The difference between Toyota VVTI and D4 Engines

WAKUU
Hili suala la mafuta la super au unleaded petrol ni muhimu na linahitaji umakini sana, hasa ukizingatia upatikanaji wake kwenye vituo vyetu hapa bongo, naomba ushauri wenu wakuu. Mimi nilikuwa sifahamu hili na athari zake.

Nawasilisha.
 
Jamani kwanza nimefurahi kukutana na hii topic..mimi nina VISTA Aldeo engen D4 lakini kiukweli inanitesa sana maana inakula mafuta sanaa..yaani inanipa shida..nifanyaje jamani??

Uza mapema kabla haijakutenda
 
haya sasa mi nauza gari yangu RAV 4 mafundi wa ilala wanaita kilitime engine yake D4. KAMA VIPI ni PM. tutaelewana.

D4 kaka ni pasua kichwa! Inasumbua sana! Waliowengi hubadilisha hiyo Engine iitwayo Kilitime na kuwekwa Engine za RAV4 Old Model aina ya 3S. Sina hakika kama tabia za gari zinaweza kubaki zilezile baada ya kubadilisha. Nahisi kwenye Dash Board kutakuwa na taa zinawaka kuonyesha mapungufu kwenye baadhi ya mifumo kufuatia kubadilisha Engine
 
Aisee D4 majanga japo gari huwa yaenda sana, mie nilishawahi kukumbana nayo kwa nadia ikabidi iwekwe option yake 3s kwan hiyo d4 ikaanza tatizo la kuchanganya oil na petrol lkn SS safi.
 
Kirefu cha VVTI ni Variable Valve Timing with Intelligence na si variable valve timing injection mkuu!
 
Niliwahi kununua D4 licha ya kushauriwa nisinunue gari ya engine hiyo, niliipenda zaidi design yake. Yaliyonipata baadae yamenifanya nichukie gari zote.
ushauri; km una D4 na umeitumia angalau miaka 3 iingize sokoni mapema.
 
Japokuwa mtoa mada alikuwa na lengo la kuelimisha, inaonesha hajui mengi kuhusiana na technology za magari, sio source zote kwenye mitandao zinaaandikwa na wataalamu waliobobea , nyingine zinaandikwa na watu wa kawaida ambao wengine hawajui lolote au ni Just tech wanna be!!! tuwe waangalifu sana na sources za kulink la sivyo tunaweza jikuta tunafanya kazi ya kupotosha badala ya kuelimishana..

Heading yenyewe tu inapotosha !! "difference between toyota vvti and d4 engines" huwezi ukalinganisha mifumo miwili yenye kazi tofauti katika engine , ni kama unasema' chungwa la muheza si tamu kama embe la kibada', watu hawatakuelewa japokuwa yote ni matunda !!! If you want to compare then compare like to like systems. kwa ajili ya jukwaa nitaeleza to the best of my knowledge...

Vvti ,vvti-l dual valve ni mifumo ya valve kwenye cylinder head , inahususha jinsi hewa inavyoingia na kutoka kwenye combustion chamber, hapo zamani magari yalikuwa na valve moja ya inlet na moja kwa ajili ya exaust , ie 2valve per cylinder, kadiri engine zilivyowa zinaongezeka performance iliuja kuonekana hewa ilikukwa haiingii nyingi kwa mtindo wa vavle mbili ,idea behind ni kuongeza hewa ili uongeze mafuta then performance , ikawekwa valve nne kwa cylinder , nadhani mnayaona madari mengi tu yameandikwa 16 valve - 4 cylinder , 24 valve - 6cylinder.. e.tc.. ok hizi zote tunaziita fixed valve timming!, variable valve ni mfumo wa valve ambao una adjust air intake kadiri ya mizunguko ya engine .

D4 ni mfumo wa jinsi mafuta( petroli) yanavyoingia na kuungua kwenye cylinder ,hapo kabla kulikuwa na EFI , kabla yake kulikuwa na carburetor.. kwa kusema hivyo namaanisha kuwa unaweza kuwa na d4 ambayo ni Vvti , Vvti-L au fixed valve , na unawezakuwa na Efi ambayo nayo ni VVti ,Vvti-L au fixed valve

kama lengo la mtoa mada lilikuwa ni kufanya comparison ya d4 ilikuwa ni vema ku compare with the predecessors systems that is EFi au Carburetors, sio d4 na vvti, nadhani utaelewa jinsi ulivyochanganya mambo !!!!
 

Kiongozi kama ulishanunua na kutumia hii gari please naomba maendeleo, I am getting confused, ni kweli zina matatizo?
 
hata zilivyoingia auto gearbox mafundi wetu walikuwa wanasema msinunue ni majanga!!!! sababu kuu ni kuwa walikuwa hawana uwezo wa kuzitengeneza zikileta shida, sasa hivi wanasema D4 mbovu wakati ndio latest and most efficient engine[japanese]....sababu ni ile ile hawana uwezo wa kuitengeneza.....
 
Niliwahi kununua D4 licha ya kushauriwa nisinunue gari ya engine hiyo, niliipenda zaidi design yake. Yaliyonipata baadae yamenifanya nichukie gari zote.
ushauri; km una D4 na umeitumia angalau miaka 3 iingize sokoni mapema.

D4 nyingi zilisumbua hapo juzi kati kwa sababu ya mafuta machafu,uchakachuaji ulizidi sana ila si kwasababu D4 ni mbovu.
 
Duh! hapa inaonekana wengi wako chaka. Ina maana mkuu gari zote sasa hivi zitakuwa na d4 engine, maana gari yenye carburator niliyowahi kuishuhudia ni zile landrover 109. Kwa maana hiyo gari ambayo injini yake haijaandikwa vvti itakuwa ni fixed valve, ambazo wengi humu wanasema injni zake zinasumbua. Naomba unifafanulie pia kuhusu hizi aina za injini, kwani kuna wengine humu wamesema kuna injini ya 3S, aina zingine ni zipi. Nitashukuru sana.
 
D4 Ni Kati ya mfumo wa engene bora kabisa kwa mjapani. Ujinga WA mafundi wa hapa mjini kushindwa kuzirekebisha ndo sababu ya haya majungu kila kukicha hapa mtandaoni.
 
Nauza gari yangu aina grand vitara v6.anayetaka tuwasiliane 0769881984,0783085858,0715075858 bei maelewano.
 


[FONT=宋体][/FONT]Vipi bwana Professor! Unaweza nisaidiafeedback ya gari lako? Nimenunua RAV4 ya hiyo engine D4 haina hata week, baadatu ya kubadilisha hydraulic oil ,engine oil na filter imeanza kuleta matatizo?plznaomba nijuze. Nashukuru
[FONT=宋体][/FONT]
 

Hydraulic uliyobadilisha ni gear box? Kama ndio huwa mafundi wengi hawajui vema kuainisha hii fluid, wanachanganya.
 
D4 zina sensor kila mahali... peleka wakafanye diagnosis kwa kifaa cha digital au wengi wanakiita computer... kupima ni kama 60 hadi 70 hivi ila ni cheap kuliko kuwapelekea wapiga nyundo Gerezani. Mafuta yeyote yakiwa chini ya kiwango aidha dash board inawaka au gari inaanza zengwe... unakumbuka gari la msafara wa raisi na mafuta yaliyochakachuliwa Moshi? Na acha kununua mafuta uchochoroni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ