Kuanzia heading ya huu uzi "Thank you so much Dear Ex" na hitimisho "tuna mawasiliano mazuri tu na Ex wangu "M" na maisha yanaendelea"Inaendelea.....
Nilifikiria sanaa nikajisemea anyways yule ni wangu tu na atabaki kuwa wangu, huku nikijipa moyo kwanza prof wala hapendwi 😂😂, alafu anakula tu ile kitu wala haiondoki (ilikuwa ni kujipa moyo tu).
Well nilirudi zangu mkoa kupambana lakini trust me kama wiki mbili zilizita hivi akili yangu yote ikawa inamuwaza "M", nikawa nashindwa kufanya hata kazi muda wote nawaza saizi "M" ndio anakazwa na prof labda, usiombe nipige simu isipokelewe 😤, ni wivu tu ukawa umenijaa napata picha kabisa prof anamkamua demu wangu akili ikawa imenitoka kabisa. Aisee hii kitu ni ngumu wakuu, ujue kabisa unachapiwa demu wako, hapana!
Nilikaa chini kutafakari, sikuweza kumshirikisha mtu yoyote swala lile, ingekuwa aibu sanaa kwangu, unaanzaje kumuhadithia mtu kuwa unachapiwa?? Honestly ile kitu ilinitoa mood sanaa nikaona siwezi kufanya lolote na nilimpenda sanaa "M" nakumbuka nilishika simu na kuandika ujumbe mfupi tu kwenye simu.
"Mimi ni kijana na bado napambana, sijui lini nitafanikiwa, i feel like i can't afford you anyway, naomba nipambane na maisha yangu, i wish you all the best, nitakupenda daima"
Hii text niliirudia zaidi ya mara 20 kuisoma kabla ya kuituma, roho iliniuma kwakuwa sikuwa na mchukia "M" na nilimpenda sanaa, na kile alichokifanya kilikiwa sahihi kwake kwa kipindi kile, lakini kwangu ilikiwa ni mwiba mchungu sanaa. Lakini hakukuwa na namna ambayo mimi ningepata amani ya moyo zaidi ya kutuma ile text na ikawa text ya mwisho kuituma kwa "M" kwa mwaka ule.
Yale yaliyotokea kwangu ilikuwa kama ndoto sikuamini kama ndio nimemuacha "M" nafsi yangu ilitaka kurudi nyuma lakini niliumia sana kile kitendo cha kugongewa, kilinivunja sanaa moyo. Nilijipa moyo kama ameweza kuliwa saizi kisa amekosa ada na kodi vipi huko mbeleni??
Niliichukua ile kitu kama changamoto ya kupambana na njaa, ilikuwa kila nikimkumbuka "M" ndio nilikuwa napata nguvu na hamasa ya kupambana huku nikijiambia Umasikini ni kitu cha kuogopwa sanaa, niliamini kukosa kwangu pesa ndio kulisababisha yote yale , niliapa kufanya kazi kwa jasho langu lote mpaka siku moja pesa iwe rafiki yangu, "M" alinipa lesson ya maisha kuwa Pesa si kila kitu ila ni kitu muhimu sanaa kwenye maisha ya binadamu.
Hivi sasa ni miaka imepita "M" amemaliza chuo na anafanya kazi kwenye organization fulani nzuri tu ambayo probably ni mkono wa professor 😅, anaishi yale maisha aliyokuwa anayaota. Lakini anakili kuna kitu kimoja tu kinamiss kwenye maisha yake(that's Me) , huku mimi nikiwa nimemove on na maisha yangu huku nikikiri kuwa sasa sina urafiki na umasikini, Chenji ndogondogo za kwenda vacation abroad its not a big deal. (am not bragging though ) , tuna mawasiliano mazuri tu na Ex wangu "M" na maisha yanaendelea.
"Everything is possible for those who believes"
Cheers 🍻
Ila professor alikuumiza kha, story yako ina uzuni ila nimelazimika kuchekaTrue say mkuu.