The less you know, the happier you are!

The less you know, the happier you are!

Mkuu umenena hapo kwenye kusaidiana;Nipo Ngara huwezi amini mkuu yaani watu wa huku ni hopless kabisa eti wamemchagua Mbunge wa CCM ambaye hajawahi wasaidia kwa chochote na kumwacha Mbunge wa CDM ambaye ni Dr.amewasamnazia Solar kwenye Vituo vya Afya,Amesaidia ujenzi wa maabara za Sekondari,Ujenzi wa madarasa,na aliahidi km wakimchagua angefanya mengi zaidi ya hayo lkn walichokifanya ni kuchagua Pumba na kuacha mchele,sasa dawa yake ni kuyaacha hivyo hivyo yateseke bila kuyaonea huruma,pumbavu kabisa.
Khaa!! Bana kwahiyo huyo Dr alifanya haya ili alipwe kwa kupewa ubunge?
 
Usipoteze muda kuhuzunika. Hakuna kisicho na gharama duniani. Ni juu yako kujipima kuhusu gharama ipi uko tayari (unaweza) kuimudu - kati ya ujinga na maarifa. Ukitaka kuzama zaidi kwenye falsafa hiyo hapo ndipo utakapogundua nguvu rasmi ya Mwenyenzi Mungu ilipo na kwa nini inabidi uitafute na kuitumaini zaidi ya vyote.
 
Ni kweli mkuu ni bora usijue kwamba tume ya taifa ya uchaguzi si huru, bora usijue kwamba katiba ya Tanzania imekaa kidikteta, ni bora usijue kwamba kinachofanya tanzania isiendelee ni mfumo mbovu wa kuanzia chini....utaishi vizuri na utashabikia vitu hivyo hivyo na maisha yatakua vizuri ila ukijua tu....inakua shida
 
Nafikiri ni uamuzi mzuri wa kuacha kusaidia watu ambao wamepewa nafasi ya kujikomboa wakaiacha, halafu mwakani wakidaiwa ada za shule wanaazna kuomba misaada...tuwachinjie baharini.
 
Hakuna haja ya kutaka kuwa mjinga na mpumbavu.

Tatizo watanzania tunaishi kijamaa sana, hata kiongozi tunamuona kama ndugu yetu.

Ndio maana tunampa kura kwasababu ametupa kanga na kofia.

Watanzania tunakosa 'exposure'. Hatuna ile hamu ya mabadiliko.
Hatuna wivu wa kimaendeleo.

Tumeridhika na ujinga na umasikini wetu.

Kwasasa sishangai kwanini kuna watu ulaya wanalala nje na wengine wanalala angani kwenye jets zao.
 
Aisee mtoa mada umenigusa mana hata mimi nna huzuni sana yani watu wote wenye shida zilizopitiliza ndo wanachagua wale ambao hawatawakomboa kutoka walipo na mimi nimedhamiria sana kuwa nikimsikia mtu analalamika kuhusu mfumo mbovu afu analia shida sitamsaidia kabisa afu bora tuzidi kupata shida ili tukumbuke makosa yetu aiseee hadi najionea huruma
 
umenena,me nahic kupasuka kabisaaaaa naomba tu kila kitu kiishs amani irudi.Sina raha kbsa!
 
Khaa!! Bana kwahiyo huyo Dr alifanya haya ili alipwe kwa kupewa ubunge?
Lengo la kuwasaidia siyo kupata Ubunge bali Yeye aligombea Ubunge ili aweze kuwasaidia vizuri zaidi Wananchi kwa kuwasemea huko kwenye vyombo vya maamuzi m.y.ni kwamba kuwasaidia kwa kuwapa misaada ya kijamii peke yake haitoshi km hujawasemea huko mjengoni.
 
Kuna aina ya watu, nashindwa jina gani zuri la kuwapa. Naomba mnisamehe, ila ili kukipa maana hiki ninachokiandika hapa, nitawaita Wajinga au Wapumbavu.

Aina hii ya watu ni wale ambao either hawajasoma kabisa au wana elimu ya msingi na wapo very little informed kuhusu mambo yanavyoendelea Tanzania na duniani!

Ninachokipenda kwa watu hawa, wana furaha muda wote! Yaani utawakuta wanatabasamu na kucheka all the time, hawana stress kabisa mioyoni mwao na ikifika usiku wanalala kwa amani kabisa.

Kadiri unavyojiongezea maarifa, unavyojua mengi zaidi na kuwa well informed kuhusu kila kitu kinachoendelea, huzuni moyoni inaongezeka. Inaongezeka kiasi kwamba moyo unakuuma mchana na usiku hulali kwa raha.

Kadiri unavyozidi kujua zaidi, unapata maswali mengi zaidi yasiyo na majibu!

Ule mstari unaosema "Kwenye wingi wa maarifa kuna wingi wa huzuni, na yeyote ajiongezeaye maarifa anajiongezea huzuni" ni wa kweli kabisa. Na leo nimejua kwamba, the less you know, the happier you are!

Bora niwe mjinga kwa kweli, nimevurugika na huu mchakato wa uchaguzi! Nahisi nitapasuka.

tunapoitwa wanywa vloba sio tunapenda kwa upande wangu sioni kabisa cha kupunguza strees!! nilie nae ndio kabisa anazidi pasuwa kichwa naona kabisa upendo ushapunguwa na sina cha kumlaumu uvumilivu umemchosha kila cku labda keshe!!angalau jamii forum huwa inanifarijisha kimtindo japo kuna manyumbu huwa yanazinguwa.mziki haupenyi tena masikioni maana ukifungulia tu mwenyenyumba kafika anadaichake ni bola uludi magetoni kimya kimya uondoke kimyakimya du!!
 
ifike hatua mambo ya kusaidiana ndugu kulipiana karo, kusaidia huduma za afya. kuwapa watu chakula sijui mavazi eti unawahurumia wana shida huo wakati umepitwa kila mtu aji fight mwenyewe sababu nina uhakika wasio utaka uongozi wa ccm hawana shida wengi wanajiweza kiuchumi na ndo watoaji msaada wakubwa kwa ndugu zao. hakuna kuchoka maandalizi ya uchaguzi wa 2020 ni sasa makosa na mafanikio ya vyama vya upinzani yanapaswa kufanyia kazi kuanzia hivi sasa. mimi sikati tamaa ndo kwanza nimepata hali ya kutoa elimu. ujinga ni ghali sana

Serikali za kidemokrasia ndizo hazina habari na mwananchi mmojammoja,

Leo VOA nimesikia wakenya wanalalamikia serikali yao kuwa ufisadi umezidi kipimo, Nigeria napo kesi ni ileile. Kwa kagame hatusikii kelele za kifisadi, serikali ya Gadafi ililea watu wake kama familia moja.
Tatizo si mfumo tatizo ni mtu anayesimamia mfumo.
 
Nakumbuka kabla ya uchaguzi wa 2010 nikawa namshawishi dada angu amchague Chadema.alinijibu 2005 alienda Mbowe kijijini kwao Singida akawaahidi maji,sista alimpa kura Mbowe awe rais lakini mpaka 2010 Mbowe hakuleta maji licha ya yeye kumpa kura,kwa hiyo hawezi kuipa chadema
 
Mi nashangaa sana watu hisia zao kuita ndio elimu,yani mtu kufuata hisia zake ndiyo anajiona ameelimika. Hivi ni kuelimika gani huko ambako kunamfanya mtu aseme bora hata jiwe awe muongozaji wake kama sio hisia? Yani kama wale wengine hutumia ujinga wa watu kama isemavyo basi hawa wengine hutumia hisia za watu,hakuna tofauti hapo.
 
Nimeumia sana, mm nahisi kuna baadhi ya watu wanashindwa kuhusianisha siasa na maisha.
 
Kuna aina ya watu, nashindwa jina gani zuri la kuwapa. Naomba mnisamehe, ila ili kukipa maana hiki ninachokiandika hapa, nitawaita Wajinga au Wapumbavu.

Aina hii ya watu ni wale ambao either hawajasoma kabisa au wana elimu ya msingi na wapo very little informed kuhusu mambo yanavyoendelea Tanzania na duniani!

Ninachokipenda kwa watu hawa, wana furaha muda wote! Yaani utawakuta wanatabasamu na kucheka all the time, hawana stress kabisa mioyoni mwao na ikifika usiku wanalala kwa amani kabisa.

Kadiri unavyojiongezea maarifa, unavyojua mengi zaidi na kuwa well informed kuhusu kila kitu kinachoendelea, huzuni moyoni inaongezeka. Inaongezeka kiasi kwamba moyo unakuuma mchana na usiku hulali kwa raha.

Kadiri unavyozidi kujua zaidi, unapata maswali mengi zaidi yasiyo na majibu!

Ule mstari unaosema "Kwenye wingi wa maarifa kuna wingi wa huzuni, na yeyote ajiongezeaye maarifa anajiongezea huzuni" ni wa kweli kabisa. Na leo nimejua kwamba, the less you know, the happier you are!

Bora niwe mjinga kwa kweli, nimevurugika na huu mchakato wa uchaguzi! Nahisi nitapasuka.

Usipende kujishughulisha na mambo ambayo unadhani ukiyajua kwa undani na ukweli yatakutesa!mfano,wewe unajua kabisa ukijua mpz wako anachepuka utaumia sana pengine kufa kwa presha,ya nini umchunguze?!Ukitaka kuijua hasara ya kutokuwa na maarifa endelea na ujinga wako yani utakuwa lofa milele!Pia ili uwe na furaha ni lzm ujue unataka nn,vinginevyo utahuzunika kwa kila jambo!Ukiona siasa zinakuvuruga achana nazo sio lzm ufuatilie siasa km zinakuvuruga na ww hutaki kuvurugikiwa!
 
Ni kweli mkuu. Kadri unavyojua ndo unavyojilimbikizia huzuni
 
Back
Top Bottom