The Other Half (Simulizi)

The Other Half (Simulizi)

Hata kwenye tovuti imeishia sehemu ya 19 tu hakuna mwendelezo!!

Usumbufu na tabia isiyofaa ni kuleta story kisha kutelekeza watu katikati!!

The Bold unakuwa kama Bongomuvi bhana!!!!!!!????
 
Hata kwenye tovuti imeishia sehemu ya 19 tu hakuna mwendelezo!!

Usumbufu na tabia isiyofaa ni kuleta story kisha kutelekeza watu katikati!!

The Bold unakuwa kama Bongomuvi bhana!!!!!!!????
Shukuru basi hata hicho kidogo mzee
 
Hata kwenye tovuti imeishia sehemu ya 19 tu hakuna mwendelezo!!

Usumbufu na tabia isiyofaa ni kuleta story kisha kutelekeza watu katikati!!

The Bold unakuwa kama Bongomuvi bhana!!!!!!!????
Usimlaumu hivyo, kwani yeye anashinda tu kwenye komputa? Hana familia, hatafutii siziki familia yake na yeye mwenyewe?

Kwanza Mimi nampongeza sana kwa jinsi anavyotupa burudani ya bure.
 
Hata kwenye tovuti imeishia sehemu ya 19 tu hakuna mwendelezo!!

Usumbufu na tabia isiyofaa ni kuleta story kisha kutelekeza watu katikati!!

The Bold unakuwa kama Bongomuvi bhana!!!!!!!????
Watu wengine hovyo sana hivi wewe unamlipa sh ngapi kwa burudani anayotoa bure ashinde kwenye computer kwa sababu yako tunga ya kwako
 
Watu wengine hovyo sana hivi wewe unamlipa sh ngapi kwa burudani anayotoa bure ashinde kwenye computer kwa sababu yako tunga ya kwako
Ngoja nikuletee ya kwangu! Kaa mkao wa kula, leo hii mpaka kufikia saa tisa usiku nitakuwa nishapakia hapa riwaya moja matata sana!! Itaitwa MTAMA KWA WATOTO.

Hii haijawahi kutokea kabisa.
 
Hata kwenye tovuti imeishia sehemu ya 19 tu hakuna mwendelezo!!

Usumbufu na tabia isiyofaa ni kuleta story kisha kutelekeza watu katikati!!

The Bold unakuwa kama Bongomuvi bhana!!!!!!!????
We kweli bomu! huoni aibu kupata burudani wakati huo huo kupanua mawazo buree buree kabisa!

jifunze kusema asante nawe utabarikiwa. Kuishi kwa lawama hautaendelea ng'ooooo

Asante The bold "wetu" kwa utamu huu

hii hadithi imenifanye niwaze "beyond my capacity"

Inamvuto flani hivi si wadunia hiii
 
Ninachoamini ni kwamba mkuu Bold amekwazwa na hii issue ya mapimbi flani kuchukua story zake na kwenda kuzipublish kwenye vyombo vyao vya habari. Hivyo kabla ya mwendelezo wa story zake atakuwa anatafuta njia ya kulinda huu ubunifu wake husitumiwe na mapimbi flani kujitengenezea kipato pasipo muhusika(Bold) kujulishwa. tuvumilie kidogo wapendwa katika jf.
 
Ninachoamini ni kwamba mkuu Bold amekwazwa na hii issue ya mapimbi flani kuchukua story zake na kwenda kuzipublish kwenye vyombo vyao vya habari. Hivyo kabla ya mwendelezo wa story zake atakuwa anatafuta njia ya kulinda huu ubunifu wake husitumiwe na mapimbi flani kujitengenezea kipato pasipo muhusika(Bold) kujulishwa. tuvumilie kidogo wapendwa katika jf.


Mbona kimya Mr. Bold.

Mzeee... the bold.. ndio umetuhukumu wote nn ???

Au kapigwa ban.
Mnisamehe bure wakuu... Last week nilikuwa busy kuangahika na wanasheria kushughulikia wanaoiba kazi zangu humu na kuchapa kwenye magazeti yao...

So sorry kwa ukimya... Am back now!!
 
93622e70b3d8fb7d943634d2e4b9fb20.jpg




THE OTHER HALF


SEASON 1 - THE LEGEND OF ANABELLE




EPISODE 20



SIKU YA PILI



Ni sauti iliyofifia ikigugumia kwa uchungu ndio pekee ilikuwa inasikika kwa mbali sana katika ghala kubwa lenye kiza totoro ambalo lilikuwa na taa moja tu ambayo ilikuwa inajitahidi kuangaza.

Japokuwa giza lilikuwa ni kubwa mno huku kukiwa na mwanga hafifu tu ndani ya ghala, lakini pua zilikuwa na uwezo kabisa wa kusikia harufu ya damu. Damu ambayo ilikuwa imetuama chini sakafuni na kutengeneza kidimbwi kidogo kama vile kisima kilichojaa mchanga na kufanya maji yabaki juu juu tu pekee.

Harufu ya damu haikuwa inaogofya kama ambavyo ilikuwa inaogofya sauti hii hafifu ya kugugumia kwa uchungu.
Haikuwa dhahiri sana ni nini hasa ambacho sauti hii hafifu iliyokuwa inalalama kwa uchungu ilikuwa inatamka. Maneno pekee ambayo labda yalikuwa yanaweza kusikia yalikuwa ni "…natalie…", ambayo yalikuwa yanasikika yakitamkwa na sauti hii hafifu kana kwamba yanatamkwa na mtu aliyeshikwa na kwikwi.

" na…ta…li..e"

Sauti iligugumia kwa uchungu huku ikirudia tena na tena ilichokuwa ikitamka.

Harufu ya damu mbichi ilikuwa imetapakaa kwenye ghala hili kubwa kiasi kwamba mtu ungeliweza kufikiria labda alikuwa ndani ya mto au kisima kinachotiririsha mifereji ya damu mbichi ya binadamu.

Katikati kabisa ya ghala hili kubwa ambapo ndipo taa ndogo ya 'balbu' ilikuwa inawaka kwa mwanga hafifu wa njano, kulikuwa na mnyororo uliofungwa kutoka juu ya paa la ghala kwa kuning'inizwa.
Mnyororo huu uliokuwa unaning'inia haukuning'inizwa hivi hivo tu, bali kuna binadamu aliyefungwa na mnyororo huu.

Mtu huyu alikuwa amefungwa katika namna ambayo alikuwa amesimama na mnyororo umefungwa mikononi mwake na mikono kuvutwa juu ya kichwa. Namna ambayo alikuwa amesimamishwa ilikuwa ni kusimama kwa maumivu makubwa kwa sababu ule myororo aliofungwa mikononi ulikuwa umekazwa kwa kuvutwa juu mpaka kufikia hatua ambayo alikuwa kama amesimama kwa kuchechemea na vidole. Yawezekana labda ni kucha tu ndizo ambazo zilikuwa zimegusa sakafu, lakini mwili wote ulikuwa unaning'inia kwa nyororo iliyofungwa mikononi na kuning'inia angani.

Mwili wake mweupe wa kizungu ulikuwa umechoka kwa maumivu na ngozi ilikuwa imebadilika na kuwa nyekundu kabisa kana kwamba alikuwa amewekwa juani kutwa nzima. Kutokana na kuning'inizwa vile angani kwa muda mrefu huku kucha tu zikiwa vimegusa sakafuni, mikono yote ilikuwa imekufa ganzi na hakuwa anahisi chochote kile kuanzia mabegani kuelekea mikononi, ilikuwa ni kana kwamba mikono imekatika tayari.

Tumboni na kifuani alikuwa na vidonda vikubwa ambavyo viliambatana na michirizi mikubwa ya damu.
Kichwa chake ambacho alikuwa amekiinamisha kama amelala kilifanya majeraha aliyonayo mdomoni yasionekane vyema lakini ikisababisha damu nyingi kuvuja kutoka mdomoni.
Damu ilionekana kwamba ilikuwa imevuja kwa muda mrefu mpaka kufikia hatua kwamba ilianza kutoka damu nzito iliyokuwa inanata kama udenda. Hii ilifanya mdomoni kwake kuwe na kama 'uzi' mwekundu wa damu unaoning'ninia.

Mwili wake haukuwa na hata kipande kimoja cha nguo, alikuwa uchi wa mnyama kama alivyozaliwa na hii ilifanya majeraha yaliyopo mgongoni mwake, kifuani na tumboni yaonekane vyema na kuogofya zaidi hata kuyatazama.

Pamoja na mtu huyu aliyeninginizwa hivi na majeraha mwili mzima ndani ya ghala hili, pembeni yake kulikuwa na mtu mwingine, mzee aliyevalia suti nyeusi tii kabisa na akiwa amenyoa upara ambaye alikuwa kwenye kiti cha chuma anavuta kiko huku anatazama mwenzake aliyening'inizwa kana kwamba anafurahia kumuona katika hali hii.

Lakini si mzee huyu tu pekee aliyekuwemo kwenye ghala hili. Bali pia kulikuwa na kijana ambaye yeye alikuwa amesimama mikono yake imeloa damu, naye alikuwa amevaa suti nyeusi huku kichwani amenyoa upara naye kama yule mzee pembeni yake aliyekaa kwenye kiti anavuta kiko.



KAMA KAWAIDA NAOMBA TWENDE KWENYE TOVUTI ILI KUSOMA EPISODE 20...


TAZAMA JUU PALE KABISA KWENYE "TRENDING" AU NENDA CHINI KABISA KWENYE CATEGORY YA "SHORT STORIES"


jamiiforums.com
 
Mnisamehe bure wakuu... Last week nilikuwa busy kuangahika na wanasheria kushughulikia wanaoiba kazi zangu humu na kuchapa kwenye magazeti yao...

So sorry kwa ukimya... Am back now!!
Nimekuelewa, naimani sasa hawataiba na itabidi wakulipe. Wizi ni mbaya aseeee.

asante kwa episode 20. All the best Kijana Jasiri....lov u
 
Back
Top Bottom