The difference between Toyota VVTI and D4 Engines


Pamoja mkuu, uwoga unawamaliza sana mafundi wetu wa kitanzania, inatakiwa wajifunze na sio kulaumu hizi techonology
Nakubaliana nawe kuwa kama kuna kitu watu wamekariri vibaya ni uhusiano wa cc na ulaji wa mafuta, nina gari mitsubishi canter moja 5200cc , na nyingine 4200cc , ajabu ni kuwa hii ya cc kubwa iko na nguvu zaidi na fuel economy nzuri kuliko hiyo ya cc 4200 zote zinafanya kazi aina moja.
 

timing belt kwa mimi nilivyo ambiwa . ukiona gari kama haija andikwa nasi unaweza uka amua wewe mwenyewe kiusalama zaidi ni km 100,000 . mimi natumia noah nabadilirisha baada ya km laki moja. Hapo kwa ninavyo ona mimi
 
gari nyingi kwa mtazamo wangu huwa zina haribika mikononi mwa mafundi. mafundi wengi wa hapa kwetu japo wanajitahidi ila sio sana.. gari nyingiza automatic zinawashinda kutengezeneza. mfano gari linaweza kuwa na tatizo la plag lakini ukimplelekea fundi atakacho kwambia huta amini tena anaweza kufungua kitu ambacho hakihusiani. Kwa wanao miliki haya magari mimi naona yakiwa na tatizo la ingini basi tutafute sehemu wanayo angalia kwa compyuta
 
Heeee Jamani Somo Hilo ni gumu sana kwenu maana pamoja na English Zenu,
Engine hizo mbili ni vitu viwili tag auto kabisa vvt I 4 D 4 wapi na wapi 1 g zipo nyingi
Model hizi huendana na matoleo tafauti huku Diesel na Petrol zikishindana kwa unorganized wa matumizi likiwemo Hilo la Emission au hewa ya ukaa sasa Diesel engine zimetoka kwenye diesel pump ya kwanza kwenda kwenye common rail hili Somo ni gumu kwa mtumiaji hata fundi wakawaida hawezi kujua namna ya utendaji wa hiyo system kwanza ni high pressure system
Ikiratibiwa na computer na ina can network fundi lazima awe na ujuzi wa computer ,electronic,
Mechanic, na hata programming sasa gari hizi zote kuanzia 2005 - 2014 siyo hadithi
Lazima uwe mkali katika kukabiliana nazo Leo na fungia hapa ila kwenye shida kuhusu hili
E mail me moto2tech@yahoo.co.uk au Simu 0759-988-988 nimefanya kazi hizi toka miaka ya 1987-2014 sina lakumficha mteja au fundi wa magari au mwanafunzi yeyote
Haji Rashid Amani
 
hembu ngoja tuone kwanza kuangalia mfumo wa uingizwaji wa mafuta ili yaweze kwenda kuchanganyikana na hewa kisha kuunguzwa kwenye combustion chember ulianzia wapi mpaka sasa hivi umefikia wapi.namaana mpaka ulipo gota sasa hivi nikwenye mfumo wa D4.

hapa mm nitazungumzia magari yanayotumia mafuta ya petrol.
tokea magari ya anze kutengenezwa kuna mifumo 3 tuu
1 CARBURETER 1970 mpaka miaka ya 1990
2 FUEL INJECTION EFI 1980 mpaka miaka ya 2000 nakuendelea mpaka hii leo
3 DIRECT INJECTION (d4 ,gdi) 1995 mpaka hivi sasa
1 CARBURETER huu ndio mfumo wakizamani zaidi na ndio ambao bado unatumika mpaka hii leo kwenye pikipiki,mageneretor na bajaji.
kwenye mfumo huu ni kuwa mafuta na hewa vinachanganyika kwenye carbureter nakupita kwenye intake port/maniford mpaka kwenye inlet valve nakuingia kwenye cumbustion chamber kwaajili ya kuunguzwa.

2 FUEL INJECTION efi kwenye huu mfumo yalifanyika maboresho ya kuitoa carbureter na kuwekwa injector/nozzel.hapa nikuwa kila cylinder inakuwa na injector yake kama gari ni ya silinda 4 basi itakuwa na nozeli 4 kama silinda 6 basi itakuwa na nozeli 6.hapa nozeli huwa zinafungwa kwenye intake port hivyo mchanganyiko wa mafuta na hewa huwa yanafanyika kwenye intake port na kuingia kwenye cumbustion chember kupitia inlet valve na kuunguzwa.

3 DIRECT INJECTION gdi/d4 huu ndio mfumo wa kisasa zaidi na ndio wa kileo na kidigital zaidi.kwenye mfumo huu mchanganyiko wa hewa na mafuta huwa unafanyika moja kwa moja kwenye cumbustion chember.nikuwa mfumo huu nozeli/injector zake huwa zinakuwa zimefungwa kwenye silinda head na kwenda moja kwa moja kwenye cumbustion chember.

FAIDA NA HASARA ZA MIFUMO HIYO 3
nazani faida na hasara za hiyo mifumo 3 zinapimwa hasa na mambo makubwa matatu
1 nguvu ya gari
2 uchafuzi wa mazingira
3 ulaji wa mafuta.
*ingawa zipo nafaida zingine nyingi kama za garama lakini huwa mara nyingi naona wanaotengeneza magari kama huwa wana bezi sana kwenye hayo mambo makubwa ma3

katika mifumo hiyo yote hapo juu mfumo ambao hautakiwi kabisa kwa sasa katika hizo faida na hasara kuu 3 wenyewe hauna hata faida 1 na unahasara zote 3 ni wa carburter ukifuatiwa na fuel injection na baba lao ni direct injection wenyewe umekomba faida zote 3 na hauna hasara hata 1 zaidi ya kuwa gharama.

labda nigusie kidogo kwanini mfumo wa DIRECT INJECTION d4/gdi unaonekana kama kusifika sana ni kuwa kwanza ni kwenye ulaji wa mafuta gari yoyote ya mfumo huu huwa inakula vizuri mafuta kwasababu mafuta yake huwa yanapelekwa moja kwa moja kwenye cumbustion chember na nozeli na kwa msaada wa high pressure pump.tofauti na hii mifumo mingine ambayo mafututa huwa yanachanganyikana na hewa nje ya chumba cha mwako na kusafirishwa mpaka kwenye chumba cha mwako kwaajili ya kuunguzwa kwahiyo kuna mafuta mengine hupotea njiani hasa kwenye mfumo wa kabureta ndio ziro kabisa sababu wenyewe kabureta 1 hutumika kwa silinda zote 4 au 6 kinachofanyika yenyewe huchanganya tu mchanganyiko wa hewa na mafuta na silinda husika ambayo itakuwa kwenye zam ya kulipua ndio mchanganyiko huo huelekea so mafuta mengi hupotea njiani.

kwahiyo kwa suala la ulaji wa mafuta sio cc pekee huwa inahusika hata aina ya mfumo huwa inahusika.

hapa kuna mengi sana katika kila mfumo yanatofautiana why mfumo moja uwe na sifa zaidi ya mwingine tambua katika kila mfumo maboresho yamefanyika katika kila idara.mungu akitujalia tutaendelea kujadili na kufahamishana kadri tufahamuvyo.

mwenye swali ruksa kuuliza nitakujibu kadri ya uelewa wangu na nilipo kosea ningeomba nisahihishwe yawezekana mm nimefaham tofauti



NAPENDA SANA MAGARI YENYE ENGINE ZA DIRECT INJECTION mm binafsi kama fundi nawashauri mnaomiliki magari au manaotaka kuyanunua msisite sababu ndio latest technologia ya mzungu why wabongo kutwa tupige madongo??.
kama unataka gari yenye nguvu ,ulaji mdogo wa mafuta kamata gari yenye engine ya D4.
m
nimtazamo wangu tu
 

ameniacha hoi hapa:cvt =complex automatic box
 
ameniacha hoi hapa:cvt =complex automatic box

Mkuu don't quote me wrong.. nimesema Cvt, "a complex autobox" sikuwa na define kirefu chake na ninategemea watu wange google tu kupata maana ya CVT, any way maana halisi ya CVT ni Continuously variable transmission , lakini nilikuwa namaanisha kuwa, ni moja ya automatic gearbox ambayo ni complex na sensitive sana, ila ina ufanisi mkubwa. Hope nimesaidia..
 
VVT-i D4 = Variable Valve Timing with Intelligence D4
Toyota's new VVT-i D4 (D4 is short for "direct injection 4-stroke") engine has been improved by a small, but very effective new idea, that makes it 8% more efficient than the award-winning VVT-i engine. Petrol is now directly injected into each cylinder through a slit-like nozzle giving VVT-i D4 the following benefits:

Increased fuel atomisation for better combustion
Petrol no longer sticks to the injection port when starting cold
VVT-i D4 engines deliver:
Fewer harmful emissions
Lower fuel consumption
Higher power output
 

Pamoja!!
 

Engine za magari yote yanayotumia mafuta ni ICE - Internal Combustion Engines na kwa uelewa wa kawaida ili combustion itokee lazima kuwepo na hewa. So its obvious kwamba D4 na VVTI zote zinaweza kutumika kwa pamoja ili kuongeza ufanisi wa hiyo chemical reaction ya kuchoma mafuta kwenye engine na kutumia nishati ya mafuta kutengeneza mwendo. Kwa nini sasa hapa mnacompare Apples na Oranges??

Ingekuwa poa kama hii toafuti ingeonyeshwa kwa VVTI/FSI etc.
 
Tunashukuru sana kwa somo husika nadhani saaa ni Muda muafaka wa kusaidiana baadhi ya Matatizo
Kama tulivyoona ugum wa kwanza unaanzia kwenye Mafundi wetu Shule zao ndogo

Mimi nimenunua Progress engine D4 vvti gari Ni Nzuri Na Shaa Allah imetenbea 50000 tu
Ina kila kitu mpaka vitabu vyake vya jins ya kuitumia vimo
Tatizo
Gari ina miss flani hivi baada ya kuichukua nikahisi labda mafuta coz taa ilikuwa inawaka nikaweka Nusu tank
Lakini bado inaendelea japo imepungua kidogo sio kama Mwanzo
 

kwamaelezo yako hayo mkuu ni ngum kukusaidia.sana sababu miss kwenye gari hasa za d4 husababishwa na mengi labda kwa ufupi tu kwakuanzia kuna miss ya systerm ya mafuta.
hapo aina ya mafuta mazuri or mabovu nozeli fuel filter safi au ishachoka pressure ya fuel pump n.k

miss ya hewa hapo lazima ucheki air clener kama safi au limechoka. air flow sensor kama ni nzuri au chafu au ishaanza kuchoka. kama kuna hose au pipe ya hewa inavuja imetoboka. check idle sensor kama iko powa.

miss ya moto/umeme hapo cheki plug kama ziko powa au zishachoka,sapersa coil or fire ring order wire,distributer ckp and cmp sensor kama ziko powa naamini ndani ya hayo hapo moja wapo au mawili ndio ugonjwa wa gari yako.
kama upo dar twaweza tafutana then tukasaidiana.
 
mna mashule kweli,nimewakubali.naomba kuuliza wataalamu wangu,carina si 7A ingine ina model gani kati ya hizo?natanguliza shukrani.
 

Gari ni Mpya mkuu ina mwezi tu toka imetoka bandarini
Me niko mwanza
Na nahofia hawa mafundi loko
Ila mwanzoni alieileta alikuwa anaweka vibaba
Mie nineijaza nusu Tank kiasi miss ikapungua
Je kwa Mwanza nitapata wataalamu Gani??
Unaowafaham Mkuu
 

Mkuu Nime ku Pm kuna Moja Muhim
 
nataka kufunga engine ya rav4 kwenye freelander2 je ni engine gani ya rav4 inafaa sana kwenye rav4
 
nataka kufunga engine ya rav4 kwenye freelander2 je ni engine gani ya rav4 inafaa sana kwenye rav4
Uzoefu wangu unaonesha kwamba. Ukiweka injini ya gari nyingine kwenye lisilo lenyewe uwa haikai vizuri pia inakuwa vigumu kuuzika pindi utakapotaka kuiuza.
 

Nimetumia Toyota premio, Engine D-4 vvti, yani Ina power na inatulia Sana barabarani, nimetumia almost 3yrs...iko safi na mlio uko Bomba sana
 
nataka kufunga engine ya rav4 kwenye freelander2 je ni engine gani ya rav4 inafaa sana kwenye rav4

MKuuu hapo bira kujiuluza sanaaa engine ya 3s ndio mpango mzima hapo na ukiniuluza ni engine ya 3s aina gani bila shaka nitakwambia ya 3s distributer coz huwa inakuwa na nguvu sana.
tena pata ya 3s distributer ya uingereza utafurahia.
au kama utaweza hapo tafuta ya 3s ge inayofungwa kwenye celica za mashindano.

then tupeane dili la kuifanyia wiring fundi umeme nipo hapa 0717228064.
mm nipo dar ila hata mkoa mpaka nje ya tz nafika tukikubaliana tuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…