Thank you so much Dear Ex

Thank you so much Dear Ex

Kosa kubwa alilofanya ni kukuambia ukweli. Wanawake wengi wanafanya haya ila hawafunguki kwa waume zao au watu wanaotegemea kuishi nao, wanaliwa kimya kimya.
 
Kosa kubwa alilofanya ni kukuambia ukweli. Wanawake wengi wanafanya haya ila hawafunguki kwa waume zao au watu wanaotegemea kuishi nao, wanaliwa kimya kimya.
Seriously?? So ebu vaa viatu vyangu kama na wewe ndio unaambiwa hivyo ungefanyaje mkuu???
 
Usimuamini mwanamke hata kidogo nitakuambia kwanini hapo chini.
Ni jumapili tulivu ya mwanzo wa mwezi february, mwezi mwekundu, mwezi wa wapendanao. Nikiwa nimeupumzisha mwili uliochoshwa na vurugu za ujana na starehe za jumamosi.

Mara fikra zinarudi miaka kadhaa nyuma na kumkumbuka kipenzi changu "M" , naaaaam! Nilimpenda kweliiii, niliona nimefika mwisho wa kupenda, sikuona sababu za wanaume wanaoangaika na wanawake wa nje (michepuko) huku wakiwa kwenye mahusiano yao, Niliapa kumpenda mbaka mwisho mpenzi wangu "M" .Mapenzi yetu yalifika kwenye peak mpaka kufikia hatua ya kumtambulisha kwa baadhi ya ndugu zangu kwenye familia, kiufupi tulipendana sanaa.

By that time nilikuwa ndio kwanza nimemaliza degree yangu ya kwanza nipo mtaani napambana na maisha huku yeye nikimuacha mwaka mmoja nyuma pale campus, nilihangaika mtaani nikiwa na hopes soon mambo yangu yatakaa vizuri na kuishi ile dream life na mpenzi wangu "M", we both had that kind of lifestyle ya kuspend tukiwa nacho.

The good things about "M" alikuwa muelewa sanaaa, nikiwa na kidogo tulikuwa tunashare, kwenye maisha yetu tuliokaa kwenye mahusiano ya boyfriend/girlfriend hakuwahi kuniomba pesa, hata jero la vocha so ilikuwa jukumu langu kumkumbuka nilipopata vinginevyo hakuweza kuniomba chochote.

Honestly speaking kuna kipindi mtaani mambo yalikuwa yanaenda hovyoo sana ilifika kipindi nakwama mpaka nakosa kabisa hata mlo mmoja wa siku and she was there for me, kiufupi alinipa backup sanaa, "M" hakunitegemea mimi kwa lolote kuanzia kodi ya chumba, mahitaji binafsi mpaka kula yake, binafsi nilijihisi nina deni kubwa kwake, kupambana ili nije siku moja kumtimizia yale aliyostahili.


Well let's make story short, i was far from her, hustle zangu zilikuwa mkoa tofauti na campus so i used to go there kila baada ya muda fulani (kuna muda nilikuwa napitisha mpaka miezi 3) . Baada ya kupiga mishe zangu na kuvuna some amount of money nikisema ngoja nikamsalimie "M", ni kipindi kidogo kilikuwa kimepita.

Baada ya kufika na kukaa gheto (kwa "M" ) kuna hali nikawa siielewi , alikuwa akizungumza na simu wakati mwingi sana usiku na mchana na muda mwingi alikuwa akitoka nje au mbali na mimi, hiyo tabia hakuwa nayo, baada ya kuzungumza nae akasema kuna mtu wa maana sana huwa anazungumza nae na hawezi kuacha calls zake, alinisisitiza sanaa nimuache awe anazungumza na yule mtu then kuna siku atanieleza ukweli.

I was Curious nilimbana sanaa mpaka tukagombana, finally she told me kuwa kuna kipindi alipitia matatizo ya kifamilia, mzee wake alikuwa anaumwa sanaa and he was the only person ambaye alikuwa anamtegemea kwenye mahitaji yake yote kuanzia Tuition fees,mahitaji binafsi, pesa ya chumba (aliwaficha wazazi wake kama amepanga out of campus) na hakuwa na mtu wa kumsaidia zaidi huku akiangalia hali yangu mimi (kwangu pakavu) akaona hata akinambia sitomsaidia chochote (i was broke like hell)

So kuna this Professor alikuwa akimtaka siku nyingi sanaa na alikuwa anamsumbua sana (alishawahi kunambia hii kitu before) so she decided to accept him na alimuhadithia shida zote prof na akawa tayari kumsaidia kwa sharti la kuwa demu wake basi akakubali kuwa na prof kwa kigezo cha kupima HIV then akawa anatoka na prof kuanzia hapo wakati mimi nipo kwenye harakati zangu,

Alinambia alipanga kunieleza ukweli lakini aliogopa hakujua aanzie wapi, She told me hana hisia hata kidogo na prof na hisia zake zote zipo kwangu, alilia kwa uchungu sanaa huku akiomba nimpe muda mpaka atakapomaliza chuo ili aachane na prof because prof ndio alikuwa sponsor wake anaemuweka mjini and by that time alikuwa amebakisha semester moja na nusu agraduate. Men i was down as ****, hasira ziliisha nikabaki kama fala sijui nifanye nini nilimuonea huruma mpenzi wangu "M" on the other side roho iliniuma kuchapiwa tena na prof ninaemjua .

Nilikuwa kwenye wakati mgumu sanaa nikashindwa hata nifanye nini nikakubaliana na hali halisi na ombi lake la kuwa na prof, lakini nafsi yangu iliniuma sanaa na kujiona falaa kwa umasikini wangu, niliuchukia umasikini, roho iliniuma zaidi nikifikiria mwanamke wangu akiwa anageuzwa geuzwa kitandani na prof.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inaendelea.....

Nilifikiria sanaa nikajisemea anyways yule ni wangu tu na atabaki kuwa wangu, huku nikijipa moyo kwanza prof wala hapendwi , alafu anakula tu ile kitu wala haiondoki (ilikuwa ni kujipa moyo tu).

Well nilirudi zangu mkoa kupambana lakini trust me kama wiki mbili zilizita hivi akili yangu yote ikawa inamuwaza "M", nikawa nashindwa kufanya hata kazi muda wote nawaza saizi "M" ndio anakazwa na prof labda, usiombe nipige simu isipokelewe , ni wivu tu ukawa umenijaa napata picha kabisa prof anamkamua demu wangu akili ikawa imenitoka kabisa. Aisee hii kitu ni ngumu wakuu, ujue kabisa unachapiwa demu wako, hapana!

Nilikaa chini kutafakari, sikuweza kumshirikisha mtu yoyote swala lile, ingekuwa aibu sanaa kwangu, unaanzaje kumuhadithia mtu kuwa unachapiwa?? Honestly ile kitu ilinitoa mood sanaa nikaona siwezi kufanya lolote na nilimpenda sanaa "M" nakumbuka nilishika simu na kuandika ujumbe mfupi tu kwenye simu.

"Mimi ni kijana na bado napambana, sijui lini nitafanikiwa, i feel like i can't afford you anyway, naomba nipambane na maisha yangu, i wish you all the best, nitakupenda daima"

Hii text niliirudia zaidi ya mara 20 kuisoma kabla ya kuituma, roho iliniuma kwakuwa sikuwa na mchukia "M" na nilimpenda sanaa, na kile alichokifanya kilikiwa sahihi kwake kwa kipindi kile, lakini kwangu ilikiwa ni mwiba mchungu sanaa. Lakini hakukuwa na namna ambayo mimi ningepata amani ya moyo zaidi ya kutuma ile text na ikawa text ya mwisho kuituma kwa "M" kwa mwaka ule.

Yale yaliyotokea kwangu ilikuwa kama ndoto sikuamini kama ndio nimemuacha "M" nafsi yangu ilitaka kurudi nyuma lakini niliumia sana kile kitendo cha kugongewa, kilinivunja sanaa moyo. Nilijipa moyo kama ameweza kuliwa saizi kisa amekosa ada na kodi vipi huko mbeleni??
Niliichukua ile kitu kama changamoto ya kupambana na njaa, ilikuwa kila nikimkumbuka "M" ndio nilikuwa napata nguvu na hamasa ya kupambana huku nikijiambia Umasikini ni kitu cha kuogopwa sanaa, niliamini kukosa kwangu pesa ndio kulisababisha yote yale , niliapa kufanya kazi kwa jasho langu lote mpaka siku moja pesa iwe rafiki yangu, "M" alinipa lesson ya maisha kuwa Pesa si kila kitu ila ni kitu muhimu sanaa kwenye maisha ya binadamu.

Hivi sasa ni miaka imepita "M" amemaliza chuo na anafanya kazi kwenye organization fulani nzuri tu ambayo probably ni mkono wa professor , anaishi yale maisha aliyokuwa anayaota. Lakini anakili kuna kitu kimoja tu kinamiss kwenye maisha yake(that's Me) , huku mimi nikiwa nimemove on na maisha yangu huku nikikiri kuwa sasa sina urafiki na umasikini, Chenji ndogondogo za kwenda vacation abroad its not a big deal. (am not bragging though ) , tuna mawasiliano mazuri tu na Ex wangu "M" na maisha yanaendelea.

"Everything is possible for those who believes"
Cheers
Mwanamke utakaempata ajihesabu kuwa kapata mwanaume wa kweli. Mkuu jitambue kuwa wanaume wa type yako nowdays ni wachache sana. U r a real man. Hongera sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani kuna nini siku 3 au 4 hizi?
Huyu kaachwa,
Yule kaacha,
Huyu kamwaga mafuta ya upako wa kifo yakauwa watu.
Yule kaweka JF video za uchi za mwanafunzi wa Sheria wa Mzumbe Uni Mbeya.
Yule kapigwa ban kukanyaga unyawemwezini.
Mara waziri mmwaga uno hadharani katumbuliwa!

Basi ili mradi mambo yawe mengi tu, kichwa inauma kwakweli!!
 
Seriously?? So ebu vaa viatu vyangu kama na wewe ndio unaambiwa hivyo ungefanyaje mkuu???
Ningemwacha si kwa sababu kanisaliti au kazini, sababu ni karuhusu nifahamu. Mwanamke mjanja ambaye hajanidharau angemkana huyo na matusi angemtukana maana anajua ni short term mngono na mm ni mumewe. Ukweli ni kwamba wanawake wengi sana wanaliwa pale wanapopewa msaada au wanahitaji msaada. Wengi sana.
 
Back
Top Bottom