HNIC
JF-Expert Member
- Sep 6, 2011
- 1,898
- 2,202
If you want to test a man's character give him power
ABRAHAM LINCOLN
Unaccommodated man is no more but such a poor bare,
forked animal
KING LEAR : Act III, scene iv
Sipendi kuandika political obituaries lakini kwa huyu mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam (Paul Makonda ) Sidhani kama atamaliza ngwe yake na Magufuli let alone kama atamaliza miezi 12 ijayo katika jiji la Dar es salaam kama mkuu wa mkoa kwa sababu naamini kabisa kuwa Rais Magufuli kashaona kuwa Makonda isnt up to the job na mbaya zaidi Magufuli kashashtuka na hataki tena haya mambo ya kusifiwa sifiwa na kupambwa badala yake anataka kuona results baada ya kumpa cheo kuongoza jiji lenye watu karibu milioni 10.
Maguli alimpatia ukuu wa Mkoa wa Dar baada ya Makonda kumpa illusion kuwa ni mchapa kazi lakini ukweli usiopingika ni kuwa Makonda has failed na sasa hivi tumeishia kupewa PR stunts, na maneno mengi yasiyo na substance.
Jiji hili ambalo lina historia na ambalo limetoa vigogo wa kila namna linahitaji mkuu wa mkoa ambaye anaendana na dunia na karne hii tuliyonayo.
So far jiji bado ni chafu, ombaomba wako palepale, foleni na traffic lights zisizofanyakazi, hakuna law wala order, marengo yanajengwa bia mipangilio huko kwenye Central Business District (CBD), kodi zinakusanywa lakini wana Dar es salaam hawaambiwi wala kuonyeshwa mchanganuo wa matumizi wa kodi zao, hakuna transparency, jiji halina strategies wala policies za mambo ya climate change, hakuna strategies za kuongeza nyumba kwa wakazi wa hili jiji (na affordable) na kuondoa ma chaka na slums ya Buguruni, Mwananyamala kinondoni, Ilala, temeke, etc.
Makonda kashindwa kutuletea alternative Transport strategy na policy (kaput DART) na hajaja na mango wowote wa kuendeleza usafiri walau Dar ikawa na network ya light rail kama walivyofanya Addis au kuongeza na kuboresha barabara zilizopo ili ziendane na ukuwaji wa watu kwenye hili jiji, na usafiri hapa nazungumzia za waenda kwa miguu, baiskeli na magari.
Paul Makonda kashindwa kuja na mikakati yoyote ile ya kusaidia kuwa na Dar es salaam ambayo in hewa safi kwa wakazi wake. Hivi how hard is it for him kushirikiana na January Makamba (waziri wa mazingira) ili kuwepo kwa comprehensive strategies za kutunza mazingira? Mfano jiji la Dar halina power points za ku chat magari ya umeme, hakuna operesheni ya kueleweka ya kupada na kutunza mimi, Makonda kashindwa kuwahizimisha na kutoa incentives ma wajenzi kutumia umeme mbadala wa solar na wind.
Mbali na hayo hana strategies zozote zile kuvuta wawekezaji wa viwanda kama vya ku assemble Solar na vinginevyo kwenye hili jiji wala hana mipango yoyote ile ya kuvutia watalii kwenye hili jiji ambalo watulii hutumia kukaa kwa siku moja kisha wanaenda zao Arusha au Zanzibar. Hili ni jiji ambalo lina historia na vivutio kem kem na linaweza kuongezewa vivutio vingi zaidi ili wall mtalii on average awes ku spend more days hapa Dar na kutumia wastani wa dollar 100 per day hapa. In addition, Makonda amefeli kwenye kuboresha Ulinzi na usalama wa hili jiji kwani sasa hivi wakazi wa Dar hawajiskii salama kutoka nje usiku na hata aliyoko ndani ya gari anaogopa kusimama kwenye traffic lights kwa kuogopa majambazi.
Hivi kuna ubaya gani wananchi wakawa organised na kuambiwa wachangie kwenye mambo ya neighbourhood policing? Mrema aliweza na police posts in the 1990's sasa sielewi leo haya mambo yanashindikana. Wananchi kila wakiona polisi ni ama watakamatwa na kusingiziwa kesi na hivyo wananchi wa hili jiji police badala ya kuwa rafiki wa wananchi wanaonekana kuwa wanashirikiana na majambazi.
Hapo sijazungumzia vikosi veytu vya zimamoto ambavyo haviko up to standards. Zimamoto zinatakiwa kuwepo kwenye kila kata ya hili jiji lakini hakuna mipango hiyo na hata habari Mkaonda hana.
Ofisi yake pia imeshindwa kushirikiana na kampuni mbali mbali za teknolojia wakaweka super fast Free Wifi maeneo mbali mbali kwenye huu mji na bila kusahau wakashirikiana na navy makampuni kuifanya Dar iwe kivutio kikubwa kwa wawekezaji wa ndani na nje. Iko wapi Konza City ya Dar? Ziko wapi tech hubs za hili jiji ambazo vijana na local companies wanaweza kuonyesha kuwa Dar inaweza ikawa na digital economy. Hapa nazungumzia local companies kama akina Uhuru One, Selcom,Max malipo ambazo zingekuwa flag bearers za tech city ndani ya Dar tuitakayo. Dar inaweza ikawa East Africa’s centre of innovation and the location of choice for tech and digital companies and investors lakini hii ingewezakana kama RC wetu angekuwa na hiyo vision ya kuleta makampuni makubwa kama Google, Oracle, HP, Facebook na and pia hilo eneo pia linge provide support to local companies seeking to expand internationally kama hawa akina JAMIIMEDIA...lakini wapi!
Kuhusu Culture na nisiseme kwani sasa hivi the only cultural thing ambacho ofisi yake inakifanya ni matamasha ya fiesta na nyama choma. Ofisi yake haina habari na vituo vya sanaa na haina mipango ya kuwezesha wawekezaji kujenga Cultural Centres.
Miwsho zaidi Makonda hana habari kama jiji hili indigo walk wawekezaji na walipa kodi wakubwa. Sasa sielewi why mpaka leo hajafanya mkutano awa wafanya biashara wakubwa ambao wanalipa kodi kubwa na kuajiri watu wengi zaidi. If anything Makonda comes across as the most anti business RC kuliko wote ambao jiji hili imewapata. Hivi anashindwa vipi kushirikiana na private sector wenye hizi infrastructure projects kwa njia ya PPP?
Kama kweli anataka kusaidiwa aseme lakini tatizo hasemi. Sisi wana Dar hatupendi kulipa kodi lakini sababu ni hatupewi wala hatuonyeshwi namna kodi zetu zinavyotumika. Tunachokitaka ni kuona tax system ya Dar inakuwa overhauled,increasing taxpayer compliance while pledging that the Local Govt (LG) chini ya ofisi ya RC Makonda will be accountable for how tax money is spent. Naamini kuwa ofisi ya RC Dar wangekuwa honest na transparent, annual tax revenues zitapanda tutu na mana yake ni kuwa hizi pesa za ziada zitatumika kumaintain barabara, kusafisha jiji, kuongeza na kuimarisha ulinzi na usalama, ange weza kuintroduce new public transit options into kwenye hili jiji ambalo watu wanatumia zaidi ya masa 5 kwenye foleni na kwa kuboresha transport systems
Sidhani na siamini kabisa kama Magufuli is impressed na yanayoendelea kwenye hili jiji. Maana huyu Makonda Hana any Strategic Plan ya hili jiji.
Makonda angeweza sana kufanikisha haya mambo kwa kushirikiana na sect binafsi wakafanya kazi kwa njia ya Public Private Partnership (PPP)
In my opinion, its fair to say kuwa Makonda is not up to the job. Tuletewe mtu mwingine,
UPDATES: