The hood of pains

The dirt paka

JF-Expert Member
Apr 11, 2011
371
66
Napenda kuudedicate wimbo huu kwa wanaJF wote mtakaotoka out na wapenzi wenu wapya leo Easter2011.

Verse 1
SAJINA :
Umechagua adhabu ya kujiua,
Iweje sumu umezee maziwa,
Si ndoto alinacha unajua,
Kwahuu wimbo nakupa ukweli,
Umependa mwenyewe kuwa njiwa,
Wivu wa nini kwa ng'ombe anayekamuliwa,
Ukawaridhisha wazazi kwa kuolewa,
Ukaniacha mwenye upendo wa kweli,
Najua sio kosa lako, Najua ni wazazi wako,
Najua mi chaguo lako,
Ila kwanini unikosee...!*2


SAJINA :
Chorus:
"SITAKI TENA KUUMIZWA,
NAMI SITAKI KUMUUMIZA MWENZANGU"*4


SAJINA :
Verse 2
Mmmmh! Aaaah! Mmmmh!
Kama kuvaa na kung'aa mamaa,(mamaa)
Kwabinadamu ni sawa,
Na kama ukinipa salamu wala sitoikataa,
Usinigande usinigande ka luba,
Wazazi wako uliwaona wako sawa,
Sitaki kumuumiza huyu mwenzangu,
Sitaki uumize moyo wangu,
Ni Sajina yule yule,
Na moyo ule ule,
Ni mimi yule yule,
Ulomtupa jongoo na mti wakee...!

SAJINA :
SITAKI TENA KUUMIZWA,
NA MIMI SITAKI KUMUUMIZA MWENZANGU, *4


LINA :
Najua sisitahili kufutwa machozi,
Japo sikuyasababisha mwenyewe,
Najua hustahili kuendelea toa machozi,
Japo naumia kuona tayari unamwingine,
Kwamiguu yangu sikuondoka,
Nilisukumwa wakafanya nipotee,
Moyo wangu bado unaishi kwakoo,
Huku ugenini upo mwili pekeeee...!,
Naumia,
Nalia.
NAumiaaa...!


SAJINA :
Najua sio kosa lako,
Najua ni wazazi wako,
Najua mi chaguo lako,
Ila kwanini unikosee!

SAJINA :
SITAKI TENA KUUMIZWA,
NAMI SITAKI KUMUUMIZA MWENZANGU,*4

* * *
Jamani wanawake mnashindwa kustand for true love?
Ona dogo Sajina anavyolalamika, na huyo Lina anavyobembeleza.

Najua mi chaguo lako,
 
mashairi safi sana. sometime hua tunafanya vitu kwa ajili yetu lakini sometime ua tunafanya kwa ajili ya wengine.

lakini kwa kila tunalofanya hua tunafanya kutoka katika msukumo binafsi ambapo hapa tuna hisia binafsi (moyoni),
akili binfsi, au msukumo wa kimwili mfano tamaa.
AU hua tunafanya kutokana na msukumo wa nje (external forces) kama mazingira, watu au exposure tulinayo n.k
kwa huyu lina(uhusika katika wimbo) inaonekana alishawishiwa au kulazimishwa na wazazi wake ndo akaolewa
na jamaa mwingine japo alimpenda SAJNA.

katika uhalisia simemi kua (SAJNA), asimlaum LINA ila pia sisemi kua SAJNA amwache huyu mpya af amrudie LINA.

Lawama kuuuuuubwa hapa ziende kwa wazazi kwa kuwaharibia hawa wawili mipango yao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom