sio umekwisha fundishwa sema umekwisha danganywa.kama unaamini astronomy ya darasani huwezi nielewa maisha.
Nimekuambia uende antarctic utaona kuta za barafu unabisha hazipo ukipewa picha unagoma kwanini usiende utuprove kwamba hazipo .
Halafu kingine kama hujui maana ya flat earther bora ukae tu kimya ,nani kakuambia ni imani ,siku ukijakujitambua utakuwa umechelewa sana.
FES ni flat earth society ambayo sisi flat earthers tunaijua kazi yake ni nini na hilo sio shirika linaotusemea chochote,FES ndio wanaseme dunia ina accelerate ,FES sio flat earthers ni branch ya system yao kutuprove inlogic,tafuta flat earther anaye amini FES.
kama unatumia akili za darasani hata kama kuna jua kali itabidi nikumulikie tochi hata 10 upate mwanga zaidi maana unaona giza.
PROVE DUNIA INAZUNGUKA na niambie kwanini astronauts hawazungushi camera 360° wakiwa angani,na kwanini wapo nje ya dunia na kwa masaa zaidi ya matatu wanarekodi video na dunia ipo palepale na haizunguki?
Sent using
Jamii Forums mobile app
Kwanza, unaelewa kuhusu uwepo wa theory ya "ukuta kuzunguka dunia" kwa mujibu wa flat-earthers?
Mwenye kutakiwa kuthibitisha kuhusu uwepo wa huo "ukuta uzungukao dunia" ni yule asemae upo na si yule abishaye kwamba haupo! Unaelewa hicho kitu?
Isitoshe pia, mwenye kutakiwa kuthibitisha kuhusu uwepo wa "dome" ifunikayo dunia si yule asemaye haipo bali yule asemaye kuwa hiyo "dome" ipo!
Yaani flat-earthers waseme wenyewe kwamba kuna "ukuta wa barafu uzungukao dunia" alafu waache jukumu kwa wengine kuthibitisha ilhali wao wameshindwa kuthibitisha?
Wasikwepe majukumu, waende wakatuthibitishie hilo!
Pia, watuthibitishie madai yao yote kuhusiana na hiyo flat-earth. Waache kusambaza uzushi na kutengeneza 'memes' mitandaoni.
Kinachofanywa na flat-earthers kinajulikana fika kuwa ni uzushi, huku wengine wakiuamini huo uzushi, wakiziamini hizo conspiracy theories bila ushahidi wowote.
Hiyo ni imani, isitoshe ni imani potofu! Imani juu ya vitu visivyoweza kuthibitika juu ya mambo yaliyo ndani ya uwezo wa binadamu kuyathibitisha.
Flat-earthers ni watu wa 'kutapa tapa' wanapobanwa kwenye hoja kwa maana si watu wa tafiti bali porojo nyingi.
Uthibitisho kuhusu dunia kuzunguka tayari umekwisha wekwa bayana katika maelezo yenye mantiki bila kuleta mkanganyiko kama uliopo katika nadharia za flat-earthers.
Nilimuuliza mwenzako, Je, ulitega vipindi vya darasani?
Ama wewe ulikuwa ukisinzia wakati masomo yanaendelea? Hukuelewa somo? Na kama ni kati ya hao, that's not my problem, shauri yako!
Kila unachouliza wewe tayari kimekwisha patiwa majibu;
Kuhusu anga za mbali, watu takribani 500 na zaidi kutoka mataifa tofauti tofauti wamethibitika kufika huko katika nyakati tofauti. Taarifa zipo kote duniani na katika mataifa yao. Unabisha! Thibitisha kinyume na hapo.
Kuhusu picha, video n.k. ni kutoka katika mashirika ya anga za mbali duniani na si NASA tu. Tayari ufafanuzi wa kina juu ya hayo maswali yako umekwisha tolewa. Mahali na sehemu vyombo hivyo vimekuwa vikitumika kupiga hizo picha zimeelezwa.
Usiwe mvivu, tafuta kufahamu.
Mataifa mbalimbali na pia kila taifa lenye uwezo wa kufanya huo utafiti halijazuiwa kufanya hivyo. Na kila taifa hufanya utafiti wa kipeke yake kulingana na mahitaji ya utafiti.
Kama wamelipwa ili waseme uongo, thibitisha hilo!
Mataifa hayo yote, kote duniani yameficha "ukweli", thibitisha hilo!
Media zote zinazokusanya hizo taarifa nazo zinadanganya, thibitisha. Walikubaliana lini? Walikaa kikao wapi? Agenda yao ilikuwa nini? Ushahidi wa hayo uko wapi?
Flat-earthers waache porojo! Wakafanye nao utafiti wao ili watuletee uthibitisho wa hiyo "dome", watuletee uthibitisho wa huo "ukuta" na madai yao mengine yote watuthibitishie.
Tafiti hazipingwi kwa porojo bali hupingwa kwa tafiti!