The new TTCL Management (2009)

Kuna watu wameongea issues za muhimu hapo juu.

Kama serikali haitavunja mkataba wake na Celtel, haya yote ni vichekesho tu. Sasktel walijitahidi sana kwa miaka miwili kutafuta mikopo toka kwenye mabenki. Ugomvi wa serikali na Celtel umewafanye waonekane si mali kitu, kwani wabia hao walishindwa kuwadhamini.

Celtel wanashika handbreak kuhakikisha kwamba TTCL haikopesheni kwa namna yoyote ile.

Tatizo jingine la TTCL ni aina ya wafanyakazi waliopo. Wapo vijana wasomi wazuri tu waliajiriwa kwa mikataba ya muda mfupi, halafu wapo shikamoo jazz wanaosema walikuwapo tangu enzi za East African Community! Matokeo yake ujima ni mwingi kuliko vitendo

Mpingo1,
Muhimu kwa sasa kwa TTCL ni kuandaa strategy mpya ya kukabilia na competition na pia kulitumikia taifa letu katika karne ya 21. Ni ngumu sana kupambana na hizi mobile companies kwenye voice market maana capital inayotakiwa huko sio kubwa sana hivyo threat of new entrants (Porter five forces) ni kubwa sana. Ndio maana kila siku makampuni mapya yanajitokeza.

Watanzania wanataka internet services kwa maana ya broadband ambayo ina speed ya kutosha kuweza kufanya shughuli zote za uzalishaji. Hili ndilo tatizo la Tanzania na mobile companies hawawezi ku provide speed and bandwidth required for 21st century ICT services. Wakitaka kufanya hivyo watahitaji network kubwa zaidi nje ya mtandao wao.

Binafsi naona hapa ndipo penye soko; kwanza soko la moja kwa moja kwa mlaji ( end user) na pia soko la jumla (whole sale market). Soko la jumla nina maana makampuni kama ya mobile yatataka customers wao ambao hawana landline au cables au fibres kwenye nyumba zao watumie huduma zao kupatia reliable ICT services.

Technology kwasasa ipo (kwa mfano fibre to home or business FTTX), kinachotakiwa ni strategy kwanza na pili uwezo wa ku raise fund kwa ajili ya kutengeneza network kama hiyo. Ni muhimu kuanza kidogo kidogo kwa kuunganisha makampuni ya binafsi na ofisi za serikali ili hao wafanyakazi waonje matunda ya internet ya kisasa na wakirudi nyumbani watataka wawe na speed kama hiyo hiyo.

Nikiwa TZ nikitaka kufungua internet inakuwa kasheshe, jamaa yangu huwa ananiambia hapo kwao ndio speed kubwa lakini hata kufungua website ya kawaida tu inakuwa kasheshe. Niko convinced mobile companies TZ hawana uwezo wa ku compete na TTCL kwenye hiyo area kama TTCL kweli wataamua.

Waachane na kupoteza muda wao kwenye PSTN maana wakifanikiwa kuwa na broadband ya kisasa hata hiyo voice (VOIP) itakuwa included tena at a very affordable price. Pia ni kupoteza muda kuanza kuhangaika kuanzisha kampuni nyingine ya mobile maana watakutana na competition kubwa na ili kupata customers itabidi watumie pesa nyingi sana kwa kupunguza bei au matangazo. Wakifanikiwa kutengeneza a reliable broadband network, hapo ndipo wanaweza kuingiza na mobile ambayo itakuwa inatumia network hiyo hiyo ya broadband. Pia network hiyo hiyo inaweza kutumika kutoa services za TV kwa mfano IPTV or on demand television au wanaweza kuform partnership na TBC au kampuni nyingine ya utangazaji na kuanza kutoa huduma bora za on demand television.

Kuna mambo mengi sana ambayo TTCL wanaweza kufanya. Aliyesema opportunities favour prepared minds hakukosea; innovation yoyote inakuja kwasababu kuna mambo mawili; kwanza kuna demand ambayo watu wa kawaida hawajui kwamba kuna njia zingine zinaweza kutumika ku satisfy hiyo demand na pili kuna watu ambao wanaweza kuliangalia jambo nje ya their comfort zone (inventors) na wakaweza kuja na solutions mbalimbali. Kwa mfano TZ kila siku viongozi wetu wako kwenye motion huku na huku kuhudhuria mikutano; je ni kweli ni muhimu wao kuwa pale physically? Je TTCL wakiamua kuwa na centers zao zenye video conference facilities, bado hao watu watataka wawepo pale physically? Kwa mfano sasa kuna bunge Dodoma, je hao watendaji wote wa wizara husika, wanahitaji kuwepo pale Dodoma? Ukiwa na reliable ICT service unaweza kuanza kufikiri mabadiliko kama haya ambayo sio tu yanaokoa muda lakini pia yanaokoa pesa.

TTCL imepoteza muda mwingi kwenye migogoro, labda hii ni nafasi ya kuanza upya na kufanya yale ambayo wengine tumekuwa tukiwashauri au kuwaombea wafanye. Huko nyuma nilikuwa na mawasiliano ya karibu na baadhi ya watendaji wa TTCL wakati wa CEO Mkumba na niliweza kuwashauri kwenye mambo mengi. Japo walikuwa slow lakini walikuwa wanaelewa na happy kutaka kujifunza. Walipokuja Wacanada hao jamaa wakawekwa pembeni.

Hata leo mimi niko tayari kabisa kuwashauri TTCL tena bure ili mradi kama hainichukulii muda wangu mwingi (sina uwezo wa kutumikia mabwana wawili). Aidha kuna Watanzania wengi sana kwenye telecom nje ya nchi; watumieni watu kama hao kwa ushauri na wengi ninaowajua mimi wanaweza kuishauri serikali au TTCL bila hata kuhitaji kulipwa senti tano.
 
Tatizo ni selekari ya tanzania kuwa na share kwenye kampuni mbili zinazofanya biashara moja, ina 40% zain tz na 60% TTCL, na MCI INT ina 40% TTCL na ilikuwa na 60% zain tz imeziuza kuwait tel.
Ili TTCL waweze kufanya kazi vizuri inabidi selekari ya tz iamue kuwa share upande moja zain tz au ttcl. pia mkumbuke kuna vigogo wamo ndani ya selekari wana share zain tz kwahiyo hawawezi kukubari kuona TTCL inafanya vizuri kushinda zain tz.
 
Mnyamwezi, Pamoja na maelezo matamu ya Mtanzania hapo juu kama handbrake ya CELTEL kuzuia mchuma wa TTCL usipae haitatolewa nakuambia huu usanii utaiua TTCL.
Jambo lingine la msingi huko bongo ni kwamba uzalendo ni kidogo sana. Kila mtu anachumia tumbo lake na matunbo ya familia yake. Pengine hao wateule wapya wa TTCL waulizwe wataitendea nini TTCL na si TTCL itawatendea nini. Maana wengi baada ya uteuzi huo utawaona sasa hivi shavu dodo wakati mikakati aliyoianisha mheshimiwa Mtanzania hapo juu itaonekana kama hekaya za ABUNUWASI
 
Mnyamwezi, Pamoja na maelezo matamu ya Mtanzania hapo juu kama handbrake ya CELTEL kuzuia mchuma wa TTCL usipae haitatolewa nakuambia huu usanii utaiua TTCL.
Jambo lingine la msingi huko bongo ni kwamba uzalendo ni kidogo sana. Kila mtu anachumia tumbo lake na matunbo ya familia yake. Pengine hao wateule wapya wa TTCL waulizwe wataitendea nini TTCL na si TTCL itawatendea nini. Maana wengi baada ya uteuzi huo utawaona sasa hivi shavu dodo wakati mikakati aliyoianisha mheshimiwa Mtanzania hapo juu itaonekana kama hekaya za ABUNUWASI


Nikwambie kitu?.

Vijana wasomi waliopo TCCL wanaliona hilo na wanalitambua ila wengi wao wapo nafasi za katikati.

Shikamoo Jazz band ndo wapo juu, either polutted by the system au wapo scared na kupoteza kazi zao au kuwa off the line na outdated hawafanyi lolote.

Wakiwapisha Vijana wasomi waliopo, nina uhakika serikali itaambiwa ukweli na "wachawi" wataanikwa na TCCL itapaa tu.

Sina haja ya kurudia aliyosema Mtanzania, TCCL ipo juu sana ya mobile phones operators kwenye big Network coverage, wangeweza sana kuteka soko la internet.

Ni uoga tu wa Viongozi wa TCCL, ila inawezekana.
 
Nangi alitokea Tigo kabla ya kwenda TTCL. Na kule Tigo alikuwa marketing manager. Ni mtu ambaye anajua vizuri marketing katika competitive telecoms environment na yuko practical.

Mrisho Shabani alitokea PWC ambao walikuwa waki audit TTCL kwa miaka mingi. Ana knowledge ya kutosha na he was cleared kwenye kashfa ya kodi. Inaonekana wizi ulifanyika TRA na NBC and TTCL haikuwa involved mbali na kutoa hela; process iliyotumika ilikuwa halali inavyosemekana. Kwa hiyo TTCL hawakuwa na hand katika wizi huo.

Priscilla amekuwa kwenye mtandao wa TTCL muda mrefu knowledge na experience yake kwenye matecknolojia mapya na ya kisasa ni bora na ni mtendaji mzuri tu.

CEO Said alikuwa director wa operations za southern highlands yaani mikoa ya Mbeya, Ruvuma, Rukwa na Iringa. Uwezo wake hauna question; ni mtu practical na ana experience kubwa mno ndani ya TTCL. Pengine alihitajika huyu kudeal na maissues ya wafanyakazi na vyama vya wafanyakazi kwani ana negotiating skills kubwa.

Kwa kifupi managment hii imeshiba na huwezi kusema zaidi. Tatizo la TTCL siku zote lipo serikalini na maamuzi yanayotokea huko ambayo mara zote yameshaprove failure. Kwa management si issue. Kampuni hii inaweza kuchukua nafasi ya Vodacom mara moja ikiwa serikali itaiachia ifanye biashara. Na hii management ina uwezo wa kufanya biashara.

Mkataba na Zain; kuna mtu kutoka Zain kwenye board ya TTCL na hawa wamekuwa wakifanya kila wanachoweza kuhakikisha TTCL haifanyi biashara ya simu za mikononi. In fact wemekuwa wakiihujumu kampuni wazi wazi. Kwa mfano; wakiwa ni wamiliki dada walijiondoa katika kutumia huduma za wholesale za TTCL wakijua kuwa uamzi huu ulikuwa na nia ya kuiua TTCL.

Lakini vile vile uhusiano huu ndo umefanya TTCL ishindwe kupata mikopo kutoka Taasisi za fedha kama Mabenki kwa ajili ya kuinvest. Hawa wakiwa kama wamiliki ni lazima wakubali ili kampuni ikopeshwe na hakuna biashara kubwa kama ya TTCL inaweza kuendeshwa bila mikopo. Zain hawataki TTCL ipate mikopo na lengo lao ni ife (ingawa wana shares; nadhani wanajua kuwa hawastahili kuwa na share hizo kwani hawakuzinunua kihalali).

Maamuzi ya serikali yamefanya hii kampuni iwe very unstable na isiwe na implementable strategic plan. Tokea mwaka 2002 hii ni management ya tano (Van der voort, Mbowe, Mkumba, Bill, sasa Said). Na kila management inakuja na structure mpya ambayo matokeo yake ni ku-destabilize middle na low level managment. Uki destabilize middle na low level management ni rahisi kuua kampuni kwani hawa ndo wanaofanya kampuni isitetereke. Sidhani kama kuna kampuni inaweza kuendelea wakati kila baada ya mwaka mmoja na miezi kadhaa inapata viongozi wapya wanaokuja na mfumo mpya wa utendaji kazi.

Serikali ndo inashikilia uzi. Inaweza ikaamua TTCL iwepo au ife mara moja kwani ndo mmiliki. Kwa sasa hivi inaelekea serikali haina cohessive strategy ndo maana hata TTCL ipo ipo tu.
 
Back
Top Bottom