunguko, linasogea "north" kisha baadaye tena linahama kuiacha "north" hapo hapo linahitaji kukamilisha mzunguko wake kamili wa kila siku. Hahaha!

Huwezi kuwa na ufahamu sahihi ukakubaliana na huo upuuzi wa flat-earthers.

Flat-earthers ni kikundi cha uzushi na mizaha tu ifanywayo na watu wajuao wakifanyacho.

Wakiwa proved wrong kuhusiana na uzushi wao, wanatunga uzushi mwingine mpya ilhali wakijua kabisa kuwa ni uzushi na kwa makusudi hawataki kukubali, hakuna uhalisia wowote wala mantiki katika hizo theories zao, wala uthibitisho wowote juu ya hayo madai yao!

Jambo la kustaajabisha ni kuwa, kuna kundi jingine ambalo linadiriki kuipokea na kuiamini hiyo mizaha bila kufikiri wala kuhoji. Miongoni mwao ndiyo hawa wadandiaji tunaokutana nao mitandaoni kila siku.

Ni wadandiaji tu ambao wameamua kuwa wavivu wa kufikiri.
 
Hiyo siyo real mkuu ni magumashi tu....

Sent using Jamii Forums mobile app
.
FB_IMG_1583530156250.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
.
Kwanza, unaelewa kuhusu uwepo wa theory ya "ukuta kuzunguka dunia" kwa mujibu wa flat-earthers?

Mwenye kutakiwa kuthibitisha kuhusu uwepo wa huo "ukuta uzungukao dunia" ni yule asemae upo na si yule abishaye kwamba haupo! Unaelewa hicho kitu?

Isitoshe pia, mwenye kutakiwa kuthibitisha kuhusu uwepo wa "dome" ifunikayo dunia si yule asemaye haipo bali yule asemaye kuwa hiyo "dome" ipo!

Yaani flat-earthers waseme wenyewe kwamba kuna "ukuta wa barafu uzungukao dunia" alafu waache jukumu kwa wengine kuthibitisha ilhali wao wameshindwa kuthibitisha?

Wasikwepe majukumu, waende wakatuthibitishie hilo!

Pia, watuthibitishie madai yao yote kuhusiana na hiyo flat-earth. Waache kusambaza uzushi na kutengeneza 'memes' mitandaoni.

Kinachofanywa na flat-earthers kinajulikana fika kuwa ni uzushi, huku wengine wakiuamini huo uzushi, wakiziamini hizo conspiracy theories bila ushahidi wowote.

Hiyo ni imani, isitoshe ni imani potofu! Imani juu ya vitu visivyoweza kuthibitika juu ya mambo yaliyo ndani ya uwezo wa binadamu kuyathibitisha.

Flat-earthers ni watu wa 'kutapa tapa' wanapobanwa kwenye hoja kwa maana si watu wa tafiti bali porojo nyingi.

Uthibitisho kuhusu dunia kuzunguka tayari umekwisha wekwa bayana katika maelezo yenye mantiki bila kuleta mkanganyiko kama uliopo katika nadharia za flat-earthers.

Nilimuuliza mwenzako, Je, ulitega vipindi vya darasani?

Ama wewe ulikuwa ukisinzia wakati masomo yanaendelea? Hukuelewa somo? Na kama ni kati ya hao, that's not my problem, shauri yako!

Kila unachouliza wewe tayari kimekwisha patiwa majibu;
Kuhusu anga za mbali, watu takribani 500 na zaidi kutoka mataifa tofauti tofauti wamethibitika kufika huko katika nyakati tofauti. Taarifa zipo kote duniani na katika mataifa yao. Unabisha! Thibitisha kinyume na hapo.

Kuhusu picha, video n.k. ni kutoka katika mashirika ya anga za mbali duniani na si NASA tu. Tayari ufafanuzi wa kina juu ya hayo maswali yako umekwisha tolewa. Mahali na sehemu vyombo hivyo vimekuwa vikitumika kupiga hizo picha zimeelezwa.

Usiwe mvivu, tafuta kufahamu.

Mataifa mbalimbali na pia kila taifa lenye uwezo wa kufanya huo utafiti halijazuiwa kufanya hivyo. Na kila taifa hufanya utafiti wa kipeke yake kulingana na mahitaji ya utafiti.

Kama wamelipwa ili waseme uongo, thibitisha hilo!

Mataifa hayo yote, kote duniani yameficha "ukweli", thibitisha hilo!

Media zote zinazokusanya hizo taarifa nazo zinadanganya, thibitisha. Walikubaliana lini? Walikaa kikao wapi? Agenda yao ilikuwa nini? Ushahidi wa hayo uko wapi?

Flat-earthers waache porojo! Wakafanye nao utafiti wao ili watuletee uthibitisho wa hiyo "dome", watuletee uthibitisho wa huo "ukuta" na madai yao mengine yote watuthibitishie.

Tafiti hazipingwi kwa porojo bali hupingwa kwa tafiti!
FB_IMG_1583528907229.jpeg
FB_IMG_1583529030239.jpeg
FB_IMG_1583528887238.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Attachments

  • FB_IMG_1583529053890.jpeg
    FB_IMG_1583529053890.jpeg
    92.5 KB · Views: 11
.
Swali hilo haliwezi kujibiwa na flat-earthers sababu muundo mzima wa flat-earth ni illogical. Hilo swali watalikimbia tu!

Jua hilo hilo katika nyakati tofauti linabadili sura ya mwangaza wake, linabadili njia katika mzunguko, linasogea "north" kisha baadaye tena linahama kuiacha "north" hapo hapo linahitaji kukamilisha mzunguko wake kamili wa kila siku. Hahaha!

Huwezi kuwa na ufahamu sahihi ukakubaliana na huo upuuzi wa flat-earthers.

Flat-earthers ni kikundi cha uzushi na mizaha tu ifanywayo na watu wajuao wakifanyacho.

Wakiwa proved wrong kuhusiana na uzushi wao, wanatunga uzushi mwingine mpya ilhali wakijua kabisa kuwa ni uzushi na kwa makusudi hawataki kukubali, hakuna uhalisia wowote wala mantiki katika hizo theories zao, wala uthibitisho wowote juu ya hayo madai yao!

Jambo la kustaajabisha ni kuwa, kuna kundi jingine ambalo linadiriki kuipokea na kuiamini hiyo mizaha bila kufikiri wala kuhoji. Miongoni mwao ndiyo hawa wadandiaji tunaokutana nao mitandaoni kila siku.

Ni wadandiaji tu ambao wameamua kuwa wavivu wa kufikiri.
FB_IMG_1583528808967.jpeg
FB_IMG_1583530025620.jpeg
FB_IMG_1583529740357.jpeg
FB_IMG_1583530025620.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom