The Magic Ring

The Magic Ring

Madame S

JF-Expert Member
Joined
Mar 4, 2015
Posts
17,187
Reaction score
34,498
RIWAYA…..THE MAGIC RING ( 01 )
MTUNZI….. HUSSEIN O. MOLITO
TRANSLATION….. GIFT KIPAPA

Upepo mkali ulioambatana na radi huku rangi ya mawingu ikizidi kuwa nyeusi . muwako na muungurumo mkali unasababisha maporomoko ya mawe yatokayo mlimani na kudondoka kwa kasi chini yalizidi kutetemesha mlima huo.
Juu ya mlima huo kulikua na viumbe wawili waliokua wakirumbana na kutoleana maneno kwa ukali. Ilisikika sauti ya kike na kiume huku kila mmoja wao akiwa hataki kuwa chini ya mwenzake. Marumbano hayo yaliishia baada ya msichana kutoa pete yake na kumrushia mwanaume ambaye hakuijali zaidi aliiacha tu hiyo pete ianze kubiringita kwa kasi kuelekea chini ya mlima.
Baada ya tukio hilo, Yule mvulana alibadilika na kua kama popo mkubwa na kupaa angani kwa kasi. Haikuchukua muda mrefu, na Yule msichana alibadilika na kuwa jamii hiyo hiyo ya popo mkubwa na kupaa angani kwa kuelekea upande wake.
Utengano huo wa majini waliokua wapenzi kwa muda mrefu na wakiwa katika hatua za mwisho kufunga ndoa,ulikua gumzo kwa jamii yote ya majini aina yao.
Hiyo ilikua na mara ya kwanza kutokea katika historia za majini ambao daima hua waaminifu na hua hawaachani mpaka kifo kinapo watenganisha.
Taarifa za ugomvi huo zilifika kwa mkuu wa majini na kuwaita kwa ajili ya usuluhishi, ila jini la kiume liligoma kuripoti hivyo zoezi hilo likafeli.
Uzito wa mahaba ya jini la kiume ulianza kuonekana baada ya kutengana kwa muda wa wiki moja tu. Jini la kike lilishindwa kula wala kupata usingizi mzuri. Alishindwa hata kuyafurahia maisha japokua alikua na uwezo wa kutembea ardhini na kupaa angani pasipo mipaka. Mateso ya moyo yaliyo muonyesha udhaifu wake juu ya mwanaume huyo aliyeziteka hisia zake, ndizo zilizomshawishi awe mpole na kukubali makosa yake.
***********************************
Baada ya jogoo la kwanza kuwika, niliamka huku nikifungua dirisha ili kuhakikisha kama kweli kulikua kumekucha. Niliindea ndoo yangu ya maji na kukuta imebaki nusu ndoo kutokana na kuoga nusu ya maji yaliyokua humo kwenye hiyo ndoo jana yake usiku nilipokua nimerudi kutoka kwenye mahangaiko yangu.
Muwako wa simu yangu ambayo mlio wake ulikua mdogo sana, ndio ulionifanya niichukue haraka na kuangalia kibox kilichoashiria kua message ilikua imeingia. Kabla sijaifungua hiyo sms, mtu aliyenitumia hiyo sms alinipigia simu. Nilipokea haraka sana kwakua siku zote huyo mtu hua hanipigii simu kama hakuna dili ya maana ambayo tunaweza kufanya.
“uko wapi we boya.” Alinisalimia salamu ambayo haikuniumiza. Japokua kama mtu mwengine akiniita hivyo naweza kugombana nae kama si kushikana nae kutokana na kutolipenda jina hilo.
“nipo geto joh” niliitikia huku kidole changu nikikielekeza sehemu iliyoandikwa LOUD ili mradi niweze kumsikia kutokana na udogo wa sauti ya simu yangu.
“njoo Tabata bima muda huu… kuna mzigo tunatakiwa tuupeleke Morogoro.” Aliongea na kunifanya niitikie haraka bila kuuliza ni mzigo gani huo.
“sawa mkuu.” Niliitikia na kuchukua shati langu na kuanza kuvaa haraka huku simu nikiwa nimeishikilia mkononi.
“chukua boda boda , hela yake nitampa huku huku.” Aliniambia hivyo ili nijue ni jinsi gani alivyokua na haraka.
“nimekuelewa mkuu.” Nilijibu hayo maneno na simu yangu ikakatika.
Nilighairi kuoga, nilivaa suruali yangu haraka na kuufunga mlango wa chumba changu na haraka nikawahi kituoni ambapo nilichukua pikipiki fasta na kumuelekeza ni wapi ambapo tunatakiwa twende.
Baada ya kufika, hakukua na story zaidi ya kuingia kwenye gari kubwa lililokua na shehena ya mzigo ambao hata mimi sikua naujua wa nini na wala sikutamani kuhoji.
“tutakunywa cha kibaha dogo.. naona mdmo umekukauka.” Aliongea BOSCO na mimi sikujibu chochote. Aliwasha gari na safari ilianza hapo. Kwakua nilikua namuamini bosi wangu hyo,wala sikuulizia maswala ya mshiko, ila nilijua tu mshiko nitakaupiga siku hiyo, nitaweza kulipia hata chumba ninachodaiwa kwa mwezi mmoja sasa.
Gari ilipamba moto huku gesi ya gari hiyo ikiendelea kulalamika. Mafuta yaliendelea kuchomeka na kusababisha matokeo ya spidi ya gari kuwa kubwa huku muendeshaji akitikisa kichwa kutokana na mziki uliokua unalia humo ndani.
“kama bado una usingizi, lala huko nyuma.” Aliongea Bosco huku akitabasamu.
“niko poa tu.” nlijibu huku nikiwa na hofu kidogo ya usalama wangu kutokana na uendeshaji mbaya wa gari aliokua nao Bosco.
Tulifka kibaha na tukapaki gari na kuingia kwenye mgahawa mmoja mkubwa.
“kula kama mwanaume ambaye anatarajia kushusha mzigo wa tani tatu peke yake. Sasa we agiza chapati mbili halafu uniambie eti huna spidi ya kazi.” Alinitania na kumuita muhudumu ambaye alikuja kutusikiliza.
Kwakua aliniruhsu mwenyewe, wala sikufanya hiyana, niliagiza msosi wa nguvu bila kujali gharama yake na kumfanya Bosco atabasamu.
“yeah… mi nataka majembe ya kula na kufanya kazi pia.. kama wewe Deo.” Aliongea maneno hayo huku na yeye akikandamiza supu ya mguu wa mbuzi uliolala pale mbele huku seheni nyingine ikiwa imejaa chapati takribani tano.
Baada ya kupiga msosi huo, tuliingia kwenye gari na kuanza safari kwa mwendo kasi zaidi wa ule wa mwanzo kutokana na kutokua na foleni wala msongamano wa magari ya hapa na pale.
Sikua napajua ni maeneo gani, ila kulikua na milima mirefu na juu ya milima hiyo ilikua kama inafuka moshi kutokana na baridi na hali ya hewa iliyokua huko juu.
Sehemu hiyo ndipo gari yetu ilipopata hitilafu na kulazimika tupaki pembeni kwa ajili ya msaada kutoka kwa mafundi ambao tumeshawapigia simu.
“ushenzi gani huu… mi nilitaka tufike leo leo na tugeuze leo hii hii ili tuje kula gambe dar usiku. Ila usijali mdogo wangu, lazima watulipe muda wote tutakao upoteza huko.” Aliongea Bosco na kuonyesha ni jinsi gani alikua amekasirika.
Baada ya muda kama wa nusu saa hivi, kila mtu alichoka na kujikuta tunatamani kunyoosha nyoosha miguu. Mimi nilitembe kwa mwendo wa kama mita hamsini hivi, ndipo nilipoona kitu kinang`aa na baadae muwako wake ukazima. Nilishawishika kujua kilikua na kitu gani huko. Nikakisogelea na nilipoyatuliza macho yangu, niliiona pete nzuri iliyokua na chata ya sura ya kinyago Fulani hivi.
Kwenye macho yake kulikua na vitu kama vichupa ambavyo mimi nilihisi itakua ni almasi. Niliokota haraka na kuiingiza mfukoni kwangu.
Niliporudi, nilimkuta Bosco akijarbu kuwasha tena gari. Nilipofika tu, gari ikakubali kuwaka na tukaendelea na safari………..
Tulifika morogoro na kuingia kwenye duka moja kubwa la nafaka. Nilishuka na kwenda nyuma ya hilo gari. Nilifungua turubai na kuuona mzigo mkubwa wa nafaka ukiwa umepangwa vizuri kwenye magunia.
“sasa wewe kazi yako ni kuwahesabia tu hawa maboya watakaokuja kubeba. Wacha mimi nikapate mambo yangu. Hakikisha wanashusha magunia mia mbili tu. Ishirini yabaki humo humo.” Aliongea Bosco na kunifanya kuikubali hiyo kazi.
Walishusha mizigo na baada ya hesabu kutimia, nilimpigia Bosco simu na nusu saa baadae alikuja huku macho yake yakiwa yameshabadilika. Alinuka pombe na muda huo alikua na chupa ya bia mkononi.
Tulienda hadi kwenye hilo duka na kukabithiwa hela.
“zihesabu kama zimetimia.” Aliniambia na mimi nikafanya hivyo.
“zimetimia bosi.” Nilimjibu baada ya kumaliza kuzihesabu zile hela.
“sawa, tuondoke kabla hawa wachawi hawajatuteka.” Aliongea na kuwafanya watu waliomsikia kuanza kucheka.
“wewe unaweza kuendesha kidogo?” aliniuliza baada ya kuingia kwenye gari.
“naweza lakini sijawahi kuendesha gari kubwa.” Niliitikia kiuoga.
“liwe kubwa liwe dogo, gari gari tu. Kama unajua kuendesha dogo basi hili halitakushinda. Maana najiona kama nitalitupa hili gari.” Alongea na kunipisha mimi kwenye kiti cha dereva.
Kwakua gari ilishawaka, alinielekeza jinsi ya kutia gia na kupangua. Baada ya kukariri, nilianza kulitaoa gari taratibu huku majasho yakiwa yananitoka.
“tunaelekea wapi?” niliuliza baada ya kuona uelekeo tuliokua tunaelekea ulikua wa kuendelea mbele na si kurudi Dar.
“kwenye duka la mpemba. Hii mifuko iliyobaki ndio cha juu chetu.” Aliongea Bosco na kunifanya nitulie. Maana kwenye hiyo mifuko ishirini niliamini sitakosa hata laki tatu nje ya posho yangu.
Nilifanikiwa kufika dukani kwa mpemba. Baada ya kuishusha mizigo na kuchukua chetu, tulienda hotel ya karibu na kuchukua chumba kwa ajili kulala.
“fedha zote utalala nazo wewe, maana mimi sijielewi muda huu.” Aliniambie na kunikabidhi zile hela.
Zilikua nyingi sana. Ila nilizichukua na kulala nazo huku mawazo yangu yakikinzana usiku kucha. Kuna wakati niliwaza kukimbia nazo, ila kwakua sikua napenda maisha ya mashaka na kukimbizana na askari, nikaona bora nitulie tu kama mjinga.
Asubuhi alikuja Bosco chumbani kwangu nilipolala na tukaelekea bar kunywa supu. Baada ya hapo, mida ya saa tatu asubuhi, tulianza safari ya kurudi Dar huku yeye akiwa ndio dereva baada ya kuwa fresh.
Tulifika Dar mishale ya saa tisa alasiri. Tulienda kupaki gari na kukabidhi hesabu. Baada ya kugaiwa chetu, alinifuata na kunipa shilingilaki tano.
“najua kwa mtoto kama wewe zinakutosha hizo kwa kugongea mademu. Maana nawajua nyie mkizikamata.” Aliongea na kunifanya nicheke.
Nilifurahi sana baada ya kuzichanganya na laki moja na nusu ambayo ilikua ujira wangu wa ile safari kama tani boy.
Nilirudi numbani na laki sita na nusu. Nilifurahi na kuzimwaga geto. Nikawaza nini nifanye ili kukibadilisha chumba changu ili kivutie. Cha kwanza kabisa nikaona ni bora niondokane na adha ya kulala kwa shida. Nikaamua kuleta kitanda na godoro lake.
“kila kitu kinahitaji uzindizi…. Na hivi nizindue na nanii?” niliwaza baada ya kufunga kitanda change na kutandika shuka jipya lililokubali vizuri na kuonekana thamani ya chumba changu kupanda ghafla.
Nilichukua simu yangu na kutafuta jina lililoandikwa Martha na kupiga.
“helloo.” Niliongea huku nikitabasamu baada ya kuweka loud speaker.
“niambie.” Aliitikia bila kuonyesha kuifurahia kuipokea simu yangu.
“safi tu wangu, umenisusa?” niliongea huku nikiwa nimekaa kwenye kiti huku nikikangalia kitanda changu kilichopendeza kutokana na upya wake.
“sijakususa wangu, mambo mengi.”
“njoo basi home.” Niliongea na kusikilizia jibu lake.
“sasa hivi nataka niende kwa mjomba adamu ili anipe hela ya kusuka. Na baadae siwezi kuja huko usafiri ni shida.” Aliongea bila kujua kua muda huo nilikua nimejaa kimtindo.
“chukua boda boda mpaka huku mi nitalipa na hela ya kusuka nitakupa pia.” Niliongea na kumfanya Martha acheke.
“usichekeshe walionuna babu wee, kama kweli unaweza kufanya hivyo nitumie kwanza elfu tano.” Aliongea na kuonyesha wazi kua alikua ananipima imani.
“subiri nikutumie.” Niliongea na kukata simu. Niliingia kwenye menyu ya tigo pesa na kumtumia shilingi elfu kumi. Haikupita hata dakika, simu yangu ikaanza kuita huku jina lililosomeka kwenye screen ikiwa ni Martha.
“niambie wangu.” Niliitikia kinyonge.
“thenks baby,… hivi hii ulionitumia ndio ya bajaji au utamlipa huko?” aliuliza huku akionekana akiwa na furaha zaidi ya mwanzo.
“hiyo nime test tu kama nikituma hela inaruka.. ukinifurahisha leo utapata hata kumi kama hizo.” Niliongea huku nikiwa najiamin na kitu niongeacho.
“nakuja sasa hivi baby.. mmmmwwwwaaaah” aliongea na kunibusu busu ambalo toka nimeanza kuwa nae hakuwahi kunibusu kama hivyo.
Baada ya dakika ishirini, nilisikia mlio wa bajaji ikiwa nje ya dirisha langu, nilitoka na kumlipa Yule dereva hela aliyotaja bila kubishana nae.
Tuliingia ndani huku nikimuacha akishika mdomo baada ya kuona kitanda na godoro vikiwa vinameremeta pale kwangu.
“kweli mpenzi wangu umekua.” Aliongea hayo maneno na kujitupa kitandani.
Hatukuongea maneno mengi baada a mimi kupanda kitandani zaidi ya kuanza kumpapasa na kuanza kula vyangu alivyokua ananibania muda mrefu.
Baada ya kumaliza, niliiendea suruali yangu na kutoa waleti mpya niliyoinunua. Hapo ndipo ile pete ikadondoka chini na kuelekea upande aliokua Martha.
Martha aliiokota na kuivaa.
“pete nzuri sana hii, umeinunu shilingi ngapi?” aliniuliza Martha na kunifanya nishindwe kumuambia ukweli.
“nimeinunua hela nyingi sana , naomba tu unipe pete yangu.”
Niliomba pete lakini Martha hakua tayari kunipa. Baada ya kumlazimisha sana anipe na kuona kua alikua ameamua kuing’ang’ania sana, niliamua kumuachia huku moyo wangu ukiwa haujaridhika Martha kuondoka na pete yangu niliyoiokota mbali.
ITAENDELEA
 
nimeinunua hela nyingi sana , naomba tu unipe pete yangu.”
Niliomba pete lakini Martha hakua tayari kunipa. Baada ya kumlazimisha sana anipe na kuona kua alikua ameamua kuing’ang’ania sana, niliamua kumuachia huku moyo wangu ukiwa haujaridhika Martha kuondoka na pete yangu niliyoiokota mbali.
*************************
Mabadiliko ya hali ya hewa ya ukaa pamoja na baridi kwa pamoja. Ndio vilivyoufanya moyo mpweke wa jini aliyeshindwa kuvumilia kukaa mbali na mpenzi wake kwenda milimani kumtafuta mpenzi wake.
“Edward, we need to talk”
(Edward, nahitaji kuongea na wewe)
aliongea Rosemary baada ya kuonana na Edward ambaye alikua amesimama kwenye ncha ya mlima.
“It’s over Rosemary, there is nothing between us”
(nimemaliza mkataba na wewe. hakuna cha ziada kati yetu.)
aliongea Edward na kumfanya Rosemary ajiinamie chini kwa sekunde kadhaa.
“I can imagine how hateful you feel to me right now. But remember we won’t travel all this miles away from home for break up. We come down here to become happiest couple whoever exist in our world and not to hurt each other s heart. I still need you Edward.”
( naweza kuvuta picha jinsi ulivyo na chuki juu yangu sasa , lakini kumbuka hatukusafiri umbali wa maili zote hizi toka nyumbani kwa ajili ya kuachana. Tumekuja huku ili tuwe wenzi wenye furaha zaidi ya wenzi wowote waliopata kutokea katika ulimwengu wetu na sio kuumiza mioyo yetu. Bado nakuhitaji Edward.)
aliongea Rosemary huku sauti yake ikionyesha mitetemo ya mifereji ya machozi yaliyojaa kwenye macho yake.
“who start all these and destroy all the happiness love which was exist between us? Who start all that ridiculous thing and jump here and there like crazy. I got hurt you know, I don’t want to get pain anymore .”
( ni nani aliyeanzisha yote haya na kuharibu penzi lote la furaha lililokuwepo kati yetu? Nani alianza mambo ya kiijinga na kuruka huku na kule kama mwenda wazimu? Hata mimi nina moyo unalijua hilo? Sitaki kuumia tena.)
aliongea Edward bila kumuangalia Rosemary ambaye kwa wakati huo alishaanza kudondosha machozi.
After stay away from you, I knew how impontant you are in my life. It more than my strength of fry all over the sky and to change blue color to yellow.”
(baada ya kuwa mbali na wewe, ndio nimeuona umuhimu wako na jinsi gani ninavyokuhitaji katika maisha yangu. Ni zaidi ya uwezo wangu wa kupaa angani na kubadilisha rangi ya bulue kuwa njano. Nimegundua makosa yangu na sasa nipo tayari kukuomba msamaha.” Alilalamika Rosemary.
“you may be able to change blue to yellow but you’re not able to change the hate I have on you and to make me love you again.”
“unaweza kubadilisha blue kuwa njano lakini huwezi kubadilisha chuki niliyokua nayo juu yako na kunifanya nikupende tena.” Aliongea Edward na kumfanya Rosemary aanze kuangua kilio. Sauti nzuri lakini iliyokua na uwezo wa ajabu wa kuyakusanya mawingu meupe n akuyabadilisha rangi na kuwa wingu jeusi ambalo lilianza kuteremsha mvua kwa kasi ya ajabu.
”Why you are doing this to me Edward, I love you so much am not ready to lose you”
(kwanini unanifanyia ivyo Edward, nakupenda sana na sipo tayari kukupoteza.)
aliongea Rosemary na kumfanya Edward ageuk e na kumtazama msicha huyo wa kizungu aliyekua amepiga magoti huku mvua hiyo ikiendelea kuwalowanisha wote wawili.
“Well, you lose me already since you drop that ring down the from the mountain, you won’t care about all that love I had when I put that ring to your finger”

(ungelikua wangu nab ado unanihitaji, usingeiachia pete niliyokuvicha kwa mapenzi makubwa idondoke chini yam lima.) aliongea Edward na kuanza kondoka.

“I wasn’t myself back there, I don’t know what I was doing, please honey, forgive me I promise I will find it at all coast but please honey give me another chance.”
( sikuwa mimi wakati ule, sikujua hata anilichokuwa nakifanya, tafadhari mpenzi, nisamehe, na kuahidi nitaitafuta pete kwa gharama yoyote lakini tafadhari nipe nafasi nyingine.)
aliongea Rosemary ambaye alikua bado amepiga magoti pale chini.
“not without a ring, rosemary, I want that ring back on your finger , perhaps we can talk , right now you do nothing but make me lose my temple “
(siwezi kufanya hivyo bila ya pete, Rosemarry, nahitaji pete irejee kwenye kidole chako, labda hapo tutaweza kuongea, sasa hivi hakuna unachokifanya zaidi ya kunifanya nighadhabike tu.)
aliongea Edwar na kumuangalia Rosemary bila kupepesa macho. Alibadilika na kuwa mfano wa popo mkubwa na kupaaa kwa kasi angani.

*************************
Baada ya siku tatu toka mpenzi wangu atoke nyumbani, nilipigiwa simu na dada yake aitwaye Neema na kunipa taarifa ambazo zilinishtusha sana.
“kimetokea nini shemu.” Niliuliza baada ya kugundua kua aongeaye si Martha, bali ni dada yake.
“yaani hata sijui nisemeje Shemu. Yaani ninavyokuambia muda huu, tumemfunga Martha kamba miguuni na mikononi. Anaongea maneno yasiyo eleweka na alishaanza kuvua nguo. Kiufupi Martha kapatwa na kichaa cha ghafla.” Aliongea shemeji yangu huyo na kunifanya nipigwe na butwaa.
“sasa mmechukua hatua gani shemeji yangu?.” Niliuliza baada ya kuona mambo yameshakua magumu.
“hakuna tulichokifanya hapa zaidi ya kumuangalia tu. Kama vinazidi ndio tumpeleke Muhimbili kwa uchunguzi zaidi.” Aliongea shemeji yangu na kunifanya niingiwe na wasi wasi.
“basi nitakuja hapo shemeji yangu.”
Niliongea na kuchukua jezi yangu niliyoitundika kwenye enga na kuivaa. Nilitoka haraka na kwenda kituo cha basi na kuchukua daladala iliyonifikisha mpaka kwakina Martha.
Nilibaki nimepigwa na bumbuwazi baada ya kumuona Martha akiwa anaongea maneno yasiyo eleweka huku akicheka cheka bila kuchekeshwa na kitu chochote.
“tumpelekeni hospitali jamani.” Nilitoa wazo baada ya kuona hakuna uzima kabisa kwa mpenzi wangu huyo.
Baada ya kufika muhimbili na kupokelewa na madokta wa magonjwa ya akili, tulipewa tarehe ya siku atakayopimwa na kuchukua majibu.
Wakati tunarudi, nilijikuta nimekumbuka kua kwenye kidole cha Martha hakukua na pete ile aliyoichukua kwangu kinguvu.
“samahani shemu, nilimpa Martha pete yangu alipokuja nyumbani na pale simuoni nayo. Kuna mahali alifanikiwa kuihifadhi kabla ya kupatwa na kichaa?” niliuliza baada ya kufika kituoni tukiwa tunasubiri usafiri wa kurudi nyumbani.
“leo hii tunvyoongea ndio tulikua wote wakati tunaiuza hiyo pete. Yaani haikupita hata masaa mawili toka tumerudi, ndio yakatokea haya yaliyotokea.”
Baada ya kuambiwa maneno hayo, nilikata tamaa ya kuipata pete yangu tena. Nilijikuta nimejisikia vibaya sana baada ya kusikia mpenzi wangu ameuza pete yangu tena bila kunishirikisha wala kuniomba afanye hivyo.
Ila nilipo yapimisha na madhila yaliyompata, niliona sio sawa kujali pete wakati mwenzangu amekumbwa na tatizo kubwa ambalo hata mimi limeniumiza na kunihuzunisha sana.
ITAENDELEA
 
******************************************************************
“leo hii tunvyoongea ndio tulikua wote wakati tunaiuza hiyo pete. Yaani haikupita hata masaa mawili toka tumerudi, ndio yakatokea haya yaliyotokea.”
Baada ya kuambiwa maneno hayo, nilikata tamaa ya kuipata pete yangu tena. Nilijikuta nimejisikia vibaya sana baada ya kusikia mpenzi wangu ameuza pete yangu tena bila kunishirikisha wala kuniomba afanye hivyo.
Ila nilipo yapimisha na madhila yaliyompata, niliona sio sawa kujali pete wakati mwenzangu amekumbwa na tatizo kubwa ambalo hata mimi limeniumiza na kunihuzunisha sana.
Baada ya wiki moja kupita. Hali ya mpenzi wangu ilionekana kuwa mbaya na kupelekwa milembe kabisa kutokana na iwango chake cha uchizi kkupanda kila siku.
Tukio hilo lilikua kama limenifunga hela. Maana nilizokua nazo zote ziliisha kama mvua bila ya mimi mwenyewe kujua zimeishaje. Nilikuja kutaharuki tu nyumbani nimebakiwa na shilingi elfu tatu. Siku hiyo nilitulia maskani kwangu ili kusubiria tenda nyingine, lakini wapi. Niliishia kuzitumia hela zote na kubaki mtuopu kabisa niliporudi nyumbani.
Niliwza sana kabla ya kulala. Nilichukua simu yangu na kuangalia salio. Nilikuta kuna kiasi cha shilingi 20. Hicho kiwngo kiliniwezesha kubipu. Nililitafuta jina la Bosco na kupiga.
“unasemaje we boya.” Alinipigia na kuanza kuongea maneno hayo bila hata ya salamu.
“kaka hakuna issue huko, mimi sina hata dala hapa nilipo.” Niliongea huku nikisikilizia majibu ya bosi wangu huyo.
“nitakushtua joh, ila kwa sasa hakuna dili yoyote.” Aliitikia Bosco na kukata simu. Hapo ndipo nilipojua kua mwanaume naanza kuumbuka kuanzia hapu.
Nilivuta shuka na kujifunika usiku huo huku nikiitafakari safari ya kesho kuelekea kilingeni kwetu kwa miguu.
Usingizi ulikuja kwa kasi lakini wazo la kutoku ana hela ndio lililonifanya niamke bila kujua ni kitu gani nitaingiza kinywani kwa siku hiyo. Nilimuomba Mungu wa viumbe wote ili anijaalie niweze kupata chakula kwa siku hiyo kwakua siku zote yeye ndie aliyekua ananipangie nile nini.
Baada ya kuoga na kujiandaa vyakutosha huku msingi ukiwa ni nguvu zangu peke.
Nilitoka mapema sana kwenda kutafuta riziki. Kwakua maskani kwangu kulikua mbali kidogo na nainapoishi, ilinichuku kama lisaa hivi nikikatisha vichochoro vya tandale ili niibukie manzese na baadae mburahati ambapo ndio kilinge chetu kilikuwepo hapo.
Mtu yeyote aliyefanikiwa kuniona, aliweza kunitambua kua nilikua na mawazo sana. Sikujua maisha yangu ya kupata hela za msimu yataisha lini. Maana huwa Napata hela na kupata hela zingine huwa ndoto.
Nikiwa kwenye mwendo wa haraka, nilishtushwa na mlio wa gari uliokuwa unalia karibu na nilipokuwepo. Nilijua kua ile gari labda ilikua inataka kukatiza njia, niliamua kusimama ili niipishe ipite. Lakini cha ajabu haikupita, zaidi ile gari ilisimama na kioo chake kilianza kushuka taratibu.
Niliona sura ngeni ya malaika ikiachia tabasamu baada ya kuniona. Sikuweza kumgundua alikua na asili gani kutokana na uweupe wake na rangi ya nywele zake. Kabla sijachukua hatua yoyote kutokana na kupigwa na bumbuwazi, yule msichana alifunga kioo cha gari yake na kuondoka.
Kusema ukweli si kumuelewa zaidi nilijawa tu mawazo juu ya kitendo kile.
Niliachana na mawazo ya msichana huyo kutokana na umaridadi aliokua nao. Pia asili yake ilitosha kabisa kunijulisha kua hakuna anaendana na mimi.
Basi nilianza kutembea taratibu huku nikisikilizia maumivu ya tumbo la njaa niliyoamka nayo asubuhi na roti hiyo ya miguu ilivyokua ndefu, ndio vilizidi kunifanya nihisi utumbo unataka kujinyonga kwa njaa.
Nilijikaza kiume na kuhakikisha kua nafika kilingeni kwetu. Baada ya kufika kilingeni, nilipokea taarifa kutoka kwa marafiki zangu kuwa kulikua na mgeni wa kizungu alikuja kuniulizia pale dakika kadhaa zilizopita.
Kabla hata sijajua ni nani, marafiki zangu walinionyesha msichana aliyekua amesimama mbali kidogo na pale kuwa ndie aliyekua ananiita.
Nilimfuata kiuoga na nilipomfikia nilimsalimia, aligeuka na kunitazama. Uzuri wa macho yake ya blue ndio ulionifanya nishindwe kuongea chochote.
Ghafla nilimuona yule msichana akinikonyeza na baada ya hapo macho yake yalibadilika na kuwa kama ya paka. Nilishtuka na nilipotaka kupiga kelele nilijikuta sauti haitoki. Hata nilijaribu kukimbia haikuwezekana hata kunyanyua unyayo wangu.

“NAITAKA PETE YANGU”

Aliongea maneno hayo huku akiwa ananitisha kwa kuikunja kunja sura yake na kuwa sura ambayo sikuweza kuvumilia kuiangalia. Ilinitisha mno…….
“hutakiwa kubisha kwa hili. Cha msingi ni kutekeleza agizo langu.” Aliongea maneno hayo na kunifanya nizidi kutetemeka.
“mbona mimi sina pete yako?” nilijikuta nimemuuliza hilo swali huku macho yangu niki yakwepesha yasikutane na macho yake.
“hii si sehemu salama ya kuongelea hili. Pia sihitaji kuisikia sauti yako kwa sasa. Nifuate.” Aliongea huyo msichana na kuanza kupiga hatua zake kuelekea kwenye gari.niliutambua uwezo wake wa ajabu ambao ulinifanya nitii amri kwa kumfuata msichana huyo. Niligeuka nyuma na kuwatazama rafiki zangu ambao walinipa ishara ya heshima wakiamini nimepata zali. Moyoni niliwaambia kua hamjui kinachoendelea huko mbele. Ni mchezo wa kuyachezea maisha yangu kabisa.
Nilikubali kua mwana kondoo na kuingia kwenye gari hiyo kinyonge.
Sikusemeshwa na mzungu huyo aliye washa gari na kuondoka mbio na kuwaachia mavumbi watu waliokua hapo.
Sikujua ni wapi alipoelekea, ila niliona akishika njia ya kuelekea ubungo na baadae alinipeleka maeneo ya kimara ndani ndani na kusimamisha gari eneo ambalo lilikua mbali na makazi ya watu.
Alishuka na kunifuata nilipo.alifungua mlango kwa hasira na kunishusha.
“nina wiki moja tu ya kubaki hapa nchini. Unatakiwa ujitahidi sana kuhakikisha unaipata pete yangu kwa usalama wako.” Aliongea huyo dada na kunisogelea.
“ile pete uliyo iokota ni yangu, na inatakiwa haraka sana muda huu.” Aliongea huyo mzungu na kunifumbua macho. Hapo ndipo nilijua ni pete gani aliyokua anaizungumzia.
“ile pete mbona nilimpa mtu na sasa ameshiuza?” niliongea huku bado moyoni mwangu kukiwa hakuna amani.
“ni wewe pekee ndio unatakiwa unikabidhi hiyo pete……… sina la ziada.” Aliongea huyo dada na kwenda kwenye gari yake na kuondoka huku akiniacha pale peke yangu.
Nilianza kurudi taratibu huku nikiutafakari umbali wa kutoka maeneo hayo kwa mguu hadi mburahati. Maana sikua na hata shilingi mfukoni.
Kabla sijaifikia bara bara, niliona kitu mfano wa hela ikipeperuka na kuja upande wangu. Niliiokota na kuitazama, ni kweli ilikua noti mpya kabisa ya shilingi elfu kumi. Nilifurahi sana na hapo ndipo nilipopata hata nguvu ya kuongeza kasi na kutokea barabarani ambapo nilikunywa soda na vitafunwa vilivyokua hapo dukani. Baada ya kupooza njaa, ndipo nilipopanda gari na kwenda kujipumzisha chumbani kwangu.
Huko mawazo yalini peleka ni jinsi gani naweza kuipata pete hiyo ambayo ilishauzwa kwa sonara. Na hata kama itakuwepo mpaka muda huo, ni wazi itakua inauzwa ghali sana gaharama ambazo mimi siwezi kuzimudu hata kidogo.
Niliwaza sana na baadae mawazo yalizidiwa nguvu na uchovu na kujikuta nimepitiwa na usigizi.
Upepo mkali usiokua wa kawaida uliokua unagongesha madirisha ya chumba changu kwa nguvu ndio kitu kilichonikurupua kutoka kwenye usingizi mzito. Giza lililotawala ndio lililonifanya nigundue kua usiku ulishaingia. Nilinyanyuka kivivu na kuwasha taa yangu iliyokua na mwanga hafifu na kwenda kufunga madirisha yaliyokuwa wazi na kurudi tena kulala.
Hazikupita hata dakika tano, nilishangaa kuona madirisha niliyoyafunga yalikua wazi na kuendelea kugongeshwa na upepo uliokua unapuliza kwa kasi huko nje.
Niliamka kwa hasira na kwenda kufunga huku nikiwa macho pima kuhakikisha kua nafunga vizuri na komeo. Nilikaa kama dakika kumi na kuhakikisha kua hali ilikua imetulia na kuamua kulala tena.
Safari hii upepo ulikua mkali na kufungua mpaka mlango. Ukulele wa mlango kujibamiza ndio ulionifanya nikurupuke na kuanza kuingiwa na hofu kutokana na upepo huo wa ajabu uliokuwepo usiku huo, nilienda kufunga mlango na madirisha kwa mara nyingine, nilipomaliza tu kufanya hivyo, niligeuka nyuma na kutazama kitandani kwangu.
Alikua amekaa Yule msichana wa kizungu niliyekutana nae mchana wa siku hiyo. Nilishtuka sana na kujikuta natamani hata kukimbia. Ila mshtuko huo uliweza kuninyong’onyesha viungo vyangu vyote vya mwili.
“unawezaje kulala wakati bado hujamaliza kazi yangu?” aliniuliza kwa ukali msichana huyo aliyesimama haraka kimiujiza na kunifikia usoni.
“nili…nilikua nasubiri kukuche kwanza.” Nilijikuta natetemeka huku nikimpa mjibu ambayo sikua naamini kama yangeweza kunitetea.
“kwa hiyo umeshajua ni wapi unaweza kuipata?” aliniuliza tena baada ya kwenda kukaa kwenye kitanda.
“bado.. ila mara ya mwisho niliambiwa kua imeuzwa kwa sonara.” Niliongea na kuyatuliza macho yangu kwa dada huyo ambaye niliamini kua sio binaadamu wa kawaida.
“itabidi uifuatilia na ujue ipo wapi.” Aliniambia na kunikazia macho. Baada ya hapo,alinyanyuka na kwenda ukutani kama alikua anataka kuitazama picha niliyo ibandika, lakini hakua anahitaji ufanye hivyo, ila alichokifanya ni kunionyeshea uwezo wake wa kijini kwa kupita kwenye kuta hiyo na kupotea.
Nilijikuta nimelowa jasho mwili mzima na mitetemo ya mdomo ndio iliyonionyesha kua hata upumuaji wangu haukuwa wa kawaida.
“ewe muumba wangu… naomba unisaidie nitoke kwenye kisanga hiki.” Nilinyanyua mikono yangu juu na kumuomba Mungu aniepushie na kila baya nililoandaliwa na jini huyo.
Sikuweza kulala tena mpaka kulipokucha, asubuhi hiyo nilifunga safari na kwenda nyumbani kwa mpenzi wangu Martha na kuonana na dada yake.
“mbona asubuhi sana shemeji, kuna usalam ahuko utokapo?” aliuliza dada yake baada ya kuona jinsi nilivyopooza usoni.
“usalama upo, ila nilikua nahitaji unisaidie kitu kwa muda huu.” Niliongea na kumuangalia usoni ili asipate nafasi ya kunikatalia.
“sema tu.” Alinipa nafasi ya kuomba ninachokihitaji.
“nahitaji unipeleke kule mlipouza ile pete.” Niliomba na kumuangalia dada yake ambaye hakuonyesha uso wa mashaka.
“sawa, ngoja basi tunywe chai.” Aliongea maneno hayo na sikupinga. Niliingia nadani na kuandaliwa chai ambayo hata siku na hamu nayo. Baada ya kumaliza kula, tulienda mpaka kwenye hiyo Sonara na kuingia ndani.
“kuna kaka mmoja anaitwa Moud, tumemkuta?” aliuliza shemeji yangu baada ya kumuona mtu tofauti na mtu waliyemkuta siku ile walipoiuza ile pete.
“dah!.... Moud yupo hospitali hivi sasa. Ame pooza mikono yote miwili na miguu.” Aliongea Yule jamaa kwa masikitiko makubwa.
“tatizo ni nini hasa lililomfanya mpaka apooze?” aliuliza dada yake Martha kwa mshangao kidogo.
“hata mimi sikuji, ila ilianza ghafla tu baada ya kuanguka alipokua anaoga nyumbani kwao. Alipopelekwa hospitali ndio ikagundulika kua hakuna mawasiliano katika mikono yake na miguu yake.” Aliongea Yule jamaa na kutufanya wote tuingiwe na imani japokua siku mfahamu huyo mtu anayezungumziwa hapo.
“kilichotulea ni pete ambayo tulikuja kuiuza hapa. Tunaihitaji kama bado ipo.” Niliongea baada ya kupeana pole.
“pete aina gani hiyo?” aliuliza huyo jamaa.
“ni pete Fulani hivi iliyokua na sura ya kinyago cha rangi ya dhahabu na macho yake ya yana mwangaza wa bluu. Pia imenakshiwa na almasi kidogo.” Niliielezea kwa ufasaha japokua siku kaanayo kwa muda mrefu.
“ile pete imeshauzwa… tena kainunua mkurugenzi wa TBU jana jioni.” Aliongea huyo jamaa na kunifanya nikae chini. Maana huyo mtu niliyetajiwa ni mtu maarufu sana na huwezi kuonana nae kirahisi kama wewe ni kapuku kama mimi. Hapo ndipo nilipoanza kuona ugumu wa kazi. Nilijuta kwa nini niliiokota ile pete.
ITAENDELEA
 
RIWAYA…..THE MAGIC RING ( 04 )
MTUNZI….. HUSSEIN O. MOLITO
TRANSLATION….. GIFT KIPAPA
UHARIRI…. HAZRAT HUSSEIN
+255 (0)718 97 56 59
+255(0)765 68 48 70
“ile pete imeshauzwa… tena kainunua mkurugenzi wa TBU jana jioni.” Aliongea huyo jamaa na kunifanya nikae chini. Maana huyo mtu niliyetajiwa ni mtu maarufu sana na huwezi kuonana nae kirahisi kama wewe ni kapuku kama mimi. Hapo ndipo nilipoanza kuona ugumu wa kazi. Nilijuta kwa nini niliiokota ile pete.
Nilirudi nyumbani nikiwa hoi kabisa huku kichwa changu kikiwa kimevurugika na sijui ni wapi nitaanzia kumpata huyo mwarabu mwenye kampuni kubwa ya madini inayotambulika kama TBU.
Njaa nayo haikuacha kuuma baada ya kuona mpka saa tisa mchana bado sijatia chochote tumboni toka ninywe chai na vitumbua viwili kwa shemeji yangu. Nilijikusanya taratibu na kwenda kwa mama ntilie wa jirani na kuagiza wali.
Nilikula huku mawazo ya pete yaliyonikosesha amani yakiwa yamenitawala kichwani mwangu.
Baada ya kumaliza kula, nilienda kituo cha basi na kupanda magari yaendayo msasani ambapo ofisi hizo zilikua zinapatikana karibu na ubalozi wa marekani. Nilifika kwenye ofisi hiyo kubwa iliyokuwa na geti lililokua na mlinzi akiuliza maswali kwenye kidirisha kidogo hata kabla hujaingia ndani. Nilikata tamaa ya kupata majibu mazuri kutoka kwa mlinzi huyo hata kabla sijaelezea shida yangu. Kwakua nilishafika na nia ndio iliyokua inaniongoza, basi sikusita kumsalimia na yeye akaitikia na kuwa makini kunisikiliza.
“namuulizia mkurugenzi wa ofisi hii, nimekuta?” niliuliza baada ya salamu.
“una appointment nae?” aliniuliza hilo swali lililonifanya ninyong’onyee kidogo. Maana huyo mkurugenzi hua namuona tu kwenye gari lake na sijawahi kuongea nae hata neno moja.
“sina, ila nina shida nae mmuhimu sana.” Niliongea na kumuangalia Yule mlinzi ambaye sura yake haikuonyesha kama alikua tayari kushirikiana na mimi kwenye jambo hilo.
“unatakiwa uandike barua ambayo itakua na namba yako ya simu, kisha utapigiwa na kupangiwa siku ya kuonana nae. Pia usisahau kuelezea shida yako unayotaka kuongea nae kwenye hiyo barua.” Alinipa maelezo hayo yaliyonifanya niage na kurudi nyumbani nikiwa hoi bin taabaani.
Masaa yaliyoyoma kwa kasi na kufikia saa tatu usiku. Niliangalia salio langu na kugundua nimebakiwa na shilingi elfu nne. Nili chukua elfu moja na mia tano na kwenda kwa mama ntilie tena na kupata chakula cha usiku. Niliporudi, nilichukua maji na kuoga kisha nikajitupa kitandani kuutafuta usingizi baada uchovu wa siku nzima niliokua nao.
Usiku wa manane, niliamshwa tena na upepo mkali ambao ulifungua mlango wangu niliofunga vizuri na komeo. Niligundua tu kua Yule jini alikua karudi tena kunipa karaha. Nilinyayuka huku nkiwa nimejawa hasira iliyochanganyika na uoga. Nilienda kuufunga mlango na niipogeuka nyuma nilimkuta kama kawaida amekaa kitandani.
“kazi yangu niliyokupa umefikia wapi?” aliuliza huku akiwa amenitumbulia macho yake ya blu yaliyotisha kidogo.
“kusema ukweli kazi yako ni ngumu na naelekea kushindwa.” Niliongea huku nikiwa naonyesha wazi kuchoka kutokana naugumu wa kupatikana hiyo pete kwa huyo tajiri.
“usiseme unaelekea kushindwa wakati wewe ndio uliosababisha mpaka pete yangu ipotee. Au ninavyokuja bila kukuonyesha kua nina uwezo wa kukutia maumivu unaniona bwege?... sasa naondoka na kesho nitarudi tena. Ole wako nisikukute na pete, …… utajuta kuzaliwa.” Aliongea kwa hasira na sauti iliyobadilika na kua ya kuogofya sana. Nilijikuta ujasiri wote niliokua nao katika kujibu hapo mwanzo ukinipotea ghafla na vinyweleo vyote vya mwili vilinisisimka na kunifanya nitiririkwe na jasho la uoga liluilonilowesha kila mahali.
Baada ya kuongea maneno hayo, aliondoka kwa hasira kwa kupitia kwenye tundu za mbao za mlango wangu ambao nilishaufunga. Ndani hakukuweza kulalika tena, niliamua kutoka na kuanza kutembea kwa mguu bila kujali madhila ya usiku na vibaka waliojaa mtaani usiku huo.
Sikuweza kuchoka miguu zaidi ya kuhema juu juu tu baada ya mwendo mrefu na wa haraka nilikua natembea kuelekea kwenye ofisi ya Al- Hadad ambaye ndio mmliki wa hiyo kampuni. Nilipofika tu, niliona malngo wa nyumba yake ambao ndio upande wa pili wa ofisi yake ukifunguliwa na gari ambayo nilizoea kuona Al- Hadad akiendeshwa ikiwa inatoka taratibu. Sikuweza kumuona kutokana na tinted iliyopigwa kwenye vioo vya gari hiyo.
Nilivuta subira mpaka saa kumi na mbili asubuhi anbapo ndio geti la wafanyakazi lilifunguliwa na mimi nikapata nafasi ya kuingia ndani mpaka reception ambapo nilimkuta dada aliyekua hapo mapokezi na kumsalimia.
“eleza shida yako.”aliuliza huyo dada baada ya kuitikia salamu yangu.
“nahitaji kuonana na mkurugenzi.” Niliongea huku nikiwa natabiria swali ambalo litahusiana na appointment kama nilivyoulizwa getini siku ya jana.
“mkurugenzi amesafiri . labda uje wiki ijayo.” Aliongea Yule dada wa mapokezi na kunifanya nishtuke kidogo.
“mbona jana tu nilifika hapa na nikaambiwa alikuwepo?” niliuliza huku nikiwa nimemkazia macho Yule binti.
“amesafiri leo hii mapema kuelekea nchini Dubai… sidhani kama nina maelezo mengine ninayoweza kukupa zaidi ya haya niliyokuambia.” Aliongea Yule dada na kunifanya niondoke bila kuaga kwa jinsi nilivyochanganyikiwa.
Wazo la kuwenda airport lilinijia ilimradi niweze kuwahi kabla hajasafiri. Maana niliunganisha maneno ya Yule secretary na lile gari nilillo liona ndio nikajua kutakua na ukweli juu ya kuondoka kwa Al- hadad.
Nilifika airport huku nikitweta kwa utembeaji wangu wa haraka baada ya kushuka tu kwenye daladala. Nilishtushwa na mungurumo mkali wa ndege irukayo huku ikiashiria kua ilikua inaelekea huko Dubai.
Nilishika kichwa na sikujua nini nifanye. Mkwara niliopigwa na Yule jinni ulinifanya nisilaze damu kwa kuhofia adhabu nitakayopewa na huyo jinni.
Niliyafuta machozi ya kidhaifu na kujipa moyo kuwa naweza kusafiri na kufika huko japokua mfukoni nilikua na elfu mbili.
Nilienda kwenye benk iliyokua karibu na hapo na kujaza statement za benk hiyo kama nlilikua nahitaji kuweka hela huku nikisoma mazingira kwa watu waliokua wanaingiza na kutoa hela. Nilimshuhudia mtu akitoa milioni kumi na kupakiwa kwenye mfuko maalumu baada ya maburungutu kupanga vizuri. Kisu kidogo nilichokua nacho kwenye mashine ya kukatia kucha, ndio niliamini itakua silaha tosha ya kufanya kitu kwa mtu huyo. Nilimpa nafasi ya kulivuka geti na nikamuwahi na kumnon’goneza masikioni.
“bastola yangu ina risasi mbili tu… lakini naamini naweza kuutoa uhai wako kama utakua mbishi wa kuniachia hivyo vijisenti ulivyoshika.” Niliongea huku mkono wangu nilioshika hiyo mashine nikiwa nimeuviringita kwenye gazeti. Nilimgusa kidogo na ubaridi ulipomfikia alishtuka na ndipo nilipomsoma na kugundua udhaifu wake katika dhana ya kuamini kua kweli nilikua nimeficha bastola kwenye gazeti.
“chukua tu .. naomba usinidhuru.” Aliongea kwa upole na kunikabidhi ule mfuko mweusi uliofungwa vizuri.
“gari lako lipo wapi?” niliuliza kwa sauti ya chini lakini iliyojaa msisitizo.
“lile pale.” Alinijibu haraka.
“twende” nilitoa amri nay eye akafuata bila wasi wasi.
Tuliingia kwenye gari huku nikimtoa wasi wasi wa maisha yake kama atatii kila nitakalomuambia.
Nilimwambia endeshe gari na kulekea kwenye msitu wa mabwepande. Huko nilimshusha na kuchukua simu zake na kuondoka na gari lake mpaka ubungo ambalo nililitelekeza huko .
Nilifika nyumbani na kubadilisha nguo, bada ya kuwa smart, nilielekea ubalozi wa dubai na kwenda kuomba passport ya kusafiria. Baada ya kupata na kulipia gharama zote, sikulaza damu. Nilienda airport na kukuta kuna ndege ielekeayo Dubai saa tano usiku. Nilitulia hapo huku nikiomba Mungu anijaalie niweze kuondoka kabla sijakamatwa kutokana na kitete nilichokua nacho muda huo. Sikuona thamani ya hela nilizokua nazo zaidi ya kuitafuta pete ya watu.
Muda ulipofika, sikuamini kua ni mimi ndie niliyekua nazikanyaga ngazi za ndege na kutafuta siti yangu na kukaa. Sikuona utamu wa ndege zaidi ya kuombea tu tuwahi kufika huko na nisipate shida kumtafuta Al-hadad.
Baada ya magurudumu ya ndege kuzunguka kwa kasi kwa muda mrefu, hatimaye ndege illianza kupaa kuelekea mawinguni kwa kasi ya ajabu kuitafuta Dubai ilipo.
ITAENDELEA
 
RIIWAYA…..THE MAGIC RING ( 05 )
MTUNZI….. HUSSEIN O. MOLITO
TRANSLATION….. GIFT KIPAPA
UHARIRI…. HAZRAT HUSSEIN
+255 (0)718 97 56 59
+255(0)765 68 48 70

Nilifika nyumbani na kubadilisha nguo, bada ya kuwa smart, nilielekea ubalozi wa dubai na kwenda kuomba passport ya kusafiria. Baada ya kupata na kulipia gharama zote, sikulaza damu. Nilienda airport na kukuta kuna ndege ielekeayo Dubai saa tano usiku. Nilitulia hapo huku nikiomba Mungu anijaalie niweze kuondoka kabla sijakamatwa kutokana na kitete nilichokua nacho muda huo. Sikuona thamani ya hela nilizokua nazo zaidi ya kuitafuta pete ya watu.
Muda ulipofika, sikuamini kua ni mimi ndie niliyekua nazikanyaga ngazi za ndege na kutafuta siti yangu na kukaa. Sikuona utamu wa ndege zaidi ya kuombea tu tuwahi kufika huko na nisipate shida kumtafuta Al-hadad.
Baada ya magurudumu ya ndege kuzunguka kwa kasi kwa muda mrefu, hatimaye ndege illianza kupaa kuelekea mawinguni kwa kasi ya ajabu kuitafuta Dubai ilipo.
Rubani wa ndege hiyo alijitahidi kukata mawingu huku watu wakiufurahia usiku huo kwa kutazama movie zilizokua zinarushwa kwenye tv zilizo kuwepo nyuma ya siti zao. Mimi nilikua naangalia lakini sikua na amani. Nilijua tu kama Yule jini akiamua kunitokea kwenye ndege basi atanitia aibu sana kama si kuonekana kichaa.
Gafla nilianza kuisikia harufu nzuri ya marashi kama kuna mtu kajipulizia na kupita karibu yangu niliangaza huku na huko na sikuona mtu yeyote. Baada ya muda, niliguswa bega . na nilipogeuka, nilikutana na uso wa huyo jinni ukiwa umejaa tabasamu kwa mara ya kwanza toka aanze kunitisha.
“wewe ndio mwanaume unayetakiwa kuishi hapa duniani. Kwa mara ya kwanza nimeona juhudi zako. Well done…. Nimekuja kukusalimia tu. Ila naakukumbusha kuwa nimebakiwa na siku mbili za kubaki duniani kabla sijarudi kwetu. Nakutakia safari njema.”
Aliongea Yule jinni na kupotea kwa mtindo usiotisha sana.
Nilimuangalia mpaka anapoishia dirishani kama vile anataka kudondoka, na baadae nikaona amebadilika na kuwa ndege wa ajabou na kuanza kushuka chini na kupotelea gizani.
Nilibaki macho mpaka palipokucha huku nikijaribu kuangalia ni wapi naweza kumpata huyo mwarabu huko nchi za watu. Ubongo wangu ulianza kuniambia kua kuna uwezekano nikafika eneo ambalo watu hawajui Kiswahili wa kiingereza zaidi ya kiarabu ambacho nlikua sijui hata maji ya kunywa yanaombwaje.
“potelea pote.”
Nilijisemea moyoni huku nikiangalia dirishani kuangalia mandhari ya nchi za wenzetu kwa juu ambayo hayakunifurahisha kutokana na hofu niliyokua nayo moyoni.
Baada ya safari ndefu, hatimaye magurudumu ya ndege tuliyopanda yalianza kuburuzika kwa kasi kwenye uwanja mkubwa wan chi hiyo. Baada ya kusimama na kuanza kushuka, nilitoka nje na kukutana na madereva waliokua wanasubiria wateja wao.
Niliingia duka la kubadilishia fedha za kigeni na kutoa milioni mbili na kumpa. Alinipe fedha zangu ambazo zilikua ndogo lakini niliamini zilikua na thamani kubwa kwa kila noti niliyopewa.
Niliangaza huko na huko baada ya kurudi kwenye kituo cha taksi na ndipo nilipomfuata mtu ambaye alikua na asili ya kiafrika ambaye naye alikua amepaki gari yake.
“I want go… hotel” niliongea huku nikiwa nababaika kwakua hata kiingereza chenyewe kilikua cha kuunga na super glue.
“any hotel?” aliuliza na kunifanya niitikie kwa kutikisa kichwa.
Niliingia kwenye gari hiyo na kunipeleka hoteli ya kimataifa ya nchi hiyo. Bado kidogo nigome kushuka kutokana na muonekano wake kwa nje. Maana ilikua nzuri na muwako wa mataa yake yaliyonipumbaza ndio yaliyonifanya nishuke na kumpa huyo jamaa noti moja nilizofanikiwa kuchaenji baada ya kushuka tu kwenye uwanja wa ndege na kunirudishia chenji yangu.
Nilianza safari ya kuingia kwenye hoteli hiyo huku watu wenye suti na wengine wakiwa na kanzu pamoja na majoho wakiwa wanaingia humo hotelini.
Kabla sijaingia kwenye mlango mkuu wa kuingilia kwenye mapokezi ya hoteli hiyo. Mnilijikuta nageuza shingo yangu nyuma kuangalia mazingira. Mara moyo wangu ukashtuka sana baada ya kumuona mtu kama Al- hadad akiwa amenipa kisogo huku akiongoe na watu waliokua wamevaa makanzu kama yeye. Japo kua sikua na uhakika, ila nilimsogelea na kuwasalimia.
“assalaamu aleykum”
Baada ya kutoa salamu hiyo, wote wliitikia na kunigeukia. Hapo ndio nikagundua kua Yule niliyemuhisi kua ni Al-hadaadi, fikira angu zilikua sahihi kabisa.
“bila shaka wewe ni mheshimiwa Al- hadad.” Niliongea Kiswahili na kumfanya Al-hadad kushtuka kidogo kusikia utambuzi wangu tena kwwa lugha ya Kiswahili.
“ndio mimi,” aliitikia huku akiwa amenikazia macho kama mtu aliyekua anajaribu kunisoma bila ya kupata majibu.
“nina shida na wewe, ukimaliza kuongea na mimi naomba nafasi nitete na wewe kama dakika mbili tu.” Niliongea hayo maneno na kumuangalia Al-hadad ambaye aliniangalia kwa muda kisha akini kubalia kwa kutikisa kichwa chake. Nilisogea pembeni na kusimama kwa dakika tano, kisha nikaitwa na kwenda pale pale.
“we ongea tu, hawa hawajui Kiswahili.” Aliniambia na mimi sikuona haja ya kuendelea kung’ang’ania kufanya vitu hivyo kuwa siri yetu.
“nimefunga safari kutoka Tanzania mpaka huku, ni kwa ajili yako. Namshukuru Mungu kunikutanisha na wewe leo hii. Kubwa lililonileta kwako ni kuhusiana na pete uliyoinunua siku za hivi karibuni kwenye duka la vito vya thamani kariakoo. Ndugu yangu nisikufiche, ile pete si ya kawaida na inanitesa sana mwenzako.” Nilionea maneno hayo na kumfanya aniangalie kwa dharau.
“kwa hiyo unataka nifanyaje.. sijakuelewa bado ni nini unachokihitaji kutoka kwangu?.” Aliongea na kuniangalia huku akionyeesha wazi kukasirishwa na mimi.
“nahitaji tu hiyo pete. Kuna milioni tano hapa kwa ajili ya kunipa tu mimi hiyo pete.” Niliongea huku nikikubali kubakiwa na hela ya tiketi ya ndege ya kurudia tu nchini kwetu.
“kwanza mimi siuzi hiyo pete. Nimenunua kwa ajili ya mapambo ya mke wangu nyumbani. Kwa hiyo hata mimi sina hapa nilipo.” Aliongea maneno hayo na kunivunja moyo. Haikupita hata sekunde mbili, simu yake ya mkononi iliita na kuipokea. Mara ghafla niliona anatetemeka na haikupita muda akadondoka chini na kuzimia.
Ambulance ya hoteli hiyo ilifika haraka na kumuwahisha hospitalini ambapo hapakua mbali na hiyo hoteli. Hata mimi nilipata nafasi ya kuingia kwenye gari hiyo ya kwenda mpaka hospitali.
Baada ya masaa mawili, alizinduka na mtu wa kwanza kumuita baada ya kuzinduka ni mimi. Nilikuja kuitwa na madaktari na kupelekwa mpaka kwa Al-hadad.
Nilimkuta analia huku akinishika mikono yangu kama avile alikua anahitaji msaada wa kum kalisha. Nilimnyanyua na kumshika begani na kumpa pole.
“nimepewa taarifa mbaya kuhusu mke wangu. Amedondoka na baada ya kupelekwa hospitali majibu yamesema ame pooza mwili mzima. Hawezi hata kujinyanyua. Na chanzo ni pale tu alipoivua ile pete.” Aliongea na kniangalia kwa macho ya huruma.
“ndio maana nikakuambia kua hiyo pete inanitesa. Hata mpenzi wangu amekua chizi. Na Yule aliyekuuzia pete nae amepooza hivyo hivyo. Cha msingi ni kurudi tu Tanzania na kunipa hiyo pete niirudishe kwa mwenyewe. Anaweza kumrudishia uzima wake mke wako na wote waliopata madhara kutokana na pete hiyo.” Nilimpa huo ushauri. Na hapo hapo akachukua simu na ku oda tiketi mbili za kesho kwa ajili ya kurudi Tanzania.
ITAENDELEA
 
RIWAYA…..THE MAGIC RING ( 06 )
MTUNZI….. HUSSEIN O. MOLITO

+255 (0)718 97 56 59
+255(0)765 68 48 70

Nilimkuta analia huku akinishika mikono yangu kama avile alikua anahitaji msaada wa kum kalisha. Nilimnyanyua na kumshika begani na kumpa pole.
“nimepewa taarifa mbaya kuhusu mke wangu. Amedondoka na baada ya kupelekwa hospitali majibu yamesema ame pooza mwili mzima. Hawezi hata kujinyanyua. Na chanzo ni pale tu alipoivua ile pete.” Aliongea na kniangalia kwa macho ya huruma.
“ndio maana nikakuambia kua hiyo pete inanitesa. Hata mpenzi wangu amekua chizi. Na Yule aliyekuuzia pete nae amepooza hivyo hivyo. Cha msingi ni kurudi tu Tanzania na kunipa hiyo pete niirudishe kwa mwenyewe. Anaweza kumrudishia uzima wake mke wako na wote waliopata madhara kutokana na pete hiyo.” Nilimpa huo ushauri. Na hapo hapo akachukua simu na ku oda tiketi mbili za kesho kwa ajili ya kurudi Tanzania.
Baada ya madaktari kuhakikisha kuwa Al-hadad yupo salama na anaruhusiwa kuendelea na mambo yake kama mkawaida. Walimruhusu.
Tulienda wote hotelini na yeye na kunilipia chumba ambacho hakikua mbali na chumba alicholipia yeye.
Asubuhi na mapema niliamka huku nikiusikilizia muda wa kwenda airport kwa ajili ya kurudi Tanzania.
Ilikuja gari kutupitia na mimi pamoja na mkurugenzi wa TBU tukapanda gari moja na kupata nafasi ya kunena maneno mawili matatu na tajiri huyo. Umoja huo uliendelea hadi kwenye ndege ambapo tulikaa siti za karibu kabisa huku mimi akinipa nafasi upande wa dirishani baada ya kuniuliza napenda kukaa upande gani.
Tukiwa angani baada ya ndege kuruka, niliwaza sana kufika haraka na kufanikiwa kuipata pete hiyo. Niliamini hiyo ndio itakua furaha yangu kwa sababu nilishachoshwa na maisha ya kufuatiliwa na viumbe wa ajabu.
Tulitua uwanja wa ndege wa taifa wa mwalimu nyerere na tukapokelewa na wafanyakazi wa Al-hadad waliyekuja na magari ya kifahari maeneo hayo.
Msafara huo wa gari tatu uliishia kwenye hospitali ya kimataifa agakhan na kwenda moja kwa moja kwenye chumba alicholala mke wake na kumuona akiwa amelala huku akiwa hana uwezo wa kusogeza kiungo chochote.
Al-hadad aliia sana baada ya kumuona mke wake akiwa katika hali kama ile. Alikua anampenda sana na kitu kilichompoozesha ilikua ni zawadi ambayo aliamni itamfurahisha kwa sababu mke wakea likua anapenda sana pete. Hakujua kua pete hiyo ingeweza kumlaza mke wake huku akiwa amepooza mwili mzima.
Baada ya kutoka hospitalini, tulienda nyumbani kwa Al-hadad ambapo huko tulimkuta mlinzi ambaye alitupa majibu ya kushangaza baada ya kuulizia kupooza kwa mke wake.
“hiyo pete nani aliichukua baada ya mke wangu kuanguka??” aliuliza Al-hadad baada kuona hakuna dalili zozote za kuwepo kwa pete hiyo maeneo hayo.
“pete nimeitupa.” Aliongea huyo mfanyakazi na kunifanya nitoe macho kama ktu aliyesikia taarifa za msiba wa mtu ninaye mtegemea kwa ajili ya jambo Fulani la muhimu kwake.
“umeitupa?” aliuliza A-l hadad kwa mshangao mkubwa.
“ndio bosi… sasa si nilipomuona mama anahangaika huku pete yake ikiwa pembeni, ndipo niliamini kua ile pete ndio inamtesa.” Alijibu Yule mlinzi huku akijiona hana hatia yoyote zaidi ya kustahili pongezi kwa kitu alichokifanya.
“twende maeneo ambayo umeitupa hiyo pete.” Aliamuru Al-hadad na wote tukaenda huko kwa ajili ya kuitafuta hiyo pete.
Tulihangaika sana kuitafuta huku tukimuuliza kua labda kuna mtu alimuona wakati anatupa, lakini alikanusha na kusema kua hakuna mtu mwengine aliyeingia mle ndani zaidi yake.
Vifaa mbali mbali vya kuchunguzia madini vililetwa baada ya Al-hhadad kuagizia kutoka ofisini ambapo hapakua mbali na anapoishi.
Mpaka kiza kinaingia , hatukuweza kufanikiwa kuiona hiyo pete.
Nilivuta taswira na kujiona mtu niliye feli kutokana na kua siku hiyo ndio siku ambayo Yule jini aliniambia kua alikua anaondoka na kurudi kwao.
Niliwaza sana jinsi atakavyo nitokea kwa ajii ya kunipa adhabu kwa kutomletea pete kwa wakati. Pia niliwaza ni jinsi gani naweza kuwaponyesha watu walio pata madhara kutokana na pete hiyo ambayo naamini kila ikitua kwa mtu lazima ilmletee maradhi ya kupooza.
Usiku ulipokua mkubwa, nilienda kulala kwenye chumba cha wageni kilichokuwepo kwenye jumba hilo la kifahari. Sikuweza kupitiwa na usingizi huku mawazo yangu na macho yangu yalikua yakicheza kwenye saa kutokana na kuijua mida anayokuja.
Mshale ulipogota na kusoma kua ilikua saa tisa juu ya alama, nilianza kuisikia harufu nzuri iliyokua inaisikia kwenye ndege. Nilitulia tuli huku nikipanga na kupangua.
Harufu hiyo ilizidi kunukia nyuma yangu na kunifanya nigeuze shngo yangu na kugeuka nyuma.
nilikutana na jini huyo aliyekua amependeza sana kuliko siku zote.
“najua kua umefanya kazi kubwa sana katika kuhakikisha kua unaweza kuipata pete yangu. Nikupongeze kwa hilo kwa sababu umeonyesha hali kwa moyo wako. Nina kila la kujivunia kwako kwa juhudi ulizozionyesha. Nimekuja na mambo mawili muda huu, jambo la kwanza ni kukutoa hofu na kukuambia kua ile pete nimeshaipata. Na jambo la pili ni kukuaga kua naondoka na sitarudi tena kukusumbua. Ni hayo tu. Kama una la ziada la kuniambia kabla sijaondoka, unaweza kusema.” Aliongea jini huyo na kunionyeshea hiyo pete. Hapo aliweza kunifanya nishushe pumzi zangu huku tabasamu hafifu likichomoza kuashiria kufurahia taarifa zile.
“mimi nina ombi tu kutoka kwako. Warudishie afya zao wale wote waliopata madhara kutokana na pete hiyo. “ niliongea huku nikimtazama jinni huyo ambaye muda huo alikua anatabasamu huku macho yenye viini vya bluu ambayo kwa sasa havikunitisha zaidi ya kuona vimemuongezea muonekano mzuri jini huyo aliye kuja ki amani.
“najua ni jinsi gani unavyofurahi , hata hivyo nakuondoa hofu kwa kukuambia kua kila aliyeathirika na hii pete, yupo safi na wa afya kama zamani. Ila nitafurahi uwaache walale ili waamke asubuhi wakiwa na furaha kama uliyokua nayo wewe.” Aliongea Yule jinni na kunifanya nifurahi sana . hali iliyonifanya nijisahau mpaka nikamfuata na kutaka kumkumbatia, aliyeyuka na kutokea upande mwengine.
“mwili wangu huguswa kwa taarifa kwanza kabla ya kitendo. Haya kwa sasa unaweza kunikumbatia.” Aliongea Yule jinni na kuonyesha mikono ya utayari kwa ajili ya kumbatio langu.
Sikua na uoga tena kutokana na sura aliyokuja nayo siku hiyo. Pia maongezi yake yalionyesha wazi kua alikua na sauti nzuri ukiachana na ile aliyokua anaitumia kunitisha.
Taratibu nilimsogelea na kumkumbatia. Nilihisi ubaridi mkali kutoka kwenye mwili wake alikua kama mtu aliyekufa vile kwa jinsi alivyokua.
Hata hivyo niliweza kugundua kua hata jini huyo alikua amekipata kitu ambacho hajawahi kukipata kama hakuwahi kukumbatiana na binaadamu. Ni joto lililmfanya aheme kwa nguvu na kutabasamu huku akinikumbata kwa nguvu ili alipate joto hilo vizuri.
Tuliachiana huku kila mmoja akimuangalia mwenzake na kumfanya Yule jini kuaga.
“nakutakia maisha mema.” Aliniambia na kuaniangalia huku anatabasamu.
“nawe pia.” Nilimjibu na kumpungia mkono baada ya yeye kuanza kupotea taratibu kwenye dirisha kupitia kwenye kioo kilichofungwa.
Sikuamini kua kweli nimemalizana na jini huyo na hawezi kunitokea tena katika maisha yangu.
ITAENDELEA
 
RIWAYA…..THE MAGIC RING ( 07 )
MTUNZI….. HUSSEIN O. MOLITO
+255 (0)718 97 56 59
+255(0)765 68 48 70

Taratibu nilimsogelea na kumkumbatia. Nilihisi ubaridi mkali kutoka kwenye mwili wake alikua kama mtu aliyekufa vile kwa jinsi alivyokua.
Hata hivyo niliweza kugundua kua hata jini huyo alikua amekipata kitu ambacho hajawahi kukipata kama hakuwahi kukumbatiana na binaadamu. Ni joto lililmfanya aheme kwa nguvu na kutabasamu huku akinikumbata kwa nguvu ili alipate joto hilo vizuri.
Tuliachiana huku kila mmoja akimuangalia mwenzake na kumfanya Yule jini kuaga.
“nakutakia maisha mema.” Aliniambia na kuaniangalia huku anatabasamu.
“nawe pia.” Nilimjibu na kumpungia mkono baada ya yeye kuanza kupotea taratibu kwenye dirisha kupitia kwenye kioo kilichofungwa.
Sikuamini kua kweli nimemalizana na jini huyo na hawezi kunitokea tena katika maisha yangu.
Asubuhi ya sikuhiyo, niliamka mapema sana na kumkuta Al- hadad ameshaamka.
“kuna taarifa nzuri mzee, japokua sina uhakika kama kweli amtekeleza yale yote aliyoniambia. Ila cha kufurahisha ni kwamba tayari huyo jini ameshaipata pete yake.” Niliongea na kumfanya Al-hadad aliyekua na sura ya huzuni kuanza kutabasamu.
“amesemaje kuhusiana na mke wangu?... atapona au?” aliendelea kuniuliza huku akiwa amenikazia macho.
“kwa maelezo yake ni kwamba wakiamka asubuhi wote watakua wazima.”
Baada ya kuongea hayo, hatukusubiri tena kwa haraka ya Al-hadad na ndipo muda huo safari ya kuelekea hospitalini ikaanza.
Tulifika na kuingia ndani. Tulimkuta bado kalala na ndipo nilipomkataza Al-hadad kumuamsha mke wake kwa sababu Yule jinni tayari alishaniambia kila kitu juu ya ubora wa kumuacha mtu aamke mwenyewe.
Tulisubiri kwa nusu saa, hapo ndipo tulipomuona mke wa Al-hadad akifumbua macho. Alituangalia na ndipo nilipomsalimia.
“Unaweza kukaa mama”
Niliongea baada ya kumsalimia. Aliniangalia na hakujua kwanini nilimwambia hivyo na isitoshe sikuvaa mavazi ya kidaktari wala hakuwahi kuniona. Baada ya kurudia mara ya pili umwambia maneno hayo, ndipo alipojaribu kuunyayua mkono wake na kushangaa baada ya kuona unanyanyuka. Hata mimi mwenyewe nilianza kuona kua Yule jinni alikua mkweli. Niligeuka na kumtazama Al-hadad na ndipo nilipomuona akiwa anatabasamu huku akishindwa kuyaficha machozi ya furaha baada ya kuona mke wake amenyanyuka mwenyewe na kukaa. Nilijikuta na mimi nafuta machozi baada ya kuwaona wawili hao wakiwa wanakumbatiana.
Niliwashika na kuwabembeleza. Baada ya wote kunyamaza, niliwaaga tayari kwa kuondoka.
“nadhani mzee. Kazi niliyokua naitaka kuifanya nimeshaimaliza. Ila najua ni jinsi gani mlivyofurahi baada ya kuushinda mtihani wa ajabu uliowapata. Kwa hiyo nawatakia maisha mema, ila mzee nitakapo kwama usisite kunisaidia kwani maisha ya mtaani ni magumu sana.” Niliomba na Al-hadad alinisogelea na kunikumbatia.
“wewe ni mwanangu kwa sasa. Na ni kosa kukaa mbali na mimi.” Aliniambia hivyo Al-hadad na kunifany anitabasamu.
“nashukuru, hata mimi nitajivunia kuwa na baba tajiri kama wewe” niliongea hivyo huku nikijiona kuwa kweli nilikua nastahili kuwa mtoto wa tajiri kama huyo baada ya kukumbatiwa kwa mara ya kwanza.
Niliwaaga na kuwaambia kua naenda kuangalia wagonjwa wengine waliopata madhara kama huyo mama. Nilitoka hapo na safari yangu ilikua hospitali ya vichaa. Baada ya kuonana na Martha, hapo ndipo nilipolipata kumbatio lake maridhawa lililonionyesha kua alikua amepona.
Madaktari walimpima na ndipo wakagundua kua hakuna dalili yoyote ya uchizi.
Niliruhusiwa kurudi nae nyumbani. Nilimpeleka kwa dada yake ambaye alifurahi sana kumuona. Nilimpigia simu jamaa wa kule sonara na kuulizia hali yake, niliambiwa kua amepona kabisa.
Ndipo niliporudi jioni kwa wazazi wangu waliojiteua na kusheherekea sherehe rasmi ya kumshukuru Mungu kwa kumrejeshea uzima mke wa Al-hadad.
****************************

Baada ya kuipata pete, Rosemary alipaa kwa kasi na kurudi kwenye ulimwengu wao. Baada ya kutua, alianza safari ya kumtafuta Edward.
Alitua kwenye nyumba ya Edward baada ya kupaa muda mrefu. Alipofika, alikutana na Edward ambaye alimpa ishara ya kupaa na kuelekea milimani ambapo hakuna jini yoyote aliyekua akiishi huko.
“kipi ulichokuja nacho ambacho kitanifanya nifurahie kuiona sura yako.” Aliongea Edward na kumfanya Rosemary aitoe ile pete.
“nimeipata mpenzi wangu. Naomba tuyamalize.” Aliongea Rosemary na kumsogelea Edward.
Edwar aliichukua ile pete na kuivaa. baada ya hapo, alitabasamu na kumuangalia Rosemary kwa dharau.
“huu ndio mwisho wa story ya mapenzi kati yangu mimi na wewe. Kwahiyo sahau kila kitu kinachonihusu mimi. Yupo ambaye anastahili kuivaa hii pete na si wewe tena.” Aliongea Edward na kumfanya Rosemary apigwe na butwaa. Hakuamini kua anaweza kuachwa kwa mtindo huo licha ya juhudi zake zote alizotumia kuitafuta pete hiyo.
Alimuita Edward bila ya mafanikio. Tayari alishachanua mbawa zake na kupotelea hewani.
“kilio kizito kilichotetemesha mpaka mlima ho kilisikika huku Rosemary akijiona hana faida kutokana na kutemwa na mwanaume anayempenda kupita kiasi.
***************
Kumbu kumbu ya maisha yao hapo awali walipokua wapenzi ndio kitu pekee kilichowafanya waonekane bora kuliko majini wote waliokua wapenzi kwa kipindi hicho. Kwanza walikua ni aina ya majini ambao walikua adimu sana kupatikana katika uzawa wao. Walijuikana kwa jina la Fundy huko kwao na kuwafanya majini wenzao wawaonee gere kwa fundy wawili hao kuanzisha uhusianao.
Majini aina ya fundy huzaliwa mwanaume na mwanamke kwa kila mwaka mara moja kwa majini ambao walikua zaidi ya milioni hamsini. Hivyo ni vigumu fundy kukutana na fundy mwenzake na kutengeneza uhusiano. Wao ndio walikua fundy wa kwanza kuwa na uhusiano wa kimapenzi, hivyo majini walitarajia uzawa wa aina mpya ya majini ambao utatokana na mbegu hizo kukutana.
Maana hhata Fundy mwenyewwe hua hazai Fundy. Hivyo kuwia ugumu kujua ni uzawa gani utabadilika na kuwa na fundy kwa mwaka huo.
Mapenzi yao yalichanua mithili ya maua ya saa nne. Na kila mmoja wapo alikua na hamu na mwenzake kila wasipo onana hata kwa lisaa.
Ghafla ukazuka upepeo usiojulikana uliokuja kuchafua hali ya hewa katika penzi hilo baada ya Edward kukutana na jini fundy mwengine alipokua kwenye masafa yake angani. Huyo Fundy alikua mzuri na wa rangi ya papo iliyochanganyika na kijani mpauko iliyozidisha uzuri wake. Huyu fundy alikua wa rangi mbili na alikua tofauti hadi maumbile. Yeye alivutia sana na alikua na sauti nzuri kama kinanda.
Mabadiliko ya tabia ya Edward ndio yaliyofanya kila siku kutokea migogoro katika penzi lao lililokua katika hatua za mwisho za kufunga ndoa baada ya kuvishana peta.
Baada ya kuchoka kutokana na manyanyaso ya mwanaume huyo, ndio maana Rosemary alipoamua kuanzshisha mtiti mkubwa.
Huko Juu ya mlima, wawili hao walikua wakirumbana na kutoleana maneno kwa ukali. Ilisikika sauti ya kike na kiume huku kila mmoja wao akiwa hataki kuwa chini ya mwenzake. Marumbano hayo yaliishia baada ya msichana kutoa pete yake na kumrushia mwanaume ambaye hakuijali zaidi aliiacha tu hiyo pete ianze kubiringita kwa kasi kuelekea chini ya mlima.
Baada ya tukio hilo, Edward alibadilika na kua kama popo mkubwa na kupaa angani kwa kasi. Haikuchukua muda mrefu, na Rosemary alibadilika na kuwa jamii hiyo hiyo ya popo mkubwa na kupaa angani kwa kuelekea upande wake.
Utengano huo wa majini waliokua wapenzi kwa muda mrefu na wakiwa katika hatua za mwisho kufunga ndoa,ulikua gumzo kwa jamii yote ya majini aina yao.
Hiyo ilikua na mara ya kwanza kutokea katika historia za majini ambao daima hua waaminifu na hua hawaachani mpaka kifo kinapo watenganisha.
Taarifa za ugomvi huo zilifika kwa mkuu wa majini na kuwaita kwa ajili ya usuluhishi, ila Edward aligoma kuripoti hivyo zoezi hilo likafeli.
Uzito wa mahaba ya Edward ulianza kuonekana baada ya kutengana kwa muda wa wiki moja tu. Rosemary alishindwa kula wala kupata usingizi mzuri. Alishindwa hata kuyafurahia maisha japokua alikua na uwezo wa kutembea ardhini na kupaa angani pasipo mipaka. Mateso ya moyo yaliyo muonyesha udhaifu wake juu ya mwanaume huyo aliyeziteka hisia zake, ndizo zilizomshawishi awe mpole na kukubali kurudi kwake na kupiga magoti kwa mawanaume huyo aliyempa majaribu ya kitafuta pete. Hata hivyo Edward anaonyesha kutomjali zaidi ya kuichukua hiyo pete kwa ajili ya kwenda kumvalisha mpenzi wake mwengine.
ITAENDELEA…………..
 
RIWAYA…..THE MAGIC RING ( 8 )
UHARIRI…. HAZRAT HUSSEIN
+255 (0)718 97 56 59
+255(0)765 68 48 70

Uzito wa mahaba ya Edward ulianza kuonekana baada ya kutengana kwa muda wa wiki moja tu. Rosemary alishindwa kula wala kupata usingizi mzuri. Alishindwa hata kuyafurahia maisha japokua alikua na uwezo wa kutembea ardhini na kupaa angani pasipo mipaka. Mateso ya moyo yaliyo muonyesha udhaifu wake juu ya mwanaume huyo aliyeziteka hisia zake, ndizo zilizomshawishi awe mpole na kukubali kurudi kwake na kupiga magoti kwa mawanaume huyo aliyempa majaribu ya kitafuta pete. Hata hivyo Edward anaonyesha kutomjali zaidi ya kuichukua hiyo pete kwa ajili ya kwenda kumvalisha mpenzi wake mwengine.
Mahaba niue yalimshinda Rosemary na kumfanya ahame alipokua ana kwenda mbali kabisa na mji kutokana na aibu ya kuachwa na Edward ambaye kwa sasa alitangaza wazi kua ameshampanda mpenzi mpya tena fundy mwenye rangi mbili.
Rosemary aliumia sana na wakati wote alikua wakulia tu. Na hakupata nafasi hata ya kusubiri ya kujishusha mbele ya mwanaume huyo aliyekua kama lulu moyoni mwake.
Hakuweza kuonana nae, ila alisikia kila kitu kutoka kwa watu waliomwambia kila kitu kinachoendelea kwa wapendanao hao wapya waliozidi kuupasua moyo wake.
Alishindwa kabisa kuvumilia kukaa kwenye jamii yao. Na hapo ndipo wazo la kwenda kwa mtu aliyemtesa kwa ajili ya kutafuta pete lilipomjia. Tabasamu lililo potea kwa takribani miezi mitatu, lili rudi tena na kujitokeza kwa mara ya kwanzo usoni mwake.
“naipenda Dunia.” Aliongea Rosemary na kunyaynyuka. Aliyatoa mabawa yake na kuanza kuruka kwa kasi mpaka kufikia usawa wa mipaka yao na ulimwengu.
********************
Miezi mitatu baadae toka matatizo yale ya kusakamwa na jini kuisha. Maisha yangu yalibadilika sana. Sikua Yule wa kutafuta dili za mizigo tena kutoka kwa watu walio nidhalilisha kila siku kwa kuniita majina ambayo nilikua nayachukia. Sasa hivi nilikua naheshimika sana na kila mtu alitamani hata kukutana na mimi.
Jina kubwa nililo libeba baada ya kutokea kwenye vituo mbali nbali vya televisheni kama mtoto wa mwarabu na tajiri mkubwa wa madini. Al- hadad.
Maisha ya kitajiri, yalinibadilisha kuanzia mwili mpaka mavazi. Nilijitahidi sana kupiga pamba na kuwa mtu ninaye lingana na hadhi ya nyumba niliyokua naishi.
Nilipewa gari moja ya kupigia misele ambayo nilikua nawekewa mafuta kwa ajii ya kutembelea tu mitaa ya matajiri na watoto wa matajiri wenzangu.
Watu hawakujua kwa nini Al-hadad alinitambulisha kama mtoto wake mpendwa, ila nyuma ya pazia nilimshukuru sana Mungu kwa kumleta Yule jini karibu yangu. Maana ile pete ndio imesababisha kila kitu.
Mara kadhaa nilienda disco na kukutana na watoto wazuri ambao nilibaki nimechanganyikiwa na sikujua nimchukue yupi. Fedha ilikua inaruhusu hata kununua wasichana ghali kutoka mataifa mengine waliokua wakijiuza kasino.
Moyo wa upendo uliodondokea kwa Martha ndio uliokua unanisuta na kuniambia kua yupo anipendaye. Na hata kama akiwa chini ya kiwango, kwa fedha zangu nitaweza kumbadilisha.
Mawazo hayo yakija, ndipo hujikusanya na kuingia kwenye gari yangu hadi uswahilini kwao.
“naona shem leo mambo sio mabaya.” Alinitania shemeji yangu baada ya kuniona nimetupia pamba mpya ambazo hajawahi kuziona.
“kawaida tu shem. Vipi, Martha nimemkuta?”niliuliza baada ya kuona utulivu uliokuwemo.
“hayupo… ila amesema hato chelewa kurudi.”aliongea dada yake Martha.
“sawa,… ila akirudi utamwambia kua namtafuta.”
Niliongea na kufungua pochi na kumuachia dada yake shilingi elfu ishirini na kuondoka zangu. Wakati napita njia ya mkato kutokea kwao, niliishuhudia Tax ikiingia maeneo hayo huku kioo kilichoshuka nusu kikionyesha uhalisia wa macho ya mpenzi wangu Martha.
Yeye hakuniona kutokana na yeye alikua anaangalia mbele ambapo uelekeo wa ile taksi ulikua haumruhusu kuniona mimi niliyekua upande wa pili.
Nilimpigia simu. Safari hii iliita baada ya muda mrefu kutopatikana. Cha ajabu hakupokea. Ila baada ya kupiga mara ya pili na kukatiwa simu, ilinipa shaka na kunifanya nigeuze gari na kuanza kuifuatilia. Nilisimama mballi kidogo na kumshuhudia mpenzi wangu akishuka gari na mwanaume mwengine na kuingia ndani kwao huko wakiwa wameshikana viuno.
Sikutaka kuishia hapo, nilitembea taratibu na kuingia ndani na kuwakuta wakiwa kwenye utambulisho mzito.
Niliweza kuwaona wakiwa wana weweseka mtu na dada yake huku Yule mwanaume akiwa anawaangalaa kwa zamu bila kuelewa ni kitu gani kilichowafanya wawe wadogo ghafla.
Sikuongea chochote zaidi ya kugeuka na kuondoka. Nilipanda gari yangu na kurudi nyumbani kwangu.
Nilijua kua sikua peke yangu wakati niliokua na dhiki na yeye alipokua anahitaji mahitaji makubwa ambayo kikawaida siwezi kummiliki. Sasa hivi tayari nimekua mmoja wa watu ambao wana fedha kutokana na kupewa hela za matumizi zilizoweza hata kulipia holteli nzuri kwa usiku mmoja. Hapo ndipo nilipoumia zaidi. Nimegewe nikiwa umasikini na hata nikiwa na hela bado tu nipokonywe?
Hilo ndio swali lililonifanya nijione nipo tofauti sana na watu wengine. Mimi nilitakiwa kua mtu wa kula bata na watu ndio niwapange foleni na si mimi kupangwa.
Ujasiri wa kuanza kumfuta kuanzia kwenye kitabu cha simu yangu mpaka moyoni ukaja na hapo ndipo utekelezaji wake ulipofuata.
Nilichelewa kidogo kupata usingizi. Na ilinichukua takribani masaa matatu kutafuta usingizi ambao ulikuja kwa nguvu zote.
Nilihisi kama ndoto baada ya kumuona msichana mzuri akiwa amekaa kitandani kwagu huku akiwa bado ana nguo zake. Muda wote alikua anatabasamu na kila nikimuagalia alinikonyeza.
Macho yalikumbwa na uzito wa kufumbuka kutoka na kilo nyingi za usingizi zilizokua zimenielemea. Ila utamu wa muendelezo wa maono hayo. Nilijitahidi kufumbua macho yangu kiugumu na kupuuzia mbali jinsi nilivyoweza kuutafuta usingizi huo kwa gaharama kubwa.
“ooh my god,.. wewe tena?”
Niliuliza baada ya kuona sura ya Yule jinni akiwa amerejea.
“sijaja kwa ubaya … ila ni furaha sana baada ya kukukuta unawaza maisha ya ndoto zako za baadae.” Aliongea Yule jini na kunifanya na mimi nikae kitandani. Mpaka wakati huo, usingizi ulipeperuka kabisa na kutobaki hata lepe.
“sijakuelewa bado… una maanisha nini?” nilimuuliza huku nikimtazama usoni ambapo bado alikua anazidi kutabasamu.
“namaanisha kua nimekuja kwa amani hivi sasa. Na napenda ui yonapo sura hii uwe unatabasamu wakati wote. .” aliongea na kunifanya nimuangalia vizuri. Niligundua utofauti wake na watu wa kawaida. Pia uzuri wa sura yake na shape ya kizungu aliyokua nayo. Vilnifanya niondokewe na hofu kabisa niliyoanza kuipandisha baada ya kumuona.
“karibu.” Nilijikuta nimeongea hivyo huku nikimuangalia na kuzidi kumkagua kwa macho.
“naomba nikuache ulale, nitakutembelea kesho nikupe issue.” Aliongea Yule jini na kuniacha kwenye njia panda.
“issue,… issue gani tena?” niliongea na kunifanya nihisi kazi za lawama kurudi tena.
“ni issue kubwa itakayokufanya ufikie malengo yako yote uliyokua unaota kufika. Lakini kwa masharti machache tu kama kweli utakua tayari kuyafuata.” Alongea Yule jinni na kunifanya nizidi kuwa na hamu ya kutaka kujua kua hiyo issue ni ipi.
“nidokeze kidogo basi ili nijue.” Niliomba chabo ilimradi mtihani usiwe mgumu sana kwangu.
“nitakuona kesho…. Bye.”
Hakunijibu zaidi ya kuniaga na kuondoka zake. Hapo ndipo kichwa kilipozunguka na kutafakari ni issue gani itakayonitimizia ndoto zangu zote. Hilo ni swali ambalo majibu ali kua nayo Yule jini mwenywe.

Aliniachia harufu nzuri chumbai kwangu iliyodumu mpaka kunakucha.
Asubuhi hiyo iliyonifanya niamke bila kuonyesha uvivu wowote. Nilianza kufanya mazoezi ya viungo. Baada ya kumaliza, nilirudi nyumbani kwa ajili ya kupata chai na kuendelea na ratiba zangu zingine kwa siku hiyo.
Baada ya kula chakula cha mchana, nilioka na kwenda kupata upepo kwenye fukwe za coco Beach. Nilitulia huku nikiangalia watu waliokua wakiogelea na wengine wakionekana wakiwa wanakatiza huku na huko ilimradi watu wanaendelea waliokuwepo siku hiyo walizidi kunifaya nisijione mpweke.
Ghafla nilijikuta kuna harufu nzuri inatoke nyuma ya kitinilichokaa.niligeuka nyuma na kumkkuta Yule jinni akiwa amevaa bikini na mtandio huku maziwa yake yaliyosimama wima yakiwa yamefunikwa kwa asilimia thelatini kuzibaba chocho zake na sidiria ndogo iliyofanana rangi na bikini aliyoivaa.
“unapenda kuogelea.”
Aliongea maneno hayo baada ya kunyanyuka na kunisogelea pale nilipokaa.
“sio sana.” Nilijibu na kumgeukia. Sikua namuogopa tena kwa sababu nilikua najua kua sina kesi nae.
“mimi napenda sana kuogelea. Tunaweza kwenda kuogelea wote?” aliniuliza na kunifanya ninyamaze bila kujibu kitu chochote.
“twenda basi.” Aliongea huku akiwa amenishika mkono na kuninyanyua.
Niliamka na kuanza kumfuata huyo jinni wa kizungu aliyekua na uzuri unaotofautiana kabia na wazunguninaowajua. Hakufanana na wamarekani wala hakuna taifa ambalo niliweza kuotea atakua katoka huko.
Watu wengi walinigeuza bango kwa kuniangalia na kunishangaa kutokanana na kuongozana na mzungu huyo ambaye alikishikilia kiuno change vizuri kabisa.
Tulienda kukodi boya na baada ya hapo, nilivua nguo zangu na kubaki na Boxer na kwenda naye kwenye maji.
Ubaridi wa mwili wake ulikua kama nimekumbatia barafu. Ila chaajabu. Nilikua nasikia ladha tofauti kabisa iliyokua na kila aina ya utamu pale alipokua akinipapasa kwa mikono yake hiyo ya baribi.
Tuliyacheea maji vya kutosha huku yeyeyakinionyesha ufundi wa kuyakata maji kwa kuzapa upande mmoja na kuibukia upande mwengine wa mbali zaidi.
Ilipofika saa kumi na mbili. Tulitoka na mimi nikaenda uvaa nguo zangu. Yeye hakupata shida. Maana nguo zilitokea kimiujiza tulipokua tumeshapanda wote gari.
“naomba tafuta eneo lolote tulivu tuongee.” Aliongea Yule jinni . name sikubishazaidi ya kufuata alichoniomba.
Tulifika kwenye hoteli moja kubwa katikati ya jiji na kukaa kwa ajili ya mazungunzo hayo aliyoniitia.
“najua kua hulijui jina langu. Mimi naitwa ROSEMARY. Na nimefurahi sana kukutana na wewe japokua hatukukutana kiamani hapo mwanzo. Na sasa nazidi kuufurahia uwepo wako karibu yangu.” Aliongea Yule jinni na kunifanya nivute chupa yangu ya soda na kuimimina kwenye glass taratibu kisha nikapiga fundo moja na kumuangalia huyo jinni.
“hata mimi nilikua najuta sana baada ya kukutana na wewe na nikahisi umekuja kuniharibia muelekeo wangu wote wa maisha. Llakini kadri siku zinvyozidi kwenda nilijikuta napiga hatua tofauti hadoi kufikia kupanda ndege. Mpaka hivi sasa naishi maisha mazuri, yote ni kwa sababu ya pete yako. So naweza sema kua nafurahia uwepo wako kwa sasa kwakua nina amani moyoni.” Niliongea na kumfanya Yule jinni atabasamu.
“umechukua uamuzi gani baada ya kumfumania msichana wako.” Aliuliza Yule jinni na kunifanya nishtuke kidogo. Nilitamai kumuuliza kua alijuaje, ila wazo la kua nilikua naongea na kiumbe tofauti na binaadamu, ndio lilinifanya ninyamaze.
“imeniuma sana kwakweli, maana kama ningekua najua kua itakuja kutokea kitu kama kile, basi nisingethubutu kukanyaga mguu wangu kule… ila sioni haja ya kupanga foleni na Yule msichana. Pia sioni haja ya kuendelea kumpenda mtu ambaye hathamini mchango wangu.” Niliongea kinyonge na kumuangali Rosemary na kumuonajinsi alivyokua na sura ya huzuni juu yangu.
“pole, ila yote ni mapito na mimi nitakuonyesha jia nzuri ya mafanikio ya ndoto zako.” Alirudia huyo kauli na kunifanya niikumbuke hasa aliponiambia usiku.
“toka jana unaniambia utanitimizia malengo ya ndoto zangu. Kwani wewe unajua mimi nawaza nini?” niljikuta nimeuliza huku macho yangu nikiwa nimeyatuliza kwake.
“najua kua ndoto zako ni kuwa maarufu kupitia fani yoyote ile. Najua ni jinsi gani unapenda ufanye kitu ambacho kitaishangaza nchi kama si dunia kwa ujumla. Hivyo na vingine vingi vipo chini ya nyayo zangu. Ina maana nafahamu ufanye nini ili ufikie malengo hayo ambayo ni ndoto kwako kuyafikia.” Aliongea Yule jinni na kunifanya niamini kua kweli alikua anajua kila kitu kuhusu mimi. Hadi vitu ninavyowaza kufanya hko mbele.
“unahitaji kufikia malengo ya ndoto yako?” aliniuliza swali lililonifumbua kutoka kwenye mawazo mazito niliyokua nawaza juu yake.
“yeah.” Nilijibu haraka.
“unatakiwa uanzishe uhusiano wa kimapenzi na mimi. Kila unachokihitaji kwenye dunia hii utaweza kukipata.” Aliongea hayo maneno na kunifanya nibaki nimetumbua macho kama mjusi aliyebanwa na mlango.
ITAENDELEA
 
RIWAYA…..THE MAGIC RING ( 9 )
MTUNZI….. HUSSEIN O. MOLITO
TRANSLATION….. GIFT KIPAPA
UHARIRI…. HAZRAT HUSSEIN
+255 (0)718 97 56 59
“unahitaji kufikia malengo ya ndoto yako?” aliniuliza swali lililonifumbua kutoka kwenye mawazo mazito niliyokua nawaza juu yake.
“yeah.” Nilijibu haraka.
“unatakiwa uanzishe uhusiano wa kimapenzi na mimi. Kila unachokihitaji kwenye dunia hii utaweza kukipata.” Aliongea hayo maneno na kunifanya nibaki nimetumbua macho kama mjusi aliyebanwa na mlango.
Nilitulia kama dakika tatu huku nikitafakari yale maneno na kuyapa uzito wake. Pia nilimuangalia ule muonekano wake na mvuto aliokua nao. Pia jina langu litakavyokua kwenye mawingu na kila mtu atakavyo litaja kwa mbwe mbwe. Pia nilizi waza hela ambazo nitakua naziogelea huku pembeni nikiwa na demu wakizungu anaye niwezesha yote hayo. Majibu ya kukubali yalikuja haraka sana kuliko kumkatalia.
Nilimuangalia na kutabasamu. Hapo hata yeye alishafahamu kitu nilichokubaliana na moyo wangu. Alinyayuka na kunifuta nilipo na kuanza kunipa denda takatifu.
Nilijihisi nipo kwenye chumba cha upepo mwanana huku utamu wa vanilla uliopo ndani ya ice cream tamu ikimiminika mdomoni kwangu. Kufumba na kufumbua, nilijikuta nipo kitandani huku kukiwa hakuna mashahidi wa kushuhudia kitu kinachoendelea.
Nilimpima kwa kupitisha mikonno yangu kwenye kiuno chake kidogo kilichokua na ulaini usioelezeka haku nikijaribu kuminya makalio yake kidogo kidogo.
Nilijikuta nimekamatwa vizuri huku macho yake yakiwa yamemtoka . hayaku nitisha zaidi ya kuni fanya nione ni jinsi gani alivyokua rahisi kumgusa na kugusika kamaa ninavyohitaji.
Niliendelea kuvitembeza vidole vyangu kwenye kila kona ya mwili wake. Na hata sikujua nguo zetu zilichojoka saa ngapi, ila nilicho kuja kugundua ni ubaridi wa hewa yake itokeayo mdomoni ikinishukuru kwa kuakikisha namfikisha kileleni. Sikujua alikua amenitumia saa ngapi, ila tayari alisharidhika na kunyayuka huku akiwa ameniacha kwenye hamu ya kufanya mapenzi.
Nilijikuta nipo kwenye taharuki baada ya kumuona jini huyo akiingia bafuni kwenye chumba hicho kigeni kwangu na kutoka akiwa ameoga vizuri.
“unanipenda?” aliniuliza hilo swali huku akiwa ananiangalia kwa macho malegevu.
“yeah.. nakupenda sana.” Nilimjibu huku kila kiungo changu cha mwili kikiwa kinasisimka kumuona msichana huyo akiwa mtupu.
“unatakiwa uvae hii pete kama kweli unahitaji kuwa na mimi milele.” Aliniambia na kutoa pete kama ile niliyoiokota kutokea mdomoni kwake na kunipa.
Niliichukua bila kusita na kuivaa. Hapo ndipo nilipomuona vizuri akiwa na rangi nzuri tofauti na binaadamu wa kawaida. Pia niliweza kuiona nywele yake ndefu iliyoburuzika mpaka chini baada ya kusukwa na kusokotwa vizuri.
Alipanda kitandani na kuanza kunipa mavituzi ya uhakika mpaka nikakubali ladha ya jini huyo. Hata mimi nilijitahidi na kumfanya asifie uwezo wangu katika mambo ya chumbani.
Baada ya kula nchi na majani yake, tulitoka na kwenda kwenye boti moja ya kukodi na kuyakata maji na kwenda umbali mkubwa ambao haukufikiwa na mtu yeyote wakati huo.
“tunahitajika tule kiapo cha damu ili tusisalitiane.” Aliongea maneno hayo Yule jini baada ya kusimamisha chombo na kuangaliana usoni .
“damu.. mi naogopa mambo ya viapo hususani kutumia damu yangu.” Niliongea huku nikiwa narudi nyuma kidogo. Maana hisia za uoga zilianza kurudi tena.
“sio damu nyingi. Mimi nitajikata kidogo kwenye kiganja changu halikadhalika na wewe utajikata kidogo kwenye kiganja chako kisha tutashikana kwa muda wa dakika moja huku tukiwa tumefumba macho yetu.”
Aliongea Yule jini na kunifanya nimuamini japokua sio kwa asilimia zote.
Alitoa kisu kidogo kimiujiza na kujikata kiganjani. Na mimi nikampa kiganja changu na kunikata. Kisha alinishika mkononi kwanguvu na kunishauri nifumbe macho. Nilitii amri hiyo na baada ya dakika moja mvua kubwa ilianza kunyesha.
Baada ya hapo, nilisikia sauti ya Rosemary ikiniambia nifumbue macho yangu. Spidi ya kope zangu katika kufumbua macho. Ndio spidi hiyo hiyo iliyotumika katika kuzimika kwa mvua.
Hatukuwepo kwenye maji tena. Zaidi nilijikuta nikiwa kwenye pango kubwa huku mpenzi wangu akiwa nyuma yangu kwa hatua zaidi ya thelathini.
“tupo wapi huku?” nilimuuliza huku nikiendelea kuya hangaisha macho yangu huku na huko.
“usipige kelele. Huku ni kwetu. Na nimekuleta uweze kupata Baraka za kuishi na mimi.” Aliongea maneno hayo na kunifanya nimuangalie bila kupata tafsiri kamili ya vitu anavyo vipanga.
Alinikabidhi mwenge na kuanza safari ambayo sikujua nini hatima ya hilo pango.
Tulitoka nje ya hilo pango na kuona mandhari nzuri yenye rangi tofauti tofauti. Mbele yake kulikua na mlima mrefu sana wenye kung’aa dhahabu kila pande.
“juu ya ule mlima. Ndio kwetu.” Aliniambia baada ya kuona naushangaa mlima huo.
“sasa tutapandaje?” niliuliza baada ya kuona hakuna njia yoyote ya kukifikia kilele cha mlima huo kirahisi.
“usijali. Nitakubeba.” Aliongea na kuniangalia huku akitabasamu.
“sasa hivi unatakiwa unizoee nikiwa na maumbo yote. Naomba nijigeuze umbo ambalo linaweza kukutisha kidogo. Lakini mimi ni Yule Yule na siwezi kukudhuru.” Aliniambia huku akinishika mkono kama ishara ya kunituliza.
“sawa.”
Niliitikia huku nikijaribu kufikicha macho yangu kuona ni kiumbe gani huyo atatokea.
Aligeuka na kuwa ndege mweusi kama popo lakini kichwa chake kilifanana kabisa na Tai lakini hakikua na manyoya. Macho yake yalikua mekundu sana na yaliyokua yana waka.
“panda tuondoke.”
Sauti nzito ya ndege huyo ilinitetemesha kidogo. Lakini nilijikaza kiume na kuondoa uoga niliokua nao na kupanda kwenye mgongo wa ndege huyo mkubwa. Kama masihara, Yule ngege alianza kupeperusha mbawa zake name nikaanza kupaa huku nikiwa nimemshikilia vizuri ili nisi dondoke.
ITAENDELEA
 
RIWAYA…..THE MAGIC RING ( 10 )
MTUNZI….. HUSSEIN O. MOLITO
+255 (0)718 97 56 59

Niliitikia huku nikijaribu kufikicha macho yangu kuona ni kiumbe gani huyo atatokea.
Aligeuka na kuwa ndege mweusi kama popo lakini kichwa chake kilifanana kabisa na Tai lakini hakikua na manyoya. Macho yake yalikua mekundu sana na yaliyokua yana waka.
“panda tuondoke.”
Sauti nzito ya ndege huyo ilinitetemesha kidogo. Lakini nilijikaza kiume na kuondoa uoga niliokua nao na kupanda kwenye mgongo wa ndege huyo mkubwa. Kama masihara, Yule ngege alianza kupeperusha mbawa zake name nikaanza kupaa huku nikiwa nimemshikilia vizuri ili nisi dondoke.
Kufumba na kufumbua, tulifika juu kabisa ya mlima na kunishusha. Aliniangalia na kubadilika kutoka kwenye umbo la Yule popo na kua kiumbe wa kawaida.
“tunakaribia nyumbani, naomba chochote kitakacho kukuta uchukulie ni sehemu ya mtihani wako kwetu.” Aliongea Rosemary na kunifanya nishushe pumzi ndefu.
Tulitembea kwa mwendo wa dakika kama ishirini hivi na kufika kwenye mji ambao ulikua na viumbe wenye rangi tofauti na Rosemary.
“wale ni wakina nani?” niliuliza baada ya kuona utofauti wao hata katika maumbile.
“waleni majini wa asili ya huku. Ni tofauti sana na mimi kwakua mimi ni mtoto wa msimu. Huzaliwa mtoto mmoja tu kwa mwaka katika jamii yote mwenye rangi na maumbile kama yangu.” Aliongea Rosemary na kunifanya nitulie na kusubiri mambo yanayoendelea kutokea kwenye safari hiyo.
Tulifika nyumbani kwao na kukaribishwa na wazazi wake. Kila kiumbe alikua ananishangaa huku macho yao yakionyesha hofu juu yangu.
“karibu nyumbani Deo.” Alinikaribisha Rosemary na kunipa kiti.
“nimeshakaribia.” Niliongea huku macho yangu yakiwa chini baada ya kushindwa kuwatazama wazazi wake waliotisha kidogo kutokana na maumbo yao.
“baba, mama… huyu ndio chaguo langu jipya. Ananipenda na mimi nampenda pia. Hivyo nahitaji kufunga ndoa naye.” Aliongea Rosemary huku akiwa amewapigia magoti wazazi wake.
“huyu ni nani na ametokea wapi?” aliuliza baba yake kwa ukali . sauti yake ilinishtua na kunitetemesha sana. Maana niliona kama vile ndio nimetelekezwa ugennini ambapo nikifa hata ndugu zangu hwatapata taarifa wala kunizika.
Nilinyayua macho yangu na kumtazama baba yake huku moyo wangu ukiwa umeshajaa hofu.
“huyu ni binaadamu na anatokea duniani. Yote kwa yote baba. Naomba usimkatae mpenzi wangu.” Aliongea Rosemary na kumuangalia baba yake ambaye alikua bize kuniangalia na kunikagua.
“sasa ukichanganya damu na binaadau, utazaa kiumbe gani wewe?” aliuliza mama yake ambaye daima hakumvunja moyo mtoto wake.
“mimi ni Fundy, hivyo nina muelekeo tofauti na nyinyi wazazi wangu. Hivi kuna kiumbe yoyote humu ameshawahi kuishi na binaadamu. Huoni kua naweza kua fundy wa kwanza kuleta kiumbe tofauti?” aliuliza Rosemary.
“hakuna kiumbe yeyote anayeweza kuishi na binaadamu zaidi ya Fundy. Acheni anioe na mimi nitangeneze familia yangu.” Aliongea Rosemary na kuwafanya wazazi wake waangaliane kwa muda.
“tunahitai furaha kutoka kwako. Kama unahisi kua huyu anatosha kua furaha yako, basi tunakuachia uhuru huo.” Aliongea baba yake na kunifanya nishtuke kidogo. Maana nilihisi kua amani ingetoweka muda sio mrefu. Ila kwa maelezo hayo, yalitosha kunifahamisha kua hakukua na matatizo kwa wazazi wake.
Nilionyeswa sehemu ya kulala na kwenda kupumzika baada ya kupata chakula cha usiku. Kilikua chakula tofauti na vyakula vya huku. Ila nililazimika kula kwa sababu hakukua na vyakula vingine zaidi ya hivyo.
Nilijikaza kiume na kula chakula hicho na kwenda kulala. Asubuhi ya siku ya pili, niliamshwa na kupelekwa jangwani. Huko nilikutana na majini wakubwa waliokua wananisubiri ili wanifanyie mila zao. Nilivuliwa nguo zangu zote na kuwekekewa vidude vmgongoni vilivyinifanya nizimie.
Nilipokuja kushtuka. Nilijikuta nipo kwenye vazi jeupe huku pembeni akiwepo mpenzi wangu Rosemary.
Nnilitulia mpaka walipomaliza, baada ya hapo, ndipo tulipotolewa na kurudishwa ukweni.
“sasa hivi umeshakubaliwa na wakuu wetu. Kwa hiyo ni ruhusa kuoana wakati wowote mtakaoamua wenyewe.” Aliongea baba mkwe na kutabasamu.
Nilitulia siku hiyo na siku ya pili tuliaga na kurudi zetu ulimwenguni kwa kutumia njia ile ile tuliyokuja nayo.
Alipofika huku, alibadilika na kuwa msichana mzuri sana. Ilizidi Yule wa mwanzo. Na hapo ndipo nilipogundua kua Yule jinni alikua anaweza kubadilika na kua na sura yoyote ile aitakayo.
Niliendelea kula maisha na jinni huyo huku mshangao wa kwanza ni kunipeleka kwenye nyumba yake iliyopo masaki na kuniambia kua ni yangu kuanzia siku hiyo. Pili alinipa funguo ya gari aina ya hamer na kuniambia kua nayo ni ya kwangu.
Nilianza kua maarufu kila kona ninyayoingia na wakati mwengine wasichana waliweza kujigonga pindi nilipokua peke yangu.
Yule jini alikua si mkazi sana wa huku. Mara nyingi alikua anaenda kwao kuweka mazingira sawa katika kuhakikisha wananipa nguvu za kuruka angalau niweze kuwa na maajabu japo kidogo.
Ilikua week end moja, niilikua nimelala mchana na kuanza kuota ndoto mbaya sana iliyonifanya jasho lnitoke. Niliota nyumba yangu na gari vyote vina teketea kwa moto huku mchomaji wa vitu vyangu akibaki anacheka sana.
Niliamka na kukaa kitandani kuitafakari ile ndoto.
“jamani motoooo.”
Sauti kali kutoka nje ya nyumba yangu ilisikika. Nilitaharuki kidogo na kutaka kwenda dirishani kutazama huo moto unatoka wapi. Kabla sijanyanyuka kutoka kitandani, kwanza nilianza kuona hali ya hewa ikibadilka mule chumbani.
Mara moshi mzito ukaanza kuingia ndani kwangu. Nilipojaribu kuufungua mlaango ili niweze kutoka nje, mlango ulikua umshajifunga na haufunguki tena.
Nilirudi dirishani na kuchungulia nje. Moto ulikua unazidi kupanba huku chumba nilichokuwemo ndio kinaongoza kwa kuwaka sana.
Kabla sijajua nifanye nini, dirisha lilianza kushika mota. Hapo ndipo nilipojua kua mwisho wa maisha yangu umefikia.
ITAENDELEA
 
RIWAYA…..THE MAGIC RING ( 11)
MTUNZI….. HUSSEIN O. MOLITO
+255 (0)718 97 56 59

Mara moshi mzito ukaanza kuingia ndani kwangu. Nilipojaribu kuufungua mlaango ili niweze kutoka nje, mlango ulikua umshajifunga na haufunguki tena.
Nilirudi dirishani na kuchungulia nje. Moto ulikua unazidi kupanba huku chumba nilichokuwemo ndio kinaongoza kwa kuwaka sana.
Kabla sijajua nifanye nini, dirisha lilianza kushika moto. Hapo ndipo nilipojua kua mwisho wa maisha yangu umefikia.
Moto ulizidi kuambaa mule ndani na joto zito liliendelea kupanda. Vipande vya mbao vilivyokua vinawaka moto vilianza kudondoka na kunifanya nifute kabisa ndoto za kutoka kwenye chumba hicho. Sikua na tumaini tena la kuishi zaidi ya kusali sala yangu ya mwisho kabla malaika wa mauti hajakuja kuichukua roho yangu.
Taratibu moto ulianza kushuka na kufikia usawa wa kitanda upande wa pili. Kitanda na vitu vingine vya kile chumba nilicho kuwemo viliannza kushia moto.
Kufumba na kufumbua, nilikuta dirisha lote halionekani, vioo vikapasuka na moto ndio ukaanza kuingia ndani na kunikaribia kabisa.
Sasa niliwekwa kati kwenye pembe ya ki le chumba baada ya kila mahali kufikiwa na moto. Nilipoinua macho yangu kuangalia juu, niliona moto taratibu ukianza kushuka usawa wangu.
“mpenzi wangu… njoo uniokoe basi.”
Nilijikuta nimemkumbuka Roemary kwa muda huo. Maana kama si uwezo wake mungu, basi maajabu ya jini wangu yangeweza kuuzima ule moto uliokua unanikaribia kuniunguza kabisa.
Mara nilikutana na ubaridi ulionifanya nigeuke nyuma na kumuona mpenzi wangu Rosemary akiwa ameshafika. Sikukubali kupoteza nafasi hiyo ya dhahabu zaidi ya kumkumbatia na kufumba macho yangu.
Dalili za upepo kuwa mkali ndizo zilizonifanya nifumbue macho huku nikiamini kua nimesalimika kutoka kwenye kinywa cha mamba.
Maana nilikua napaa angani huku nikiwa nimeshikilia mabega ya Rosemary ambaye alikua anakata mawingu kuelekea kusiko julikana.
Baada ya muda, alitua na kniangalia kwa huruma.
“pole mpenzi wangu kwa yaliyo kukuta. Ila nimeshamjua alyefanya hivi” aliongea mpenzi wangu na kunifanya nimuulize.
“ni nani huyo aliyeedhamiria kuitoa roho yangu?” niliuliza uku nikionyesha uso uliojaa ghadhabu.
“utamfahamu taratibu. Acha niende nikamtolee uvivu.” Alionea Rosemary na kunibusu. Baada ya hapo, alibadilika na kuwa ndege wa ajabu na kupaa anagani kwa spidi ya ajabu.
**********************
Rosemary aliendelea kuyakata mawingu huku akiangaza huku na huko kumtafuta mbaya wake.kwa mbali aliona nyumba kubwa ikiwa imesjitenga umbali kidogo na alipokua anaishi zamani yeye na Edward. Alitua nje ya nyumba hiyo na kujibadilisha na kuwa Fundy wa kawaida kabisa.
“karibu.”
Alikaribishwa kistaarabu na Fundy mwenye rangi mbili. Rosemary alimuangalia Yule jini mwenzake mwenye uzuri wa kumzidi kwa jicho kali kisha akamshika begani.
“mimi sina ubaya na wewe kabisa. Tena sina haja ya kukuchukia, ila nakuomba mfikishie bwana wako salamu. Acheze kote atakapoamua kucheza, lakini si kwa maisha ya mpenzi wangu. Ukimuambia hivyo ataelewa mimi namaanisha nini. Nakuomba usisahau kumuambia kama kweli unampenda bwana wako.”
Aliongea Rosemarry na kupaa angani bila kuaga.
Masaa mawili baadae, Edward alirudi nyumbani kwake na kumkuta mpenzi wake amepooza.
“vipi mpenzi wangu, mbona hivyo. Waumwa nini?” aliuliza Edward huku akimshika mke wake na kumtomasa mashavuni.
“siumwi. Ila msichana wako amekuja leo nyumbani kwangu.” Aliongea Yule Fundy wa rangi mbili na kumfanya Edward ashtuke.
“Melina, … unaweza kuniambia amekufanya nini nikammalize mtu wake sasa hivi?” aliongea Edward kwa hasira.
“hajannifanya kitu chochote, amekuja kistaarabu tu. Ila ameniambia nikufikishie ujumbe kua uachane na habari za kumfuatilia mpenzi wake. “ aliongea Melina huku akiwa amemkazia macho mpenzi wake.
“anhaa… mi nilifikiri amekuja kukuletea fujo hapa.” Aliongea Edward na kutoka nje.
“sasa unaenda wapi?” aliuliza Melina baada ya kumuona mpenzi wake akiwa na dalili zote za kuondoka tena.
“nakuja…. Kuna mahali naenda mara moja.”
Aliongea Edward na kupaa angani haraka bila kusubiri jibu lolote kutoka kwa Melina.
**********************
Miamba miwili ikakutana tena kwa mara ya kwanza toka walipo tengana mara ya mwisho kwenye mlima huo.
Safari hii kila mmoja alionekana akiwa na hasira na mwenzake na hakua na uso wenye tabasamu kama mara kadhaa walipokutana maeneo hayo.
“nadhai huna jipya zzaidi ya kuomba urudiane na mimi…. Si ndio?” aliongea Edward baada ya kukutana na Rosemary maeneo hayo.
“umekosea sana kusema hivyo. Sana sana naweza kukupongeza kwa kunifanya nikutane na kiiumbe kilichokuzidi kila kitu katika uwezo binafsi wa mapenzi. Hivyo basi, nimeamua kukutana na wewe mwenyewe baada ya kuhakikisha ujumbe unafika kwako. Kama unahitaji wewe na familia yako muishi kwa amani, basi kaa mbali kabisa na mpenzi wangu. Nimegundua kla kitu unachotaka kufanya kwa mpenzi wangu kwa chuki ulizokua nazo. Ila umshachelewa.”
Aliongea Rosemary na kutaka kupaa, lakini alizuiwa kwa kushikwa mkono na Edward.
“nafahamu mapenzi uliyonayo juu yangu. Hivyo kiumbe dhaifu kama Yule hawezi kulinunua penzi kirahisi. Hivyo nakuahidi kua huyo jamaa atashindana na mimi.” Aliongea Edward kwa hasira na kumuachia mkono Rosemary.
“unajidanganya Edward. Kabla hujamgusa, nitakua nimeshakumaliza wewe na mwanamke wako.” Aliongea Rosemary na kuondoka zake kwa kupaa bila kujigeuza Yule ndege anayefananana popo.
“nitakula sahani moja na Yule kiumbe…. Hawezi kula matunda yangu halafu nikabaki namuangalia tu.”
Aliongea Edwrd kwa hasira nay eye akapaa na kkurudi kwake.
ITAENDELEA...
 
RIWAYA…..THE MAGIC RING ( 12)
MTUNZI….. HUSSEIN O. MOLITO
+255 (0)718 97 56 59

Aliongea Rosemary na kutaka kupaa, lakini alizuiwa kwa kushikwa mkono na Edward.
“nafahamu mapenzi uliyonayo juu yangu. Hivyo kiumbe dhaifu kama Yule hawezi kulinunua penzi kirahisi. Hivyo nakuahidi kua huyo jamaa atashindana na mimi.” Aliongea Edward kwa hasira na kumuachia mkono Rosemary.
“unajidanganya Edward. Kabla hujamgusa, nitakua nimeshakumaliza wewe na mwanamke wako.” Aliongea Rosemary na kuondoka zake kwa kupaa bila kujigeuza Yule ndege anayefananana popo.
“nitakula sahani moja na Yule kiumbe…. Hawezi kula matunda yangu halafu nikabaki namuangalia tu.”
Aliongea Edwrd kwa hasira nay eye akapaa na kkurudi kwake.
***********************
Baada ya kukaa kwa muda wa masaa mawili, nilianaza kuhisi baridi huku mwili wangu wote ukipatwa na vipele. Muda mfupi baadae, ndipo nilipo muona mpenzi wangu kwa mbali akirejea kwa kutumia mabawa yake bila kujigeuza Yule ndege mkubwa.
“hapa si salama tena.tunatakiwa kuondoka.” Aliongea maneno hayo Rosemary baada tu ya kushuka .
“vipi kwani, maana nakuona unavyo hangaika.sema kuna nini kinatarajia kutokea?
niliongea baada ya kuona napelekeshwa tu bila kuelewa kitu chochote.
“kuna vitu vingi vipo nyuma ya pazia mpenzi wangu. Na huwezi kuvijua kwa wakati mmoja. Ninachokuomba kwa sasa ni kukubali tu kufuata maagizo yangu ninayokuagiza bila kuangalia yatakua na uzito kiasi gani. Ila niamini tu na ujue kila nikifanyacho ni kwa ajili ya kuku komboa wewe na mimi. Nakupenda sana Deo.” Aliongea mpenzi wangu na kunifanya nikubaliane nae.
Alijigeuza ndege Yule ndege mkubwa na kuniangalia.
“panda.”
Aliongea nami nikatii. Nikapanda na safari ya kuelekea nisipopajua ilianza.
Ilituchukua muda wa saa nziama tukiwa anagani bila kutua. Baridi ya mawinguni ilinishinda na kunifanya nianze kukohoa kwa fujo. Rosemary alipunguza kasi kidogo na kupaa mwendo wa kawaida ambao haukuniumiza kama mwanzo.
Tulifika kwenye pango moja kubwa sana. Rosemary alitua na kuniangalia. Kisha punde tu akabadilika na kurejea kwenye umbo lake la kawaida.
“nisubiri hapa. Ila ukihisi kitu tofauti, naomba upige mluzi.” Aliniambia na mi nikaitikia kwa kutikisa kichwa.
Aliingia ndani na kuniacha pale nje nikiwa nayashangaa mazingira.
Niliganda kwa muda mrefu sana bila mpenzi wangu kutokea. Ndpo nilipochoka kusimama na kuamua kukaa chini ya pembe ya lile pango.
Hapo ndipo nilipojikuta napitiwa na usingizi mzito sana. Mara baada ya muda, nilianza kuota ndoto ya iliyoniduwaza sana. Maana niliota kuna msichana mzuri sana akikatiza mbele yangu huku akinifunulia mapaja yake mazuri na kujibaraguza kwangu.
Alikua na mabawa na kichwani alikua na kofia kama ya malikia Fulani hivi. Nilikurupuka usingizini na kufumbua macho yangu. Niliukutana na sura ile ile niliyoiona wakati naota.
Nilimuona msichana huyo akiwa amesimama mbali na pale na kuanza kuniita huku akijifunua funua.
Nilijikuta natamani kumuangalia huku nikibadilisha pozi mmbali mbali zilizo mvutia sana.
Muito wake wa kimahaba ndio uliovunja thabiti yangu iliyopo moyoni na kujikuta natamani kuwa karibu nae ii niweze kuona kila kitu alichokificha msichana huyo.
Nilijikuta nime nyanyuka na kuanza kupeleka miguu yangu kwa Yule msichana. Kila nikimkaribia, nahisi umbali wake unazidi kusogea inagawaje sikuona utembeaji wake.
Nliweza kuongeza mwendo wa hatua zangu ili mradi nimfikie, lakini sikuweza kufanikiwa zaidi ya kuendelea kutengeneza umbali nae.
Milizidi kutemea na wakati mwngine nilikimbia kabisa katika kuhakikisha napata nafasi nzuri ya kumsogelea kama si kushikana mikono na msichana huyo.
Baada ya muda, nilijikta nipo mahala ambapo kuna miti mingi mirefu. Halafu hakukua na dalili hata moja ya uwepo wa kiumbe chochote maeneo hayo.
Sikumuona tena Yule msichana aliyenivuta mpaka nikafika ameneo hayo. Mara nikaanza kuona mavumbi mazito yakitokea mbele yangu. Kabla hata sijajiuliza yale mavumbi ya nini, mara nikamuona kiumbe mkubwa mwenye umbo la binaadamu akiwa ameshanifikia nilipo.
Nilishtua sana. Na nilipo jaribu kuita, sauti yangu iligoma baada ya kutulizwa na pigo moja kali lililnipeleka mpaka chini.
Nilijikusanya kivivu mna kuamka tena.
“huwezi kutoka huku. Na hata ukitoka huku, hautakua hai tena.”
Aliongea Yule kiumbe na kunitolea meno yake ambayo yalikua ya njano na yalionyesha kua ni makali sana.
Alinifuata na kunifunga kamba kisha akanipeleka kwenye mti mmoja mkubwa na kunifunga hapo. Kisha yeye akaenda pembeni na kuongea kwa sauti kubwa maneno nisiyo yaelewa.
Nguvu za kiumbe huyo nilizipima kwa macho, na kubundua kua zinaweka kua hata mara mia ya nguvu nilizokua nazo.
Nilinyamaza kimya bila kujibu kitu chochote. Baada ya muda, nilimuona kiumbe moja ambaye yeye alikua mzuri zaidi yake akija taratibu karibu na mimi. Nilikutana na uso wake baada ya kuinua uso wangu pale nilipoinama chini muda mrefu.
Niliona Yule kiumbe mkubwa aliye nikamata na knifunga kamba, akiinama chini kama ishara ya kumheshmu Yule kiumbe mwenye umbo dogo tu kama la binaadamu wa kawaida.
“nimefurahi sana kukuona kijana ukiwa katika himaya yangu.” Aliongea Yule kiumbe na kuniangalia kwa dharau.
“mimi naitwa Edward. Nadhani jina hilo sio geni masikioni mwako.” Aliongea maneno hayo na kunifanya nianze kuisumbua akili yangu juu ya kuangalia ni wapi niliweza kulisikikia jina hilo.
“hapana, sikumbuki chchote kuhusiana na Edward.” Nilijibu kwa sauti ya upole.
“kama hujui chochote kuhusiana na Edward, basi utakua unamjua mischana anayeitwa Rosemary. Au hata hilo nimekosea?” aliniuliza na kunisogelea usoni kabisa.
“huyo namjua.” Nilijibu huku nikitetemeka.
“hilo ndio kosa lako kubwa kama ulikua hujui kosa lililokufanya uwe hapa au kukamatwa kawako…. Unajisikiaje kula tunda la mtoto wa mfalme tena bila kuona haya?”
aliniuliza swali lillonifanya alarm ya hatari kuanza kugonga kichwani. Wazo la kua hapo nilipo nilikua nipo katika mikono ya watu wabaya ambao Rosemary alikua anapambana nao muda wote, lilinijia na kunipa amri ya kupiga mluzi kama nilivyo elekezwa na mpenzi wangu.
“uluzi wako hauwezi kumfikia alipo… ni mbali sana. Kilomita 50 toka alipo Rosemary. Tena ukipiga kwa mara nyingine muda huu, utanifanye nikuue kabla ya kumaliza kujibu maswali yangu.”
Alinitisha na kunitolea panga kubwa lilikua na makali kila upande na kunielekezea shingoni. Alinigusa kidigo tu, lakini damu zilianza kutokana na ukali wa hilo panga.
Hapo ndipo nilipofumba macho yangu na kusubiri miujiza ya Mungu, maana kupona na kubaki kuwa hai tena ilikua ngumu sana kwa muda huo.
ITAENDELEA
 
RIWAYA…..THE MAGIC RING ( 13)
MTUNZI….. HUSSEIN O. MOLITO
+255 (0)718 97 56 59
“uluzi wako hauwezi kumfikia alipo… ni mbali sana. Kilomita 50 toka alipo Rosemary. Tena ukipiga kwa mara nyingine muda huu, utanifanye nikuue kabla ya kumaliza kujibu maswali yangu.”
Alinitisha na kunitolea panga kubwa lilikua na makali kila upande na kunielekezea shingoni. Alinigusa kidigo tu, lakini damu zilianza kutokana na ukali wa hilo panga.
Hapo ndipo nilipofumba macho yangu na kusubiri miujiza ya Mungu, maana kupona na kubaki kuwa hai tena ilikua ngumu sana kwa muda huo.
Nilifumba macho yangu huku nikivuta hisia ya kifo cha kikatili kilichokua mbele yangu. Niliwaza sana jinsi atakavyoweza kubararua mwili wangu kwa panga lake lililo kua na makali yasiyo elezeka.
“usijaribu kumgusa huyo kiumbe.”
Nilisikia sauti iliyo nifanya nifumbue macho kumtazama mtu aliyeongea. Ilikua ni sauti ya matuamaini ambayo nilitamani kuisikia muda wote. Hakuwa mwengine, bali ni mpenzi wangu Rosemary.
“kipenzi changu… nakuomba tukae chini tuyamalize. Mimi nipo tayari kuachana na mke wangu kwa ajili yako Rosemay.”
Nilisikia sauti ya kidhaifu kutoka kwa Yule mwanaume aliyeniwekea panga. Aliniacha na kumgeukia huku akiendelea kulalamika.
“ni tamaa tu zilizonifanya nikutendee yote yale. Sasa hivi ndio nameona umuhimu wako katika maisha yangu. Nakupenda sana na naumia ninapokuona na huyu kiumbe.” Aliongea Yule kiumbe huku sauti yake ikiashiria kilio kutoka kwake.
“sikiliza Edward. Hayo unayo ongea yote ni hadithi za kale kabisa ambazo kwa sasa hazina ladha masikioni kwangu. Machozi yangu ya thamani niliyadondosha kwako japokua mimi sikua mkosaji. Nilikubali kujishusha licha ya kuwa wewe ndio msaliti mkubwa wa mapenzi yetu. Ila ukaniona sina maana licha ya kunipa mtiahani wako na kuufaulu kwa wakati. Narudia kusema tena kua. Huyu ndio mwanaume nimpendae. Hata nyuumba ni kwetu wameafiki mimi kuwa nae. Pia muda sio mrefu kutoka sasa atakua na nguvu za kijini kama mimi inagawaje yeye ni binaadamu.”
Aliongea mpenzi wangu maneno yaliyonipa faraja kabisa. Sikuamini kua mpenzi wangu angeweza kunikubali mimi mbele ya Yule jini ambaye alikua ni mzuri na mwenye nguvu nyingi.
“siwezi kukubali wewe uishi na binaadamu wakati mimi nikupendae nipo. Bora tukose wote.”
Aliongea Yule jini na kumshuhudia akilichukua lile panga na kuanza kupambana na mpenzi wangu.
Mwanzoni kabisa Rosemary alionekana akihimili mtanange huo wa kuiokoa nafasi yake, lakini baada ya dakika kumi tu, niliona akiishiwa nguvu na baadhi ya sehemu za mwili wake zilianza kuloa damu kutoakana na kuchanjwa na panga kali analolitumia.
Mara nikaanza kunisikia kama kuna vitu nvinacheza cheza kwenye mikono yangu. Kabla sijagundua utofauti mwengine uliopo kwenye mikono yangu. Nilianza kuhisi kutanuka kifuani na baadae nilitanuka mwili mzima na kukata zile kamba.
Nilimuangalia mpenzi wangu ambaye alikua hoi chini kutokana na kupoteza damu nyingi.
Nilidaka kwa mkono wangu lile panga ambalo lilikua linakaribia kutua sawia kabisa kwenye shingho ya mpenzi wangu.
“huwezi kufanya hivyo kwa mwanamke nimpendaye.”
Nilijikuta naongea hayo huku nikijishangaa mwenyewe kwa jinsi sauti yangu ilivyobadilika.
Nilijikuta nina nguvu za kulipora lile panga kwa makali na kumfanya mpaka Yule kiumbe ayumbe.
Alitoa macho kwa jinsi nilivyokua na uwezo wa jabu. Alijua kua muda aliokua anauzungumzia Rosemary kua nittapata nguvu za ajabu ulikua umeshafika.
Alichokifanya ni kukimbia na kumuacha Yule kiumbe mwengine mkubwa kuniinamia kama ishara ya kuniomba niwe kkiongozi wake.
Nilimfuata mpenzi wangu na kumuweka mgongoni.
“ningekuwa na uwezo wa kupaa. Hivi sasa ninge chanua mabawa yangu na kuwahi nyumbani kumpa matibabu mpanzi wangu.”
Nilipowaza tu hivyo, hapo hapo nilijikuta nimebadilika sana mara nikaanza kusikia kama vitu viwili kwa pamoja vikitoka kwenye mbavu zangu na ndipo nillipokuja kuona mabawa yakiwa yametokea kwenye mbavu zangu baada ya seknde kadhaa.
Niliwaza kupaa. Hapo ndipo nilichokiwaza kikatokea. Nilijikuta yale mabawa yamefunguka na hapo hapo nikajibuta nimeanza kupaa huku nikiyaongoza mabawa hayo kwa fikra zangu ambazo nitakua nimeziwaza kwa wakati huo wapi nielekee.
Nilimuwahisha mpenzi wangu nyumbani na kumpaka madawa aliyonielekeza. Kisha nikampumzisha kwa muda wa masaa matatu. Alipozinduka. Nilimkanda maji na kumpaka dawa ya kukausha vidonda.
“sasa hivi umeshakua kiumbe tofauti na binaadamu wengine. Nadhani ndio muda mzuri wa kuandaa mazingira yetu kwa ajili ya kuoana.”
Aliongwea mpenzi wangu baada ya kumkumbatia kifuani kwangu.
“mimi sina kipingamizi. Nipo tayari kwa lolote mpenzi wangu.” Niliongera maneno hayo na kujikuta nambusu busu mashavuni .
“hata mimi nafurahia uwepo wako.” Aliongea na kuanza kukipapasa kifua changu.
“utaamsha mashetani yaliyolala mpenzi wangu wakati wewe mgonjwa.” Niliongea na kuutoa mkono wake ulioanza kunisisimua sehemu zangu nyeti.
“waache wapande… kiti nipo imara kuwapa chochote wanachokihitaji.” Alinijibu hivyo huku akiyalegeza macho yake malegevu na kuwa malegevu zaidi ya asili yake. Sasa alinigeukia na kutumiamikono yake yote miwili katika kuhakikisha anakipapasa vizuri kifua changu na kunifanya na mimi nimsaidie katika kutaliiw a mbuga zake kwa kuanza na maziwa yaliyofanya nianze kuhisi tukio la kihistoria kutokea.
Nilianza kuziminya chuchu zake changa huku nikizi papasa taratibu na kumfanya aanze kuhema huku mabadiliko ya mwili wake ukizidi kunipa mshawasha wa kuupapasa. Nilianza kumchojioa nguo zake huku nikivionea huruma vidonda vyake alvyokua navyo.
Baada ya mambo yote kuwa live bila chenga, ndipo nilipoanzisha mchezo huo uliotumia dakikika 120 kumalizika huku kukiwa hakuna mshindi. Kila mmoja alisikfia kiwango cha mwenzake. Na sana sana mimi ndio nilipewa sifa za pekee na kuniambia kua hakuna jinni yeyote wa jamii yao ambaye ameshawahi kupata ladha ya binaadamu kama aipatavyo yeye.
Baada ya kuamka na kumuangalia mpezi wangu, ndipo nilipogundua kua hakua na alama yoyote ile ya kuchajwa wala kidonda sehemu yoyote. Nilishangaa sana. Ila nilipokumbuka kua Yule ni kiumbe tofauti na binaadamu, sikuuliza swali tena.
“kesho twende kwa wazazi. Kufanya hivi kabla ya kuoana ni kinyume na taratibu zetu.”
Aliniambia baada ya kulala pamoja usiku na kusifiana maujuzi tuliyo onyeshana.
“sawa…. Mimi ni wako.”
Nilimjibu hivyo na kumfanya atabasamu. Tulipgana mabusu kadhaa na kluala mpaka asubuhi ambapo alinichukua na kunipeleka kwa wazazi wake. Nilipokelewa vizuri sana na wote walifurahi baada ya kusikia kua nimeshapewa nguvu za kijini.
Iliandaliwa mikakati kabambe ya haruhi yetu . kila kiumbe wa huko alipata taarifa juu ya harusi yetu iliyopangwa kufungika siku tatu mbele.
“Edward akisikia atachanganyikiwa eeh?” nilimuuliza mpenzi wangu tulipokua katika maandalizi ya mwisho ya harusi.
“kuna hatari ya kupoteza maisha kabisa kama atachukulia hii ni malipizo kwa aliyonitendea.”aliongea mpenzi wangu kinyonge. Baada ya kumtazama alitabasamu na kuwa mpole tena.
ITAENDELEA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom